STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 14, 2013

Kocha Stars kuiteta Morocco kwa wanahabari

Kocha Kim Poulsen anayetarajiwa kuzungumza na wanahabari keshokutwa

Na Boniface Wambura
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya tiketi kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco. Mkutano huo utafanyika keshokutwa (Mei 16 mwaka huu) saa 5 kamili kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu kwenye jiji la Marrakech nchini Morocco. Taifa Stars ilishinda mechi yake iliyopita jijini Dar es Salaa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco.


No comments:

Post a Comment