STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 19, 2013

Mabondia Juma Fundi , Nassib Ramadhani kuzipiga Idd Pili


Bondia Juma Fundi kushoto akitunishiana misuri na Nasibu Ramadhani wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika sikukuu ya Idi pili wengine kushoto ni mratibu Duni Lianjara Promota wa Mpambano huo Side Mkigoma na kocha wa Nasibu Christpher Mzazi.
PROMOTA WA MPAMBANO WA MASUMBWI SIDE MKIGOMA KATIKATI AKIWAINUA MIKONO JUU MABONDIA JUMA FUNDI KUSHOTO NA NASSIBU RAMADHANI
Mabondia wakisaini mkataba

Ticha la twisheni lanaswa kwa kumbaka denti wa miaka 10

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athmani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba lilitokea juzi hivi karibuni katika kijiji cha Itunge wilaya ya Kyela mkoa wa Mbeya.


JESHI la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia Mwalimu wa Masomo ya Ziada akituhumiwa kumbaka Mwanafunzi wa darasa la nne mwenye umri wa miaka 10.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba lilitokea hivi karibuni katika kijiji cha Itunge wilaya ya Kyela mkoa wa Mbeya.
Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Ipyana Gidion (30) mkulima na mwalimu wa masomo ya ziada (tuition) katika kituo cha Itunge Moravian   mtaa wa Mbugani Wilayani Kyela Mkoani hapa.
Alisema Mtuhumiwa huyo alimbaka mtoto mwenye umri wa  miaka 10, kyusa,mwanafunzi  darasa  la  nne  katika Shule ya msingi Mbugani mkazi wa Itunge “a” na kumsababishia maumivu makali mwilini.
Kamanda Diwani alisema  mbinu iliyotumika ni kuwaruhusu wanafunzi aliokuwa akiwafundisha  kuondoka na kubaki na mhanga kisha kumbaka katika chumba anachotumia kufundishia (darasani).
Aliongeza kuwa  mtuhumiwa  aliwahi kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani kwa kosa la kubaka na kutoka kwa rufaa na kwamba mhanga amepatiwa matibabu na kuruhusiwa ambapo taratibu zinafanywa ili mtuhumiwa afikishwe mahakamani
MBEYA YETU

Mbunge Nassari haamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi


MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amehamishiwa hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi kutokana na majeraha aliyoyapata kutokana na kushambuliwa na watu wasojulikana katika vurugu zilizotekea wakati wa uchaguzi wa udiwani mjini Arusha hivi karibuni.
Awali Mbunge huyo alilazwa hospitali ya Seriani kisha kuhamishiwa KCMC Moshi kwa matibabu kutokana na kushambuliwa na watu wanaodaiwa wafuasi wa CCM kwenye uchaguzi wa udiwani wilayanmi Monduli.

  DIAMOND PLATINUMZ ASAMBAZA VIDEO YAKE YA UKIMWONA



Na Elizabeth John

MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ ameisambaza video ya ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Ukimwona’ ambayo inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Diamond alisema kazi hiyo ameisambaza juzi katika vituo mbalimbali vya televisheni na kwamba anaamini itafanya vizuri kutokana na ubora wa mazingira aliyotumia kushuti video hiyo.

 “Najua mashabiki wangu wananijua vizuri sijaja kuuza sura mjini, naomba mashabiki wangu wakae mkao wa kula kwajili ya kuzipokea kazi zangu zingine zinazofuata kwani nina mashairi mengi yanasubiri muda tu wa kuingia mtaani,” alisema.

Diamond ni kati ya wasanii ambao wanafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya huku akitamba na baadhi ya ngoma zake kama Kesho, Mapenzi basi, Ritha na nyinginezo.

EPIQ BSS 2013 YAZINDULIWA DAR

Mkurugenzi Mtendaji wa Benchmark Production Rita Paulsen akisisitiza jambo wakati akiongea na wandishi wabari wakati wa uzinduzi wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star Seach uzinduzi huo uliofanywa na kampuni ya simu za mkononi ya Zantel (katikati)  ni Afisa Biashara mkuu wa Zantel Sajid Khan na kushoto ni Mshindi wa Bss Walter Chilambo wa BSS