
Bao pekee lililowekwa kimiani na Blaise Mataudi dakika moja kabla ya pambano hilo kwisha lilitosha kuwa ushindi muhimu kaioka pambano hilo lililoshuhudia wageni wa PSG wakicheza pungufu.
Beki Kassim Abdallah wa Evian alilimwa kadi ya njano ya pili dakika ya 61 na kusindikizwa na nyekundu na kuacha pengo kwa timu yake iliyoelekea kuikomalia wenyeji wao kabnla ya Mataudi kufunga bao hilo na kuifanya PSG kufikisha jumla ya pointi 82, 10 zaidi ya Monaco yenye 72.

Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa pia leo, Toulouse ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu ya 0-0 dhidi ya wageni wao Olympique Lyon