STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 16, 2014

Yametimia! CCM yaibuka kidedea Jimbo la Kalenga, Chadema hoi


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya chama cha CCM,Ndugu Godfrey Mgimwa akiwa amebebwa juu na wafuasi wa chama hicho usiku huu,kwenye Ofisi za CCM mkoa,huku wakisubiri matokeo rasmi kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi muda wowote kuanzia sasa.
TOSA no.1
CCM 98 ,Chadema 20, CHAUSTA 0
Ipamba no2. CCM 104, Chadema 10,CHAUSTA 0
Isakulilo CCM 83,Chadema 8,CHAUSTA 0


Kilindi A CCM 69 ,Chadema 23, CHAUSTA 0
Ofisi ya Kijiji(Kilindi) CCM 117, Chadema 53, CHAUSTA0
Zahanati CCM 117,Chadema 67, CHAUSTA 1
Ifunda
Kivalali A CCM 99 Chadema 19 CHAUSTA 0
Kivalali B CCM 109 Chadema 14, CHAUSTA 1
Muwimbi CCM164, Chadema 22 CHAUSTA 0


Mahanzi CCM 130 Chadema 46 CHAUSTA 0
Ikungwe A CCM 131 Chadema 23 CHAUSTA 0
Ikungwe B CCM 216 Chadema 13 CHAUSTA 0
Magunga CCM 184 ,Chadema 4 CHAUSTA1
Wasa CCM 149,Chadema 15 CHAUSTA 0
Usengelidete CCM 260,Chadema 46,CHAUSTA O

KAMANDA WA UVCC MKOA WA IRINGA SALIM ASAS AKICHEZA KWA SHANGWE VIWANJA VYA CCM MKOA KUSHEREKEA USHINDO WA CCM KALENGA

Arsenal yaibutua Spurs yaendelea kuibana Liver

Arsenal's Tomas Rosicky after scoring against Tottenham
Kitu! Arsenal ikijipatia bao pekee lililowarejesha kwenye nafasi ya tatu


BAO la dakika ya pili lililofungwa na Romas Rosicky liliiwezesha Arsenal kuibuka na ushindi muhimu ugenini dhidi ya Tottenham Hotspur na kuendelea kufufua matumaini ya kumaliza ukame wa mataji iliyonayo kwa muda mrefu.
Tottenham ambayo imetoka kuchezea kichapo cha aibu cha mabao 3-1 katikati ya wiki kwenye Ligi ya Europa dhidi ya Benfica, licha ya kucharuka kusaka bao la kusawazisha walijikuta wakimaliza dakika 45 za kwanza wakiwa nyuma.
Hata pamoja na kufanya mabadiliko ya wachezaji, Spurs ilishindwa kulipa kisasi kwa wapinzani wao waliowafunga pia katika mechi ya mkono wa kwanza walipowafuata Emirates na kujikuta wakiendelea kusalia kwenye nafasi ya tano wakiwa na pointi 53, huku Arsenal ikichupa hadi nafasi ya tatu nyuma ya Liverpool ilitoka kuitoa nishai Manchester Utd ikiwa kwao.
Timu hizo mbili zina pointi 62 ila zinatofautiana mabao ya kufungwa na kufungwa nyuma ya Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 66, Manchester City walikuwa wakishika nafasi ya pili mpaka mchana wa leo imerejea kwenye nafasi yake ya nne ikiwa na pointi 60.

CCM yaelekea kunyakua kiti cha Kalenga



TUPO Live Kutoka Kalenga Kunakofanyika Uchaguzi wa Mbunge wa Jimbo hilo hii leo.
Matokeo ya AWALI nikama Ifuatavyo 
KATA YA IFUNDA Ambapo Chadema ilikuwa hai kiasi chake Matokeo niliyopokea haya hapa.
CCM kura 451,CHADEMA 261 NA CHAUSTA 2 JIMBO LA KALENGA LINA KATA 13,JUMLA YA KATA 11 ZOTE CCM WAMESHINDA BADO KATA 2 TU,MATOKEO HAYA NI LIVE KUTOKA KALENGA HAPA
MCHANGANUO MBALI MBALI WA MATOKEO
 Kata ya nzi kituo cha tanroad 
CCM 142, CDM 26, CHAUSTA  1.KITUO CHA OFISINI A  CCM 116  CDM 2, OFISINI B  CCM 112, CDM 34, CHAUSTA 1. KITUO CHA NZI SHULE  CCM 137, CDM 37, CHAUSTA3
DJ SEK

Rais JK aipa Simba Mil 30, Rage hagombei Mei 4

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEillaEEFMRuqEODNSQRGBkBteyU-tWto8t7FPCWBeEN2r1d-xO2jNixNWM-VkoRqBJeiw4CrRDXErKqSwhUIuFSAyqmjeODBu4YTaIGEn7lwje6TcZZxFdbtuNMG6uFDg0o8fLktGlHx04/s1600/IMG_7676.jpg

RAIS Jakaya Kikwete ameipa klabu ya Simba Sh. Milioni 30 ili washughulikie hati ya kiwanja chao kilichopo maeneo ya Bunju B, Dar es Salaam. Akizungumza kwenye Mkutano maalum wa marekebisho ya Katiba ya klabu hiyo uliofanyika asubuhi ya leo Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay mjini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema pamoja na mchango huo, Rais JK aliwatakia heri katika mkutano huo huku akimkabidhi hundi ya fedha hizo kwa ajili ya upatikanaji wa  hati hiyo.  
“Tunamshukuru Rais kwa msaada wake ameonyesha yeye ni mwanamichezo wa timu zote hivyo huu ni ushindi wa Simba na sio wa Rage,”alisema
Alisema kuwa Jumamosi ijayo atapitisha greda kwa ajili ya kusafisha Uwanja huo ili wachezaji waanze mazoezi kwenye Uwanja wao.
Rage alisema kuwa fedha hizo watazitumia vizuri ikiwa sambamba na kupunguza deni la wizara ya Ardhi wanaowadaiwa Sh41 Milioni kati ya Sh92 walizokuwa wanadaiwa.
Simba iliuziwa Kitalu 226 namba 1. Bunju mwaka 2006, uongozi wa Simba ulilipa Sh 50 Milioni Desemba 29, 2011.
Katika hatua hiyo hiyo, Simba imefanya marekebisho kwenye ibara ya 26(5 )sifa za wagombea ambapo kipengele hicho awali kilikuwa kinasomeka “Asiwe aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai kwa kuhukumiwa kifungo.
Kipengele hicho sasa kinasomeka “Asiwe ametiwa hatiani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita bila mbadala wa adhabu. Na endapo ametiwa hatihani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita, awe amemaliza muda wa miaka 5, tangu kuisha kwa kifungo husika bila kitiwa hatiana kwa jingine lolote la jinai.
Wanachama hao hao wamegoma kukipitisha ibara ya 26 (9) Mgombea awe ametimiza angalau miaka mitatu ya uanachama. Ambapo sasa kinasomeka angalau awe na mwaka mmoja wa wanachama.
Pia ibara ya 25 (8) (iii) wajumbe watano wa kamati ya utendaji. Mwenyekiti aruhusiwe kuteuwa wajumbe wengine watano wa kamati ya utendaji ambao anaweza kubadilisha kwa kadri anavyoona inafaa.wajumbe hawa wa kuteuliwa wanatakiwa kuwa na sifa zilizile wanazotakiwa kuwa nazo wajumbe wa kuchaguliwa na wanachama.
Aidha Rage amesisitiza kuwa hana mpango wa kugombea uongozi kwenye uchaguzi mkuu ujao wa klabu hiyo utakaofanyika Mei 4.

Liverpool yawachinja Mashetani Wekundu Old Trafford

Steven Gerrard
KOCHA David Moyes ameendelea kuvunja rekodi za Manchester Utd baada ya Liverpool kupata penati mbili kwenye uwanja wa Old Trafford na kuifumua Mashetani Wekundu kwa mabao 3-0 katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England na kuchupa hadi nafasi ya pili.
Penati hizo za vipindi viwili vimeifanya Manchester Utd kubaki kwenye nafasi ya 7 ikiwa na pointi 48 na Liverpool kufikisha pointi 62 na kuiengua Manchester City yenye pointi 60.
Mikkwaju miwili ya penati ya dakika ya 34 ya kipindi na jingine la dakika ya 46 kupitia nahodha Steve Gerrard na bao jingine la dakika ya 84 la Luiz Suarez lilitosha kumnyamazisha Moyes na vijana wake nyumbani kwa mara nyingine.
Penati ya kwanza ilitokana na Raphael da Silva kuunawa mpira  kabla ya Phil Jones alimvamia na kumuangusha Joe Allen wa Liverpool na kumsukuma na penati hiyo kumwamisha dakika moja baada ya kuanza kwa kipindi cha pili.
Liverpool ilipata penati nyingine ya tatu na Gerrard lakini mkwaju wake ukagonga mwamba na kurejea uwanjani kabla ya Luiz kuja kumalizia shuti la Daniel Sturridge baada ya kuzamisha bao la tatu lililoipa Liverpool ushindi mnono kuelekea kwenye mbio za ubingwa wa England.
Dakika chache baadaye  Arsenal itakuwa uwanja wa White Hartlane kuumana na mahasimu wao wa London Kaskazini, Tottenham Hotspur.