STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 24, 2016

Klopp amfungia kazi Sadio Mane, ataka kumng'oa Southampton

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/04/2626524.main_image.jpg
Sadio Mane aliyeingia rada za Liverpool
VIJOGOO vya Anfield, Klabu ya Liverpool imeingia mawindoni  kumwinda straika wa Southampton, Sadio Mane katika uhamisho wa kitita cha Pauni Milioni 30.
Mkufunzi wa klabu hiyo, Jurgen Klopp anamtaka nyota huyo wa Senegal mwenye  miaka 24 ili kuimarisha safu ya ushambuliajina amepanga kuufanya uhamisho wake kuwa wa kihistoria katika klabu hiyo.
Liverpool na Southampton zitaendelea kufanya mazungumzo kuhusu mpango huo, huku kitita hicho cha uhamisho huo kikiwa kuwa ni suala muhimu zaidi.
Southampton inadaiwa kutaka Pauni Milioni 40 kwa Mane aliyefunga mabao 11 katika mechi 37 alizocheza msimu uliopita wa EPL.
Kitita hicho ni zaidi ya Pauni Milioni 10 ya kile kinachopendekezwa kutolewa na Liverpool, jambo ambalo limefanya mazungumzo kurefushwa zaidi ili kupata muafaka kabla ya njyota huyo kuachiwa atue Anfield.
Southampton ipo mbioni pia kumsaka mrithi wa Ronald Koeman aliyejiunga na klabu ya Everton hatua ambayo huenda ikachelewesha mpango huo.
Klopp alipendezwa na Mane ambaye alihusishwa sana na uhamisho wa Old Trafford wakati wa Louis Van Gaal wakati alipofunga mara mbili baada ya Southampton kutoka nyuma 2-0 na kuiadhibu Liverpool 3-2.

Southampton yampotezea Pellegrini, njia nyeupe kwa Puel

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/06/nintchdbpict000233254556.jpg?w=688
Manuel Pellegrini
http://i.eurosport.com/2016/02/06/1790003-37797351-2560-1440.jpg?w=1050
Claude Puel
http://e0.365dm.com/16/06/768x432/victor-wanyama-spurs_3489343.jpg?20160623221243
Victor Wanyama aliyetua Spurs
IKIWA imeshampoteza kiungo mkabaji wake, Mkenya Victor Wanyama, klabu ya Southampton imedaiwa kuachana na mpango kumnyakua kocha wa zamani wa Manchester City, Manuel Pellegrini.
Klabu hiyo ilidaiwa ilikuwa mbioni kumpa ajira Kocha Pellegrini mwenye miaka 62 ili kuziba nafasi ya Ronald Koeman aliyetimkia Everton, hata hivyo mpango huo umefutwa na sasa inaelezwa njia nyeupe kwa Mfaransa, Claude Puel wa klabu ya Nice.
Imeelezwa Southampton imeachana na Pellegrini na kumgeukia Puel anayeinoa Nice kutokana na kubaini katika mazungumzo yao Kocha huyo kutoka Chile hawezi kuendana na falsafa ya klabu hiyo katika suala zima la maendeleo ya soka la vijana.
Mashabiki wa klabu hiyo wamekuwa na shauku kubwa ya kumuona bosi huyo wa zamani wa Real Madrid na Villareal, aliyetwaa taji la Ligi Kuu ya England miaka miwili iliyopita akitua klabu kwao ili kuchukua nafasi ya Kocha Ronald Koeman aliyewakacha na kuhamia Everton mapema mwezi huu kwa ajili ya msimu ujao.
Southampton inahaha kusaka kocha wakati kiungo wake Mkenya Victor Wanyama akiwa ametimka zake Tottenham Hotspur aliposaini mkataba wa miaka mitano kwa ajili ya msimu ujao na kumpa nyota huyo fursa ya kukipiga Ligi ya Mabingwa Ulaya
.

Mchezaji alimwa kadi nyekundu kwa kupupua uwanjani

http://cdn.adelove.com/wp-content/uploads/2016/06/Adam-Lindin-Ljungkvist.jpg
PERSHAGEN, Sweden
SIKIA hii. Inawezekana haijawahi kutokea kokote, ila mwamuzi mmoja wa soka nchini Sweden amemlima kadi mbili za njano kisha kumtoa kwa nyekundu, beki wa  Pershagen SK, Adam Lindin Ljung-kvist kwa kosa la kupupua (kujamb**) uwanjani.
Beki huyo wa timu hiyo ya ligi ya daraja la chini alikumbwa nakisanga hicho katika mechi dhidi ya
Järna SK na alipokuwa katika harakati za kushangaa kuhusiana na hatua ya refa huyo, alipigwa kadi nyekundu na kuondolewa uwanjani.
Mwamuzi huyo alitaja kitendo cha Adam cha kutoa ushuzi kama tabia isiyo njema kwa mchezaji.
Lakini kulingana na Adam, alidhani alikuwa akifanya hivyo kimaumbile tu na wala hakuwa na nia ya kumchafulia refa hewa.
Taarifa hiyo imeibua malumbano makubwa kote duniani katika mtandao wa kijamii, huku wengine wakisema kuwa hiyo ni mara ya kwanza kwa mchezaji soka kupigwa kadi nyekundu kwa sababu ya kuchafua hewa.

Yanga yakwama kotekote dhidi ya Tp Mazembe


Kikosi cha Yanga

Mashabiki wa Yanga
WAMEKWAMA kotekote. Klabu ya Yanga ilipanga mechi yao dhidi ya TP Mazembe ichezwe usiku wa Jumatano, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) likaigomea. Haikuchoka ikatafuta mbinu nyingine na kuzuia kigoma cha Wakongo kinachoshangilia bila kuchoka wakiungane na watani zao, Simba kwenye Uwanja wa Taifa kwa kutaka kuhodhi majukwaa yote, nalo likagonga mwamba mbele ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyowagomea leo Ijumaa.
TFF kupitia Afisa Habari wake, Alfred Lucas imesema Yanga hairuhusiwi kuyakalia majukwaa yote kama walivyoomba na wakidhubutu wataipata freshi, kwani Kamati ya Mashindano imegomea mchongo wao huo.
Akizungumza leo, Lucas alisema mpango huo wa Yanga hakubaliki na kwamba watatumia jukwaa lao na mengine watatumia wapinzani na watu wengine watakaofika uwanjani Jumanne ijayo, siku itakayopigwa mechi hiyo.
Mechi hiyo itapigwa Saa 10 jioni ya Juni 28 na sio Saa 1:30 usiku wa Jumatano kama walivyoomba awali Yanga kwa sababu wamechelewa kuwasilisja ombi hilo ofisi za CAF ambazo zimewajibu kuwa ratiba itakuwa ile ile ya awali ya Juni 28.
Yanga inahitaji ushindi kwenye mchezo huo wa pili kwao na wa kwanza nyumbani katika Kundi A ya michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kulala ugenini 1-0 dhidi ya MO Bejaia ya Algeria.
Mazembe wanatarajia kutua nchini Jumapili wakipishana saa chache tu na Yanga ambao kwa sasa wapo kambini Antalya wakijifua kujiandaa na mchezo huo.
Baada ya mechi hiyo Yanga inayonolewa na Kocha Hans Pluijm itawasubiri Waghana wa Medeama kwa mchezo wao mwingine katikati ya Julai kabla ya kuifuata kwao Ghana, ambapo ni lazima ishinde mechi hizo tatu kufufua tumaini ya kutinga nusu fainali ili waogelee mihela ya CAF kupitia michuano hiyo ya pili kwa ukubwa Afrika kwa ngazi za klabu baada ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Msimamo wa Kundi A:

Mazembe  1 1 0 0 3 1 3
Bejaia       1 1 0 0 1 0 3
Yanga       1 0 0 1 0 1 0
Medeama  1 0 0 1 1 3 0 

Mbeya City yaibomoa Prisons, yamnyakua mfungaji wao mkali

IMG_20160623_220042
Mkopi akisaini mkataba wa kuichezea Mbeya City
MSHAMBULIAJI nyota wa kikosi cha Prisons-Mbeya, Mohammed Mkopi ameikacha timu hiyo na kutua Mbeya City FC.
Mkopi aliyesaidia na Jeremiah Juma kuibeba Prisons katika Ligi Kuu Bara msimu uliopita wakifunga jumla ya mabao 21 amesaini kandarasi ya mwaka mmoja.
Mara baada ya kusaini kandarasi hiyo, Mkopi, aliyewahi kucheza pia timu ya Mtibwa Sugar alisema  kuwa anamshukuru Mungu kwa kufanikiwa kujiunga na City timu ambayo alikuwa na ndoto za kuichezea  hata kabla ya kusajiliwa na Prison msimu uliopita.
“Kabla sijasajiliwa na Prisons ndoto yangu ilikuwa ni kucheza kwenye timu hii, nashukuru Mungu baada ya msimu mmoja hili limefanikiwa, nitakuwa hapa msimu ujao, lengo langu ni kufanya kazi kwa nguvu  ili niendelee kuwa sehemu ya kikosi hiki kwa muda mrefu zaidi” alisema aliyefunga mabao matano msimu uliopita.

Hivi hili ni soka kweli au vita?

Magoli yaliyowavuruga Waarabu wa ES Setif na kulianzisha

CAF yaing'oa ES Setif kwa vurugu Ligi ya Mabingwa Afrika

http://www.aps.dz/en/media/k2/items/cache/4e4b1fc9eeea638a4484d9ff6d1e996c_XL.jpg
Entente Sportivo Setif iliyong'oka Afrika kwa vurugu
Hali ilivyokuwa katika mechi hiyo kwa vurugu za mashabiki wa ES Setif
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeiondoa klabu ya ES Setif ya Algreia kutokana na vurugu za mashabiki wao wakati wa pambano lao dhidi ya Mamelodi Sundowns, ambapo matokeo yake yamefutwa kwa sasa.
Katika mchezo huo uliopigwa wiki iliyopita mjini Setif, Algeria, Mamelodi iliitambia wenyeji kwa mabao 2-0 na kuibua hasira kwa mashabiki wa klabu hiyo ya Algeria kwa kulianzia mbungi wakirusha mawe, chupa na kufyatua fataki kasi cha kuhatarisha usalama na kufanya mwamuzi kulisimamisha pambano kabla ya muda.
Baada ya Kamati ya Utendaji ya CAF inayohusika na mashindano ngazi ya klabu kukutana na kupitia ripoti ya mchezo huo imeridhika na kuamua kuiondoa Setif kwa kukutwa na hatia ya kushindwa kuthibiti mashabiki wake.
Kwa maana hiyo matokeo ya mchezo huo yamefutwa na Mamelodi pamoja na timu za Enyima ya Nigeria na Zamalek ya Misri wamebakishwa kwenye kundi hilo la B, ambalo kwa sasa litakuwa likiongozwa na Zamalek waliifunga Enyimba ugenini kwa bao 1-0.
Kwa muda mrefu klabu kutoka Afrika Kaskazini kupitia mashabiki wake wamekuwa wepesi wa kufanya vurugu na kuvuruga mechi zinazochezwa viwanja vyao vya nyumbani na hata ugenini kwa kurusha fataki na vikokoro vingine hasa zikifungwa.

Vurugu hizi ndizo zilizoing'oa ES Setif Ligi ya Mabingwa Afrika