STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 10, 2015

UHONDO WA LIGI KUU BARA UMERUDI TENA

Kagera Sugar
Azam

Mbeya City

Yanga

Africans Sports

Simba
UHONDO unarudi. Ndio ule uhondo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara unatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii wakati viwanja sita vitakavyowaka moto, gumzo zikiwa mechi nne tofauti zikiwamo za wapinzani wa jadi wa mikoa ya Tanga na Shinyanga.
Mjini Shinyanga Stand United itavaana na Mwadui, huku Mkwakwani kutakuwa na vita vya Wagosi Wa Kaya dhidi ya Wana Kimanumanu.
Hata hivyo mechi zinazotolewa macho ni za Jumamosi wakati watetezi Yanga watakapokuwa ugenini kwenye dimba la Mkwakwani kuvaana na Mgambo JKT, huku watani zao Simba watakuwa jijini Dar es Salaam kupepetana na vinara, Azam FC.
Ligi Kuu ilisimama kwa muda wa mwezi mmoja na ushei kupisha maandalizi na mechi za kimataifa za timu za taifa, Taifa Stars na Kilimanjaro Stars zilizokuwa zikishiriki michuano ya kuwania fainali za Kombe la Dunia na Kombe la Chalenji.
Yanga iliyoondoka asubuhi ya leo kwenda Tanga ikiwa na kiungo mshambuliaji wake mpya kutoka Niger, Issofou Boubakar Garba, ikiwa na pengo la nahodha wake, Nadir haroub 'cannavaro' aliye majeruhi na kukiwa na hatihati ya kumtuma Donald Ngoma aliyeumia mkono juzi mazoezi, ingawa ameandamana na timu hiyo.
Yanga yenye pointi 22 itavaana na Mgambo ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kuitambia timu hiyo katika mechi yao ya msimu uliopita ilipoifunga mabao 2-0 siku chache tangu Maafande hao walipoitoa nishai Simba, lakini nahodha wa Mgambo, Fully Maganga ametamba kulipa kisasi.
Azam wanaoongoza msimamo ikiwa na pointi 25 itaikaribisha Simba kwenye dimba la Taifa, ikiwa na sura mpya kikosini akiwamo Haji Ugando na Novatus Lufuga waliosajiliwa katika dirisha dogo.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa kali kutokana na upinzani wa timu hizo hasa ikikumbukwa msimu uliopita walikuwa wakiwania nafasi nyuma ya Yanga na kusababisha kutuhumiana 'kuumiza'.
Mechi nyingine za wikiendi hii ni Mtibwa Sugar kuvaana na Mbeya City ugenini, Majimaji kuialika Toto Africans na Kagera Sugar kuikaribisha Ndanda na  watani wa jadi Stand Utd na Mwadui watamaliza udhia Kambarage Shinyanga.
JUmapili kutakuwa na mechi mbili ikiwamo ya Coastal Union dhidi ya watani zao wa jadi Africans Sports, huku timu zote zikiwa katika hali mbaya katika msimamo sawa na JKT Ruvu watakaokuwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam kuvaana na Prisons Mbeya.
Baada ya mechi hizo za wikiendi hii, Yanga itasalia Mkwakwani Tanga kucheza na Sports katika mechi ya kiporo siku ya Jumatano ambapo pia siku hiyo Azam itaikaribisha Mtibwa Sugar huku kiporo kingine cha Simba na Ndanda kitasubiri kuchezwa Januari Mosi mwakani.

Msimamo kamili wa ligi hiyo inayorejea tena ni huu hapa:
1. Azam                9   8   1   0   20 5  25
2. Yanga               9   7   2  0   22  5  23
3. Mtibwa Sugar    9   7   1    1   12  5  22
4. Simba               9   7  0   2   15  5  21
5. Stand Utd         10  6   1  3   11  4  19
6. Prisons             10  5  2   3   10 10 17
7. Mwadui Fc         10  4   3   3   11  10  15
8. Toto Africans     10  3   4   3   6  12  13
9. Mgambo           10  3   2   5   6   9   11
10. Majimaji          10  3   2   5   6   14  11
11. Mbeya City       10  2   3   5   8   9   9
12. Ndanda             9   1    5   3   6   8   8
13. Coastal Union  10  1    4   5   2   8   7
14.JKT Ruvu           10  1   2    7   6   16  5
15. Kagera Sugar    10 1    2   7    2   13  5
16. African Sports  9   1   0   8    1    11  3

Wafungaji:
9- Elias Maguli                      (Stand)
8- Donald Ngoma                (Yanga)
     Hamis Kiiza                      (Simba)
6-Kipre Tchetche                 (Azam)
5-Amissi Tambwe               (Yanga)
4-Fully Maganga            (Mgambo)
   Miraji Athuman                  (Toto)
   Shomary Kapombe          (Azam)
  Jeremiah Juma               (Prisons)
3-Atupele Green              (Ndanda)
   Ibrahim Ajibu                   (Simba)
   Jerry Tegete                  (Mwadui)
   John Bocco                        (Azam)
   Mohammed Mkopi       (Prisons)
   Paul Nonga                   (Mwadui)
   Raphael Alpha                (Mbeya)
   Said Bahanuzi               (Mtibwa)
   Simon Msuva                   (Yanga)
   Didier Kavumbagu          (Azam)
2-Shiva Kichuya                (Mtibwa)
   Malimi Busungu              (Yanga)
   Edward Christopher         (Toto)
   Ally Myovela                 (Prisons)
   Pastory Athanas              (Stand)
   Mohamed Ibrahim       (Mtibwa)
   Mussa Kindu               (JKT Ruvu)
   Samuel Kamuntu        (JKT Ruvu)
1- Farid Mussa                       (Azam)
   Frank Domayo                   (Azam)
   Peter Mapunda            (Majimaji)
   Rodgers Fred                 (Mtibwa)
   Paul Ngway                      (Kagera)
   Themi Felix                      (Mbeya)
   Allan Wanga                      (Azam)
   Jumanne Alfadhil           (Prisons)
   Joseph Mahundi             (Mbeya)
   David Kambole               (Mbeya)
   Justice Majabvi                (Simba)
    Vincent Barnabas          (Mtibwa)  
   Mbuyu Twite                    (Yanga)
   Stamili Mbonde           (Majimaji)
   Rashid Mandawa          (Mwadui)
   Thabani Kamusoko          (Yanga)
   Michael Aidan             (JKT Ruvu)
   Najim Magulu              (JKT Ruvu)
   Kenneth Masumbuko   (Kagera)
   Kiggy Makassy              (Ndanda)
   Salim Mbonde              (Mtibwa)
   Mudathir Yahya                (Azam)
   Hassan Materema          (Sports)
   Joseph Kimwaga             (Simba)
   Alex Kondo                   (Ndanda)
   Salim Kipanga                 (Sports)
   Fabian Gwanse             (Mwadui)
   John Kabanda        (Mbeya City)
   Juuko Murshid                (Simba)
   Ally Shomary                (Mtibwa)
   Hassan Hamis             (Majimaji)
   Ismail Mohammed       (Coastal)
   Geofrey Mlawa      (Mbeya City)
   Abuu Daud                 (Mgambo)
   Malik Ndeule               (Mwadui)
   Bakar Kigodeko          (Mwadui)
   Samir Luhaba              (Majimaji)
   Nassor Kapamba         (Coastal)
   Mohammed Hussen     (Simba)
   Ditram Nchimbi         (Majimaji)
   Seleman Kibuta          (Mtibwa)
   Deus Kaseke                  (Yanga)
   Jabir Aziz                    (Mwadui)
   Juma Abdul                    (Yanga)  

Straika wa Simba atwaa tuzo Kenya

Michael Olunga
MFUNGAJI Bora wa Kombe la Kagame, na Striaka anayemezewa mate na Simba, Michael Olunga ametwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL) katika sherehe za tuzo hizo zilizofanyika usiku wa jana Jumatano nchini humo.
Simba imekuwa ikimfukuzia Olunga tangu alipofanya vizuri na Gor Mahia katika michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika Tanzania Julai mwaka huu na Azam kutwaa ubingwa wa michuano hiyo.
Olunga amefanikiwa kutwaa tuzo hiyo baada ya kufunga mabao 19 na kuisadia Gor Mahia kutwaa ubingwa wa KPL.
Kiungo, Khalid Aucho wa Gor Mahia pia aliyekuwa akiwaniwa na Yanga alishika nafasi ya pili katika tuzo ya Kiungo Bora wa msimu.
Kipa Boniface Oluoch ambaye naye alikuwa akinyemelewa na Simba mwanzoni mwa msimu huu alifanikiwa pia kung'ara katika tuzo hizo kwa kuwatwaa tuzo ya Kipa Bora.
Olunga hata hivyo ametajwa kuwa mbioni kutua klabu ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL) ya Mamelodi Sundown ambayo awali ilikuwa ikimvizia Donald Ngoma wa Yanga ila ikampotezea.

Dk Magufuli atangaza Baraza lake la Mawaziri, Nape aula

http://cdn2.yatosha.com/wp-content/uploads/2015/12/jbb1.jpg
Rais Magufuli (kati) akitangaza baraza lake la mawaziri leo pembeni yake ni Makamu wa Rais, Samia Suluhu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEixVj-oa8o8h5mtB7qrIg9WGVDM6DXh5u6ZCW-onFLhTkXs-61vgU9X7eaqUoCx8GWrXRqX9ue_A7SEYgiDS6_ax4QIF8Nqf2St4KsqRNJI5bi4jLzfOrkAVdVHMOHWcl5fOJIS4j7gkR4/s640/NAPELAANA-620x400.jpg
Waziri Mteule wa Wizara ya Habari Michezo na Wasanii, Nape Nnauye
Na Tareeq Badru
HATIMAYE Rais Dk John Magufuli ametengua kitendawili cha muda mrefu juu ya sura ya Baraza lake la Mawaziri, baada ya mchana huu kulitangaza Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Rais Magufuli ametangaza Baraza lenye watu 19, huku mawaziri wanne wa wizara nyeti ikiwamo ya Fedha na Mipango ikikosa watu wa kuzishikilia.
Jumla ya Wizara 18 zimeundwa na Dk Magufuli, huku akitangaza kufuta semina elekezi ambayo katika Utawala wa Awamu ya Nne ilikuwa kama fasheni kufanya. Dk Magufuli alisema uamuzi huo wa kufuta semina elekezi hiyo ina lengo la kuokoa Sh Bilioni 2 ambazo zingetumika na kusema ni bora zitapelekwa kwenye Elimu kusaidia kutatua tatizo la Madawati.
Baraza hilo jipya la Awamu ya Tano ina sura mchanganyiko ikiwamo wazoefu waliokuwa katika uongozi uliopita, wengine wapya na mmoja Prof Sospter Muhongo ambaye alikuwa gumzo katika sakata ya Escrow lililoibuliwa mwishoni mwa Bunge la 10. Wizara ya Habari, Michezo na wasanii imepewa Katibu Mwenezi na Itikadi wa CCM Bara, Nape Nnauye.


Baraza hilo jipya la Dk Magufuli lipo hivi:

Wizara ya Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora: George Simbachakene  na Angella Kairuki
Naibu: Seleman Jaffo
Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, Muungano na Mazingira: January Makamba
Naibu: Luhaga Mpina
Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu: Jenista Muhagama
Manaibu: Dk. Possy Abdallah na Anthony Mavunde.
Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi: Mwigulu Nchemba
Naibu: William Ole Nasha
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano: Hajapatikana
Naibu: Inj. Edwin Ngonyani
Wizara ya Fedha na Mipango:Hajapatikana
Naibu: Ashantu Kizachi
Wizara ya Nishati na Madini: Prof. Sospter Muhongo.
Naibu: Medalled Karemaligo.
Wizara ya Katiba na Sheria: Dk. Harrison Mwakyembe
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika Mashariki, Kikanda na Kimataifa: Dk. Augustino Mahiga
Naibu: Dk. Susan Kolimba.
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa: Dk. Hussein Mwinyi
Wizara ya Mambo ya Ndani:Charles Kitwanga.
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi: William Lukuvi
Naibu: Angelina Mabula
Wizara ya Maliasili na Utalii: Hajapatikana.
Naibu: Inj. Ramol Makani
Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji: Charles Mwijage.
Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi: Hajapatikana
Naibu: Inj. Stella Manyanya
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto: Ummy Mwalim
Naibu: Dk. Hamis Kigwangala
Wizara ya Habari, Utamadu, Wasanii na Michezo: Nape Nnauye
Naibu: Anastasia Wambura.
Wizara ya Maji na Umwagiliaji: Prof. Makame Mbarawa
Naibu:Inj. Isack Kamwela

Friday, September 11, 2015

Hapa Javu, kule Bahanuzi, hivi mnatokaje kwa Mtibwa Sugar?

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdEulqye6NB2gXsPi5nX52ruKNuZkwLExeKIBZx9YhfvRv9i-1GRUvXwcGWe-uVRRKZzgwsiMkZgmzbo80RFdgxlHnANAjRcCAnSAEfyBFFwRCrJPMxsv_FBRuFjUHKP11ERryy3d8XlE/s640/Javu.jpg
Hussein Javu
STRAIKA Hussein Javu, ameziangalia timu 15 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara inayoanza kesho Jumamosi. Kisha akakiangalia kikosi cha Mtibwa Sugar atakachokichezea msimu huu kwa mkopo akitokea Yanga ambacho kimesafiri mpaka Shinyanga ili kuanza msimu wa ligi dhidi ya Stand United, kisha akatabasamu huku akisema 'lazima heshima itarudi safari hii'.
Javu aliyesajiliwa na Yanga misimu miwili iliyopita akitokea Manungu, alisema kukutana kwake tena na Said Bahanuzi 'Spiderman' na wakali wengine ndani ya Mtibwa kumempa uhakika wa kurejesha heshima yake na ya klabu hiyo kwa mjumla katika ligi hiyo ya msimu huu.
Mtibwa iliyoanza kwa kasi katika ligi ya msimu uliopita kabla ya kutetereka, itaanzia mechi zake ugenini kabla ya kurudi Manungu kuzisubiri Ndanda na Majimaji kisha kuikaribisha Yanga katika pambano litakalochezwa Sept 30 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
"Kwa mziki huu uliopo Manungu, sioni wa kuizuia Mtibwa kurejesha heshima yake msimu huu, ni kazi pevu lakini tumejiandaa kufanya makubwa, hasa kutokana na kurudi nyumbani chini ya kocha Mecky Maxime," alisema Javu.
Javu, Bahanuzi ni baadhi ya wachezaji wapya nane waliotua kwa Wakata Miwa hao kwa ajili ya kuunda kikosi cha msimu huu cha Mtibwa Sugar chenye wachezaji 28, wakiwamo 20 waliokuwa msimu uliopita.
Wengine nane wapya ni kipa Hussen Sharrif 'Casillas' na Issa Rashid 'Baba Ubaya' ambao nao wamerudisha majeshi nyumbani wakitokea Simba.

Lazima pachimbike Chanika, Ndonga zitapigwa hivi hivi!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEje2A78vXEe4Uo4cv-6s9mPx6Wq0Kif0wcoRpp930ZWk7OtAr3bMYet3LfivlK4JOjJVKxsPedLOpmffHtjd8sUlXJ6TL__ItbNw2pPa5ln6JBd4j88n55qMINxDsDLkfem7sagV3-nZwKR/s640/super+d+boxing+promotion.jpg
IWE isiwe ni lazima pachimbike Chanika, hii ni kutokana na mabondia Said Mbelwa na George Dimoso wanatarajiwa kupanda ulingoni ili kuzichapa katika pambano la kuwania Ubingwa wa Taifa wa ngumi za kulipwa.
Mabondia hao watazichapa siku ya Septemba 26 kwenye Ukumbi wa Butiama Villa Club, Chanika ambapo siku hiyo mashabiki wa soka hasa wa Simba na Yanga watakuwa wameshafahamukitu gani walichovuna kwenye pambano lao la  watani litakalofanyika kwenye Uwanja wa Taifa katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2015-2016.
Mratibu wa pambano hilo, Rajabu Mhamila 'Super D', alisema kuwa Mbelwa na Dimoso ambao tayari wapo kwenye kambi zao za maandalizi huku wakitambiana watazipiga katika pigano la raundi 10.
Super D alisema pambano hilo la uzito wa kati litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi likiliwemo la Seleman Zugo dhidi ya  Abdallah Luanje, Adam Ngange atakayeumana na Shaaban Mtengela.
Siku hiyo pia Said Uwezo ataonyesha uwezo wake dhidi ya Hassan Mgosi, Hamza Mchanjo yeye ataumana na Ally Maiyo katika mipambano tofauti isiyo ya ubingwa.
Super D alisema siku hiyo kutakuwa na uuzwaji wa DVD mpya za michezo kadhaa ya ngumi za kimataifa likiwamo pambano lililofunika mwaka huu wa 2015 kati ya Manny Pacquiao na Floyd Mayweather ambalo liliisha kwa Mmarekani Money Man kumchapa Man Pac

KUMEKUCHA LIGI KUU YA TANZANIA BARA 2015-2016

http://www.soka25east.com/wp-content/uploads/2015/08/image17.jpg
Watetezi Yanga
http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/07/Kikosi-cha-azam.jpg
Azam Fc washindi wa pili wa msimu uliopita
http://simbasports.co.tz/file/2015/08/simba-sports-club-212.jpg
Simba waliokamata nafasi ya tatu msimu uliopita
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/07/MBY-CITY.jpg
Mbeya City iliyokimbiwa na nyota wake wengi
VITA vya takriban miezi tisa vitakavyohusisha klabu 16 vinatarajiwa kuanza kesho Jumamosi wakati pazia la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2015-2016 litakapofunguliwa rasmi.
Michezo saba itakayopigwa kwenye viwanja saba tofauti inatarajiwa kukata utepe wa ligi hiyo, kabla ya keshokutwa Jumapili kupigwa pambano la kukamilisha raundi ya kwanza litakalozikutanisha mabingwa watetezi, Yanga na mabingwa wa zamani Coastal Union ya Tanga.
Mechi za fungua dimba zitakazopigwa leo Jumamosi ni pamoja na lile la mabingwa wa Tanzania wa mwaka 1988 waliorejea Ligi Kuu baada ya miaka zaidi ya 20 itakayovaana na Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Simba haijaonja ushindi kwenye Uwanja huo tangu mwaka 2012 pale Patrick Mafisango alipofunga bao pekee na la ushindi wakati timu hiyo ikiizamisha Coastal Union kwa bao 1-0.
Mechi nyingine ni ile itakayozikutanisha Stand United dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Kambarage Shinyanga, Mwadui itakuwa wageni wa Toto Africans Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza na Majimaji Songea itaialika JKT Ruvu katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Ndanda watakuwa wenyeji wa maafande wa Mgambo JKT pale Nangwanda Sijaona, Mtwara, huku Azam itaikaribisha Prisons Mbeya Uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es Salaam na Mbeya City kuvaana na wakata Miwa wa Kagera Sugar Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.


Msimu wa 52
 Huu utakuwa ni msimu wa 52 tangu kuanzishwa kwa ligi hiyo mnamo mwaka 1965 ikiwa na maana mwaka huu wa 2015 ni mwaka wa 50 tangu kuanza kwa michuano hiyo mikubwa nchini.
Klabu 16, nne zikiwa zilizopanda daraja na kurejea Ligi Kuu ya Bara na nyingine 12 zilizosalimika kwenye ligi iliyopita zitachuana kuwania taji hilo ambalo kwa sasa linashikiliwa na mabingwa wa kihistoria wa ligi hiyo, Yanga.
Yanga ndiyo klabu iliyotwaa mara nyingi ubingwa wa ligi hiyo tangu mwaka 1965, ikitwaa mara 25, huku wakifuatiwa kwa mbali na watani zao, Simba walionyakua mara 18.
Mtibwa Sugar ya Morogoro ndiyo klabu inayovisogelea vigogo hivyo ikiwa imeshinda ubingwa mara mbili mwaka 1999 na 2000, huku timu nyingine sita za Cosmo, Mseto, Pan Africans, Tukuyu Stars na Azam kila moja zikinyakua mara moja moja na kuhitimisha orodha ya mabingwa wa ligi.

Haina ugeni

 Majimaji-Songea, African Sports, Toto Africans na Mwadui Shinyanga ndizo klabu zilizopanda daraja msimu huu zikitokea katika Ligi Daraja la Kwanza (FDL), ila ukweli ni kwamba hazina ugeni na ligi hiyo.
Kwa nyakati tofauti timu hizo zimeshaichezea ligi hiyo kabla ya baadhi kuzama kimoja kama ilivyokuwa kwa Mwadui iliyoshuka daraja mwaka 1986, Sports (1991) na Majimaji na Toto Africans zikipanda na kushuka kila zilipokuwa zikijisikia.
Kwa maana hiyo ligi ya msimu huu haina klabu ngeni za ligi hiyo, japo baadhi zimerejea kuichezea ikiwa imepita miaka mingi.
Ujio wa Mwadui na Sports na hata Majimaji unakumbusha enzi za Ligi Daraja la Kwanza ambapo klabu hizo zilijijengea jina kubwa kwa mafanikio iliyopata kwa nyakati tofauti kabla ya kupotea.
Zinakutana na klabu zilizolowea kwenye ligi hiyo kama Yanga, Simba, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar, Azam na JKT Ruvu ambazo tangu zianze kushiriki ligi hiyo kwa misimu tofauti hazijawahi kushuka daraja.
Mbali na klabu hizo ngangari, pia zitakumbana wakali wengine kama Coastal Union, Prisons-Mbeya, Stand United, Mgambo JKT, Mbeya City na Ndanda.

Mchuano 

Kama misimu mingine iliyopita, ligi ya safari hii inatarajiwa kuwa na mchuano mkali kati ya klabu shiriki na hata kwa wachezaji waliosajiliwa na klabu hizo. Inatarajiwa kuwepo kwa mchuano wa wachezaji wazawa na wale wa kigeni (mapro) sambamba na makocha kutunishiana misuli.
Jumla ya makiocha 16 wakuu, wakiwamo sita wa kigeni watakuwa na kazi ya kuthibitisha ubora wao katika msimu huu, sawa na itakavyokuwa kwa wachezaji mapro dhidi ya wazawa ambao msimu uliopita walifunika mwanzo mwisho kwa kunyakua tuzo karibu zote za VPL 2014-2015.
Simon Msuva aliweka rekodi ya kunyakua tuzo ya Mfungaji Bora akiwa na mabao yake 17 na pia tuzo ya Mchezaji Bora wa msimu, huku Kipa Bora akiwa ni Shaaban Kado na Kocha Bora ikienda kwa Mbwana Makata.
Je, wazawa wamezinduka na kuendelea kuwafunika mapro au ni nguvu ya soda tu baada ya misimu kadhaa ya kukimbizwa mchakamchaka na wachezaji wa kigeni waliotawala kila kona? Tusubiri, japo inatarajiwa msimu huu inatabiriwa kuibuka kwa nyota wapya ambao watafunika kutokana na vipaji vyao turufu ikiwabeba akina Geofrey Mwashiuya, Matheo Simon, Farid Mussa, Deus Kaseke, Malimi Busungu na wengineo.

Utabiri 

Kwa namna klabu zilizofanya usajili mzuri na kufanya maandalizi ya kutosha ni vigumu kutabiri moja kwa moja klabu zenye nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa msimu huu, lakini kwa kuangalia kikosi kimoja kimoja turufu inaziangukia timu za Yanga, Azam, Simba na Mwadui Shinyanga.
Hata hivyo kwa kuwa soka ni mchezo usiotabirika kirahisi siyo ajabu kuziona Stand United, JKT Ruvu, Majimaji, Coastal Union na Mtibwa Sugar zikichanua na kusumbua msimu huu.
Katika janga la kushuka daraja mwishoni mwa msimu kura inaziangukia Ndanda, Mgambo JKT, African Sports, Toto Africans na Prisons-Mbeya, kama hazitakaza buti na kupambana zitaenda na maji. Hii ni kwa sababu zilionekana kutojipanga kama klabu nyingine, japo siri ya mtungi...!
Zikikaa vibaya zinaweza kujikuta mwishoni mwa msimu zikifuata mkumbo wa Ruvu Shooting na Polisi Moro zilizoshuka msimu uliopita, pia zinapaswa kufahamu msimu huu timu tatu ndizo ambazo zitakazoteremka daraja hivyo zijipange kwelikweli. 


Ratiba:

Kesho Jumamosi:
Ndanda     v Mgambo JKT
African Sports v Simba
Majimaji    v JKT Ruvu
Azam         v Prisons
Stand Utd   v Mtibwa Sugar
Toto Africans   v Mwadui Fc
Mbeya City   v Kagera Sugar
 

Jumapili:
Yanga    v Coastal Union
 

Jumatano:
Yanga v Prisons
Mgambo JKT v Simba
Majimaji  v Kagera Sugar
Mbeya City v JKT Ruvu
Stand Utd  v Azam
Toto Africans v Mtibwa Sugar
Ndanda v Coastal Union
Alhamisi:

Mwadui FC v African Sports
 

Orodha ya Mabingwa tangu 1965-20151965- Sunderland (Simba)
1966- Sunderland (Simba)
1967- Cosmopolitan
1968- Yanga
1969- Yanga
1970- Yanga
1971- Yanga
1972- Yanga
1973- Simba
1974- Yanga
1975- Mseto
1976- Simba
1977- Simba
1978- Simba
1979- Simba
1980- Simba
1981- Yanga
1982- Pan Africans
1983- Yanga
1984- Simba
1985- Yanga
1986- Tukuyu Stars
1987- Yanga
1988- Coastal Union
1989- Yanga
1990- Simba
1991- Yanga
1992- Yanga
1993- Yanga
1994- Simba
1995- Simba
1996- Yanga
1997- Yanga
1998- Yanga
1999- Mtibwa Sugar
2000- Mtibwa Sugar
2001- Simba
2002- Yanga
2003- Simba
2004- Simba
2005- Yanga
2006- Yanga
2007- Simba
2007/08- Yanga
2000/09- Yanga
2009/10- Simba
2010/11- Yanga
2011/12- Simba
2012/13- Yanga
2013/14- Azam
2014/15- Yanga
2015/16   ???

Vinara
25-Yanga
18-Simba
2-Mtibwa
1-Cosmo, Mseto, Pan, Tukuyu, Coastal, Azam

Saturday, August 22, 2015

Nafasi nyingine kwa Manchester Utd EPL


http://strettynews.com/wp-content/uploads/2015/02/UnitedvPreston.jpg
Mashetani Wekundu ambao wamekuja kivingine msimu huu
Chelsea
Watetezi Chelsea wanaopepesuka
KIVUMBI cha Ligi Kuu England kinaendelea leo kwa michezo kadhaa, lakini mapema saa 8;30 mchana Mashetani Wekundu watakuwa wakisaka nafasi ya kurejea kileleni japo kwa sasa kadhaa wakati watakapovaana na vibonde Newcastle United kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Manchester United yenye pointi sita inaweza kuiengua Man City ambayo yenye itacheza kesho dhidi ya Everton kwa kufikisha pointi 9 kama itashinda huku ikiombea Leicester City ipoteze mchezo wake wa leo dhidi ya Tottenham Hotspur.
Ratiba kamili ya ligi hiyo kwa leo, kesho Jumapili na Jumatatu ambapo Arsenal itakuwa na kibarua kigumu cha kuibakaribisha Liverpool ipo hapo chini jionee mwenyewe;
Leo Jumamosi:
Manchester United     11 : 45    Newcastle United        
Crystal Palace     14 : 00    Aston Villa        
West Ham United     14 : 00    AFC Bournemouth        
Norwich City     14 : 00    Stoke City        
Sunderland     14 : 00    Swansea City        
Leicester City     14 : 00    Tottenham Hotspur        
Kesho Jumapili
West Bromwich Albion 12 : 30    Chelsea        
Everton     15 : 00    Manchester City        
Watford     15 : 00    Southampton        
Jumatatu
Arsenal     19 : 00    Liverpool

PATACHIMBIKA TAIFA, YANGA v AZAM NI SHEEDA!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjpjkGwXmOK250PzIJkj4gA7pkZ1mMpkKFXP2MG3mX3y_l3IHb7aHldzJdHcS2u-VTXyZldrrwgZtbd-yV0ndewKQDYjerOJ3aSNEVPxtJHCgeoHY8UgogGyJ-jYXVUU7COyj83XDERC6g/s1600/IMG_8065.JPG
Azam FC
Yanga
MABINGWA wa soka wa Tanzania, Yanga pamoja na Mabingwa wa Kombe la Kagame, Azam jioni ya leo wanatarajia kuonyeshana undava wakati zitakapokutana kwenye mchezo wa Ngao ya Hisani.
Mchezo huo maalum kwa ajili ya kuzindua msimu mpya wa Ligi kuu ya Tanzania Bara utapigwa dimba la Taifa, huku timu zote zikitarajiwa kuwakosa baadhi ya nyota wake kutokana na matatizo mbalimbali.
Yanga ambao imeonyesha kuupania mchezo huo hasa baada ya kutolewa nishai na Azma kwenye robo fainali ya Kombe la Kagame, huenda isiwe na Amissi Tambwe aliyekuwa akisumbuliwa na Malaria, japo Donald Ngoma anaweza kucheza akitoka kuuguza maumivu ya nyonga.
Azam wenyewe wanaosaka ushindi wa kwanza wa mchezo huo wa Ngao ya Hisani na pia kujaribu kufuta uteja kwa wapinzani kila wakikitana kwenye pambano hilo inaweza kumkosa Kipre Tchetche.
Hata hivyo vikosi vyote chini ya makocha wao, Stewart Hall kwa Azam na Hans van Pluijm wa Yanga wamenukuliwa wakitamba kuwa leo itakuwa kazi tu, na kuzipa matumiani timu yao kushinda.
"Yanga ni wazuri na ni timu kubwa na unapocheza nao ni kama ina wachezaji 12 kutokana na mashabiki wanaoiunga mkono, lakini tupo tayari na vijana wanagu wana ari ya kushinda," alisema.
Pluijm alisema kuwa ameandaa vijana wake kwa ajili ya kazi moja ya kushinda Taifa, hasa baaada ya kuridhishwa na mabadiliko aliyoyaona kwa safu yake ya mbele wakiwa jijini Mbeya kwenye kambi.
Bila ya shaka mashabiki wa soka watapata uhondo katika mchezo huo utakaochezeshwa na mwamuzi Martin Saanya baada ya refa wa awali, Israel Nkongo kupatwa na dharura ya kuugua na kuenguliwa.
Rekodi Azam Ngao ya Hisani:
2012: Simba 3-2 Azam
2013 Azam 0-1 Yanga
2014: Yanga 3-0 Azam
2015: Azam v Yanga???

Friday, August 21, 2015

3 zachemsha usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2015-2016

Stand United
Toto Africans
WAKATI dirisha la usajili kwa klabu vya Ligi Kuu nchini (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) likifungwa juzi klabu tatu za VPL vimeshindwa kuwasilisha usajili wao wa wachezaji katika muda uliopangwa.
 Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) alivitaja Klabu za Coastal Union ya Tanga, Stand United ya Shinyanga na Toto African ya jijini Mwanza kuwa zimeshindwa kuwasilisha usajili wao na kusema faini ni 500,000  kwa mchezaji mmoja hivyo klabu iliyochelewesha usajili au itakayobadili majina au kuongeza majina baada ya usajili kufungwa italazimika kulipia faini
“Usajili umefungwa jana (juzi) na timu tatu hazijawasilisha usajili wao hata wa mchezaji mmoja pamoja na TFF kuongeza muda wa usajili kwa wiki mbili”, alisema Kizunguto
Pia alisema si kwamba timu zingine zimefikisha idadi ya wachezaji wote kulingana na kanuni bali zingine zimesajili wachezaji 18, 24 hivyo hata wao endapo wataongeza watalipia faini.
Kizuguto alikumbusha timu ambazo zimesajili wachezaji wa kigeni kuwasilisha ada zao ili waweze kupata kbali cha kucheza ligi.
Awali TFF ilitoa muda wa wiki mbili kwa vilabu vyote nchini kukamilisha usajili, ambapo vilabu 13 vya ligi kuu vimeweza kukamilisha ndani ya wakati, klabu 24 vya ligi daraja la kwanza, klabu 24 ligi daraja la pili pia vimeweza kukamilisha usajili wao ndani ya muda uliopangwa.


Mkwasa ataja majembe yake ya Uturuki, Dida aachwa

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/06/Mkwasa-Stars.jpg
Kocha Mkwasa (kushoto) na Msaidizi wake, Hemed Morocco
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wachezaji 22 atakaoondoka nao kuelekea Uturuki kupiga kambi ya kuiwinda Nigeria.
Wachezaji hao 22 wanatarajiwa kuondoka nchini Jumapili  usiku kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria utakaochezwa Septemba 05, 2015. Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto, alisema kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa ametoa orodha ya wachezaji 22 watakaosafiri usiku wa jumapili. “Orodha ya wachezaji 22 imetoka katika kikosi kilichotangazwa wiki mbili zilizopita na Mkwasa ambapo walipata nafasi ya kufanya mazoezi kwa takribani wiki moja katika uwanja wa Karume”, alisema Kizuguto. Kizuguto alisema wachezaji wote waliochaguliwa kujiunga na timu ya Taifa wanapaswa kuripoti kambini Tansoma Hotel Jumapili saa 5 asubuhi kwa maandalizi ya mwisho ya safari hiyo. Wachezaji waliochaguliwa ni All Mustafa Aishi Manula, Said Mohamed, walinzi Shomari Kapombe, Abdi Banda, Mohamed Hussein, Hassan Isihaka, Juma Abdul, Haji Mngwali, Kelvin Yondani, Nadir Haroub. Wengine ni Mudathir Yahya, Himid Mao, Frank Domayo, Salum Telela, Deus Kaseke, Said Ndemla, John Bocco, Farid Musa, , Rashid Mandawa, Saimon Msuva, na Ibrahim Ajib. Taifa Stars kwa usafiri wa shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines), na itafika jijini Istambul jumatatu asubuhi, ambapo itaelekea katika mji wa Kocael   kuweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Green Park Kartepe.

Man United wakatwa maini kwa Sadio Mane

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/05/16/16/28BDB01200000578-3084365-Southampton_s_Sadio_Mane_celebrates_the_first_of_the_first_half_-a-3_1431789411065.jpgKLABU ya Southampton imekiri kuwa Manchester United wanamuwania winga wao wa kimataifa wa Senegal Sadio Mane, lakini ikatamka wazi kwamba mkali huyo hauzwi ng'o.
Wiki iliyopita Southampton walikanusha taarifa za kupokea ofa yeyote kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23. Mshambuliaji wa Barcelona Pedro amekuwa akihisiwa kujiunga na United lakini kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za kijiunga na Chelsea kwa dau la pauni milioni 21. 
Kutokana na hali hiyo United wameamua kuongeza nguvu zao katika kumsajili Mane kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi. Mane amefunga mabao 10 katika mechi 32 alizocheza msimu uliopita baada ya kujiunga na klabu yake ya sasa akitokea Red Bull Salzburg ya Austria na yumo pia katika orodha ya wachezaji waliowahi kufunga magoli matatu -hat-trick kwa muda mfupi zaidi.
Hata hivyo mapema leo Ijumaa klabu hiyo ya Southampton imeweka bayana kwamba mchezaji huyo hauzwi hivyo Man United watafute pengine pa kupata mchezaji mpya.
Meneja wa The Saints, Ronald Koeman amefunguka kuwa mchezaji huyo hauzwi kwa bei yoyote.

Straika Msenegal atua Msimbazi, amtia tumbo joto Kiiza

Niang mwenye kofia akiwasili
Niang akipokea simu mara baada ya kuwasili kwenye hoteli aliyofikia jijini Dar es Salaam
Akiwaskiliana alipowasilia hotelin
KLABU ya Simba imezidi kujiimarisha baada ya mchana huu kumpokea straika kutoka Senegal, Papa Niang, ambaye anatarajiwa kupimwa Jumatatu wakati Simba ikiumana na Mwadui Shinyanga kabla ya kusainishwa mkataba wa kukipiga Msimbazi.
Niang ambaye ni mdogo wa nyota Mamadou Niang, mshambuliaji ambaye itachukua muda Watanzania kumsahau baada ya kuizamisha Taifa Stars kwa mabao 4 ametua akiambatana na meneja wake, Massouka Ekoko.
Ujio wa straika hutyo aliyekuwa akicheza soka la kulipwa El Salvador kunamaanisha kuwa kama mipango itaenda sawa basi kuna uwezakano wa dili la Mrundi Kevin Ndatisenga aliyeifungia Simba moja ya mabao mawili wakati wakiiua URA ya Uganda likafa.
Pia hata kibarua cha Hamis Kiiza 'Diego' ambaye ameanza kuwekewa zengwe huenda nacho kikaota nyasi, ili kutimiza idadi ya wachezaji saba wa kimataifa wanaohitajiwa na timu hiyo.
Mpaka sasa ina wachezaji sita wa kigeni ambao ni Justice Majabvi, Emiry Nibomana, Hamis Kiiza, Juuko Murshid na Simon Sserunkuma, huku pia ikiwa imetoa kwa mkopo Raphael Kiongera aliyepo KCB ya Kenya.
Wakati Niang akitua leo zipo taarifa kutoka Msimbazi kwamba straika mwingine mkali atatua siku yoyote kuanzia leo kumaliza na mabosi wa Simba, ikiwa ni mikakati ya kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa misimu mitatu hakijaonja ladha ya ubingwa wa Tanzania Bara.

Dondoo kuhusu Niang
Jina kamili: Papa Niang
Tarehe ya kuzaliwa: 5 Disemba, 1988 (miaka 26)
Mahali alipozaliwa: Matam Senegal
Urefu: Mita 1.81 
Nafasi anayocheza: Mshambuliaji
Klabu alizowahi kuzitumikia:
Kwasasa: Mchezaji huru
2005-2006: ASC Thies 
2007: FC OPA
2008: AC Oulu
2009-2012: FF Jaro
2013: FC Vostok
2013-2014: Al -Shabab SC
2014-2015: FC Mounana

Wednesday, August 19, 2015

Kocha Man City aanza kuchonga mapema

http://s.ndtvimg.com/images/content/2015/aug/806/pellegrini-smile-man-city-chelsea-win.jpgUSHINDI una raha bhana we acha tu!, Meneja wa vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester City, Manuel Pellegrini ameanza kuchonga baada ya chama lake kupata ushindi katika mechi mbili mfululizo.
Kocha huyo ambaye ameiongoza Man City kuitoa nishai mabingwa watetezi, Chelsea, wikiendi iliyopita amesema wachezaji wake wana njaa na kiu baada ya kulikosa taji la Ligi Kuu msimu uliopita. 
City walimaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya mabingwa Chelsea wakitofautiana kwa alama nane. 
Akihojiwa mara baada ya kikosi chake kuichapa Chelsea kwa mabao 3-0 jana, Pellegrini amesema pengine kilichotokea msimu uliopita kilikuwa ni uzoefu tosha kwao. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji wake hivi sasa wana njaa na kiu ndio maana wanataka kushinda katika kila mchezo. 
Mabao ya City katika mchezo huo yalifungwa na Sergio Aguero, nahodha Vincent Kompany na Fernandinho.
Kikosi hicho kinatarajiwa kushuka dimbani wikiendi hii ugenini kuvaana na Everton siku ya Jumapili.

Hii ni zaidi ya bao! Chelsea yaizidi ujanja Man United kwa Pedro

http://unitednews.club/wp-content/uploads/2015/07/pedro-rodriguez-barcelona-cordoba-liga-bbva-12202014_nkvqt53jxhxb1dqfil0bns4ci.jpgHII huenda ni taarifa isiyopendwa kusikika masikioni mwa mashabiki wa Chelsea, Vyombo vya Habari nchini Hispania vimetoa taarifa kuwa klabu ya Chelsea imefanikiwa kuizidi maarifa mahasimu wao Manchester United katika usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania Pedro Rodriguez kutoka Barcelona. 
Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na gazeti la Marca, zimedai kuwa taratibu zote za Pedro kujiunga na Chelsea zimeshakamilika baada ya klabu hizo kuafikiana uhamisho wa Euro Mil. 28, huku kukiwa na nyongeza ya Euro Mil. 2 itakayolipwa baadaye. Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa Pedro tayari ameshatua jijini London kufanyiwa vipimo vya Afya baada ya kupewa ruhusa na Barcelona. Mashetani Wekundu, Man United ilikuwa wakitajwa kwa wiki kadhaa kumuwania mshambuliaji huyo kwa kutoa ofa ya Euro milioni 25.

Beki Mtogo apewa namba ya 'gundu' Jangwani

BEKI mpya wa Yanga kutoka Togo, Vincent Bossou ameichagua jezi yenye namba inayodaiwa kuwa na 'gundu' klabuni hapo, iliyowahi kumtesa mapro wengine waliowahi kuichezea timu hiyo hivi karibuni.
Mastraika Gelinson Santos 'Jaja' kutoka Brazil na Kpah Sherman wa Liberia waliwahi kuivaa jezi namba 9 na kupata wakati mgumu Jangwani, kiasi Mliberia kutaka maombi ya kichungaji kurejesha makali.
Hata hivyo Bossou ambaye alianza kuichezea Yanga juzi Jumapili katika pambano lao dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya amesisitiza jezi hiyo namba 9 ndiyo chaguo lake.
"Napenda kuvaa jezi namba tisa, popote ninapoenda kucheza hupenda kuitumia hjata kwenye timu ya taifa, licha ya kwamba mimi ni beki, navaa jezi yenye namba hiyo na hapa Yanga vivyo hivyo," Beki huyo alinukuliwa, huku akiwataka Wanayanga kumpa muda kuzoea mazingira na kuwapa burudani.
Kauli ya Bossou ilikuja baada ya kutokung'ara vema katika pambano hilo la Mbeya ambalo Yanga ilishinda mabao 3-2, huku dakika 45 alizocheza akishirikiana na Kelvin Yondani kabla ya kutolewa kipindi cha pili Yanga ilikuwa mbele kwa mabao 2-1.
Jaja alishindwa kung'ara Yanga na jezi namba 9 na kutimuliwa baada ya mechi chache tu, huku Sherman alihenyeka na namba hiyo mpaka kuhitaji maombi kabla ya kutulia na kufanya yake akimaliza msimu uliopita na mabao manne na katika Kombe la Kagame alivalia jezi namba 10 iliyokuwa ikitumiwa na Jerry Tegete.
Kwa sasa Mliberia huyo yupo Afrika Kusini akicheza soka la kulipwa baada ya kuuzwa hivi karibuni.

Hassan Dalali ajivunia rekodi yake Msimbazi

Mwenyekiti wa zamani wa Simba, Hassan Dalali
Hassan Dalali akisalimiana na wachezaji wa Bongo Movie siku ya Simba day
MWENYEKITI wa zamani wa Simba, Hassan Dalali amesema yapo mambo matano ambayo anajivunia kuiongoza klabu hiyo na jambo moja linamtia simanzi mpaka sasa kwa kuona hakufanikiwa kutekeleza.
Akizungumza na MICHARAZO, Dalali aliyataja mambo anayojivunia kwa kuiongoza Simba kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2008-2010 ni kuanzisha Simba Day mwaka 2009 ambayo inaendelezwa mpaka sasa na viongozi waliomfuata.
"Kuipatia Simba kiwanja kule Bunju ni suala jingine, kuwaunganisha wanachama wote wa Simba na kuongea idadi yao ni mambo mengine yanayonipa faraja," anasema.
Mwenyekiti huyo ambaye kwa sasa amejikita zaidi kwenye masuala ya kisiasa akiwa Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Kinondoni na Mjumbe wa Kamati ya Siasa wa Wilaya ya Kinondoni alisema kubwa la kujivunia ni kuiwezesha Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu bila kufungwa hata mchezo mmoja msimu wa 2009-2010.
"Hili linanifanya nitembee kifua mbele na kujivunia, kuifanya Simba isifunguke, tukishinda mechi 18 kati ya 20 na mbili tukitoka sare, Azam walijitahidi msimu wa 2013-2014, lakini hawakufikia rekodi kwani walishinda mechi 18 na kutoka sare 8, japo tulitofautiana idadi ya michezo, wao walicheza mechi 26 sisi 22," alisema Dalali.
Kuhusu linalomtia simanzi ni kitendo cha kushindwa kufanikisha ujenzi wa uwanja wa klabu hiyo, na kitendo cha viongozi wenzake kushindwa kuuendeleza ingawa alimfagilia Ismail Aden Rage kwa kuweza kupunguza deni lililokuwapo kujimilikisha kiwanja hicho.
"Naamini kwa namna mimi na Mwina Kaduguda tulipokuwa tumefikia, hivi sasa Simba ingekuwa na eneo la kujivunia la kufanyia mazoezi yao kwa kujinafasi kwani tulikuwa tumeingia mkataba na kampuni ya kuuza jezi ya Marekani, ambapo hata hivyo ilisitisha."
"Ila naamini Simba itakuja kuwa na Uwanja wake na kama nitakufa basi wanachama wa Simba watanikumbuka kwa mambo hayo,  ya kiwanja na tamasha la Simba Day," alisema Dalali.

RATIBA KAMILI YA LIGI KUU MSIMU WA 2015-2016 HII HAPA


Mabingwa watetezi Yanga

Azam
Simba
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) imeachia hadharani ratiba ya Ligi Kuu msimu wa 2015-2016, ikionyesha mabingwa watetezi wataanzia nyumbani katika mechi tano kaba ya kutoka kwenda Morogoro kuumana na Mtibwa Sugar.
Watetezi hao watavaana na watani zao, Simba Septemba 26, lakini ikianza mechi zake nyingi nyumbani huku wakitaabika kwa kumaliza mechi zao za mwisho mfululizo ikiwa ugenini.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ligi itaanza Septemba 12 na kumalizika Mei 7, huku pia kukiwa na michuano ya Kombe la FA ambalo limerejeshwa upya baada ya miaka mingi ya ukimya.
MICHARAZO imekuweka ratiba nzima ya Ligi hiyo kwa msimu huu ili kujua nani na nani wataanzia wapi na ligi;

Sept 12, 2015
Ndanda vs Mgambo JKT
African Sports vs Simba
Majimaji vs JKT Ruvu
Azam vs Prisons
Stand Utd vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Mwadui Fc
Mbeya City vs Kagera Sugar
 

Sept 13, 2015
Yanga vs Coastal Union
 

Sept 16, 2015
Yanga vs Prisons
Mgambo JKT vs Simba
Majimaji  vs Kagera Sugar
Mbeya City vs JKT Ruvu
Stand Utd  vs Azam
Toto Africans vs Mtibwa Sugar
Ndanda vs Coastal Union
 

Sept 17, 2015
Mwadui FC vs African Sports
 

Sept 19, 2015
Stand Utd vs  Africans Sports
Mgambo JKT vs Majimaji
Prisons vs Mbeya City
Yanga  vs JKT Ruvu
 

Sept 20, 2015
Mwadui Fc vs Azam
Mtibwa Sugar vs  Ndanda
Simba vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Toto Africans
 

Sept 26, 2015
Simba vs Yanga
Coastal Union vs Mwadui Fc
Prisons  vs Mgambo JKT
JKT Ruvu vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Majimaji
Kagera Sugar vs Toto Africans
 

Sept 27, 2015
African Sports vs Ndanda
Azam vs Mbeya City
 

Sept 30, 2015
Simba vs Stand Utd
Azam vs Coastal Union
Mtibwa Sugar vs Yanga
Ndanda vs Majimaji
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
African Sports vs Mgambo JKT
Prisons vs Mwadui FC
 

Okt 01, 2015
Toto Africans vs Mbeya City


Okt 03, 2015
Mgambo JKT vs  Coasta Union
Majimaji vs Mwadui Fc
Toto Africans vs JKT Ruvu
Okt 04, 2015Stand Utd vs Mbeya City
Kagera Sugar vs Prisons
Azam vs Mtibwa Sugar
Ndanda vs Simba
African Sports vs Yanga
 

Okt 5-13, 2015
Afcon 2017QFL/Kirafiki/WC 2018 QFL
 

Okt 17, 2015                                            Yanga vs Azam
Majimaji vs African Sports
Mbeya City vs Simba
Ndanda vs Toto Africans
Stand Utd vs Prisons
Coastal Union vs Mtibwa Sugar
 

Okt 18, 2015Mgambo JKT vs Kagera Sugar
Mwadui vs JKT Ruvu
 

Kagera Sugar
Okt 21, 2015Yanga vs Toto Africans
Stand Utd vs Majimaji
JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar
Prisons vs Simba
Coastal Union vs Kagera Sugar

 
Okt 22, 2015Mwadui vs Mgambo JKT
Mbeya City vs African Sports
Ndanda vs Azam
Okt 25, 2016

Uchaguzi Mkuu wa Taifa                                 
Okt 28, 2015                                            Toto Africans vs Mgambo JKT
Mwadui vs Yanga
Mtibwa Sugar vs  Kagera Sugar
Mbeya City vs Majimaji
Ndanda vs Stand Utd
Simba vs Coastal Union
 

Sept 29, 2015JKT Ruvu vs Azam
Prisons vs African Sports
 

Okt 31,2015Simba vs Majimaji
Kagera Sugar vs Yanga
Mtibwa Sugar vs Mwadui
Prisons vs Ndanda
Coastal Union vs Mbeya City
 

Nov 01, 2015African Sports vs JKT Ruvu
Azam vs Toto Africans
 

Nov 02, 2015
Mgambo JKT vs Stand Utd
 

Nov 07, 2015Mgambo JKT vs Yanga
Kagera Sugar vs Ndanda
Stand Utd vs Mwadui
Mbeya City vs Mtibwa Sugar
Azam vs Simba
Majimaji vs Toto Africans
 

Nov 08, 2015JKT Ruvu vs Prisons
Coastal Union vs African Sports
Nov 9-17, 2015
Kirafiki/ WC 2018 QFL/Challenge/Mini Window (Nov 15-Dec 15)/ Nani Mtani Jembe (Dec 12)
 

Mtibwa Sugar
Dec 19, 2015Yanga vs  Stand Utd
Mwadui vs Ndanda
Kagera Sugar vs African Sports
Prisons vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Simba
Majimaji vs Azam

 
Dec 20, 2015JKT Ruvu vs Coastal Union
Mbeya City vs Mgambo JKT
 

Dec 26, 2015Ndanda vs JKT Ruvu
Yanga vs Mbeya City
Majimaji vs Prisons
Mwadui vs Simba
Mtibwa Sugar vs  Mgambo JKT
Coastal Union vs Stand Utd
 

Dec 27, 2015Azam vs Kagera Sugar
Toto Africans vs African Sports
Jan 01-13, 2016
Mapinduzi Cup                                           
 

Jan 16, 2016JKT Ruvu vs Mgambo JKT
Toto Africans vs Prisons
Simba vs Mtibwa Sugar
Stand Utd vs Kagera Sugar
Mbeya City vs Mwadui
Coastal Union vs Majimaji
Azam vs  African Sports
 

Jan 17, 2016Yanga vs Ndanda
 

Jan 20, 2015Ndanda vs Mbeya City
Prisons vs Coastal Union
JKT Ruvu vs Simba
Stand Utd vs Toto Africans
Mgambo JKT vs Azam
 

Jan 21, 2016Mwadui vs Kagera Sugar
African Sports vs Mtibwa Sugar
Yanga vs Majimaji
 

Jan 23-24
FA CUP
 

Jan 30, 2016    Coastal Union vs Yanga
Simba vs African Sports
JKT Ruvu vs Majimaji
Prisons vs Azam
Mtibwa Sugar vs Stand Utd
Mwadui vs Toto Africans
Kagera Sugar vs Mbeya City
 

Jan 31, 2016Mgambo JKT vs Ndanda
 

Feb 03, 2016                                            Prisons vs Yanga
Simba vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs  Majimaji
JKT Ruvu vs Mbeya City
African Sports vs     Mwadui
Mtibwa Sugar vs Toto Africans
Azam vs Stand Utd
 

Feb 04, 2016Coastal Union vs Ndanda

Feb 06, 2016Kagera Sugar vs  Simba
Mbeya City vs  Prisons
JKT Ruvu vs Yanga
African Sports vs Stand Utd
Ndanda vs Mtibwa Sugar
 

Feb 07, 2016Azam vs Mwadui
Toto Africans vs  Coastal Union
Majimaji vs Mgambo JKT
Feb 12-14, 2016 CAF-CC&CL 

Feb 13, 2016Stand Utd vs Simba
Mgambo JKT vs African Sports
Yanga vs Mtibwa Sugar
Mbeya City vs Toto Africans
Ndanda vs Majimaji
JKT Ruvu vs Kagera Sugar
Mwadui vs Prisons
Coastal Union vs azam
 

Feb 20, 2016Yanga vs Simba
Mgambo JKT vs Prisons
Stand Utd vs JKT Ruvu
Mbeya City vs Azam
Majimaji vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Kagera Sugar
Feb 21, 2016Ndanda vs  African Sports
Mwadui vs Coastal Union
 

Feb 26-28, 2016 CAF-CC& CL
 

Mar 05, 2016Azam vs Yanga
African Sports vs Majimaji
Toto Africans vs Ndanda
Kagera Sugar vs Mgambo JKT
JKT Ruvu vs Mwadui
Prisons vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Coastal Union
 

Mar 06, 2016Simba vs Mbeya City
Yanga vs African Sports
Mtibwa Sugar vs Azam
 

Mar 09, 2016Prisons vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Mgambo JKT
Mwadui vs Majimaji
JKT Ruvu vs Toto Africans
 

Mar 10, 2016Simba vs Ndanda
Mbeya City vs  Stand Utd
Mar 11-13, 2016 CAF-CC&CLToto vs Yanga
Azam vs  Ndanda
 

Mar 12, 2016African Sports vs Mbeya City
Mtibwa Sugar vs JKT Ruvu
 

Mar 13, 2016Majimaji vs Stand Utd
Kagera Sugar vs  Coastal Union
Simba vs Prisons
Mgambo JKT vs Mwadui 

Mar 18-20, 2016 CAF-CC&CL                               
 

Mar 19, 2016                                    Coastal Union vs Simba
Yanga vs Mwadui
Azam vs JKT Ruvu
Kagera Sugar vs Mtibwa Sugar
Majimaji vs Mbeya City
Stand Utd vs Ndanda
 

Mar 20, 2016African Sports vs Prisons
 

Mar 21, 2016Mgambo JKT vs Toto Africas
 

Mar 21-29, 2016 Kirafiki/FA Cup
 

Apr 02, 2016Majimaji vs Simba
Yanga vs Kagera Sugar
Toto Africans vs Azam
Stand Utd vs Mgambo JKT
Ndanda vs Prisons
Mbeya City vs Coastal Union
 

Apr 03, 2016JKT Ruvu vs African Sports
Mwadui vs Mtibwa Sugar
 

Apr 08-10, 2016 CAF-CC&CLStand Utd vs Yanga
 

Apr 09, 2016Ndanda vs Mwadui                                   
African Sports vs Kagera Sugar
Mtibwa Sugar vs Prisons
Azam vs Majimaji
 

Apr 10, 2016Coastal Union vs JKT Ruvu
 

Apr 11, 2016Mgambo JKT vs Mbeya City
 

Apr 16, 2016Simba vs Azam
Ndanda vs Kagera Sugar
African Sports vs Coastal Union
Mwadui vs Stand Utd
Mtibwa Sugar vs Mbeya City
Prisons vs JKT Ruvu
Toto Africans vs Majimaji
 

Apr 17, 2016Yanga vs Mgambo JKT
 

Apr 18-20, 2016 CAF-CC&CL
 

Apr 23-24, 2016 FA Cup                                           
Apr 26, 2016JKT Ruvu vs Ndanda
 

Apr 27, 2016Mbeya City vs Yanga
Kagera Sugar vs Azama
Simba vs Mwadui
Stand Utd vs Coastal Union
African Sports vs Toto Africans
 

Apr 28, 2016Prisons vs Majimaji
Mgambo JKT vs Mtibwa Sugar
 

Apr 30, 2016Mtibwa Sugar vs Simba
Mgambo JKT vs JKT Ruvu
 

Mei 01, 2016Ndanda vs Yanga
Kagera Sugar vs Stand Utd
Mwadui vs Mbeya City
Majimaji vs Coastal Union
African Sports vs Azam
Prisons vs Toto Africans
 

Mei 07, 2016                            Mbeya City vs Ndanda
Coastal Union vs  Prisons
Simba vs JKT Ruvu
Toto Africans vs Stand Utd
Azam vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs Mwadui
Mtibwa Sugar vs African Sports
Majimaji vs Yanga
 

Mei 14, 2016 FA Cup