STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 19, 2015

Hii ni zaidi ya bao! Chelsea yaizidi ujanja Man United kwa Pedro

http://unitednews.club/wp-content/uploads/2015/07/pedro-rodriguez-barcelona-cordoba-liga-bbva-12202014_nkvqt53jxhxb1dqfil0bns4ci.jpgHII huenda ni taarifa isiyopendwa kusikika masikioni mwa mashabiki wa Chelsea, Vyombo vya Habari nchini Hispania vimetoa taarifa kuwa klabu ya Chelsea imefanikiwa kuizidi maarifa mahasimu wao Manchester United katika usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania Pedro Rodriguez kutoka Barcelona. 
Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na gazeti la Marca, zimedai kuwa taratibu zote za Pedro kujiunga na Chelsea zimeshakamilika baada ya klabu hizo kuafikiana uhamisho wa Euro Mil. 28, huku kukiwa na nyongeza ya Euro Mil. 2 itakayolipwa baadaye. Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa Pedro tayari ameshatua jijini London kufanyiwa vipimo vya Afya baada ya kupewa ruhusa na Barcelona. Mashetani Wekundu, Man United ilikuwa wakitajwa kwa wiki kadhaa kumuwania mshambuliaji huyo kwa kutoa ofa ya Euro milioni 25.

No comments:

Post a Comment