STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 16, 2013

Beckham astaafu soka, Lampard akomaa Chelsea

David Beckham

Frank Lampard akiwa na taji la Europa ililotwaa Chelsea usiku wa jana
WAKATI nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya England, David Beckham akitangaza kustaafu rasmi soka siku chache baada ya kufanikiwa kuiwezesha PSG kunyakua taji la Ligue 1 baada ya miaka 19 mwishoni mwa wiki, kiungo nyota wa Chelsea, Frank Lampard yeye ameongeza mkataba mpya na klabu yake hiyo.
Beckham amenukuliwa kuwa atatundika rasmi daluga zake mara baada ya pambano la kufungia msimu la timu yake hiyo aliyoichezea kwa mkataba wa mwaka mmoja, itakaposhuka dimbani Mei 26.
Mkali huyo aliyewahi kutamba na timu kadhaa kama Manchester United, Real Madrid na LA Galaxy ambako kote huko alkiweza kunyakua matji ya ligi ya nchi hizo.
Kustaafu kwa Beckham aliyeichezea timu ya taifa jumla ya mechi 115 na kuifungia mabao 17, ameishukuru klabu ya PSG kwa kumpa nafasi ya kujiunga nayo na kusema kuwa anadhani ni muda muafaka wa yeye kupumzika baada ya kucheza soka kwa kiwango cha juu.
Nyota huyo aliyekuwa mahiri kwa mipira ya faulo, amemshukuru kocha Carlo Ancelloti na wana PSG kwa ujumla kwa muda aliokuwa nao na kuisaidia timu hiyo kufika ilipofikia kwa kunyakua taji hilo la Ligi ya Ufaransa.
Wakati Beckham akitangaza kung'atuka akimfuata aliyekuwa kocha wake wakati akiichezea Manchester United, kiungo mwingine mkongwe wa England, Frank Lampard amesaini mkataba mwingine wa mwaka mmoja baada ya tetesi kwamba angeondoka klabu hapo kwenye kucheza Ligi Kuu ya Marekani (MSL).
Taarifa zilizotangaza jioni hii zinasema kuwa Lampard amesaini mkataba huo saa chache baada ya kuisaidia Chelsea kunyakua taji la Ligi Ndogo ya Ulaya na siku chache tangu aweke rekodi ya ufungaji mabao katika klabu hiyo ya 'Darajani'.
"Napenda kumshukuru Roman Abramovich kwa kunipa nafasi ya kuitumikia klabu ninayoipenda kwa dhati ya Chelsea, pia wachezaji wenzangu, maafisa wote wa timu hii na wote wanaoiunga mkono Chelsea kwa namna walivyonipokea na kuishi nami tangu nilipotua kwa mara ya kwanza," alinukulia Lampard.
Mkataba wa mchezaji huyo ulitarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimui na kulikuwa na taarifa kwamba alikuwa tayari kuondoka kuelekea Marekani kufuatiwa kuonyesha kutohitajiwa tangu alipotua timu ilipokuwa chini ya AVB anayeinoa Tottenham Hotspur kabla ya rafa Benitez kumpa nafasi na kuvunja rekodi ya ufungaji wa maboa klabu hapo mwishoni mwa wiki iliyopita.

Tiketi za Simba na Yanga kuanza kuuzwa kesho

Wakali wa Jangwani

Wakali wa Msimbazi
Na Boniface Wambura
TIKETI  kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Yanga litakalochezwa keshokutwa (Jumamosi) kwenye Uwanja wa Taifa zitaanza kuuzwa kesho (Ijumaa) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Vituo vitakavyouza tiketi hizo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live Mbagala na Sokoni Kariakoo.

Tiketi hizo zitakuwa zikiuzwa katika magari maalumu yaliyoegeshwa katika vituo hivyo. Viingilio katika mechi hiyo ya kufunga msimu ni sh. 5,000 kwa viti vya kijani, sh. 7,000 viti vya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 VIP B n ash. 30,000 kwa VIP A.


Kim Poulsen ataja silaha 26 za kuiangamiza Morocco

Kocha Kim Poulsen
Na Boniface Wambura
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Mei 16 mwaka huu) ametaja kikosi cha wachezaji 26 watakaoingia kambini kujiwinda kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.

Katika kikosi hicho, Kim ameita wachezaji wapya sita ingawa baadhi yao wamewahi kuchezea timu hiyo, huku akiacha wengine watatu aliokuwa nao kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Morocco ambapo Taifa Stars ilishinda mabao 3-1.

Wapya aliowaita katika kikosi hicho kitakachoingia kambini Mei 20 mwaka huu, saa 1 jioni kwenye hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam ni Ally Mustafa, Vicent Barnabas, Juma Luzio, Haruna Chanongo, Mudhathiri Yahya na Zahoro Pazi. Wachezaji aliowaacha ni Shabani Nditi, Nassoro Masoud Cholo na Issa Rashid.

Kikosi kamili cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ambacho kabla ya kwenda Morocco kitapita jijini Addis Ababa, Ethiopia kucheza mechi ya kirafiki Juni 2 mwaka huu dhidi ya Sudan ni kama ifuatavyo;

Makipa ni nahodha Juma Kaseja (Simba), Aishi Manula (Azam), Ally Mustafa (Yanga) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Shomari Kapombe (Simba), Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar) na Waziri Salum (Azam).

Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mudathiri Yahya (Azam) na Salum Abubakar (Azam).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Juma Luzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC) na Zahoro Pazi (JKT Ruvu).

Kocha Kim amesema kikosi kitakachoingia kambini kitakuwa na wachezaji 24 ambapo Samata na Ulimwengu watajiunga na timu jijini Marrakech, lakini wachezaji atakaondoka nao Dar es Salaam kwenda Addis Ababa ni 22 ambapo ataacha kipa mmoja na mchezaji mmoja wa ndani.

Awali TFF ilikuwa imeitafutia Taifa Stars mechi ya kirafiki Juni 1 mwaka huu dhidi ya Algeria, Libya au Misri. Lakini baadaye Algeria ikasema itacheza na Togo, wakati Misri ilitaka mechi hiyo ichezwe Juni 4 jijini Cairo, jambo ambalo lisingewezekana kwa Stars kwani ina mechi ya mashindano Juni 8 mwaka huu.

Kwa upande wa Libya mechi hiyo ilikubaliwa ichezwe Tunis, Tunisia, Juni 2 mwaka huu. Lakini baadaye Libya ikataka mechi hiyo ichezewe jijini Tripoli ambapo TFF ilikataa kutokana na sababu za kiusalama.

Hatimaye Stars yajiondoa michuano ya COSAFA

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah

Na Boniface Wambura
Tanzania (Taifa Stars) imejitoa kwenye michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika nchini Zambia kuanzia Julai 2-26 mwaka huu.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah amesema Stars ambayo iliingizwa katika michuano hiyo kama timu mwalikwa imejitoa kutokana na mwingiliano wa ratiba kati ya michuano hiyo na mechi za Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).

Amesema awali Tanzania ilithibitisha kushiriki michuano kwa matarajio kwamba Uganda ingekubali ombi la TFF la kubadilisha ratiba ya mechi za CHAN, lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Uganda (FUFA) likagoma kwa vile kipindi ambacho kilipendekezwa lenyewe litakuwa na uchaguzi wa viongozi wao.

Taifa Stars itacheza na Uganda (The Cranes) katika mechi za CHAN ambapo mechi ya kwanza itachezwa jijini Dar es Salaam kati ya Julai 12-14 mwaka huu wakati ya marudiano itafanyika jijini Kampala kati ya Julai 26-28 mwaka huu.

Akizungumzia michuano ya COSAFA, Kocha Kim amesema angependa kushiriki michuano hiyo kwani ingekuwa kipimo kizuri kwa kikosi chake, lakini kwa sasa malengo makubwa ya Stars kwenye mechi za mchujo za Kombe la Dunia na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ambayo fainali zake zitafanyika mwaka 2015.

IBF yamweka sokoni bondia Francis Cheka


Bondia Francis Cheka

The most celebrated “IBF Continental Africa Champion” Francis Cheka of Tanzania is shopping for an opponent outside Africa continent for his optional defense of his title for the fourth time. Cheka’s desire for foreign boxers derived from the dismal performances exhibited by Africa boxers he had met so far. “I have yet to see any African boxer who has challenged me aggressively” said the “IBF Continental Africa Super Middleweight King” recently.

Francis Cheka won the “IBF Continental Africa Super Welterweight Title” for the first time in 2005 and vacated it the following year to vie for other “less colorful titles” only to recapture it in 2011 and has since defended it successfully! He is the most celebrated boxer in Tanzania and the whole of East & Central African region.

His metaphor of the country’s name and status out pass that of many sportsmen and women before him as he has accumulated a lot of respects from various quarters within African boxing fraternity! This is one boxer who enjoys boxing and when he is the ring his body language connect with that of the spectators in the venue as they sing and cheers him throughout the fight punch after punch to victory!

Born in Dar Es Salaam and raised in Morogoro, Francis Boniface Cheka is a great boxing entrepreneur who know how to tilt the sport to his favor. He is so popular in Tanzania that youths emulate how he dress and walk. Francis Boniface Cheka is larger than life as far as boxing in Tanzania and East Africa is concern. He epitomizes glory and the success which come with the prize fighting!

Cheka's investments portfolio calls for admiration in that very few sportsmen/women in Tanzania have invested to so many enterprises without proper formal education!  He owns string of business enterprises springing from plastic recycling factories to environment management! He is the role model to many young people in Tanzania.

And now, he is shopping for a pound to pound boxer from outside Africa to march his boxing caliber saying that he is above the level of many opponents from the Dark Continent! If you happen to hear him speaking for the first time you would compare him with a professor lecturing students. He is so organized in his life as well as in the ring.
                                                                                                                                                            
Cheka is the only boxer who cannot take a fight if he is not well prepared not matter what the price can be. When preparing for a fight he secluded himself from all luxuries in the world including staying away from his beloved wife saying that sex and wine are the greatest destructions for sportsmen/women!

Joto la pambano la watani wa jadi lazidi kupanda


Kikosi cha Simba
Mabingwa Yanga wakiwa na taji lao la Kagame

JOTO la mechi ya wapinzani jadi baina ya Yanga na Simba lilizidi kupanda jana kwa miamba hao wa soka nchini kujikuta wakilumbana kwa kitu ambacho shirikisho la soka nchini (TFF) limesema ni uzushi mtupu.
Viongozi wa Simba, Yanga walihusika katika mijadala mizito huku mashabiki wakitoa maoni mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii kufuatia taarifa kwamba refa wa mechi hiyo alipaswa kuwa ni Israel Nkongo lakini TFF imembadilisha na kumweka Martin Saanya.
Ofisa habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kwamba shirikisho hilo halikuwahi kumtangaza mwamuzi wa mechi hiyo kabla ya kumtangaza Saanya.
"Hizo habari kwamba mwamuzi amebadilishwa zimetoka wapi? Tulikuwa hatujamtangaza refa wa mechi na tulipotangaza tumemtangaza Saanya kwa hiyo hamna refa aliyebadilishwa," alisema.
Uvumi wa kubadilishwa refa ulizua kauli mbalimbali za viongozi huku kiongozi mmoja wa Simba akidaiwa kusema kwamba hawataingiza timu uwanjani, jambo ambalo kwa mujibu wa kanuni litawashuhudia wakishushwa daraja.
Kanuni za ligi, hata hivyo, zinaruhusu mwamuzi kubadilishwa hadi saa nane kabla ya mechi.
Akizungumza jana Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage alisema "Simba itacheza dhidi ya Yanga hata kama TFF itabadili uwanja na kuipeleka kwenye Uwanja wa Kaunda" unaomilikiwa na Yanga, huku akisisitiza kwamba kubadili mwamuzi kunaipaka matope TFF kwani jambo hilo halipo katika nchi nyingine.  
Katibu Mkuu wa Lawrance Mwalusako alisema kuwa wao hawajali ni mwamuzi gani amepangwa kuchezesha mechi hiyo.
"Sisi hatuna tatizo katika hilo, TFF ndiyo wenye jukumu la kuamua mwamuzi gani achezeshe, Simba kulalamika ni dalili za mchecheto dhidi yetu," alisema.
Mwalusako alisema tishio la Simba ni dalili za wazi za kuanza mapema kutafuta visingizio baada ya kubaini kuwa kikosi chao hakina ubavu wa kuwahimili vijana wa Jangwani.
Bungeni Dodoma nako wabunge waliendeleza kuizungumzia mechi hiyo.
Mbunge wa Mufindi Kaskazini, Mahmoud Mgimwa (CCM), alisema ubingwa wa Yanga hautanoga iwapo timu hiyo haitaifunga Simba katika mechi ya marudiano keshokutwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
“Naipongeza Yanga kwa kutwaa ubingwa lakini nawaagiza viongozi wake kuwa bila kuifunga Simba ubingwa huo hautanoga,” alisema.
Mgimwa aliyasema hayo bungeni jana mara baada ya kusoma maoni ya Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara kuhusiana na hotuba ya bajeti ya Viwanda na Bishara kwa mwaka 2013/2014.
Alisema kwa kuifunga Simba, kutaboresha safari ya mtani wao ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Aden Rage (Mbunge wa Tabora Mjini-CCM).
Awali, mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha asubuhi cha maswali na majibu kilichokuwa kinaongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya Bunge, Mussa Zungu, aliipongeza Yanga kwa kuchukua ubingwa.
“Na humu ndani tupo wengi sana na nina fanya hivyo kwa kuwa mimi ni Mbunge wa Ilala ambaye Yanga ipo jimboni kwangu,” alisema.
Tangu Jumatatu wiki hii, kumekuwa na matambo kati ya wabunge wanaoziunga mkono timu hizo ndani ya Bunge mara wanapopata nafasi.
Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani, (CCM), ambaye ni shabiki wa Simba, alikaririwa na gazeti hili akiwataka wabunge wenzie kwenda katika eneo wanalofanyia vikao vyao la Msalato (nje kidogo ya Mji wa Dodoma), kupanga mikakati ya ushindi dhidi ya Yanga.
Simba iko Unguja na Yanga iko Pemba katika kambi za kujiandaa na mechi hiyo ya kukamilisha ratiba baada ya Yanga kuwa imeshatwaa ubingwa huku Simba ikiwa haiwezi kufuzu kucheza michuano ya Afrika.
 

Tanzania hatihati kwenda COSAFA


KOCHA wa timu ya soka ya taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen, amesema kwamba Tanzania iko katika hatihati ya kushiriki mashindano ya Ukanda wa Nchi za Kusini mwa Afrika (COSAFA) kama ilivyotarajiwa kutokana na ratiba ya michuano hiyo kuwa karibu na mechi ya kusaka nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN).
Tanzania imepangwa kucheza ugenini dhidi ya Uganda kati ya Juni 21 na 23 mwaka huu jijini Kampala na zitarudiana kati ya Julai 5 na 7 jijini Dar es Salam wakati na michuano ya COSAFA ambapo Taifa Stars ni timu mwalikwa mwaka huu itaanza Julai 2 hadi 16 huko Zambia. Inatarajia kuanza dhidi ya Shelisheli Julai 6.
Akizungumza na gazeti hili jana, Poulsen alisema kwamba Shirikisho la Soka Nchini (TFF) lilifanya mawasiliano na Chama cha Soka cha Uganda (FUFA) ili kusogeza mbele tarehe za mechi hiyo lakini wapinzani wao wameonyesha nia ya kukataa kufanya mabadiliko yoyote.
Alisema kwamba alikubali Stars ishiriki mashindano hayo mwaka huu ili kuiandaa na mechi hiyo dhidi ya Uganda Cranes, lakini inaonekana kwamba nafasi haitapatikana.
"Sidhani kama tunaweza kwenda kushiriki kama tulivyotarajia, nilitaka kutumia mashindano hayo kujiandaa na mechi za CHAN lakini Uganda hawataki kusogeza mbele au kufanya mabadiliko yoyote tofauti na tarehe zilizopangwa awali," alisema kocha huyo raia wa Denmark.
Aliongeza kwamba bado anaamini mazungumzo kati ya TFF na FUFA yanaweza kuzaa matunda na watakapofanikiwa itasaidia kuijenga Stars.
"Hatujakata tamaa, bado tunasubiri majibu ya Uganda, nitasikitika endapo tutakosa nafasi ya kushiriki mashindano ya COSAFA, ni muhimu kwa ajili ya kujenga timu kama ilivyokuwa mwaka juzi tulipopeleka wachezaji vijana," aliongeza kocha huyo.
Tanzania ilifuzu kushiriki fainali za CHAN za mwaka 2009 zilizofanyika Ivory Coast baada ya kuwaondoa Kenya na Uganda iliyokuwa chini ya Bobby Williamson.

Chanzo NIPASHE

Vijana Jazz 'Wana Saga Rhumba' wafufuka na 3 mpya

                Wanamuziki wa Vijana Jazz Band wakiwa mazoezi katika ukumbi wa Vijana Social

Wanamuziki wa Vijana Jazz Band wakiwa mazoezi katika ukumbi wa Vijana Social

BENDI ya muziki wa dansi iliyowahi kutamba zamani, Vijana Jazz 'Wana Saga Rhumba' imeanza kujipanga upya kwa kunyakua wanamuziki wapya na kufyatua nyimbo tatu mpya.
Nyimbo hizo ambazo mmoja umeshatolewa video yake ni pamoja na 'Wanawake Wanaweza' wenye video, 'Mtanieleza Nini' na 'Mwanangu Njoo Nikuusie'.'
Katibu wa bendi hiyo, Mgonahazeru, aliiambia MICHARAZO nyimbo hizo tatu zimetungwa na yeye, Saburi Athuman na muimbaji wao mpya waliyemnyakua toka Tango Stars, Julius Mwesiwe.
"Baada ya kupata vyombo vipya, Vijana Jazz tumeanza kujipanga upya kurejesha makali yetu kwa kuwanyakua wanamuziki wapya na kufyatua nyimbo tatu mpya ikiwemo wenye video," alisema.
Alisema nyimbo iliyotolewa video ni 'Wanawake Wanaweza' ambao ameutunga yeye, huku nyimbo zilizosalia zikiwa mbioni kufanyiwa hivyo huku wakijiandaa kuanza kufanya maonyesho.
Mgonahazeru alisema mbali na Mwesiwe, Vijana Jazz iliyowahi kutamba na nyimbo kadhaa kama Nimeruka Ukuta, Maria, Bujumbura, Shoga, Mpiga Debe na vingine pia imewanyakua wanamuziki wengine wawili.
Wanamuziki hao ni muimbaji wa zamani wa Mchinga Soudn, Roshy Mselela na Hussein Bomu aliyewaji kuwika na UDA Jazz.

BENITEZ AIPA CHELSEA TAJI LA EUROPA WAKITUNGUA BENFICA

On the continent: Chelsea added the Europa League to their Champions League success last year
Chelsea wakishangilia na taji lao usiku wa jana
Boss: Rafa Benitez smiles as he lifts the Europa League trophy in Amsterdam
Kocha Rafa Benitez akiwa ameshikilia taji hilo la Europa League

WHAM, BAM, THANK YOU BRAN ... Ivanovic wins it for Chelsea
Branslav Ivanovic akiifungia Chelsea bao la pili
KOCHA aliyekuwa kwenye shinikizo kubwa ndani ya klabu ya Chelsea, Rafa Benitez usiku wa kuamkia leo alionyesha ubora wake baada ya kuipa timu hiyo taji la Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europa League) baada ya kuwatungua Benfica ya Ureno kwa mabao 2-1 katika pambano la fainali lililochezwa  nchini Uholanzi.
Bao la dakika za ziada  la pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Amsterdam Arena, lilitumbukizwa kimiani kwa kichwa na beki kutoka Serbia Branslav  Ivanovic akiunganisha mpira wa kona iliyopigwa na Juan Mata.
Kabla ya bao hilo timu hizo zilijikuta zikimaliza dakika 45 za awali zikiwa nguvu sawa kwa kutofungana licha ya kwamba Benfica walionyesha soka la kuvutia wakiwakimbiza Chelsea kabla ya kujikuta kipindi cha pili wakianza kwa kutunguliwa bao kupitia Fernando Torres kuipangua ngome ya Benfica akiwamo kipa wao na kuutumbukiza wavuni katika dakika ya 60.
Hata hivyo dakika nane baadaye Benfica walirejesha bao hilo kwa mkwaju wa penati iliyopigwa kiufundi na nyota wa timu hiyo Oscar Cardozo na kuonyesha huenda mwechi hiyo ingeisha kwa sare ndani ya dakika 90 kabla ya Ivanovic kubadilisha matokeo dakika moja kabla ya dakika tatu za ziada kumalizika.
Hilo ni taji la pili kubwa kwa Chelsea kwa miaka miwili mfululizo, baada ya mwaka jana kutwaa taji la Ligi ya Ulaya ikiwa na kocha Roberto Di Matteo ambapo hata hivyo mwaka huu walishindwa kulitetea na kujikuta wakitupwa kwenye Europa na kufanya kweli kwa kulitwaa licha ya kocha Benitez kuwa na bahati mbaya ya kutokubalika tangu aliporithi nafasi ya Di Matteo.