STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 15, 2013

Familia ya Sheikh Ponda yalaani kutolewa kwa sheikh huyoi hospitalini akiendelea na matibabu kupelekwa Segerea

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda (wa pili kulia), ambaye kwa sasa anakabiliwa na tuhuma za uchochezi,  akitolewa katika taasisi ya mifupa MOI, kuelekea katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam majira ya asubuhi leo. (Na Mpiga Picha Wetu)

DAR ES SALAAM, Tanzania

Kwa upande wao familia ya Sheikh Ponda wamesema wanalaani kitendo kilichofanywa na serikali cha kumuondoa ndugu yao hospitalini huku akiwa anaendelea kupata matibabu.

Msemaji wa familia hiyo Is-haq Rashid, alisema kutokana na hali hiyo kama familia wanalirudisha suala la Sheikh Ponda kwa uongozi wa jumuiya na Taasisi za kiislamu kwa ajili ya hatua zaidi ya kuhakikisha kiongozi mwenzao anakuwa salama.

“Uporaji huu wa mgonjwa unazidi kutupa mashaka juu ya dhamira ya serikali hasa ikiwa tunalituhumu jeshi la polisi katika kumdhuru Sheikh,hatujui kwanini kila wakati wanafanya mambo yao kwa kuvizia kama mwanzonui tuliwaomba viongozi wenzie wawe na subira juu ya yaliyotokea sasa tunaachia hili walizungumzie wao.”alisema Is-haq.


Wakati huo huo taarifa zilizopatikana zinaeleza kuwa viongozi wa jumuiya na taasisi za kiislamu jana walikuwa katika kikao kizito cha kujadili hatua hiyo ya kuporwa kwa Sheikh Ponda akiwa katika matibabu na kwamba leo watakutana na waandishi wa habari kuelezea msimamo wao.

Dk Mwakyembe aanza mambo, Rasta anaswa na dawa za kulevya JNIA




Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akionesha picha ya kijana Leonard Jeremiah Monyo ( Edwin Jeremiah Monyo) ambaye amekamatwa na kete 86 za madawa ya kulevya aina ya heroine.


Kijana Leonard Jeremiah Monyo ( Edwin Jeremiah Monyo) ambaye amekamatwa na kete 86 za madawa ya kulevya aina ya heroine.


Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akizungumza na vyombo vya habari leo.
JUHUDI za Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe za kupambana na dawa za kulevya nchini Tanzana zimeanza kuzaa matunda baada ya jana akiwa katika ukaguzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Julius Nyerere kunaswa kijana akijaribu kupita na dawa za kulevya katika uwanja huo.
Kwa kile kuoneshwa kukerwa na tabia hizo, Dk. Mwakyembe amempiga picha kijana huyo ambaye ni rasta na pita yake itasambazwa maeneo tofauti, huku kesi yake ikiendelea ya kupatikana na madawa hayo ya kulevya.
Akizungumza na vyombo vya habari leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Dk. Mwakyembe alimtaja kijana aliyekamatwa jana kuwa ni Leonard Jeremia Monyo (Edwin Jeremiah Monyo) ambaye amekamatwa na kete 86 za madawa ya kulevya aina ya heroin akitaka kusafiri nazo kuelekea misokoto ya bangi 34 akiwa ameficha kwenye begi lake.
Alisema kijana huyo rasta alinaswa na mtambo wa kukagua mzigo baada ya wakaguzi kuushuku mzigo wake hivyo kuamuru ukaguliwe ndipo alipokutwa na madawa hayo haramu akijaribu kusafiri nayo kwa ndege.


Baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Dk. Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe
Alisema kijana huyo kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa uchunguzi zaidi kabla ya kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kukutwa na dawa hizo haramu. Alisema kwa kile kuoneshwa kukerwa na vitendo hivyo na kuamua kwa dhati kupambana navyo wamempiga picha kijana huyo na picha zake zitasambazwa maeneo mbalimbali ili aonekane na umma kujua watua ambao wamekuwa wakilichafua taifa nje na ndani kutokana na biashara hizo haramu.
Dk. Mwakyembe amesema atahakikisha anafuatilia kesi ya kijana huyo hadi itakapoishia ili uona hatua za kisheria zinachukuliwa kwa wahusika na vitendo hivyo kukomeshwa. Alisema maofisa wakaguzi wa mizigo wawili (wote wasichana) ambao walimnasa kijana huyo watazawadiwa na kupandishwa daraja kutokana na kazi nzuri waliyoifanya.
“Jana tu baada ya ukaguzi wenzetu ambao wanaona kama tunafanya mzaha jana tena wakapitisha mzigo wa madawa ya kulevya kiwanja cha ndege cha Dar es Salaam, kwa sababu vijana wetu sasa wameamka na hawataki mchezo wakamkamata kijana huyo…,” alisema.
“Picha yake itasambazwa kila sehemu…sidhani kama tunahitaji upelelezi kwa sababu tumekukamata na dawa za kulevya. Mimi na viongozi wangu kupitisha dawa za kulevya akikisha kuuhakikisha.
Alisema kijana huyo alikamatwa majira ya saa mbili na nusu usiku akiwa anasafiri kwenda nchini Italia kwa kutumia ndege ya kampuni ya Swissair. Alisema kwa sasa kila atakayekamatwa na dawa za kulevya picha yake itasambazwa maeneo mbalimbali ya nchi ili watu hao wajulikane.
Alisema kwa sasa taratibu zinafanywa ili kuhakikisha mizigo ya abiria wanaowasili kutoka nje ya nchi kuingia Tanzania nao mizigo ikaguliwe ili kuwabaini wanaoingiza bidhaa hiyo haramu ichini pia. Aliongeza zoezi hilo litafanyika katika viwanja vya ndege na bandarini kwa kila mizigo inapowasili.
Alisema lengo ni kuhakikisha viwanja vya ndege vinakuwa salama na kuacha kutumika vibaya na baadhi ya watu, jambo ambalo limeendelea kulichafua taifa. Alisem kiwanja cha Dar es Salaam ni kizuri na kina vifaa vya usalama vya kutosha ila mapungufu yaliyopo ni kwa baadhi ya wafanyakazi ambao wanatumia vibaya madaraka yao.
Dk. Mwakyembe ameahidi kuwataja na kuweka picha zao hadharani watu ambao wanajihusisha na madawa hayo ya kulevya. Amesema wanatarajia kutaja majina ya Watanzania ambao hivi karibuni walinaswa na dawa za kulevya nchini Afrika Kusini katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo. Alisema Watanzania wengine wamekamatwa Hong Kong wakihusishwa na dawa hizo na wanafuatilia pia picha na majina yao yatawekwa hadharani muda wowote.

thehabari.com

Wakili Nassoro asikitishwa na kitendo cha Sheikh Ponda kupelekwa Segerea


Picture
Wakili Nassor Jumaa
WAKILI Nassor Jumaa anayesimamia Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda (54) ambaye kwa sasa anakabiliwa na kesi mpya ya kufanya uchochezi katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo hii majira ya saa 7 mchana nje ya viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar  es Salaam amesema kuwa amesikitishwa na hatua  ya vyombo vya dola kumuondoa Sheikh Ponda aliyekuwa amelazwa katika wodi ya Kitengo  cha Taasisi ya Tiba  ya Mifupa  na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI) alikokuwa akipatiwa matibabu na kisha kumhamishia katika gereza la Segerea.

Wakili Jumaa alisema amesikitisha na kitendo hicho kwani muda mfupi baada ya wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka kumaliza kumsomea Sheikh Ponda shitaka linalomkabili, Hakimu Hellen Riwa alitoa amri kuwa Sheikh Ponda aendelee kukaa chini ya ulinzi.

Jumaa akasema ameshangazwa kuona leo, wanausalama wamemtoa Sheikh Ponda wodini na kumpeleka katika gereza la Segerea na kwamba atalazimika kurudishwa tena mahakamani siku kesi yake itakapojatwa Agosti 28 mwaka huu, ambapo upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika: “Kwa kweli kitendo hicho kime nisikitisha na kunishitua sana… ila tunatafakari ni hatua gani za kisheria tutazichukua huko siku za usoni,”alisema Jumaa. 
 
(via Habari Mseto)

Hivi ndivyo alivyozikwa Bilionea Erasto Msuya





MAZISHI ya kufuru ya yule bilionea mfanyabiashara wa madini ya tanzanite mkoani hapa, marehemu Erasto Saimon Msuya, yameacha gumzo kubwa.
Mfanyabiashara huyo aliuawa kwa kumiminiwa risasi zaidi ya 20 na watu wawili wasiojulikana Agosti 7, mwaka huu maeneo ya Kia wilayani Hai, Kilimanjaro kabla ya kupumzishwa Jumanne wiki hii kijijini kwao Kairo huko Simanjiro mkoani Manyara
Baada ya kutokea kwa mauaji hayo, iliundwa kamati ya mazishi ikihusisha  wafanyabiashara wa madini ya tanzanite pekee ambayo ilitengeneza bajeti ya maziko ya takribani shilingi milioni 100.
Habari kutoka ndani ya kamati hiyo zilieleza kuwa gari maalum la kifahari na jeneza lililobeba mwili vilinunuliwa Nairobi nchini Kenya
KUHUSU JENEZA
Ilisemekana kuwa jeneza hilo liliagizwa na kampuni inayojishughulisha na shughuli za maziko ya Montezuma & Monalisa Funeral Home.
Ilielezwa kuwa jeneza hilo lilinunuliwa shilingi milioni nane ikidaiwa kuwa lilikuwa lina uwezo wa kufunga na kufunguliwa kwa kutumia ‘rimoti’.
Ilidaiwa kuwa jeneza hilo lilikuwa na vishikio maalum vilivyokuwa viking’aa kama dhahabu au tanzanite na kulifanya kuonekana la aina yake
MSHANGAO
Hali hiyo iliwaacha na mshangao maelfu ya waombolezaji waliofika kuaga mwili wakati wa ibada iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, maeneo ya Kwaiddi, barabara inayoelekea Ngaramtoni wilayani Arumeru kabla ya kusafirishwa kwenda Simanjiro kwa maziko.

MAGARI
Pamoja na lile lililobeba mwili wa marehemu, msafara wa magari ya kifahari kuelekea kijijini huko ulisababisha Jiji la Arusha kuzizima kwa majonzi huku wengi wakishindwa kuamini kama jamaa huyo amefariki dunia na kuacha utajiri wa kutisha.
“Hebu ona, hakuna gari la ovyo, yote ni makali. Ingekuwa utajiri unaweza kumfufua mtu, basi Erasto angefufuliwa,” alisema mmoja wa waombolezaji akimwelezea jamaa huyo kuwa alikuwa mtu ‘smati’.

SUTI KUTOKA KWA MALKIA ELIZABETH
Habari za ndani zilidai kuwa hata suti aliyozikwa nayo ilitoka nje ya nchi, London, Uingereza kwa Malkia Elizabeth.
Pia ilidaiwa kuwa jamaa huyo alizikwa na cheni ya dhahabu (gold) shingoni yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 10.

VYAKULA, VINYWAJI
Habari zilinyetisha kuwa huduma kama vyakula, vinywaji, mapambo na magari ya kukodishwa kutoka Arusha kwenda kijijini na kurudi viligharimu zaidi ya shilingi milioni 80
MC NI JB
Ili kuthibitisha kuwa msiba huo haukuwa wa kitoto, Msema Chochote ‘MC’ alikuwa ni staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Jacob Steven ‘JB’.

KAIRO, SIMANJIRO
Habari zilidai kuwa waombolezaji walipofika kijijini kwa ajili ya maziko Jumanne mchana, watu walikanyagana makaburini huku vijana wakitaka azikwe na mtu hai wa kumlinda.

KABURI
Walipofika walikuta kaburi la kifahari limeshajengwa ambapo kulikuwa na zulia maalum la kufuta miguu kabla ya kukanyaga marumaru za madini ya tanzanite zilizolizunguka.
Kuthibitisha kuwa ilikuwa ni kufuru, baadhi ya wachimbaji wadogo ‘nyoka’ walikuwa wakiwataka matajiri kulifungia kaburi hilo umeme na kiyoyozi.

MNARA WA KUMBUKUMBU
Baada ya mazishi hayo, inaelezwa kuwa familia ilikubaliana kufanya juu chini kulinunua shamba alilouliwa katika Mji wa Bomang’ombe, Mtaa wa Wasomali eneo la Mjohoroni wilayani Hai, Kilimanjaro ili kujenga mnara wa kumbukumbu.
Ilidaiwa kuwa baada ya kujenga mnara huo, familia itakuwa inatembelea eneo hilo Agosti 7, kila mwaka kwa ajili ya tambiko.

KAKA WA MAREHEMU
Kaka wa marehemu, Israel Msuya, alisema kuwa walifikia uamuzi wa kufanya mazishi hayo kwenye makaburi ya familia ya mzee Elisaria Msuya ‘Kikaango’ ambaye ni baba wa marehemu Erasto.
KUNA KULIPIZA KISASI?
Kwa mujibu wa kaka huyo wa marehemu, familia haitalipiza kisasi kwa watu waliomuua Erasto bali wao wanamwachia yote Mungu.

VIPI KUHUSU KESI?
Katika hatua nyingine, polisi mkoani hapa wanaendelea kuwahoji wafanyabiashara maarufu wa madini ya tanzanite wa mji mdogo wa Mererani wanaodaiwa kuhusika na kifo hicho.
Habari za kipolisi zilieleza kuwa mfanyabiashara mmoja wa madini, kijana ambaye aliibuka ghafla kuwa tajiri mkubwa kutokana na biashara ya madini ya tanzanite, anashikiliwa kwa mahojiano.
               
Chanzo:GlobalPublishers

Timu ya Taifa ya Ngumi yakumbukwa kumwagiwa vifaa, fedha kesho Dar



TIMU ya taifa ya mchezo wa Ngumi iliyopo kambini ikijiandaa na ushiriki wa michuano ya kimataifa inatarajiwa kukabidhiwa vifaa vya michezo na nauli kwa wachezaji tuko litakalofanyika mchana wa leo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) vifaa na fedha hizo zinatolewa na Mkurugenzi wa  Shule za St Mary na Hoteli ya Kitalii iliyopo Bagamoyo, Rutta Rwakatare na ifanyika kwenye ofisi za BFT, jijini Dar.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, inasema hafla hiyo itafanyika saa 6;30 ikiw na lengo la kuisaidia kamb ya mazoezi ya timu hiyo ambao inajiandaa na michuano ya Afrika itakayofanyika mezi ujao nchini Mauritius.
Uongozi wa BFT umedai umefurahishwa na kitendo hicho kinachotarajiwa kufanyika leo ukiwa umekuja wakati muafaka wakati timu hiyo ikihitaji msaada kwa sasa kwa maandalizi ya michuano hiyo na le ya mwakani ya Jumuiya ya Madola.
BFT ikatoa wito kwa wadau wengine wa michezo kujiokeza kuisaidia timu hiyo kwa madai ina hali mbaya kifedha.
"BFT tumefurahishwa mno na mwitikio wa Mkurugenzi huyo kwa kusikia na kuguswa kuhusu timu ya taifa ya ngumi na BFT, tunawaomba watanzania wengine wajitokeze zaidi kusaidia timu yetu ya taifa ili uwakilishi katika mashindano ya kimataifa uwe na tija," taarifa hiyo ya BFT inasomeka hivyo.
Pia BFT imeviomba vyombo mbalimbali vya habari kujitokeza kuhamasisha ili watanzania wengine kujitokeza kuendelea kusaida zaidi kwa madai msaada unahitajika wa vifaa vya mazoezi, matibabu, chakula, maji,nauli, nguo za mazoezi na posho za wachezaji.

Kuziona Yanga na Azam Buku 7 tu

Na Boniface Wambura
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga na makamu bingwa Azam wanavaana keshokutwa (Jumamosi) kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria uzinduzi wa msimu mpya wa 2013/2014.

Mechi hiyo inayotarajiwa kuwa kivutio kwa wapenzi wa mpira wa miguu nchini itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni ambapo mshindi atakabidhiwa ngao.

Iwapo dakika 90 za mechi hiyo hazitatoa mshindi, timu hizo zitatenganishwa kwa mikwaju ya penalti huku asilimia 10 ya mapato ya mechi hiyo yakienda kwa kituo cha kulelea watoto cha SOS.

Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya kijani na bluu wakati viti vya rangi ya chungwa ni sh. 10,000. Watakaiongia viti vya VIP C watalipa sh. 15,000, viti vya VIP B ni sh. 20,000 wakati VIP A watalipa sh. 30,000.