STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 9, 2015

HII NDIYO SHOW TIME YA H-BABA

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/10/H-baba.jpg
H-Baba


IVORY COAST NDIYO VIDUME AFRIKA, YARUDI YA 1992

The Ivory Coast team and staff pose with their Africa Cup of Nations trophy having defeated Ghana 9-8 on penalties on Sunday night
Waflame wa soka Afrika, Ivory Coast
The Ivory Coast team celebrate landing the Africa Cup of Nations on penalties, their first AFCON title since 1992
Oyooooooooooooooooo!
Ivory Coast captain and Manchester star Yaya Toure is presented with the Africa Cup of Nations trophy on Sunday evening
Nahodha Yaya Toure akipokea Kombe toka kwa Rais  Nguema
HISTORIA imejirudia tena nchini Guinea ya Ikweta baada ya Ivory Coast kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Fainali za Mataifa ya Afrika 2015  kwa kuichapa Ghana kwa mikwaju ya penati kama ilivyokuwa katika fainali za mwaka 1992.
Katika fainali za mwaka huo, Ghana maarufu kama Black Stars walikufa kwa mikwaju ya penati 11-10 na usiku wa kuamkia leo walikubali tena kipigo cha penati 9-8 kwa wapinzani wao na kuliacha taji likienda kwa Ivory Coast ikiwa ni mara ya pili kwao.
Timu hizo zililazimika kupigiana penati baada ya kumaliza dakika 120 bila ya kufungana na katika upigaji wa penati, Ivory Coast walianza vibaya kwa Wilfried Bony kukosa penati, lakini haikuweza kuwakatisha tamaa Tembo wa Afrika kumaliza udhia na ukame wa miaka zaidi ya 20 tangu wanyakue taji la kwanza 1992.
Ghana wanaweza kujilaumu kwa kushindwa kuibuka mabingwa kwa mara ya tano kutokana na kipindi cha pili cha dakika 90 kutawala sehemu kubwa ya pambano hilo lililosisimua kutokana na lilivyokuwa kali.
Katika hatua ya mikwaju ya penati Black Stars walianza kwa Mubarak kufunga kabla ya Bony kukosa, Jordan Ayew akapata penati ya pili ya Ghana na Tallo wa Ivory Coast naye akaikosa penati yake na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Hata hivyo Acquah na Acheampong walikosa penati  zilizofuata za Ghana, wakati Aurierna Doumbia walifunga zao na matokeo kuwa 2-2.
Andre Ayew alifunga mkwaju wake na Yaya Toure akasawazisha, John Mensah akafunga na Solomon Kalou akasawazisha kabla ya Agyemang-Badu kufunga mkwaju wake na Koro Toure kusawalisha.
Afful aliifungia Ghana na Kanon kusawazisha zoezi likawa piga nikupige hadi katika penati ya tisa ambapo Ghana kupitia kipa wake Razak Brimah ilikosa na Ivory Coast kutumbukiza yao iliyowapa ubingwa wa pili katika historia za michuano hiyo kupitia kwa Boubacar Barry aliyegeuka kuwa shujaa kabla ya nahodha Yaya Toure kukabidhiwa taji na Rais wa Guinea ya Ikweta, Nguema kwenye uwanja wa Bata.

Irene Uwoya awataka mashabiki wake kupokea Kisoda

Na Rahma White
MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Irene Uwoya 'Oprah' amewataka mashabiki wake kujiandaa kuipokea kazi yake mpya iitwayo 'Kisoda' akidai ni kazi kali kuliko hata filamu yake ya awali iitwayo 'Apple' aliyoitoa mwaka jana.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Irene alisema 'Kisoda' ni moja ya kazi zitakazoleta mapinduzi makubwa katika fani ya uigizaji nchini kwa namna ilivyoandaliwa ikishirikisha wasanii wa ndani na nje ya nchi.
Irene alisema filamu hiyo iliyomtafuna fedha nyingi ipo katika hatua ya uhariri na itaachiwa wakati wowote zoezi hilo likikamilika akiwataka mashabiki wajiandae kuipokea kwa mikono miwili.
"Kama kuna waliodhani nilibahatisha kwenye 'Apple', wamekosea safari hii naja na 'Kisoda', moja kati ya filamu kali ambayo imewashirikisha wasanii wa Tanzania na Afrika Kusini, chini ya kampuni yangu ya Apple Entertainment," alisema Irene.
Msanii huyo alisema amekusudia ndani ya mwaka 2015 awape burudani ya kutosha mashabiki wake na kwa kuanza ameanza na Kisoda kabla ya kufuatiwa na mambo mengine makubwa zaidi.
Irene aliwataja baadhi ya wasanii walioshiriki filamu nchini wa hapa nchini ukiondoa yeye (Irene) ni Islam, Mariam Ismail na Msami.
Kimwana huyo aliyewahi kunyakua tuzo ya Muigizaji w Kike Chipukizi wa tuzo za Kinara kupitia filamu ya Diversion of LOve' kabla ya kuanza kuzalisha filamu zake na kuwahi  kuendesha kipindi cha kwenye runinga cha 'Paradise Show' ameshiriki filamu zaidi ya 30 zilizomjengea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya kazi hizo ni; 'Ngumi ya Maria', 'Nyati',  'Zawadi Yangu', 'Aliyemchokoza Kaja', 'Figo','Rosemary', 'Snitch', 'The Return of Omega', 'Money Talk', 'Omega Confusion', 'Question Mark', 'Safari', 'Innocent Case', 'Nyota Yangu', 'Last Card', 'Doa la Ndoa', 'Offside' na 'Oprah'.