STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 11, 2015

Mbeya City yawatunuku nyota wake, kocha Mwambusi

IMG-20150510-WA0010KLABU ya Mbeya City imewapa tuzo wachezaji wake pamoja na Kocha Juma Mwambusi kwa kuiwezesha timu hiyo kukamata nafasi ya nne katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2014-2015.
Tuzio hizo zilitolewa mara baada ya mchezo wao wa mwisho wa Ligi Kuu kati yao ya Polisi Moro ambapo Mbeya iliibuka washindi wa bao 1-0.
Kwenye tuzo hizo Kocha mkuu Juma Mwambusi alipata tuzo kama kocha mwenye mafanikio makubwa ndani ya kikosi cha city na ligi kwa ujumla Paul Nonga, Deus Kaseke, Themi Felix walipata tuzo ya heshima kwa kufanya vizuri misimu miwili  Rafael Alfa na Kenny Ally walipata tuzo ya  wachezaji chipukizi waliofanikiwa Haningtony Kalyusubula alipata tuzo ya  mlinda lango bora  na Juma Nyosso, Hassan Mwasapili na Peter Mwalyanzi walipata tuzo ya uchezaji bora
IMG-20150510-WA0009
Halikadhalika wachezaji wengine 18 nao walipata zawadi  ikumbukwe kuwa zawadi na tuzo hizo walizopata wachezaji wa City zimeambatana na bahasha iliyonona vizuri kutoka uongozi na mashabiki wa Mccfc.

IMG-20150510-WA0004
Hanington Kalyesubula akipokea tuzo

Carlo Ancelotti ajipa matumaini kwa Juventus

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02921/ancelotti_2921770b.jpgMENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti anaamini kikosi chake kinaweza kugeuza matokeo ya mabao 2-1 waliyochapwa na Juventus na kutinga hatua fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Pamoja na kutoka sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa La Liga dhidi ya Valencia juzi. Mabingwa hao wa Ulaya sasa wako nyuma ya vinara Barcelona kwa alama nne huku kukiwa kumebaki michezo miwili katika ligi. 
Akihojiwa kocha Ancelotti amesema wanahitaji kuwa mawazo chanya na kuthamini jinsi walivyocheza vyema katika mchezo huo. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa makosa madogo madogo ndio yaliyowagharimu, lakini wanahitaji kutulia na kujiandaa kwa ajili ya mchezo wao wa keshokutwa (Jumatano) dhidi ya Juventus.
Katika mfululizo wa michuano hiyo kesho Jumanne, Bayern Munich watakuwa nyumbani Alliaz Arena ikli kubadilisha matokeo ya mabao 3-0 iliyonyukwa katika mechi ya wiki iliyopita nchini Hispania.

Moyes anogewa La Liga, azipotezea klabu za EPL

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01727/moyes_1727193a.jpgAMENOGEWA! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Meneja wa klabu ya Real Sociedad, David Moyes amezipasha klabu za Ligi Kuu zinazomuwinda kuwa hana mpango wa kwenda popote kufuatia tetesi kuwa atarejea nchini Uingereza. 
Kocha huyo raia wa Scotland alitimuliwa na Manchester United baada ya kuinoa katika kipindi cha miezi 10, Novemba mwaka jana kutokana na klabu hiyo kutofurahishwa na matokeo. 
Moyes alirejea tena uwanjani akiwa kocha wa klabu hiyo katika  mazingira ambayo alikuwa hana mazoea nayo katika Ligi Kuu ya Hispania. 
Wiki za karibuni kumezuka tetesi kuwa klabu za West Ham United na Newcastle United zimekuwa zikitaka saini yake, lakini mwenyewe amedai hana mpango wa kuondoka Hispania kwa sasa. 
Akihojiwa Moyes amesema kwa sasa anataka kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao, jambo ambalo amefikia hatua nzuri hivyo hawezi kuacha mpaka azma yake itimie.

Maskini Dk Ndumbaro, TFF yakomaa naye!

http://static.goal.com/401800/401857_heroa.jpgNa Rahim Junior
TUMAINI la Mjumbe wa Bodi ya Ligi na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa klabu ya Simba, Dk Damas Ndumbaro kutoka kifungoni, limefifia baada ya Kamati ya Rufaa ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutupilia mbali rufaa yake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa ya Nidhamu ya TFF, Revocatus Kuuli, inasema kwa maamuzi hayo yaliyofikiwa kwa turufu ya kura, ambapo wajumbe watatu waliafiki kupiga chini hoja za mrufani na mmoja kukubaliana naye ni kwamba, Ndumbaro ataendelea kutumikia adhabu yake kutojihusha na michezo kwa muda wa miaka saba.
Dk Ndumbaro alikata rufaa katika kamati hiyo kupinga maamuzi ya Kamati ya nidhamu iliyomkuta na hatia kwa kitendo chake cha kupinga maamuzi ya TFF ya kutaka klabu za Ligi Kuu kukatwa asimilia tano za fedha za wadhamini na kumtia kifungoni Oktoba mwaka jana.
Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa hizo za TFF ni kwamba baada ya mahojiano kati ya mrufani Dk Damas Ndumbaro na Wakili wa TFF, Emmanuel Muga, pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Rufaa ya Nidhamu iliamuriwa kutupiliwa mbali kwa hoja za mrufani kwa maamuzi ya kura 3-1.
"Kwa uamuzi huu kamati inadhibitisha uamuzi wa Kamati ya Nidhamu iliyosomwa Oktoba 13, 2014 uamuzi huu umefikiwa baada ya wajumbe kupiga kura na uamuzi kupitishwa kwa wingi wa kura za wajumbe watatu, dhidi ya mjumbe mmoja wa kamati hii kwa hoja ya 2,3 na 4 na wajumbe wote 4 walikubaliana kutupiliwa mbali hoja ya kwanza.
"Kwa hiyo Dk Damas Ndumbaro ataendelea kutumikia adhabu yake kwa kutojihusisha na shughuli yoyote ya Mpira wa Miguu (Soka) kwa kipindi cha miaka saba.
"Hata hivyo mrufani Dr Damas Ndumbaro anayohaki ndani ya siku 10 kuanzia leo Mei 10,2015 ya kuomba marejeo ya uamuzi huu mbele ya kamati ya Rufaa ya Nidhamu ya TFF chini ya Ibara 142 ya kanuni za nidhamu za TFF ya mwaka. " sehemu ya taraifa hiyo inasomeka hivyo.
Ebu isome taarifa hiyo ya Kamati ya Rufaa ya Nidhamu:


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAREHE 11 MEI 2015
 

  MAAMUZI YA KAMATI YA RUFAA YA NIDHAMU
BAADA ya mahojiano kati ya mrufani Dr Damas Ndumbaro na Wakili wa TFF     Nd Emmanuel Muga, pamoja na Wajumbe wa Kamati ya rufaa ya nidhamu kuwahoji wote, Mrufani na Wakili wa TFF, Kamati ya rufaa ya nidhamu ilichukua uamuzi ufuatao:-
Hoja ya kwanza cha rufaa, kwamba kamati ya nidhamu haikuwa na nguvu za kisheria kusikiliza shauri lake, Kamati ya rufaa ya nidhamu baada kusikiliza hoja za pande zote mbili, kwa uamuzi wa Wajumbe wote kwa maana ya kuwa zote nne za Wajjumbe wa kamati ya rufaa ya nidhamu, ilitupilia mbali hoja hiyo na kuona kwamba kamati ilikuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri hilo kwa kuwa mkata rufaa ni afisa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF kwa mujibu wa Katiba ya TFF ya 2013. Uamuzi katika hoja hii uliamuliwa kwa kura 3 dhidi ya moja.
Hoja ya pili inayosema kwamba kamati ilikosea kisheria kwa kutompa muda wa kuleta utetezi wake wala vielelezo vyovyote vile kwenye shauri lake.
Kamati ya rufaa ya Nidhamu kwenye Shauri hili, baada ya kufanya maamuzi kwa kupiga kura, kura za Wajumbe watatu zilitupiliwa mbali hoja yake na kura moja kati ya kura nne ilikubaliana na hoja yake kwa uamuzi huo, kamati ya rufani ya nidhamu ilitupilia mbali hoja hiyo kwa uamuzi wa wingi wa kura kwa maana ya kuwa tatu dhidi ya kura moja.
Sababu za kutupilia mbali hoja hizo ni kwamba mrufani alipata wito wa kwenda kwenye shauri, na akawakilishwa na wakili wake ( Nestory Peter Wandiba ) kwenye Shauri hilo. Shauri liliposikilizwa kwa mara ya kwanza tarehe 10/10.2014 shauri lilipangwa kusikilizwa tarehe 11/10/2014 Lakini siku hiyo ya pili si wakili wala Dr Ndumbaro alifika kwenye shauri hilo kwa maana hiyo basi shauri lililazimika kusilikizwa upande mmoja kwa mujibu wa kanuni za nidhamu za TFF ibara ya 94 (3).
    3. Hoja ya tatu linalosema kwamba kamati ilikosea kusiliza shauri upande mmoja bila ya mtuhumiwa kuwepo, ni kukiuka haki yake ya msingi ya  kusikilizwa.
    Kamati baada ya kusikiliza utetezi kutoka pande zote mbili kamati ilifanya uamuzi kwa kupiga kura, na kura tatu (wajumbe watatu) walitupilia mbali hoja hiyo, dhidi ya kura moja (mjumbe mmoja) aliyeikubali hoja hiyo. Sababu za kutupilia mbali hoja hiyo ni kutokana na ukweli kwamba mrufani alipata wito wa kuhudhuria shauri hili na akamtuma wakili wake, lakini mrufani alishindwa kuonyesha vielelezo vya kuonyesha kwamba angesafiri kwenda nje ya nchi ili kamati ya nidhamu iweze kuahirisha shauri mpaka wakati ambao angekuwa amerejea lakini hakufanya hivyo.
   Hata hivyo kwa mujibu wa Ibara 144(2) (3) za kanuni ya nidhamu za TFF, mrufani  angeweza pia kuomba kamati ya nidhamu ibatilishe uamuzi iliyoutoa dhidi yake ili aweze kusikilizwa utetezi wake pia hakufanya hivyo na aliamua kukata rufaa.
    4. Hoja ya nne inayosema kwamba kamati ilikosea kisheria katika uchambuzi wa ushahidi wa mlalamikaji na hatimaye kutoa uamuzi uliomtia hatiani.
    Kamati ya rufani ya nidhamu ilisikiliza kwa umakini hoja za pande zote mbili na kujiridhisha kwamba mrufani alifanya makosa kwa kutoa taarifa isiyosahihi na kupotosha maamuzi ya TFF kinyume na kanuni ya 41 (6) ya kanuni za ligi kuu ya Tanzania toleo la 2014 (4) na pia kushawishi, kupotosha au kuzuia maamuzi/utekelezaji wa maamuzi ya TFF kinyume na kanuni ya 41(16) ya kanuni za ligi kuu za Tanzania ya (2014).
    Wakati wa kufanya maamuzi, wajumbe watatu(3) kwa maana ya kura tatu zilitupilia mbali hoja hiyo, na kura moja, kwa maana ya mjumbe mmoja alikubaliana na hoja hiyo. Kwa maana hiyo, kamati ya rufaa ya nidhamu ya TFF imetupilia mbali hoja hiyo.
    Kwa uamuzi huu kamati inadhibitisha uamuzi wa kamati ya nidhamu iliyosomwa tarehe 13/10/2014, uamuzi huu umefikiwa baada ya wajumbe kupiga kura na uamuzi kupitishwa kwa wingi wa kura za wajumbe watatu, dhidi ya mjumbe mmoja wa kamati hii kwa hoja ya 2,3 na 4 na wajumbe wote 4 walikubaliana kutupiliwa mbali hoja ya kwanza.
    Kwa hiyo Dr Damas Ndumbaro ataendelea kutumikia adhabu yake kwa kutojihusisha na shughuli yoyote ya Mpira wa Miguu (Soka) kwa kipindi cha miaka saba.
    Hata hivyo mrufani Dr Damas Ndumbaro anayohaki ndani ya siku 10 kuanzia leo tarehe 10/05/2015 ya kuomba marejeo ya uamuzi huu mbele ya kamati ya Rufaa ya Nidhamu ya TFF chini ya Ibara 142 ya kanuni za nidhamu za TFF ya mwaka.
    Kila upande utabeba gharama zake Hukumu inasomwa leo tarehe 10/05/2015/
Revocatus L. K. Kuuli.
MAKAMU MWENYEKITI.
IMETOLEWA NA TFF