STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 21, 2015

3 zachemsha usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2015-2016

Stand United
Toto Africans
WAKATI dirisha la usajili kwa klabu vya Ligi Kuu nchini (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) likifungwa juzi klabu tatu za VPL vimeshindwa kuwasilisha usajili wao wa wachezaji katika muda uliopangwa.
 Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) alivitaja Klabu za Coastal Union ya Tanga, Stand United ya Shinyanga na Toto African ya jijini Mwanza kuwa zimeshindwa kuwasilisha usajili wao na kusema faini ni 500,000  kwa mchezaji mmoja hivyo klabu iliyochelewesha usajili au itakayobadili majina au kuongeza majina baada ya usajili kufungwa italazimika kulipia faini
“Usajili umefungwa jana (juzi) na timu tatu hazijawasilisha usajili wao hata wa mchezaji mmoja pamoja na TFF kuongeza muda wa usajili kwa wiki mbili”, alisema Kizunguto
Pia alisema si kwamba timu zingine zimefikisha idadi ya wachezaji wote kulingana na kanuni bali zingine zimesajili wachezaji 18, 24 hivyo hata wao endapo wataongeza watalipia faini.
Kizuguto alikumbusha timu ambazo zimesajili wachezaji wa kigeni kuwasilisha ada zao ili waweze kupata kbali cha kucheza ligi.
Awali TFF ilitoa muda wa wiki mbili kwa vilabu vyote nchini kukamilisha usajili, ambapo vilabu 13 vya ligi kuu vimeweza kukamilisha ndani ya wakati, klabu 24 vya ligi daraja la kwanza, klabu 24 ligi daraja la pili pia vimeweza kukamilisha usajili wao ndani ya muda uliopangwa.


Mkwasa ataja majembe yake ya Uturuki, Dida aachwa

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/06/Mkwasa-Stars.jpg
Kocha Mkwasa (kushoto) na Msaidizi wake, Hemed Morocco
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wachezaji 22 atakaoondoka nao kuelekea Uturuki kupiga kambi ya kuiwinda Nigeria.
Wachezaji hao 22 wanatarajiwa kuondoka nchini Jumapili  usiku kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria utakaochezwa Septemba 05, 2015. Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto, alisema kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa ametoa orodha ya wachezaji 22 watakaosafiri usiku wa jumapili. “Orodha ya wachezaji 22 imetoka katika kikosi kilichotangazwa wiki mbili zilizopita na Mkwasa ambapo walipata nafasi ya kufanya mazoezi kwa takribani wiki moja katika uwanja wa Karume”, alisema Kizuguto. Kizuguto alisema wachezaji wote waliochaguliwa kujiunga na timu ya Taifa wanapaswa kuripoti kambini Tansoma Hotel Jumapili saa 5 asubuhi kwa maandalizi ya mwisho ya safari hiyo. Wachezaji waliochaguliwa ni All Mustafa Aishi Manula, Said Mohamed, walinzi Shomari Kapombe, Abdi Banda, Mohamed Hussein, Hassan Isihaka, Juma Abdul, Haji Mngwali, Kelvin Yondani, Nadir Haroub. Wengine ni Mudathir Yahya, Himid Mao, Frank Domayo, Salum Telela, Deus Kaseke, Said Ndemla, John Bocco, Farid Musa, , Rashid Mandawa, Saimon Msuva, na Ibrahim Ajib. Taifa Stars kwa usafiri wa shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines), na itafika jijini Istambul jumatatu asubuhi, ambapo itaelekea katika mji wa Kocael   kuweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Green Park Kartepe.

Man United wakatwa maini kwa Sadio Mane

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/05/16/16/28BDB01200000578-3084365-Southampton_s_Sadio_Mane_celebrates_the_first_of_the_first_half_-a-3_1431789411065.jpgKLABU ya Southampton imekiri kuwa Manchester United wanamuwania winga wao wa kimataifa wa Senegal Sadio Mane, lakini ikatamka wazi kwamba mkali huyo hauzwi ng'o.
Wiki iliyopita Southampton walikanusha taarifa za kupokea ofa yeyote kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23. Mshambuliaji wa Barcelona Pedro amekuwa akihisiwa kujiunga na United lakini kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za kijiunga na Chelsea kwa dau la pauni milioni 21. 
Kutokana na hali hiyo United wameamua kuongeza nguvu zao katika kumsajili Mane kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi. Mane amefunga mabao 10 katika mechi 32 alizocheza msimu uliopita baada ya kujiunga na klabu yake ya sasa akitokea Red Bull Salzburg ya Austria na yumo pia katika orodha ya wachezaji waliowahi kufunga magoli matatu -hat-trick kwa muda mfupi zaidi.
Hata hivyo mapema leo Ijumaa klabu hiyo ya Southampton imeweka bayana kwamba mchezaji huyo hauzwi hivyo Man United watafute pengine pa kupata mchezaji mpya.
Meneja wa The Saints, Ronald Koeman amefunguka kuwa mchezaji huyo hauzwi kwa bei yoyote.

Straika Msenegal atua Msimbazi, amtia tumbo joto Kiiza

Niang mwenye kofia akiwasili
Niang akipokea simu mara baada ya kuwasili kwenye hoteli aliyofikia jijini Dar es Salaam
Akiwaskiliana alipowasilia hotelin
KLABU ya Simba imezidi kujiimarisha baada ya mchana huu kumpokea straika kutoka Senegal, Papa Niang, ambaye anatarajiwa kupimwa Jumatatu wakati Simba ikiumana na Mwadui Shinyanga kabla ya kusainishwa mkataba wa kukipiga Msimbazi.
Niang ambaye ni mdogo wa nyota Mamadou Niang, mshambuliaji ambaye itachukua muda Watanzania kumsahau baada ya kuizamisha Taifa Stars kwa mabao 4 ametua akiambatana na meneja wake, Massouka Ekoko.
Ujio wa straika hutyo aliyekuwa akicheza soka la kulipwa El Salvador kunamaanisha kuwa kama mipango itaenda sawa basi kuna uwezakano wa dili la Mrundi Kevin Ndatisenga aliyeifungia Simba moja ya mabao mawili wakati wakiiua URA ya Uganda likafa.
Pia hata kibarua cha Hamis Kiiza 'Diego' ambaye ameanza kuwekewa zengwe huenda nacho kikaota nyasi, ili kutimiza idadi ya wachezaji saba wa kimataifa wanaohitajiwa na timu hiyo.
Mpaka sasa ina wachezaji sita wa kigeni ambao ni Justice Majabvi, Emiry Nibomana, Hamis Kiiza, Juuko Murshid na Simon Sserunkuma, huku pia ikiwa imetoa kwa mkopo Raphael Kiongera aliyepo KCB ya Kenya.
Wakati Niang akitua leo zipo taarifa kutoka Msimbazi kwamba straika mwingine mkali atatua siku yoyote kuanzia leo kumaliza na mabosi wa Simba, ikiwa ni mikakati ya kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa misimu mitatu hakijaonja ladha ya ubingwa wa Tanzania Bara.

Dondoo kuhusu Niang
Jina kamili: Papa Niang
Tarehe ya kuzaliwa: 5 Disemba, 1988 (miaka 26)
Mahali alipozaliwa: Matam Senegal
Urefu: Mita 1.81 
Nafasi anayocheza: Mshambuliaji
Klabu alizowahi kuzitumikia:
Kwasasa: Mchezaji huru
2005-2006: ASC Thies 
2007: FC OPA
2008: AC Oulu
2009-2012: FF Jaro
2013: FC Vostok
2013-2014: Al -Shabab SC
2014-2015: FC Mounana