STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 5, 2014

SIMANZI! Kidume Sheikh Ilunga Hassan Kapungu afariki dunia

Sheikh Ilunga Hassan Kapungu enzi za uhai wake.
MMOJA wa Wanaharakati na viongozi machachari wa Kiislam,  Sheikh Ilunga Hassan Kapungu amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ugonjwa wa Kisukari jijini Dar es Salaam. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Sheikh Mohammed Kassim, Marehemu Sheikh Ilunga ambaye kwa siku za karibuni alikuwa akiandamwa kutokana na DVD zenye hotuba zake za kusisimua za kiharakati zilizokuwa zikiwaamsha waislam kutambua na kutetea haki zao  amezikwa leo majira ya saa 10 jioni baada ya mwili wake kuswaliwa msikiti wa Kichangani. Magomeni.
Inna Lillah Waina Illah Rajiun, Sheikh Ilunga katangulia nasi tu nyuma yake kwa sababu Kila Nafsi ni Lazima Itaonja Mauti.

Juventus mabingwa wapya Italia

http://cdn.bleacherreport.net/images_root/slides/photos/003/467/801/hi-res-454028537-gianluigi-buffon-of-juventus-fc-celebrates-victory-at_crop_650x440.jpg?1386971109MABINGWA watetezi wa Italia, Juventus ambao usiku huu wataingia uwanjani kupepetana na Atalanta wamejihakikishia ubingwa wa Ligi Kuu ya nchi hiyo, Seria A baada ya wapinzani wao Roma kupoteza 4-1.
Kipigo hicho kimeifanya Roma kusaliwa na pointi 85 na michezo miwili ambapo hata kama wakishinda mechi hizo hawataweza kuzifikia pointi ilizonazo Juve ambazo ni 93 na kuwafanya kibibi cha Turin kuingia uwanja wa nyumbani wakiwa tayari mabingwa wa Seria A.
Katika mechi nyingine za jana nchini humo, AC Milan iliwashikika adabu wapinzani wao wa jiji la Milan, Inter Milan kwa kuwalaza bao 1-0, huku Parma wakishinda nyumbani mabao 2-0 dhidi ya Sampdoria, Udenese ikishinda pia nyumbani mabao 5-3 dhidi ya Livorno, Torino ikiiduwaza  Chievo Verona kwa kuwalaza bao 1-0 na Genoa na Bologna zilishindwa kutambiana kwa kutofungana.

Suarez ashinda tena tuzo England

http://thebeastbrief.com/wp-content/uploads/fbl-eng-pr-man_city-liverpool_yat6982_33846537.jpgNYOTA ya neema imeendelea kumuangazia Mshambuliaji mahiri wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez baada ya kutajwa tena kuwa Mchezaji bora wa Mwaka wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini Uingereza. 
Strika huyo kutoka Uruguay, aliyefunga mabao mabao 30 (kabla ya mechi ya usiku huu)msimu huu katika Ligi Kuu na kuiwezesha timu yake kufukuzia taji la ubingwa toka walipofanya hivyo mwaka 1990. 
Suarez, 27, alipata asilimia 52 ya kura zilizopigwa na waandishi hao akimshinda nahodha wake Steven Gerrard, huku Yaya Toure wa Manchester City akishika nafasi ya tatu. 
Mshambuliaji huyo hiyo ni tuzo ya pili baada ya wiki iliyopita alitajwa kama mchezaji bora na Chama cha wachezaji wa Kulipwa nchini humo (PFA) anatarajiwa kupokea zawadi yake hiyo katika sherehe za chakula cha usiku zitakazofanyika jijini London Mei 15.