STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 30, 2012

More 120,000 US Dollars from UAE Embassy for iftar and Zakatul fitr in Tanzania

The Embassy of the United Arab Emirates(UAE)in the country through Sheikh Khalifa bin Zayed Al Hahyan, Sharjah Charity Internation and Red Cresent organizations will use more $120,000 to provide Itfal and Zakatul Fitr to seven regions of the country during this holly months of Ramadan. Speaking in Dar es Salaam on behalf of UEA ambassador in the country H.E Ambassador Mallalla Mubarak Al Ameir and his second secretary, Mohammed Obaid Salem AlZaabi,the embassy accountant Abdallah Ahmedina said the money will benefit seven regions of the country, he named the regions as Dar es Salaam, Iringa, Kilimanjaro, Arusha, Pwani, Dodoma and Morogoro . Ahmedina was speaking this when he donated Iftal at Al Makbool Mosque in Msasani, Dar es Salaam. He explained that his embassy gave the money to the mentioned regions and that the remaining money will be given to, widows, orphans , disabled and other less privileged people during Zakatul Fitr cerebrations. Ahmedina said this is not the first time for his embassy to provide Iftal and Zakatul Fitr and promised that his embassy is committed to continue providing Iftal and Zakatul Fitr to all Muslims in the country during the period of Ramadan . "Its our tradition to give people Iftal and also zakatufitr,and this year we will use $122,000 for that purpose , this money has come from organizations which are Sheikh Khalifa ($80,000), Red Cresent ($36,000)and Sharjah Charity (6,000),"he said On his speech , Al Makbool mosque clergy, Sheikh Mussa Abdallah,thanked the embassy for the donation which he said will help fasting Muslims during this holly months of Ramadan. "There are some muslims who are fasting but do not have food for iftal , we thanked the Embassy of United Arab Emirates (UAE)and the other three organizations for the donation which we strong believe will help many Muslims” he said

UAE's Embassy gave iftar to Moslims in Dar

Al Rahman Mosque Sheikh, Abdullah Salim Bahssany has asked companies , organizations and individuals to provide free Iftal to Muslims during fast breaking time in this months of Ramadan. The sheikh said there are some Muslims who are lacking iftal and its good to help them with food, he was speaking this on Saturday in Dar es Salaam when the Embassy of the United Arab Emirate (UEA)in the country through Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan group gave iftal to Muslims during fast breaking at his mosque. The embassy and the group will provide the food to members of Al Rahman Mosque and other surrounding areas the whole months of Ramadan. He thanked the Embassy and the group for the iftal and he asked other people to emulate the gesture shown by the embassy and the group . “Am asking all Muslims in Kinondoni District who are observing the holly months of Ramadan but are not sure of getting the iftal to come here for the food and also prayers , we are very happy and thank the Embassy of United Arab Emirates(UAE) is giving us the iftal, am asking others to emirate this welcome gesture” he said Some members of the mosque thanked the embassy for the iftal saying it will ease some of the problems which they face to get the iftal at selling points. “This is good as it helps us to get the iftal within the mosque premises , buying this at some selling points is very tiresome as there are queues and also some people may lack money to buy Iftal ” said one member of the church who identified himself as Mustafa Ali .

Kipemba sasa vitani na Waanchari, Warenchoka

MUIGIZAJ
MUIGIZAJI mkongwe nchini, Issa Kipemba anajipanga kufyatua filamu mpya inaozungumzia uhasama wa makabila mawili makuu ya mkoani Mara ya Warenchoka na Waanchari. Nyota huyo wiki iliyopita alikuwa mkoani humo kuonana na 'machifu' wa koo hizo ili kujua chanzo vita vyao na pia kupata baraka za kuicheza filamu hiyo. Akizungumza na NIPASHE juzi siku moja baada ya kurejea toka safarini, Kipemba aliyewahi kutamba na Kaole Sanaa, alisema safari yake ilikuwa na mafanikio tofauti na alivyofikiri. Kipemba alisema amejifunza mengi katika safari yake hiyo na kwa sasa anajipanga ili kufyatua filamu hiyo itakayokuja baada ya kazi yake ya 'Injinia' kuingiza sokoni. Alisema hajajua filamu hiyo itawashirikisha wasanii wapi kutokana na ukweli inahitaji umakini wa hali ya juu kama alivyofanya katika kazi yake ambayo inakaribia kutoka hewani ya 'Injinia'. "Unajua sitaki kulipua kazi, nataka kuonyesha mfano kwa wadau wengine wa filamu, kwamba kazi hii si ya kulipuliwa kwa nia ya kujipatia fedha tu," alisema.

Machejo wa ITV ana Ngekewa

MSANII nyota wa maigizo aliyepo kundi la Jakaya Theatre linaloonyesha michezo yake kupitia kutuo cha ITV, Halid Chihame maarufu kama 'Alex Machejo' au 'Mzee wa Rivasi', amefyatua wimbo mpya uitwao 'Ngekewa' ikiwa ni maandalizi yake ya kupakua albamu kamili. Akizungumza na MICHARAZO, Machejo, alisema wimbo huo ameurekodia katika studio za Kili Records chini ya mtayarishaji wake mahiri, C9 na tayari ameshakisambaza kwenye vituo vya redio na kuanza kuchezwa hewani. Machejo alisema kibao hicho amekiimba peke yake na kipo katika miondoko aliyoipa jina la 'Flava Champlin', huku akiwa tayari ameshakamilisha nyimbo nyingine tano kwa ajili ya kuzirekodi kuwapa burudani mashabiki wake. "Kaka nimeanza kusambaza kibao changu kipya kiitwacho 'Ngekewa' wakati huo huo nikiwa na nyimbo nyimbo tano zilizokamilika ambazo natarajia kuzifyatua wakati wowote kuanza wiki ijayo," alisema. Alizitaja nyimbo hizo nyingine zitakazofuatia baada ya 'Ngekewa' ni 'Wa Kwalu', 'Mtoto kwa Mama Hakui', 'Tanzania', 'Nasubiri' na Kimanzichana'. Msanii huyo aliyetamba na michezo kama 'Kovu la Siri', 'Kivuli', 'Utelezi', 'Riziki' na 'Bakora', alisema mipango yake ni kufyatua albamu kamili hapo baadae, ingawa alisema itategemeana na maamuzi ya menejimenti inayomsimamia kazi zake.

Simba, Yanga zatishia Super8

USHIRIKI wa Simba na Yanga katika michuano mipya inayotarajiwa kujumuisha timu nane za Tanzania Bara na Visiwaniinayokwenda kwa jina la "BancABC Super 8" uko katika hatikati kutokana na timu hizo kutoiweka ligi hiyo kwenye kalenda zao, imefahamika. Ligi hiyo inayofanana na Ligi ya Muungano inatarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 4 hadi 18 mwaka huu chini ya udhamini wa benki ABC na itajumuisha timu nane. Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alisema jana kwamba ligi hiyo ni nzuri kwa lengo la kuiandaa timu lakini klabu yake itakuwa radhi kushiriki endapo mgawanyo wa mapato ya mlangoni utabadilishwa na kuwa zaidi ya yale yanayopatikana kwenye mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Rage alisema kwamba klabu zimechoka kunyonywa na hivyo Simba itakuwa tayari kushiriki endapo klabu zitapata mgao wa zaidi ya asilimia 60 ya mapato ya mlangoni. "Ni lazima kwanza tukae na kukubaliana tunapata nini sisi klabu, wakati wa kuona klabu zinanyonywa umepita na sasa kila mkataba ambao TFF watakuwa wameingia wanatakiwa kutushirikisha vilabu ili tujue maslahi yetu," alisema Rage. Katibu Mkuu wa Yanga, Mwesigwa Selestine aliliambia gazeti hili jana kwamba klabu yake inaona ligi hiyo imeingiliana na programu zao za maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu hivyo maamuzi ya kushiriki au kutoshiriki yatajulikana baada ya kufanyika kwa kikao cha pamoja na benchi la ufundi la timu hiyo. Mwesigwa alisema kwamba mara baada ya kocha mpya, Tom Saintfiet kutua, alipewa ratiba ya michuano iliyopo na hivyo kocha huyo aliandaa programu yake ambayo itaanza kutekelezwa hivi karibuni baada ya mapumziko ya wachezaji kumalizika. "Uwezekano wa timu yetu kushiriki ni mdogo, haikuwa kwenye programu na hivyo inabidi uongozi na benchi la ufundi tujadiliane na kufanya maamuzi yatakayoisaidia timu," alisema katibu huyo. Shirikisho la Soka Nchini (TFF) lilitangaza kusaini mkataba wa miaka mitatu na benki ABC ambayo itadhamini ligi hiyo mpya yenye lengo la kuziandaa klabu kwa ajili ya msimu mpya wa ligi. CHANZO:NIPASHE

Azam yakana kuchunguza kipigo cha Yanga

WAKATI taarifa zilizagaa jana kwamba Azam imewasimamisha wachezaji wake wawili Mrisho Ngassa na Salum Aboubakar 'Sure Boy' kwa tuhuma za kucheza chini ya kiwango dhidi ya Yanga katika fainali ya Kombe la Kagame waliyolala 2-0 Jumamosi na kwamba nyota wengine watatu Aggrey Morris, Said Morad na kipa Deogratius Munishi 'Dida' wanachunguzwa, uongozi wa klabu hiyo ya Chamazi umesema walifungwa kihalali na hakuna mchezaji wa wanayemtuhumu kwa chochote. Afisa Habari wa Azam FC, Jaffer Idd alisema Yanga walitumia makosa machache yaliyofanywa na mabeki wa Azam na kupachika mabao yaliyowapa ushindi wana Jangwani hao. "Timu yetu ilicheza vizuri kwenye mechi ya fainali lakini Yanga ilituzidi ujanja na kutumia vizuri nafasi chache walizopata," alisema Jaffer. Alisema hawawezi kumlaumu mchezaji yeyote kwa kipigo hicho kwa sababu wachezaji walioifikisha fainali timu hiyo ndio waliocheza mechi hiyo ya fainali na akawasifu wachezaji wa timu hiyo kwa ushujaa wa kuifikisha Azam fainali licha ya kwamba ilikuwa ikishiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza. Jaffer alisema uongozi wa Azam umeridhika na matokeo hayo na kwamba sasa wanaelekeza nguvu zao katika maandalizi ya Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Afrika. Akizungumza na gazeti hili jana, Ngassa alisema kuwa timu yake juzi haikuwa na bahati ya kutwaa ubingwa huo lakini wanamshukuru Mungu kwa kufika fainali. Ngassa alisema kwa dakika chache alizopewa kucheza, zikiwemo za mechi ya fainali alijituma na kuisaidia timu yake. "Sidhani kama kuna aliyecheza chini ya kiwango, tumejituma na tumefika mbali licha ya kutochukua ubingwa," alisema Ngassa na kuongeza kwamba hajasimamishwa na uongozi wa timu yake kama ambavyo ilikuwa inazungumzwa jana. Ilidaiwa pia kwamba uongozi wa Azam haukufurahishwa na kitendo cha Ngassa kwenda upande wa mashabiki wa Yanga na kushangilia baada ya kufunga goli kwenye mechi ya nusu fainali ya Kombe la Kagame dhidi ya Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Wachezaji wa Azam wamepewa mapumziko ya siku mbili ambapo kesho wataanza mazoezi ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Kidunda adundwa Olimpiki

BONDIA pekee wa Tanzania katika mashindano ya Olimpiki, Seleman Kidunda jana alipigwa kwa pointi 20-7 na bondia Vasilli Beraus toka Jamhuri ya Moldova.

Batungi: Mkali wa Kikapu achekeleaye ajira jeshini

LICHA ya mchezo wa kikapu kumpatia rafiki wengi na kufahamika ndani na nje ya nchi, nyota wa klabu ya ABC, Gilbert Batungi 'B10' amesema kitu kikubwa anachojivunia kupitia mchezo huo ni elimu na ajira aliyopata jeshini. Batungi, aliyeingia kwenye kikapu kwa ushawishi wa kaka yake aitwaye Jerome, alisema ajira hiyo aliipata mwaka 2006 kutokana na umahiri wake dimbani. Alisema anaifurahia ajira hiyo kwa vile hakuwahi kuiota kuja kuipata maishani mwake. Batungi, anayemudu nafasi ya kati, alisema pia kikapu kilimwezesha kupata nafasi ya kusoma Shule ya Sekondari Jitegemee baada ya kung'ara katika UMISSETA mwaka 2000 iliyofanyikwa jijini Mwanza. Alisema wakati akishiriki michuano hiyo alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Binza, kwa jinsi alivyong'ara aliuvutia uongozi wa Jitegemee iliyomchukua akiwa kidato cha pili na kusoma hadi alipohitimu kidato cha nne. Alisema kutua kwake Jitegemee kulimwezesha kuonwa na kuitwa timu ya mkoa wa Dar tangu mwaka 2001 na ile ya taifa 2005 na kuzichezea mpaka sasa bila kutarajia. Juu ya pambano gumu alilowahi kukutana nalo, Batungi apendae kula ugali kwa dagaa na mboga za majani na kunywa juisi ya embe, alitaja mchezo wa mwaka 2005 kati ya Tanzania na Kenya wa kuwania ubingwa wa Afrika Mashariki. "Naikumbuka mechi hii kwa vile ilikuwa mara yangu ya kwanza kuichezea timu ya taifa, pia licha ya ugumu wake niliisaidia Tanzania kuilaza Kenya kwa mara ya kwanza." Alisema mchezo huo uliochezwa Nairobi na kuisha kwa Tanzania kuiduwaza Kenya kwa vikapu 61-60. "Hakika mafanikio niliyopata katika mechi hiyo hasa kuaminiwa na makocha na kutiwa moyo na wachezaji wenzangu, ni jambo linalonifanya nisiisahau," alisema. Batungi, aliyekuwa mmoja wa wawaniaji wa Tuzo za TASWA za 2012 kama Mchezaji Bora wa Kikapu kwa mara ya pili mfululizo, alisema safari yake ya michezo kwa kiasi kikubwa imechangiwa na makundi matatu ya watu asiowasahau milele. Alitaja kundi la kwanza ni wazazi wake waliomuunga mkono kwa kumtia moyo tangu utotoni, pili makocha wote waliomfundisha katika timu tofauti, na wachezaji wenzake waliomtia nguvu kwa kukitambua kipaji chake katika mchezo huo. "Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sintowashukuru watu hawa kwa hapa nilipofika," alisema. Batungi, aliyetwaa ubingwa wa Majiji akiwa na timu ya mkoa wa Dar 'The Dream Team', ubingwa wa Taifa wa Kikapu (NBL) na ule wa Muungano akiwa na klabu ABC ni mnazi mkubwa wa soka mchezo alioupenda kabla ya kaka yake kumbadilisha. Ni shabiki mkubwa wa klabu za Chelsea na Simba akivutiwa na kiungo Mwinyi Kazimoto na Didier Drogba. B10 Mkali huyo alitoboa siri ya jina lake la utani la 'B10', akisema ni kifupi cha ubini wake na jezi namba 10 anayopenda kuivaa tangu alipoibukia katika kikapu mwaka 1998. "Naipenda mno jezi namba 10, nimekuwa nikiivaa tangu naanza kucheza kikapu na ndio maana wengi huniita B10, ikimaanisha Batungi Namba 10," alisema Batungi, anayechizishwa na rangi nyekundu na nyeupe akimzimia nyota wa kikapu nchini Abdallah Ramadhani 'Dullah', alisema ndoto zake ni kuiona Tanzania ikitamba kimataifa na kuwasaidia vijana chipukizi kuja kuvaa 'viatu' vyao mara wakistaafu. Nyota huyo anayependa kucheza Pooltable, alisema mchezo wa kikapu umedidimia kwa kukosekana viongozi makini na wenye uchungu na mchezo huo. Alisema wengi wa viongozi wa sasa ni wababaishaji wanaojali masilahi yao na ndio waliochangia hata wadhamini kuukimbia mchezo huo na kutoa rai kwa wadau wenzake kubadilika kwa kuwachagua watu makini. "Tusipozinduka na kuchagua watu wenye mapenzi na uchungu na kikapu, tutarajie mchezo huo kudidimia zaidi," alisema. Alidai kama angekutana na Rais au Waziri wa Michezo, angeomba serikali isaidie michezo yote badala ya kuangalia soka tu, pia angeiomba ishinikize makampuni kuwekeza kwenye michezo kwa kusaidia udhamini. "Pia ningeiomba serikali iwekeze nguvu katika michezo ya vijana ili kusaidia taifa kuwa na nyota wa baadae kwa michezo yote ili itambe kimataifa," alisema. Batungi, ambaye hajaoa ila ana mtoto mmoja, alisema hakuna ujinga anaoujutia kama tabia aliyokuwa nayo enzi akiibuka katika kikapu ya kutega mazoezi magumu kwa kusingizia ugonjwa alipokuwa akisoma Jitegemee. Alisema kitu kinachomhuzunisha ni kifo cha nyota wa Netiboli, Grace Daudi 'Sister' na kudai kitu kimngine anachokifanya nje ya ajira yake jeshini ni biashara ya kuuza nguo. ALIPOTOKA Gilbert Paul Batungi, alizaliwa Januari 5, 1983 mkoani Shinyanga akiwa wa sita kati ya watoto saba wa familia yao. Alisoma Shule ya Msingi Binza ya Maswa-Shinyanga na kuendelea na masomo ya Serkondari Shule ya Binza na baadae Jitegemee. Kimichezo alianza kucheza soka na kutamba katika timu ya shule kabla ya kaka yake kumshawishi kucheza kikapu ambapo aliianza kuucheza rasmi mwaka 1998 katika klabu ya Black Wizard ya Shinyanga. Baada ya kung'ara katika UMISSETA mwaka 2000 iliyofanyika Mwanza na kuonwa na Jitegemee alihamia jijini Dar na kupata fursa ya kuzichezea timu za Mgulani JKT, Chang'ombe Boys na Vijana. Mwaka 2004 akiwa ameshamaliza masomo yake ya Sekondari, aliitwa JKT Mgulani kama mchezaji wa kiraia na miaka miwili baadae akapata fursa ya kuwa miongoni mwa walioajiriwa jeshini na kuhamia timu ya ABC anayoichezea mpaka sasa. Batungi, anayetamani kuwa na watoto wawili pale atakapooa, aliwakumbusha wachezaji wenzake kujibidiisha kufanya mazoezi na kuwa makini na ugonjwa wa Ukimwi aliodaai unapoteza nguvu kazi kubwa ya taaifa. Alisema rai hiyo ya kujikinga Ukimwi sio kwa wachezaji tu bali jamii kwa ujumla kwa kuitaka kuepuka ngono zembe, wawe waaminifu na kutumia kinga, huku akisisitiza kinga sahihi ni kufanya ibada na kufanya mazoezi ili kupunguza mihemko. Aliwasihi wachezaji wenzake kujituma uwanjani na kuwa na nidhamu ili kusaidia kushawishi wadhamini kuwasaidia.
Mwisho

Ubalozi wa UAE kutumia zaidi ya Dola 1200,000 kufuturisha mikoa saba nchini

UBALOZI wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE) nchini, kupitia taasisi za Sheikh Khalifa bin Zayed Al Hahyan, Sharjah Charity Internation na Red Cresent, unatarajia kutumia zaidi ya dola 120,000 za Marekani, kuifadhili mikoa saba nchini kwa ajili ya futari na Zakatul Fitr kipindi chote cha mfungo wa mwezi wa Ramadhani. Akizungumza kwa niaba ya Balozi wa UAE nchini Tanzania, Mallalla Mubarak Al Ameir na msaidizi wake, Mohammed Obaid Salem AlZaabi, baada ya kugawa futari katika msikiti wa Al Makbool, Msasani Dar es Salaam juzi, Mhasibu wa ubalozi huo, Abdallah Ahmedina, alisema baadhi ya msikiti ya mikoa hiyo ndiyo itakayonufaika. Ahmedina, aliitaja mikoa ambayo waumini wake tangu kuanza kwa mfungo wa mwezi wa ramadhani wamekuwa wakifuturishwa na watakuja kupewa Zaka kwa ajili ya Eid El Fitri ni Dar es Salaam, Iringa, Kilimanjaro, Arusha, Pwani, Dodoma na Morogoro. Mhasibu huyo alichangua kuwa kiasi cha dola 80,000 zinatoka asasi ya Khalifa, dola 36,000 kutoka Red Cresent na dola 6,000 zinatoka Sharjah na kusema utaratibu huo wa kusaidia waumini wa misikiti ya mikoa hiyo umeanza tangu ubalozi wao uwe nchini na utaendelea kwa lengo la kuwasaidia waumini kutekeleza ibada yao ya funga bila ya hofu ya kukosa futari au kuisherehea Eid. Alifafanua, kati ya fedha hizo zilizotolewa na asasi hizo tatu zinatumika kwa futari na zilizosalia ni kwa ajili ya kugawa Zakatul fitr ambayo huwalenga waumini wajane, yatima, walemavu, maskini na fukara ili kuisherekea sikukuu kwa furaha na amani. "Miaka yote huwa tunatoa futari na kugawa zakatufitr, mwaka huu tutatumia kama dola 122,000 za Marekani zinazotolewa na asasi zilizopo chini ya ubalozi wetu za Sheikh Khalifa, Red Cresent na Sharjah Charity," alisema. Akitoa shukrani kwa niaba ya waumini wake, Imamu wa msikiti wa Al Makbool, Sheikh Mussa Abdallah, aliushukuru ubalozi huo kwa kile walichosema umewasaidia kutimiza moja ya nguzo za dini yao. "Waumini wengine hawana uwezo wa kupata futari kama hii, tunashukuru ubalozi na asasi zote zilizochangia msaada huu na Inshallah, Mwenyenzi Mungu awazidishie," alisema Imamu Abdallah. Alisema baadhi ya watu waliokuwa hawafungi kwa kutokuwa na hakika ya kupata futari kwa sasa hawana sababu tena kwa vile wamepata uhakika wa kupitia ufadhili huo wa ubalozi wa UAE.

Sunday, July 29, 2012

Mapembe: Fundi 'mvunja mbavu' aliyejitosa kwenye muziki

TANGU utotoni, aliwavutia watoto na wanafunzi wenzake kwa kipaji cha kuchekesha, ila hakujitambua au kuota kama kipaji hicho kingemtoa kimaisha. Ndio maana mara alipohitimu darasa la saba katika Shule ya Kiwalala, Lindi alijitosa kwenye ufundi uashi na baada umakenika katika miji tofauti. Hata hivyo alivyotua Dar na kufanya kazi ya udereva wa daladala ndipo alipobaini alikuwa amechelewa mno, baada ya msanii Khalfan Ahmed 'Kelvin' kukitambua kipaji chake na kumshawishi kuingia kwenye sanaa. Wengi wanamfahamu kama 'Mapembe' ila majina yake kamili ni Ismail Makomba mmoja wa wachekeshaji mahiri nchini. Mapembe alisema wazo la Kelvin alilipuuza kwa kudhani angepoteza muda bure, lakini alipong'ang'aniwa aliamua kujiunga na kundi la msanii huyo la Simple Production na kuanza kuonyesha makeke. Mkali huyo aliyevutiwa kisanii na Abdallah Mkumbira 'Muhogo Mchungu' alicheza kazi yake ya kwanza mwaka 2003 iitwayo 'Sheria' kisha kufuatiwa na 'Lugha Gongana', 'Talaka ya Mdundiko', 'Msela Nondo' na 'Ngoma Droo' na nyingine. Alijitoa kwa ruksa Simple Production na kuanzisha kampuni binafsi ya Karena Production iliyozalisha filamu tano za Trafiki, Mdimu, Mbagala, Kiduku, Mpambano na sasa akijiandaa kuingiza sokoni 'Posa' akiwa pia ni muajiriwa wa kampuni ya Al Riyamy. Mapembe ambaye pia ni mwanaharakati anajishughulisha pia na muziki akiwa ameshatoa nyimbo kadhaa na kwa sasa yupo studio kukamilisha kibao kiitwacho 'Gesi ya Kusini'. Nyimbo zake nyingine zinazotamba hewani kwa sasa zikiwa katika miondoko ya Zouk ni Mwalimu, Nandenga, Usalama wa Raia, Muungano na Ubaya wa Mafisadi. Mapembe anayemshukuru Kelvin na kampuni ya Al Riyamy kumfikisha alipo, anajipanga kurudi 'darasani' Chuo cha Taifa cha Sanaa Bagamoyo ,TaSUBA, ili kuongeza maarifa. Mume huyo wa mtu na baba wa mtoto mmoja aitwae Makomba, alisema sanaa Bongo imepiga hatua kubwa, isipokuwa tatizo la wizi unaofanywa na watu wachache. Aliiomba serikali iwasaidie wasanii kunufaika na kazi zao kwa kuweka sheria kali za kuthibiti maharamia hao, huku akiwataka wasanii wenzake kupendana na kushirikiana. Pia aliwakumbusha wasanii wenzake wasijikite kutoa kazi zao katika nyanja za mapenzi na kusahau mambo mengine ikiwemo masuala ya kisiasa na kijamii, kama anavyofanya yeye kupitia muziki aliojitosa hivi karibuni. Mapembe alizaliwa Januari, 1972 Kiwalala, Lindi akiwa ni mtoto wa pili kati ya watatu wa familia yao, alisoma Shule ya Msingi Kiwalala kabla ya kujishughulisha na kazi za ufundi uashi, magari na udereva na baadae kuingiza kwenye uigizaji.

Mobby Mpambala: Asiyeamini kama filamu zimempa nyumba, gari na kampuni

ALIPOSHAWISHIWA na nyota wa filamu nchini, Single Mtambalike 'Rich', aingie katika fani ya uigizaji, Mobby Mpambala, hakutilia maanani wazo hilo kutokana na imani aliyokuwa nayo juu ya sanaa ya Tanzania kwamba hailipi. Hata hivyo baada ya ushawishi wa muda mrefu na kuamua kujitosa rasmi mwaka 2000, msanii huyo amejikuta 'akiisujudia' fani hiyo kwa jinsi ilivyomwezesha kiuchumi na kimaisha tofauti na alivyofikiria mwanzoni. Mkali huyo wa filamu za mapigano na zile za kutisha, alisema kipindi kifupi cha kuweko kwake kwenye sanaa hiyo imemwezesha kujenga nyumba katika kiwanja alichokuwa nacho eneo la Gongolamboto, kununua gari na kumudu kuanzisha kampuni binafsi ya kuzalisha filamu ya 'Wizaga Entertainment'. Pia, msanii huyo anamiliki kundi la sanaa la Mtazamo Family linalojihusisha na sanaa za ngoma, maigizo na sarakasi huku akiendesha kiwanda kidogo cha kutengeneza masofa na samani nyingine za majumbani eneo la Amana-Ilala. "Sio siri kabla ya kuingia kwenye sanaa niliidharau fani hii kutokana na hali ya mambo ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo wasanii hawakuwa na chochote cha kujivunia, lakini leo nakiri sanaa Bongo inalipa kutokana na mafanikio makubwa niliyoyapata katika kipindi kifupi," alisema. Mpambala alisema alikutana na Rich mwaka 1996 na kumtaka ajiunge kwenye sanaa baada ya kugundua kipaji chake na umahiri wake wa michezo ya Kungfu na utunisha misuli, ila alimpuuza kwa vile aliringia ujuzi wake wa ufundi seremala. Alisema hata hivyo shinikizo la Rich pamoja na ndugu na jamaa zake waliotambua kipaji alichonacho, ndipo mwaka 2000 alipojitosa kwa kushiriki filamu ya 'Kidole Tumbo' iliyozuiwa na serikali kutoka. Mpambala alisema Rich 'alimbeba' kwa kumshirikisha katika kazi zake kadhaa kama 'Swahiba', iliyomtambulisha kwa mara ya kwanza yeye na Rose Ndauka, 'Mahabuba' na 'Heshima ya Penzi'. Alisema kazi hizo zilimfungulia neema kwa kushirikishwa kazi nyingine kadhaa zinazofikia 30 kwa sasa, akizitaja baadhi kuwa ni; 'Kamanda', 'Jozani', 'Signature', 'Secretary', '007', 'Time to Fight, 'Zuadiswa', 'Before Death', 'Hii ni Tatu', 'Criminal', 'Jamal' na 'The Chase' aliyoitaja kama filamu bomba kwake. AMRI PURI Mpambala, alisema licha ya kwamba hakuwahi kuota kuwa msanii, lakini alimzimia mno nyota wa zamani wa filamu za Kihindi, Amri Puri 'Mzee Ashanti', ambaye kwa sasa ni marehemu. Alisema alivutiwa na Amri Puri, kwa aina yake ya uigizaji kama mbabe na jitu katili, kitu alichodai amekuwa akimuiga katika baadhi ya picha alizocheza kama njia ya kumuenzi mkali huyo wa Bollywood. Mpambala anayezishabikia Simba na Manchester United, akipenda kula ugali kwa dagaa na kunywa soda ya Pepsi, alisema hakuna kitu cha furaha kwake kama siku alipomuoa mkewe wa kwanza aitwae, Jasmine mwaka 2004 na ndoa nyake ya pili dhidi ya Zola mwaka 2011. "Kwa kweli siku nilipofunga ndoa na wake zangu hawa ndio tukio la furaha kwangu, na ninahuzunishwa na kifo cha baba yangu mlezi, Abdul Ally Kibena aliyefariki mwaka 1999," alisema. Mpambala, anayechizishwa na rangi ya bluu, alisema kingine kinachompa furaha ni kufanikiwa kufyatua kazi zake binafsi tano za filamu kupitia kampuni yake ya Wizaga. Alizitaja kazi hizo kuwa ni 'I Wonder', My Brother', 'Criminal' aliyoshirikiana na 'Carlos', 'Fuvu' na 'Anti Virus' anazotarajia kuziingiza sokoni hivi karibuni. SKENDO Mpambala anayemzimia 'swahiba' wake Haji Adam 'Baba Haji', alisema kati ya vitu vinavyomkera ni tabia ya baadhi ya wasanii chipukizi kupenda kujihusisha na skendo kwa nia ya kutafuta umaarufu. Alisema vitendo vinavyofanywa na wasanii hao wasiojitambua vinaidhalilisha fani yao pamoja na kuzichafua familia za wasanii hao, licha ya wenyewe kuonekana kutojali. Mkali huyo mwenye watoto sita, alisema ifike wakati wasanii watambue umaarufu hupatikana kupitia umahiri wa kazi zao na sio kujidhalilisha ovyo magazetini. Mpambala anayependa kutumia muda wake wa ziada kufanya mazoezi na kuendesha kazi za useremala katika kiwanda chake na kundi lake la sanaa lililotoa ajira kwa vijana 30, alisema kama angekutana na Rais au Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, angeomba sanaa isaidiwe. "Ningewaomba wasaidie iundwe kwa sheria kali ya kuthibiti wizi wa kazi za wasanii sambamba na kuwepo kwa mipango mizuri ya kutambuliwa kwetu kama ilivyo kwa watu wa kada nyingine wanaothaminiwa na kuenziwa nchini." ALIPOTOKA Mobbi Nassor Saleh Mpambala 'Mobby Mpambala', alizaliwa Novemba 28, 1965 katika wilaya ya Igunga,Tabora akiwa mtoto wa tatu kati ya nane wa familia yao. Alisoma elimu yake ya Msingi katika Shule ya Makurumla, jijini Dar kabla ya kurejea Tabora kumfuata mama yake aliyekuwa ametangana na baba yake na kujishughulisha na biashara ndogo ndogo huku akijiendeleza kwenye michezo ya sarakasi na kungfu aliyoicheza tangu utotoni. Mpambala anayewashukuru wazazi wake, Rich na mkewe wa kwanza Jasmine kwa namna walivyomsaidia kufika mahali alipo, amejaliwa kuwa na watoto sita watatu akiwapata katika ndoa yake ya kwanza nao ni Edo, 27, Mariam22 na Saleh,20. Watoto wake wengine ni Goodluck, 18, anayesoma Sekondari jijini Arusha, Zuwena, 13 aliyepo darasa la sita katika Shule ya Msingi Mapinduzi-Kigogo jijini Dar na Munira, 5 anayesoma chekechea.

TPBO yasitisha mapambano kisa....!

ORGANAIZESHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), imesitisha kwa muda mapambano yao yote ya ngumi ili kupisha mfungo wa Mwezi wa Ramadhani. Rais wa TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh' alisema wamechukua uamuzi huo ili kuwapa nafasi mabondia na mashabiki wa ngumi kujikita kwenye ibada hiyo ya funga ambayo ni moja ya nguzo tano na muhimu kwa maisha ya waumini wa dini ya Kiislam. Ustaadh, alisema kusitishwa kwa michezo hiyo haina maana kwamba TPBO haifanyi kazi, kisha akafafanua kuwa ofisi zao zinaendelea kufanya kazi kama kawaida isipokuwa haitaruhusu pambano lolote katika kipindi hiki cha mfungo. "TPBO, tumesimamisha mapambano yote ya ngumi ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuungana na waislam katika utekelezaji wa ibada yao ya funga, ingawa ofisi zetu zilizopo Temeke Mwembeyanga zinaendelea kufanya kazi ikiratibu mapambano yatakayofanyika baada ya mfungo huo," alisema Ustaadh Yasin. Aidha, alisema TPBO inawatakia mfungo mwema mabondia na wadau wa ngumi wenye imani na dini ya Kiislam ili waweze kufunga na kumaliza bila matatizo. Mwisho

YANGA KAMA KAWA KAMA DAWA YABEBA TENA KOMBE LA KAGAME

KLABU ya soka ya Yanga jana ilitwaa kwa staili ya aina yake ubingwa wake wa pili mfululizo na wa tano jumla wa Kombe la Kagame, la klabu bingwa ya soka ya Afrika Mashariki na Kati, kwa kuifunga Azam mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa. Ushindi huo si tu uliiwezesha kwa namna nyingi kulipa kisasi cha kudhalilishwa kwa mabao 3-1 na Azam kulikoandamana na kupigana uwanjani na kufungiwa wachezaji wake katika mchezo wa ligi kuu ya Bara Mei, bali pia ulikuwa wa kikatili. Bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Hamisi Kiiza katika dakika ya 44 likiwa la tano kwa mchezaji huyo katika michuano ya mwaka huu, baada ya kunasa pasi ya nyuma ya beki wa pembeni wa Azam Ibrahim Shikanda. Lakini goli ambalo lilinogesha ushindi huo, na ambalo litakuwa liliikata maini vibaya Azam ni la mshambuliaji mpya hatari Said Bahanuzi la dakika ya mwisho ya majeruhi. Zikiwa zimeongezwa dakika tatu za majeruhi, mpira mrefu uliopigwa toka nyuma na beki Kelvin Yondani katika dakika ya 93 ulimkuta Bahanuzi akikabiliana na Said Morad. Akitumia ubavu aliojaaliwa na Mola, pande la mtu Bahanuzi alimzungusha Morad kabla ya kumtoka na kuachia shuti kali lililotinga kwenye nyavu za juu za goli na kumfanya mfungaji-mwenza aliyeongoza kwenye Kombe la Kagame kwa pamoja na Kiiza. Tedy Etekiama wa Vita ya JK Kongo pia alifunga mabao sita lakini CECAFA, shirikisho la soka la ukanda huo, liliwatunuku wauaji hao wa Yanga kutokana na kuipa timu yao ubingwa. Tofauti na mechi zilizotangulia, Azam ambayo ilifika fainali ya Kombe la Kagame kwa mara ya kwanza ikishiriki mara ya kwanza jana ilijenga mashambulizi yake taratibu kutokana na mpira wake wa pasi fupi fupi za kasi kuikauka. Kocha wa Yanga Tom Sentfiet aliwashukuru wachezaji wake kwa kumudu kucheza kwa "mbinu tulizopanga" na kwamba kufungwa kwao katika mechi ya kwanza kuliisadia kurekebisha makosa yaliyoipa ushindi wa mechi zote tano zilizofuata. Yanga ilikuwa pia bingwa wa Kombe la Kagame katika miaka ya 1975, 1993 na 1999 na mbali na kukata tiketi ya michuano hiyo tena mwakani imebakiza kikombe kimoja kufikia rekodi ya Simba ambayo ndiye bingwa pekee mara sita. Pia iwapo kama mwakani itafanikiwa kutetea taji hilo itakuwa timu ya pili baada ya AFC Leopard ya Kenya iliyowahi kufanya hivyo mfululizo wakati ikitamba katika soka la Afrika.
Katika vurugu za ushindi wa Azam Mei, wachezaji sita wa Yanga walitozwa faini zinazofikia jumla ya sh. milioni nane ambazo sasa zinaweza kulipwa kutoka katika zawadi ya sh. milioni 45 ya bingwa wa Kombe la Kagame. Azam inapata sh. milioni 30 wakati Vita imezawadiwa sh. milioni 15 kwa kushika nafasi ya tatu baada ya kuifunga APR ya Rwanda 2-0 mapema jana. Timu zilikuwa: YANGA: 'Barthez', Oscar Joshua, Stephano Mwasika, 'Cannavaro', Kelvin Yondani, Haruna Niyonzima, 'Chuji', Rashid Gumbo (Juma Seif dk.74), Hamisi Kiiza, Said Bahanuzi', David Luhende. AZAM: 'Dida', Ibrahim Shikanda (Samir Haji dk.68), Erasto Nyoni, Said Morad, Aggrey Moris, Jabir Aziz, Kipre Tchetche (Mrisho Ngasa dk.68), Salum Abubakar, John Bocco, Ibrahim Mwaipopo, 'Redondo'.

UBALOZI WA UAE WAFUTURISHA WAUMINI DAR

UBALOZI wa Nchi ya Falme za Kiarabu, UAE nchini kupitia taasisi ya kutoa huduma za kijamii ya Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan, umeamua kuwafuturisha waumini wa dini ya kiislam wa Msikiti wa Al Rahman wa Dar es Salaam kwa mwezi mzima wa mfungo wa Ramadhani. Msaada huo wa futari ulianza kutolewa tangu kuanza kwa mfungo wa mwezi huo siku 10 zilizopita na juzi MICHARAZO lilishuhudia ugawaji wake kwa waumini hao ambao imewafanya wapate fursa ya kuwa na uhakika wa kula baada ya funga zao. Imamu wa Msikiti huo wa Al Rahman uliopo eneo la Kinondoni, Sheikh Abdullah Salim Bahssany, akiwahutubia waumini wake wakati wakigawiwa futari hiyo, alisema huo ni msaada toka ubalozi wa UAE na utakuwa ukitolewa hapo kila siku hadi mwezi mtukufu wa Ramadhani utakapomalizika mwishoni mwa mwezi ujao. Imamu huyo aliwaambia waumini hao kuwa wale waliokuwa na shaka na kupata futari katika funga zao, waondoe hofu kwani sasa watakuwa wakipata chakula hicho, huku akiushukuru ubalozi huo kwa ukarimu iliyouonyesha kwa waumini hao. "Jamani futari mnayokula leo imetolewa na ubalozi wa nchi za Falme za Kiarabu na msaada huu utakuwa ukitolewa kwa mwezi mzima katika mfungo huu wa Ramadhani hivyo msiwe na hofu katika funga zenu,"alisema Sheikh Bahssany. Nao baadhi ya waumini waliofuturishwa msikiti hapo waliushukuru ubalozi huo na kuomba watu wengine wenye uwezo kuiga mfano huo wakidai mwezi huu ndio wa waumini wa kweli kuonyesha upendo, ukarimu na kuhurumiana katika kutekeleza nguzo ya nne kati ya tano za Imani za Kiislam. "Wengine wetu tunafunga lakini hatuna hakika ya kupata futari, lakini kwa hili linalofanywa na ubalozi huu ambao hata mwaka jana walitusaidia tunashukuru na kuomba wengine wawe wanatukumbuka wanyonge kama sisi," alisema muumini mmoja aliyekataa kutajwa jina lake gazetini. Mwisho

Monday, July 2, 2012

Yanga yakubali kwenda Zenji kushiriki Kombe la Urafiki

HATIMAYE timu ya soka ya Yanga imeamua kubadili msimamo wake wa kushiriki michuano ya Urafiki kwa kukubali kwenda visiwani Zanzibar kushiriki, ambapo inatarajiwa kuondoka leo sambamba na watani zao Simba. Awali uongozi wa Yanga 'ulichomoa' kushiriki michuano hiyo, lakini baada ya 'vikao' na waandaji wake, uongozi huo umelegea na kukubali kwenda kushiriki. Katibu Mkuu wa Yanga, Celestine Mwesigwa, alisema wamekubali baada ya kuridhiana na waandaaji na pia kwa vile michuano hiyo ina lengo la kudumisha urafiki baina ya timu za Tanzania Bara na Visiwani, hawakuona sababu ya kuigomea. "Tunaenda kushiriki, tutaondoka kesho asubuhi kuwahi michuano hiyo na tunaamini tutafanya vema na tutaaitumia kwa ajili ya fainali za Kombe la Kagame," alisema Mwesigwa. Mwesigwa alisema Yanga itaenda Zanzibar ikiwa na kikosi chake kamili ambacho Jumamosi iliitoa nishai Mabingwa wa Uganda, Express kwa kuilaza mabao 2-1 kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa jijini Dar. Yanga ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo ya Kagame na itafungua dimba Julai 14 kwa kuumana na Atletico ya Burundi. Timu nyingine za Tanzania Bara zitakazoshiriki michuano hiyo ya Urafiki ni Simba ambao jioni ya leo inatarajiwa kushuka dimba la Amaan kuumana na Mafunzo.

Hispania wabeba tena ubingwa wa Ulaya

WAFALME wa soka wa Dunia, Hispania usiku wa kuamkia leo iliweka rekodi ya aina yake kwa kutwaa ubingwa wa Ulaya kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuisambaratisha Italia kwa mabao 4-0. Ushindi katika mechi hiyo ya kusisimua iliyokuwa ya kushambuliana mwanzo mwisho , imeifanya mabingwa hao wapya wa Ulaya kuwa timu ya kwanza katika historia kutwaa mataji mawili mfululizo, huku ikiwa pia na taji la Dunia iliyotwaa katika fainali za mwaka 2010 zilizochezwa barani Afrika. Hispania imefuata nyayo za Argentina iliyowahi kutwaa mataji matatu mfululizo kwa kutwaa ubingwa wa Copa Amerika wakati michuano hiyo ikichezwa kila mwaka kati ya a 1945 hadi 1947. Ikiwa na kiu ya kutaka kudhihirisha kuwa wao ni wababe wa kweli wa soka duniani kwa sasa, Hispania iliucheza mchezo huo kwa kushambulia mwanzo mwisho na kujiandikia bao la kwanza katika dakika ya 14 kupitia kwa David Silva aliyefunga kwa kichwa. Bao la pili la wakali hao wanaonolewa na Vicente del Bosque liliingizwa kimiani na dakika nne kabla ya mapumziko kupitia beki wa kushoto Jordi Alba baada ya kuwatambuka walinzi wa Italia na kumtungua kipa Gianluigi Buffon. Italia iliyokuwa ikijaribu kurejea tukio lililowashtua mashabiki wengi wa soka kwa kuikwamisha Ujerumani katika mechi ya nusu fainali, kwa kuilaza mabao 2-1 ilishindwa katika kufurukuta Kwa Hispania hasa baada ya kuumia kwa Thiago Motta wakati wakiwa wameshamaliza orodha ya wachezaji wa akiba na kucheza pungufu dimbani. Wengi wakiamini huenda mechi ingeisha kwa idadi ya mabao 2-0, Fernando Torres 'El Nino' alikuwa mchezaji wa kwanza kufunga goli katika mechi mbili za fainali za Euro wakati alipopachika bao la tatu dakika ya 84. Torres, pia alifunga goli la ushindi katika fainali mwaka 2008 wakati walipotwaa ubingwa. Dakika mbili kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kiungo matata wa Chelsea, Juan Mata aliifungia Hispania bao la nne lililoikatisha tamaa kabisa Italia ambao walitawala mchezo huo dakika za mwanzoni kabla ya kupoteana na kukimbizwa.

Sunday, July 1, 2012

Azam Marine yaleta meli ya kisasa, abiria kusafiri na magari yao

Kampuni za meli za Azam Marine, imeamua kufanya kweli ambapo hivi karibuni inatarajia kuzindua meli kubwa ya kisasa ambayo itawawezesha abiria wake kwenda na magari yao visiwani Zanzibar. Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Hussein Mohammed Said, amesema Julai 15 mwaka huu meli hiyo yenye urefu wa mita 100 itazinduliwa. Mohamedi alisema shida ya usafiri itapungua kwa asilimia kubwa kutokana na meli hiyo kuwa na uwezo wa kubeba abiria 1500, Mizigo tani 500 na magari 200 ambapo abiria atakae jisikia kwenda na gari lake Zanzibar, Pemba au Dar es Salaam ataweza kufanya hivyo. Waziri Mwenye dhamana ya Mawasiliano na Miundombinu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hamadi Masoud, alithibitisha kwamba ana taaarifa za ujio wa meli hiyo ambayo alisema kwa kiasi kikubwa itakuwa ni ya kutoa huduma tu na siyakutengeneza faida. Meli hiyo inauwezo wa kwenda kasi ya notkomail 20.
MELI HIYO INAVYOONEKANA NDANI NA NJE

Lamata: Muongozaji anayeota kuwafunika 'madume' kimataifa

HUENDA akawa ndiye muongozaji pekee wa kike anayewapeleka puta waongozaji wengine wa kiume waliojaza nchini kwa namna anavyoifanya kazi yake kwa ufanisi wa hali ya juu. Wengi wanamfahamu kwa jina la 'Lamata', ingawa majina yake halisi ni Leah Richard Mwendamseke, mmoja wa waandishi wa miswada na waongozaji mahiri wa filamu nchini. Lamata, alisema aliipenda kazi hiyo tangu akiwa mtotoni na ndio maana alitumia muda mfupi kama muigizaji akiwa na kundi la Amka Sanaa lililorusha michezo yake katika kituo cha ITV kabla ya kugeukia uongozaji wa filamu. Mwanadada huyo alisema, mara alipoosha 'nyota' kwa kushiriki igizo la 'Ndoano' alijiunga na kampuni ya RJ chini ya Vincent Kigosi 'Ray' na Blandina Chagula 'Johari' kuandaa filamu huku akijifunza uongozaji kabla ya kuianza rasmi kazi hiyo mwaka 2010. Lamata, anayemiliki kampuni yake binafsi iitwayo 'Lamata Enterteinment, alisema kupenda kwake kuangalia filamu na kusoma vitabu vimechangia kuwa 'malkia' wa uandishi miswada na kuongoza filamu kazi aliyodai imemsaidia kwa mengi kimaisha. Alisema mbali na Ray, pia hawezi kuwasahau Salles Mapunda na Adam Kuambiana waliomnoa sambamba na kujifunza uongozaji wa filamu kupitia njia ya mtandao kiasi cha kuwa muongozaji pekee wa kike anayeifanya kazi hiyo kama ajira rasmi. Baadhi ya kazi alizoziandika na kuziongoza ni pamoja na Candy, All about Love, My Angel, Rude, My Princess, Tears Forever, Time After Time, Dunia Nyingine, Mke Mwema, Mr President, Chocolate, Life to Life, The Avenger, Family War na kazi zilizopo njiani kutoka za House Maid na Injinia. Lamata anayependa kula pilau na chips kwa kuku na kunywa vinywaji laini, alisema kati ya kazi zote alizoziandika na kuziongoza zilizo bomba kwake na kujivunia ni Candy na Rude. Mwanadada huyo anayechizishwa na nguo za rangi ya zambarau na pinki, alisema kabla ya kuingia kwenye filamu aliwazimia mno Desire Washington, Mel Gibson na James Canon, Juu ya filamu Bongo, Lamata ambaye hajaolewa wala kuwa na mtoto ingawa anatamani kuja kuzaa watoto watatu atakapoolewa, alisema imepiga hatua kubwa kulinganisha na miaka ya nyuma ila alisema wapo watu wachache wanaoikwamisha kuvuka mipaka ya kimataifa. Alisema ni watayarishaji wabishi wasiokubali kukosolewa na kugawa majukumu ya kazi kwa wengine na wasanii wasiotambua wapo katika fani hiyo kwa ajili ya kitu gani. Pia alisema wizi na uharamia uliokithiri katika fani hiyo na kukosekana kwa wasambazaji wengi wa kutosha ni tatizo ambalo aliiomba serikali kujaribu kuwasaidia ili wasanii wainuke kimaisha. Lamata mwenye ndoto za kuja kuwa muongozaji wa kimataifa na kujikita kwenye biashara, alimtaja msanii Jacklyne Wolper kama msanii anayemkubali na kumuona yupo makini katika fani hiyo nchini na anayefurahia kufanya nae kazi kama ilivyo kwa Jennifer Kyaka 'Odama'. Muongozaji huyo aliyewaasa wasanii na wadau wote wa filamu kupendana na kushikiana, alisema ukimuondoa Mungu na Yesu Kristo wengine anawashukuru kumfikisha alipo ni Ray, Wolper na Daniel Basila. Leah Richards Mwendamseke 'Lamata' alizaliwa miaka kadhaa iliyopita mjini Mbeya akiwa mtoto wa mwisho wa familia ya watoto sita na alisoma Shule za Msingi Ikuti na Karobe kabla ya kujiunga na Shule ya Sekondari za Arage Mbeya aliyosoma hadi kidato cha pili. Alimalizia masomo yake ya sekondari katika shule ya Wanging'ombe ya mjini Iringa na kisha kuendelea na masomo ya juu ya Sekondari Shule ya Perfect Vision kabla ya mwaka 2008 kujitosa kwenye sanaa akianzia kundi la Amka Sanaa lililotamba katika kituo cha ITV.

LEO NDIO LEO FAINALI ZA UERO 2012

MABINGWA watetezi wa Kombe la nchi za Ulaya, Hispania leo inatarajiwa kushuka dimbani kujaribu kuendeleza rekodi yake katika michuano ya kimataifa kwa kuvaana na Waitalia. Timu hizo mbili zilizofuzu fainali za mwaka huu za barani humo, zitaavanaa kila moja ikitaka kudhihirisha ubabe wake baada ya mechi yao ya awali ya makundi kuisha 1-1. Baina ya nchi hizo Hispania na Italia zimetoa mabingwa 25 wa Ulaya katika ngazi ya klabu lakini hii itakuwa mara ya kwanza kwa timu zao za taifa kukutana katika fainali ya kombe la Mataifa ya Ulaya. Ni wachache watahoji uhalali wa timu hizo kufika fainali. "Mshindi atakuwa bingwa anayestahili," alisema kiungo wa Hispania Cesc Fabregas. "Nadhani timu hizi mbili ndiyo zimekuwa na matokeo mazuri mfululizo katika michuano hii." Italia ni mabingwa mara nne wa Kombe la Dunia, mara ya mwisho 2006, wakati Hispania inajaribu kufanya kitu cha kipekee kwa kuwa timu ya kwanza kutwaa mfululizo vikombe vitatu vikubwa baada ya Euro 2008 na Kombe la Dunia miaka miwili iliyopita. Wakati mafanikio ya Vicente Del Bosque na Hispania yamejengwa katika safu imara ya ulinzi na kukaa muda mrefu na mpira, Italia imefika fainali kutokana na kufanya mashambulizi mfululizo yakiongozwa na mtukutu Mario Balotelli ambayo yaliiwezesha kuitoa Ujerumani katika nusufainali. Mfumo wa Hispania, wa pasi fupi-fupi 'Tiki Taka' umewapa mafanikio ya kujivunia - hakuna timu ya Ulaya tangu Ujerumani Magharibi mwanzoni mwa miaka ya 1970 imefanikiwa kucheza fainali tatu mfululizo za michuano mikubwa. Lakini 'enzi ya Hispania' kwa namna nyingi itaelezewa na jinsi itakavyokabiliana na timu iliyoshangaza kwa kucheza soka la kuvutia ya Italia leo. Kuweka historia ya kutwaa taji la tatu mfululizo, huku vigogo Ujerumani na Uholanzi vikiwa vilishafunga virago kwenye fainali hizi, kutaiweka Hispania kama moja ya timu kabambe zaidi zilizowahi kutokea. Lakini kipigo, mwishoni mwa fainali ambazo wameshindwa kuchengua mashabiki, kutaendelea kuitambulisha 'La Roja' kama moja ya timu za kawaida miongoni mwa vigogo vya soka. Hispania imefika hatua hiyo ya fainali kwa kuiondosha kwa mikwaju ya penati 4-2 wareno wakiongozwa na nahodha wao Cristiano Ronaldo, huku Waitalia maarufu kama 'Azzurri' waliwanyamazisha waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kuwa mabingwa wa mwaka huu, Ujerumani kwa mabao 2-1, magoli yaliyofungwa na 'mtukutu' Mario 'Super Mario' Balotelli ambaye ana asili ya Afrika hususani nchini Ghana.

Ratiba ya Kagame Cup 2012 hadharani

Release No. 102 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Juni 29, 2012 YANGA KUANZIA KWA ATLETICO KOMBE LA KAGAME Mabingwa watetezi wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) wataanza kutetea ubingwa wao Julai 14 mwaka huu dhidi ya Atletico ya Burundi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye ametangaza ratiba ya michuano hiyo leo (Juni 29 mwaka huu) katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Timu 11 zitashiriki katika michuano hiyo itakayoanza Julai 14 hadi 28 mwaka huu ambapo kwa siku zitachezwa mechi mbili (saa 8 mchana na saa 10 jioni) huku Tanzania Bara ikiwakilishwa na Yanga, Simba na Azam. Mechi ya kwanza siku ya ufunguzi (saa 8 mchana) itakuwa kati ya APR ya Rwanda na Wau Salaam ya Sudan Kusini. Kundi A lina timu za Simba, URA ya Uganda, Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na Ports ya Djibouti. Azam, Mafunzo ya Zanzibar na Tusker ya Kenya ziko kundi B. Yanga inaunda kundi C lenye timu za APR ya Rwanda, Wau Salaam ya Sudan Kusini na Atletico ya Burundi. Timu nane zitaingia robo fainali itakayochezwa Julai 23 na 24 mwaka huu. Kundi A na C kila moja litatoa timu tatu kwenda robo fainali wakati B litatoa timu mbili. El Merreikh ya Sudan, Red Sea ya Eritrea, Coffee ya Ethiopia na Elman ya Somalia hazitashiriki katika mashindano ya mwaka huu ambayo yanafanyika Tanzania Bara kwa mwaka wa tatu mfululizo kutokana na sababu mbalimbali. Coffee haitashiriki kwa vile ligi ya Ethiopia inaanza Julai 14 mwaka huu wakati El Merreikh wikiend ya Julai 13-15 mwaka huu itakuwa na mechi ya michuano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Bingwa wa michuano hiyo atapata dola 30,000, makamu bingwa dola 20,000 na mshindi wa tatu dola 10,000. Michuano hiyo itaoneshwa moja kwa moja (live) na Televisheni ya SuperSport. KAGAME CUP 2012 FIXTURE Sat. 14th July 1 APR vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa 2pm 2 YANGA vs ATLETICO Uwanja wa Taifa 4pm Sun. 15th July 3 AZAM vs MAFUNZO Chamazi 4pm Mon. 16th July 4 VITA CLUB vs PORTS Uwanja wa Taifa 2pm 5 SIMBA vs URA Uwanja wa Taifa 4pm Tue. 17th July 6 ATLETICO vs APR Uwanja wa Taifa 2pm 7 WAU SALAAM vs YANGA Uwanja wa Taifa 4pm Wed. 18th July 8 VITA CLUB vs URA Uwanja wa Taifa 2pm 9 PORTS vs SIMBA Uwanja wa Taifa 4pm Thu. 19th July 10 ATLETICO vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa 2pm 11 MAFUNZO vs TUSKER Uwanja wa Taifa 4pm Fri. 20th July 12 PORTS vs URA Uwanja wa Taifa 2pm 13 YANGA vs APR Uwanja wa Taifa 4pm Sat. 21st July 14 AZAM vs TUSKER Uwanja wa Taifa 2pm 15 SIMBA vs VITA CLUB Uwanja wa Taifa 4pm Sun. 22nd July REST DAY QUARTER FINALS Mon. 23rd July 16 B2 vs C2 17 A1 vs C3 Tue. 24th July 18 C1 vs A2 19 B1 vs A3 Wed. 25th July REST DAY SEMI FINALS Thu. 26th July 20 Winner 16 vs Winner 17 21 Winner 18 vs Winner 19 Fri. 27th July REST DAY FINALS AND 3rd PLACE PLAY OFFS Sat. 28th July 22 Loser 20 vs Loser 21 23 Winner 20 vs Winner 21 Boniface Wambura Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Licha ya mafanikio, Diamond hajamsahau Mungu wake

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' amesema licha ya mafanikio makubwa aliyonayo katika sanaa hiyo, bado haachi kufanya ibada kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kumfikisha hapo alipo. Akizungumza na MICHARAZO, Diamond anayetamba na nyimbo kama 'Moyo Wangu', Lala Salama' na Nimepende Nani, alisema ni vigumu kumsahau Mungu kwani anaamini ndiye aliyemnyanyua hapo alipo kisanii. Diamond, alisema jambo la kumkumbuka Mungu na kufanya ibada ni kitu kinachopaswa kufanywa na kila mtu hususani wasanii ambao hutumia muda wao mwingine katika kufanya shughuli zao kiasi cha kubanwa kufanya ibada. "Kaka huwezi amini sijamsahau Mungu, naendelea kufanya ibada kama kawaida kwa sababu najua bila ya uwezo na mapenzi yake Mungu, nisingefika kokote," alisema. Mkali huyo alisema, kumtanguliza Mungu katika kila analofanya pamoja na kujibidiisha kufanya mazoezi na kuumiza kichwa kuandaa kazi makini, zimemfanya awe mmoja wa wasanii wenye majina makubwa kwa sasa nchini na ukanda mzima wa Afrika Mashariki. Aliongeza kwa sasa anajiandaa kupakua kazi mpya ambazo zitazidi kumweka katika matawi ya juu nchini. "Nipo katika maandalizi ya kupakua kazi mpya, hivyo mashabiki wangu wakae mkao wa kula," alisema.

Watayarishaji wengi wa filamu wabishi- Lamata

MMOJA wa waongozaji wa filamu wa kike nchini, Leah Richard Mwendamseke 'Lamata' amesema baadhi ya watayarishaji wa filamu hawataki kukosolewa katika kazi zao na kufanya filamu nyingi kukosa ubora wa kimataifa. Pia, alisema kama watayarishaji hao hawatawadharau waongozaji na kuwathamini wasanii wanaozicheza filamu zao, huenda soko la filamu katika anga la kimataifa likapanuka na kuchuana na zile za nchi za Nigeria, Ghana na kwingineko. Lamata, aliyasema hayo alipozungumza na MICHARAZO na kusema, licha ya kwamba waongozaji ndio wenye nafasi kubwa ya kubebeshwa lawama kazi ikiwa mbaya, ila ukweli wengi wao wanaangushwa na ubishi walionao watayarishaji wa filamu wasiopenda kuelekezwa. Muongozaji na mwandishi huyo wa filamu, alisema wapo watayarishaji hata wakielekezwa kufanya mabadiliko katika kazi zao ili kuziboresha hukataa na kuamini wapo sahihi na kusababisha kazi nyingi kulipuliwa na kushindwa kutamba sokoni. "Pia wamekuwa wakiwadharau waongozaji na kuwathamini zaidi wasanii bila kujua injini ya filamu kuwa nzuri ni muongozaji makini anayeweza kupangilia kazi kulingana na hadithi ilivyo na namna ya kuiboresha ili iendane na uhalisi unaosisimua," alisema. Alisema kama watayarishaji na baadhi ya wasanii wataamua kubadilika na kufanya kazi kwa lengo la kuiinua sanaa hiyo ni wazi filamu za Tanzania zinaweza kutamba kimataifa na kuchuana na kazi za mataifa mengine ambayo wamekuwa vinara kwa miaka mingi iliyopita. Mwanadada huyo aliyeziongoza filamu kadhaa kama 'My Princess', 'Candy', 'Mr President', 'Rude' na sasa akimalizia kazi mpya ya 'Injinia', alisema wapo baadhi ya wasanii hawajui wapo katika sanaa hiyo kwa sababu ipi kwa mambo wanayoyafanya.

Okwi kupaa kwenda Parma ya Italia

MSHAMBULIAJI wa kutumaini wa kimataifa wa timu ya soka ya Simba, Emmanuel Okwi anatarajiwa kutua nchini Italia kwa ajili ya kufanyiwa majaribio katika klabu ya Parma inayoshiriki Ligi ya Seria A, baada ya kuzitosa ofa za timu za Afika Kusini. Mganda huyo ambaye amekuwa chachu kubwa ya Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu uliopita, anatarajiwa kwenda nchini humo, keshokutwa. Habari za kuaminika toka ndani ya Simba na kuthibitishwa na mmoja wa wajumbe wa kamati ya Utendaji aliyekataa kutajwa jina lake, zinasema kuwa Okwi anaenda huko kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Parma. "Ni kweli Okwi anatarajiwa kutua Italia Julai 4 kwa ajili ya kufanya mazungumzo na klabu ya Seria A ya Parma kwa ajili ya kujiunga nao kwa msimu ujao baada ya kuachana na ofa za klabu za Orlando Pirates, Mamelodi Sundowns na Super Sports zilizokuwa zikimtaka," chanzo hicho kilidokeza. Chanzo hicho kilidokeza kuwa, iwapo Mganda huyo atafanikuwa kunyakuliwa na Parma huenda Simba ikavuna mamilioni ya fedha kwa usajili huo. Hata hivyo Simba italazimika kugawana mgao huo unaokadiriwa kufikia Sh Bilioni 2 na klabu ya Sc Villa ya Uganda iliyowauzia nyota huyo ambaye aliidhalilisha Yanga kwenye mechi ya kufungia msimu kwa kufunga mabao mawili na kusaidia jingine moja. Hiyo haitakuwa mara ya kwanza Simba kuuza wachezaji wake na kuvuna fedha, kwani mwaka jana iliwauza Mbwana Samatta na Patr
ick Ochan kwa TP Mazembe na kuvuna fedha za kutosha hiyo ni mbali na zile za akina Danny Mrwanda, Henry Joseph na wengineo.

Yanga yatamba 'MTATUKOMA' safari hii

UONGOZI wa
klabu ya soka ya Yanga umetamka neno moja tu 'Mtatukoma' wakitambia kikosi chao katika ushiriki wao wa michuano ya Kombe la Kagame. Yanga watashiriki michuano hiyo itakayoanza Julai 14 na kumalizika mwishoni mwa mwezi huu kama mabingwa watetezi, michuano itakayofanyika kwenye ardhi ya Tanzania Bara. Afisa habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema kwa namna kikosi chao kilivyoimarishwa na kujifua wana hakika ya kutetea taji hilo, na pia kufanya vema kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao. Sendeu, alisema kwa halili yoyote wapinzani wao watakaopambana kwenye michuano hiyo ya Kagame na Ligi Kuu wanapaswa kujipanga kwani vinginevyo watakiona cha moto. "Kwa kweli Watatukona kwa namna tunavyoendelea vema na maandalizi yetu ya michuano ya Kagame na kujipanga kwa Ligi Kuu msimu ujao kama unavyojua tumeshaanza kujifua na tumeimarisha kikosi kwa kunasa wachezaji kadhaa," alisema. Sendeu alisema, anaamini wachezaji wapya waliosajiliwa kwa ajili ya michuano hiyo na ligi ijayo wataisaidia Yanga kurejesha makali yake baada ya kumaliza msimu wakiambulia patupu wakipoteza ubingwa na kukosa hata nafasi ya kuiwakilisha nchini katika michuano ya kimataifa. Yanga ilimaliza ligi ikiwa nafasi ya tatu, ikiziacha Simba iliyotwaa ubingwa na Azam walioshika nafasi ya pili wakiwatambia na kupata fursa ya uwakilishi wa nchini katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho. Kikosi hicho cha Yanga kinaendelea kunolewa kwa sasa na Kocha Msaidizi ambaye ndiye Kaimu Kocha Mkuu, Fred Felix Minziro baada ya aliyekuwa kocha mkuu, Kostadin Papic kutimika kwao baada ya kutoongezewa mkataba mwingine na klabu hiyo. Tayari uongozi wa juu ya Yanga umesema wakati wowote utalitangaza jina la kocha mkuu wa timu hiyo baada ya kupitia maombi ya makocha bora watano waliopita katika orodha ndefu ingawa majina ya makocha hao haijawekwa bayana zaidi ya tetesi wapo wa ndani ya Afrika na Ulaya. Timu hiyo jana ilikitambulisha kikosi chake kwa mashabiki wa soka jijini Dar kwa kuumanana na Express ya Uganda na kuikandamiza mabao 2-1, mabao yote ya Yanga yakitupiwa nyavuni Jerry Tegete kwa pasi murua za kinda la Stars, Simon Msuvah na Bahanuzi.