STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 1, 2012

Licha ya mafanikio, Diamond hajamsahau Mungu wake

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' amesema licha ya mafanikio makubwa aliyonayo katika sanaa hiyo, bado haachi kufanya ibada kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kumfikisha hapo alipo. Akizungumza na MICHARAZO, Diamond anayetamba na nyimbo kama 'Moyo Wangu', Lala Salama' na Nimepende Nani, alisema ni vigumu kumsahau Mungu kwani anaamini ndiye aliyemnyanyua hapo alipo kisanii. Diamond, alisema jambo la kumkumbuka Mungu na kufanya ibada ni kitu kinachopaswa kufanywa na kila mtu hususani wasanii ambao hutumia muda wao mwingine katika kufanya shughuli zao kiasi cha kubanwa kufanya ibada. "Kaka huwezi amini sijamsahau Mungu, naendelea kufanya ibada kama kawaida kwa sababu najua bila ya uwezo na mapenzi yake Mungu, nisingefika kokote," alisema. Mkali huyo alisema, kumtanguliza Mungu katika kila analofanya pamoja na kujibidiisha kufanya mazoezi na kuumiza kichwa kuandaa kazi makini, zimemfanya awe mmoja wa wasanii wenye majina makubwa kwa sasa nchini na ukanda mzima wa Afrika Mashariki. Aliongeza kwa sasa anajiandaa kupakua kazi mpya ambazo zitazidi kumweka katika matawi ya juu nchini. "Nipo katika maandalizi ya kupakua kazi mpya, hivyo mashabiki wangu wakae mkao wa kula," alisema.

No comments:

Post a Comment