STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 10, 2016

Yanga yawafuata Simba Dar, watolewa na URA

YANGA imeifuata Simba baada ya kutolewa na URA kwa penalti 4-3 baada ya kumaliza dakika 90 matokeo yakiwa 1-1.

Pambano limeisha Yanga, URA kwenye penalti

PAMBANO la nusu fainali ya pili ya Kombe la Mapinduzi, kati ya Yanga na URA limemalizika baada ya dakika 90 kuisha matokeo yakiwa bao 1-1.
Kwa sasa timu zinajiandaa kupigiana penalti. Ngoja tuone mambo yatakuwaje kwa wababe hao wa Tanzania na Uganda.

SAMATTA NAHIODHA MPYA WA TAIFA STARS

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa, amemtangaza mshambuliaji Mbwana Ally Samatta kuwa Nahodha mpya wa timu hiyo, akichukua nafasi ya Nadir Haroub Ali ‘Cannavaro’. Akizungumza na leo, Mkwasa amesema kwamba uamuzi huo umetokana na kazi nzuri ya Samatta kuitangaza Tanzania na Taifa Stars kimataifa. “Anastahili kuwa Nahodha wa Taifa Stars kuanzia sasa, na ingawa tumekuwa na Nahodha ambaye anastahili kuendelea, lakini tumeona kitu pekee cha kumlipa Samatta kwa sasa ni beji ya Unahodha,”amesema Mkwasa.

Mkwasa amesema kuanzia sasa Cannavaro atakuwa Nahodha wa kikosi cha wachezaji wanaocheza nyumbani kwa ajili ya michuano ya CHAN, wakati John Bocco atakuwa Nahodha Msaidizi wa Taifa Stars chini ya Samatta.
Samatta ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora Anayecheza Afrika katika sherehe zilizofanyika usiku wa Alhamisi ukumbi wa mikutano wa Kimataifa mjini Abuja.
Samatta alipata pointi 127, mbele ya mchezaji mwenzake wa TP Mazembe, kipa Robert Muteba Kidiaba wa DRC, aliyepata pointi 88, wakati mshambuliaji wa Etoile du Sahel ya Tunisia na timu ya taifa ya Algeria, Baghdad Bounedjah amepata pointi 63.
Mafanikio ya Samatta anayeweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa ukanda w Afrika Mashariki na Kati kushinda tuzo kubwa ya Afrika, yanakuja baada ya kuiwezesha Mazembe kutwaa taji la tano la Ligi ya Mabingwa Afrika, huku akiibuka mfungaji bora kwa mabao yake nane.
Aidha, Samatta sasa ndiye anaweza kuitwa Mchezaji Bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania – bada ya miaka mingi ya kutokuwa na uhakika wa nani apewe sifa hiyo.
Samatta alijiunga na Mazembe mwaka 2011 akitokea Simba SC aliyoichezea kwa msimu mmoja akitokea African Lyon iliyomtoa Mbagala Market, ambayo ilimuibua Kumbagulile FC ya kwao, Mbagala.
Chanzo-Bin Zubeiry

URA wanachomoa bao URA 1, Yanga 1

http://urafc.co.ug/wp-content/uploads/2015/02/URA-Peter-Lwasa-300.jpg
PETER Lwasa aliyeingia kipindi cha pili, anaisawazishia bao URA kutokana na wachezaji wa Yanga kucheza Offside-trick ambapo mabeki walidhani mfungaji ameotea, lakini bado ndivyo tena. Yanga 1 URA 1

Tetesi za usajili majuu zipo hivi

http://i2.walesonline.co.uk/incoming/article6494703.ece/ALTERNATES/s615/1Gareth-Bale.jpgDIRISHA la usajili kwa mwezi Januari lipo wazi na klabu kadhaa zimeanza kuchangamkia kwa kunyakua nyota mbalimbali, huku tetesi nyingine zikizidi kuenea kila uchao.
Straika wa Real Madrid, Gareth Bale anatarajiwa kukataa maombi ya kutoka Manchester United na Chelsea kufuatia nyota huyo wa kimataifa wa Wales kutaka kuendelea kubakia Santiago Bernabeu. Pia inaelezwa kuwa Klabu ya Manchester United inaripotiwa kujipanga kumchukua meneja wa Tottenham Hotspurs Mauricio Pochettino kama mbadala wa Louis van Gaal, huku meneja wa Paris Saint-Germain Laurent Blanc naye akitajwa kufikiriwa katika nafasi hiyo. Hii ni kwa mujibu wa Sunday Mirror. 
Kwingineko klabu ya Tottenham Hotspurs inajipanga kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Loic Remy kwa mkopo majira haya ya kiangazi, huku Manchester United inataka kitita cha paundi milioni 24 kwa ajili ya Marouane Fellaini lakini hawatakubali kiungo huyo kuondoka kwa mkopo. Pia klabu hiyo ya Manchester United inakaribia kumsajili mshambuliaji wa Mainz Yoshinori Muto kwa kitita cha paundi milioni 12 hii ni kwa mujibu wa Sunday Mirror.
The Suna lenyewe limeeleza kuwa Klabu ya Manchester City imeingia katika kinyang’anyiro cha paundi milioni 80 na Real Madrid na Paris Saint-Germain kama Eden Hazard ataamua kuondoka Chelsea kipindi hiki cha majira ya kiangazi, huku Chelsea nayo ikidaiwa kuwa inamuwinda meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone ili aweze kuwa mbadala wa Guus Hiddink pindi atakapomaliza muda wake mwishoni mwa msimu huu.

Tambwe aifungia Yanga bao

AMISSI Tambwe ameifungia Yanga bao la mapema na kuifanya iende mapumziko ikiwa mbele dhidi ya URA ya Uganda. Kipindi cha pili kimeanza matokeo yakiwa bado ni 1-0, Yanga wakiwa mbele.
Matokeo yakibaki hivi Yanga itakutana na Mtibwa katikam fainali za Kombe la Mapinduzi kama ilivyokuwa mwaka 2007.

Spurs chupuchupu, Chelsea yapeta Kombe la FA

Harry Kane akishangilia penalti yake iliyoiokoa Spurs kulala nyumbani
WAKATI Chelsea ikivuka hadi raundi ya nne baada ya kuifunga timu ya Scunthorpe kwa mabao 2-0 katika mechi ya mfululizo wa michuano ya Kombe la FA, Tottenham hotspur ikiwa nyumbani ilinusurika kulala baada ya kutoka sare ya mabao 2-2.
Penalti ya Harry Kane katika dakika za lala salama iliiokoa Spurs kulala kwa Leichester City, huku Swansea City iking'olewa na Oxford United kwa mabao 3-2.
Chelsea wenyewe wakiwa nyumbani kwao Stamford Bridge ilipata ushindi wa mabao 2-0 na kuungana na vigogo wengine wa Ligi Kuu kufuzu raundi nyingine ya michuano hiyo ambayo bingwa mtetezi ni Arsenal iliifumua Sunderland jana Jumamosi kwa mabao 3-1.



Simba yatemeshwa taji, Mtibwa hiyoo fainali za Mapinduzi

Ibrahim Rajab 'Jeba', akichuana na Mohammed Tshabalala wa Simba jioni ya leo na Simba kulala bao 1-0
NDIVYO hivyo tena. Simba imetemeshwa taji lake la Kombe la Mapinduzi baada ya kulala bao 1-0 kwa Mtibwa Sugar.
Bao pekee la sekunde chache kabla ya mapumziko lililofungwa na Ibraihm Rajab 'Jeba' lilitosha kuirudisha Simba jijini dar es Salaam na kuiacha Mtibwa ikitangulia fainali yao ya tano.
temesha Simba ubingwa wa Kombe la Mapinduzi na kuifungasha virago kurudi jijini Dar es Salaam.
Katika pambano hilo la kwanza la nusu fainali lililochezwa jioni kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani humu, Simba itabidi ijilaumu kwa kutemeshwa taji.
Na kama kuna mtu ambaye atajuta kwa kung'oka kwa Simba ni kipa Peter Manyika aliyeizawadia Mtibwa bao baada ya kushindwa kudaka mpira uliiopigwa na Shiza Kichuya na kumfanya Jeba kumpoka na kufunga bao hilo.

Mtibwa sasa inasubiri kujua itacheza na nani kati ya Yanga na URA ambazo zinaendelea kuumana muda huu.
Hizo ni fainali za tano kwa Mtibwa tangu michuano hiyo ilipoasisiwa mwaka 2007 ikikutana na Yanga kwa mara ya kwanza mwaka huo na kufungwa.
Pia hii itakuwa fainali ya pili mfululizo ya Mtibwa baada ya mwaka jana kucheza fainali dhidi ya Simba na kufungwa kwa mikwaju ya penalti.
Pamoja na Simba kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Mtibwa na hasa katika kipindi cha pili baada ya kufanya mabadiliko, lakini umakini mdogo wa washambuliaji wa Msimbazi wakiongozwa na Danny Lyanga, Mussa Mgosi na Ibrahim Ajib.

Friday, January 8, 2016

Simba yaikwepa Yanga kiaina, kuvaana na Mtibwa

Mashabiki wa Simba wanaosubiri kuipa sapoti timu yao Jumapili jioni dhidi ya Mtibwa Sugar
BAO pekee la Jonas Mkude la dakika ya 65 limeiwezesha Simba kutinga nusu fainali na sasa itaavana na Mtibwa Sugar jioni ya Jumapili, ikikwepana kuvaana na Yanga iliyotangulia mapema tangu jana.
Kulikuwa na dalili za Simba kuvaana na Yanga kama matokeo yangeisha kwa sare ya 0-0, lakini bao la Mkude liliweka mambo sawa na sasa vijana wa Msimbazi watakuwa wakinoa makucha yao ili kuvaana na Mtibwa waliocheza nao fainali za mwaka jana na kuichapa kwa mikwaju ya penalti.
Yanga wenyewe itakuwa na kibarua dhidi ya URA ambayo mapema jioni ya leo ilipata ushindi wa baoa 1-0 dhidi ya Jamhuri.
Kama Yanga na Simba zitavuka hatua hiyo zitaumana Jumatano usiku kwenye fainali ikirejea fainali za mwaka 2011, ambazo Simba ilitwaa taji lake la pili kwa kuizabua Yanga mabao 2-0.

Simba inaoongoza kwa bao 1-0 dhidi ya JKU

SIMBA inaongoza bao 1-0 baada ya Jonas Mkude kuipatia bao la kichwa katika dakika ya 65. Pambano bado ni kali na kuna dalili za wapinzani wajadi Simba na Yanga kutokutana katika hatua ya nusu fainali.

Claudio Makelele apewa shavu Monaco


http://img1.cfstatic.com/psg/claude-makelele_35549_wide.jpg
Claudio Makelele
KLABU ya Monaco ya Ufaransa, imemteua kiungo wa zamani wa Chelsea na Real Madrid, Claudio Makelele kuwa Mkurugenzi Mpya wa Ufundi. 
Klabu hiyo ilitangaza jana Alhamisi uteuzi wa nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa, ikielezea kuwa, kibarua chake kikubwa kitakuwa ni kumsaidia Makamu wa Rais Vadim Vasilyev kuongoza upande wa michezo wa timu hiyo. 
Makelele alitimuliwa kibarua cha kuinoa Bastia Novemba 24, 2014 baada ya kufanya kazi kama Kocha Msaidizi katika klabu ya Paris Saint-Germain. Akihojiwa na mtandao wa klabu hiyo, Makelele amesema amefurahi kujiunga na klabu hiyo muhimu katika soka la Ufaransa na kuahidi kufanya bidii na kuisaidia timu hiyo.
Enzi za uchezaji wake, mkali huyo alikuwa akitawala dimba la kati kiasi cha kuwapa wakati mgumu wapinzani wake.
 

Simba yaisaka Yanga kimtindo

DAKIKA 45 za kwanza za pambano la kukamilisha ratiba kati ya Simba na JKU zimemalizika matokeo yakiwa bao 0-0.
Pambano ni kali na Simba itajilaumu kwa kukosa angalau bao hata moja katika dakika hizo kutokana na kukosa mabao ya wazi.
Kama matokeo yataendelea hivi Simba itakuwa imeangukia mikononi mwa Yanga waliomaliza nafasi ya kwanza kwenye kundi B. URA wanaoongoza kundi A tayari imeshatinga nusu fainali, kama ilivyo kwa Mtibwa Sugar, lakini hakuna anayejua atacheza na nani Jumapili ijayo mechi za nusu fainali zitakazpochezwa jioni na usiku.

Sunderland wanasa kifaa toka Bayern Munich

https://i.guim.co.uk/img/media/714c8f8cc7ab15b56bb5fb6c9eb01c24b719ae6c/0_149_5128_3080/master/5128.jpg?w=620&q=85&auto=format&sharp=10&s=daec3160be3fec2cb53a6ae0d3112b65IKIWA na kibarua kigumu wikiendi hii dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Sunderland imetangaza kumsajili beki wa Bayern Munich, Jan Kirchhoff kwa ada ambayo haikuwekwa wazi.
Beki huyo wa kati mwenye umri wa miaka 25, alianza soka lake katika timu ya Mainz kabla ya kujiunga na Bayern mwaka 2013, akiwa pia amecheza kwa mkopo Schalke ametua kwa Paka Weusi hao kabla ya kuvaana na Arsenal kwenye mechi ya mzunguko wa tatu wa michuano ya Kombe la FA.
Meneja wa Sunderland, Sam Allardyce aliuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa Jan ni mchezaji mzuri na mwenye uzoefu pamoja na umri mdogo alionao hivi sasa. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa anaamini beki huyo atazoea haraka mazingira katika klabu hiyo na kuwasaidia kufikia malengo yao waliyojiwekea msimu huu.
Sunderland iko katika mapambano ya kutoshuka daraja wakishika nafasi ya 19 katika msimamo wakiwa na alama 15 katika michezo 20 waliyocheza.

Sanchez bado hakijaeleweka Emirates

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2015/01/11/14/Alexis-Sanchez.jpgBADO hakijaeleweka tu. Kocha wa  Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa straika wake matata, Alexis Sanchez ataukosa mchezo wa mzunguko wa tatu wa Kombe la FA dhidi ya Sunderland ikiwa kama tahadhari.
Nyota huyo wa kimataifa wa Chile amekuwa nje ya Uwanja kwa zaidi ya mwezi mmoja baada ya kupata majeruhi ya misuli katika mchezo dhidi ya Norwich City, Novemba 29 mwaka jana.
Sanchez alikuwa akitegemewa kurejea uwanjani kabla ya Krismasi, lakini alichelewa kupona na Wenger hayuko tayari kumwahisha kutokana na kukabiliwa na mechi ngumu za za Ligi Kuu dhidi ya Liverpool na Stoke City wiki ijayo.
Akizungumza katika mtandao wa klabu hiyo, Kocha Wenger amesema taarifa mbaya aliyonayo wiki hii ni kukosekana kwa Sanchez ambaye pamoja na kupona, lakini ameamua kumpa muda zaidi kama tahadhari.
Wenger ameendelea kudai kuwa kiungo Mikel Arteta atakuwepo katika kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza toka Novemba 21 wakati Tomas Rosicky naye ataanza mazoezi rasmi wiki ijayo baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua.
Arsenal ndio wanaoongoza kwa sasa msimamo wa Ligi Kuu ya England  ikiwa na pointi 42, mbili zaidi na ilizonazo Manchester City wanaofuata nyuma yao.

Dortmund na sizitaki mbichi kwa Januzaj

http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/67/590x/Adananjjjj-604533.jpgKLABU ya Borussia Dortmund imedai ulikuwa ni uamuzi wa Adnan Januzaj mwenyewe kurejea Manchester United na kukiri dili lake halikuwa na manufaa kwa klabu yoyote. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 alijiunga na Dortmund kwa mkopo wa msimu mzima mwishoni wa Agosti mwaka jana, lakini amefanikiwa kuichezea timu hiyo mechi 12 pekee. 
Kurejea kwa Januzaj Old Trafford kulifanywa rasmi jana na mkurugenzi wa michezo wa Dortmund amekiri kuwa kusitisha mkataba wa nyota huyo ni jambo bora kwa pande zote husika. 
Mkurugenzi huyo amesema yalikuwa ni mapendekezo ya Januzaj mwenyewe kurejea United na uwepo wake Dortmund haukuwa na faida yeyote kwa klabu hiyo.
Man imemrejesha winga huyo kwa ajili ya kuimatrisha kikosi chake baada ya Kocha Louis Van Gaal kuuza wachezaji wake kadhaa nyota akiwamo Nani, Chicharito na Angel di Maria

Samatta sasa kina kona, anukia Nantes

KLABU ya Ligi Kuu ya Ufaransa, Ligue 1 ya Nantes inaripotiwa kuanza mazungumzo rasmi na wawakilishi wa Mbwana Samatta pamoja na klabu ya TP Mazembe. 
Klabu hiyo imedaiwa kuwa ina nia ya kupata saini ya Samatta katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili ili iweze kumtumia kwa msimu uliobakia. 
Kwa mujibu wa mwakilishi wa Samatta, Nantes inataka kila kitu kimalizike kabla ya Januari 20. Nantes inamtaka Samatta ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji ambayo msimu huu inaonekana kuwa butu kwa kufunga mabao 14 pekee. 
Nantes inashikilia nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi hiyo baada ya kucheza michezo 19 ikikusanya jumla ya pointi 24.
Timu hiyo Jumapili itashuka uwanjani kuvaana na St Entienne katika mfululizo wa ligi hiyo.

HIKI NDIKO KIKOSI AMBACHO SAMATTA NAYE NDANI

MBWANA Samatta jana alirejea tukio lililowahi kufanywa na straika wa kimataifa nchini, Haji Dilunga alipoteuliwa timu ya Afrika sambamba na kipa Omary Mahadhi mwaka 1973 baada ya kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha Afrika 2015 sambamba na nyota wengine.
Kikosi kamili kipo hivi;


NI SIMBA VS YANGA MAPINDUZI AU YANGA V JKU?

http://24tanzania.com/wp-content/uploads/2013/09/9072Simba-Yanga.jpgKLABU ya Yanga inasubiri kujua itacheza na nani kati yake na watani zao Simba au URA ya Uganda katika mechi za nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar.
URA imekuwa timu ya tatu kutinga hatua hiyo baada ya jioni ya leo kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Pemba na kuiacha nafasi moja kwa 'Mnyama' ili kujua itaangukia kileleni au nafasi ya pili.
Kama Simba ambayo usiku huu itavaana na JKU ya Unguja, itashinda mchezo huo, itaikwepa Yanga na hivyo kusubiri kuona kama zitakutana fainali Jumatano ijayo.
Iwapo Simba itatokla sare au kupoteza itaangukia nafasi ya pili na kuingia 18 za vijana wa Jangwani ambao usiku wa jana ilipasta ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mtibwa.
Simba ambao ni mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo ya Mapinduzi iliyoasisiwa mwaka 2007 ina pointi nne mpaka sasa ikiwa nafasi ya pili, nyuma ya URA ilitimiza pointi 6 baada  ya ushindi wake wa jioni huu kwa bao la Saio Kyayune  la dakika za lala salama.
Kama timu hizo kongwe nchini zitakwepana hatua hiyo ya nusu fainali kulingana na matokeo ya usiku wa leo, basi zinaweza kukutana fainali na kurejea fainali za mwaka 2011 ambapo Yanga ilikubali kichapo cha mabao 2-0 mbele ya Simba kwa mabao ya Mussa Hassan Mgosi na Shija Mkina.

Nusu fainali:
J'Pili Jan 10
Samba/JKU v Mtibwa Sugar Saa 10:15 jioni
Yanga v Simba/JKU Saa2:15 usiku

Msimamo
Kundi A

                P  W D  L  F A Pts
URA          3   2  0  1 4 2  6*
Simba       2   1  1  0 3 2  4
JKU           2   1  0  1 4 3  3
Jamhuri     3   0  1  2 2 6  1

Kundi B

               P  W D  L  F  A Pts
Yanga      3   2  1  0  6  2  7*
Mtibwa     3   1  1  1  3  3  4*
Mafunzo   3   1  0  2  2  5  3
Azam       3   0  2  1  3  4  2
* Zimefuzu nusu fainali

Wafungaji:

2-Donald Ngoma (Yanga)
   Awadh Juma (Simba)
   Villa Oromuchan (URA)
   Mohammed Abdallah (JKU)
  Kipre Tchetche (Azam)
1-Paul Nonga (Yanga)
  Hussein Javu (Mtibwa)
  John Bocco (Azam)
  Oscar Aggaba (URA)
  Emmanuel Martin (JKU)
  Said Bahanuzi (Mtibwa)
  Vincent Bossou (Yanga)
  Mwalimu Khalfan (Jamhuri)
  Ammy Bangaseka (Jamhuri)
  Nassor Juma      (JKU)
  Ibrahim Ajib      (Simba)
  Rashid Abdalla (Mafunzo)
  Sadick Rajab   (Mafunzo)
  Saio Kyayune   (URA)
  Shiza Kichuya  (Mtibwa)
  Issofou Boubacar (Yanga)
  Malimi Busungu  (Yanga)

Orodha ya Mabingwa

2007  Yanga SC
2008  Simba SC
2009  Miembeni
2010  Mtibwa Sugar
2011  Simba SC
2012  Azam FC 
2013   Azam FC
2014  KCCA      
2015  Simba SC
NB:Simba imeingia fainali nyingi za Mapinduzi (5) ikifuatiwa na Mtibwa (4)

Samatta aanza kupokea pongezi za tuzo yake

HONGERA. Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi amempongeza mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya TP Mazembe ya Congo DR kwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani.
Samatta ameshinda tuzo ya mchezaji bora kwa wachezaji wanaocheza Afrika baada ya kwashinda Robert Kidiaba (Congo DR) alieshika nafasi ya pili na Bounedjah Baghdad (Algeria) aliyeshika nafasi ya tatu.
Kwa kushinda tuzo hiyo, Samatta amekua mchezaji wa kwanza kwa ukanda wa Afrika Mashariki kushinda tuzo kubwa barani Afrika.
Pamoja na kushinda tuzo hiyo, Samatta pia amejumuishwa katika kikosi bora cha wachezaji wa Afrika kwa mwaka 2015 sambamba na Robert Kidiaba (Congo DR), Sergie Aurier (Ivory Coast), Aymen Abdenmor (Tunisia), Mohamed Meftah (Algeria), Sadio Mane (Senegal), Yaya Toure (Ivory Coast), Yacine Ibrahim (Algeria), Andrew Ayew (Ghana), Mbwana Samatta (Tanzania), Pierre-Emercik Aubameyang (Gabon) na Baghdad Bounedjah (Algeria).
Mshambuliaji Mbwana Samatta alieyambatana na Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine wanatarajia kuwasili nchini leo saa 8 usiku kwa shirika la ndege la Ethiopia.
Wakati Huo huo Shirikisho la Soka Tanzania, TFF limetuma salamu za rambirambi kwa kocha msaidizi wa Taifa Stars Hemed Suleiman “Morocco” kufutia kifo cha baba yake mzazi Suleiman Ally Hemed kilichotokea juzi kisiwani Zanzibar.
Katika salamu hizo za rambirambi, TFF imewapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wapo pamoja na familia ya marheemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Aidha pia TFF imetuma rambirambi (ubani) wa shilingi laki mbili (200,000) kwa familia ya kocha Hemed Moroco kufuatia kifo cha baba yake Suleiman Ally.
Mazishi ya marehemu Suleiman Ally Hemed yamefanyika jana Alhamisi jioni mjini Zanzibar.

MWANAUMEEEEEEEEEEEEEEEE NI MBWANA SAMATTA

 
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/samatta-1.jpg
Add caption
MWANASOKA Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani ni Mbwana Samatta, huku Yaya Toure MBWANA Samatta kila kona. Mwanasoka wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta usiku wa kuamkia leo ameweka rekodi ya kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani. Samatta amekuwa Mtanzania wa kwanza kunyakua tuzo hiyo baada ya kuwashinda Robert Kidiaba na Baghdad Bounedjah.
Hiyo ni tuzo ya pili kwa Samatta baada ya ile ya Mfungaji Bora wa Afrika akiwa ameisaidia klabu yake ya TP Mazembe kutwaa ubingwa wa Afrika mwaka 2015.
Klabu hiyo ya Mazembe ilishinda tuzo ya Klabu Bora Afrika, huku timu ya taifa ya Ivory Coast ikishinda tuzo Timu bora ya Afrika kwa wanaume na Cameroon ikishinda kwa upande wa wanawake.
Mfaransa Herve Renard, Kocha wa Ivory Coast alitwaa tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka kwa mara ya pili baada ya mwaka 2012 kunyakua pia tuzo kama hiyo alipoisaidia Zambia kutwaa ubingwa wa Afrika na  kufikia rekodi ya  Bruno Metsu aliyenyakua mwaka 2001-2002
Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mwaka 2015 ni Pierre-Emerick Aubameyang, akimpikua Yaya Toure wa Ivory Coast na Andre Ayew wa Ghana.

ORODHA KAMILI YA WASHINDI
MCHEZAJI BORA WA AFRIKA - Pierre-Emerick AUBAMEYANG (Gabon)
MCHEZAJI BORA ANAYECHEZA AFRIKA – Mbwana Aly SAMATTA
MCHEZAJI BORA WA KIKE - Gaelle ENGANAMOUIT (Cameroon)
MCHEZAJI BORA KIJANA - Victor OSIMHEN (Nigeria)
MCHEZAJI BORA ANAYECHIPUKIA VIZURI - Etebo Peter OGHENEKARO (Nigeria)
KOCHA BORA WA MWAKA- Herve RENARD (Ufaransa) – Kocha wa zamani wa Ivory Coast
REFA BORA WA MWAKA - Bakary Papa GASSAMA (Gambia)
TIMU BORA YA TAIFA – Ivory Coast
TIMU BORA YA TAIFA YA WANAWAKE- Cameroon
KLABU BORA YA MWAKA - TP Mazembe (DRC)
GWIJI WA AFRIKA - Charles Kumi GYAMFI (Ghana)
Samuel MBAPPE LEPPE (Cameroon)

KIKOSI BORA AFRIKA

Kipa: Robert Muteba KIDIABA (DRC)
Mabeki: Serge AURIER (Ivory Coast), Aymen ABDENNOUR (Tunisia), Mohamed MEFTAH (Algeria)
Viungo: Andre AYEW (Ghana), Yaya TOURE (Ivory Coast), Sadio MANE (Senegal), Yacine BRAHIMI (Algeria),    
Washambuliaji: Mbwana Aly SAMATTA (Tanzania), Pierre-Emerrick AUBAMEYANG (Gabon), Baghdad BOUNEDJAH (Algeria) 

WACHEZAJI WA AKIBA;

Djigui DIARRA (Mali)
Azubuike OKECHUKWU (Nigeria)
Kelechi NWAKALI (Nigeria)
Zinedine FERHAT (Algeria)
Adama TRAORE (Mali)
Victor OSIMHEN (Nigeria)

Kermit ERASMUS (Afrika Kusini)

Thursday, January 7, 2016

Yanga 2 Mtibwa 1, Henry Joseph alimwa red card

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/Yanga-vs-Mtibwa-znz-3.jpg
Mtibwa iliyolala kwa Yanga usiku huu
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/Yanga-vs-Mtibwa-znz-2.jpg
Yanga iliyomaliza kazi Amaan dhidi ya Mtibwa Sugar
PAMBANO la Yanga na Mtibwa limeisha kwa matokeo ya 2-1, Yanga ikiibuka kidedea dhidi ya Wakata Miwa.
Yanga iliandika bao la pili na la ushindi lililofungwa na mtokea benchi Malimi Busungu aliyemalizia kazi nzuri ya Simon Msuva aliyepiga krosi murua iliyomkuta Busungu pekee yake na kupiga kichwa kilichompita kipa Said Mohammed.
Bao hilo lilifungwa dakika ya 82 na kuifanya Yanga kuongoza kundi B ikiwa na pointi 7 na Mtibwa kumaliza ya pili na pointi 4 na sasa wanasubiri kujua wanacheza na timu zipi kutoka kundi A ambapo Simba na JKU wataumana usiku wa kesho na mapema jioni, URA ya Uganda itakwaruzana na Jamhuri-Pemba.
Simba ndio inaoongoza kundi hilo kwa sasa ikiwa na pointi 4 ikifuatiwa na JKU kisha URA zote zikiwa na pointi 3 kila mmoja isipokuwa kutofautiana mabao ya kufungwa na kufunga, huku Jamhuri ikiburuza mkia ikiwa na pointi moja iliyotokana na sare dhidi ya Simba.

Bado matokeo ni 1-1

YANGA na Mtibwa zinaendelea kupambana kwenye Uwanja wa Amaan, matokeo yakiwa ni yale yale ya 1-1, huku kila timu ikifanya mabadiliko ya wachezaji katika kuongeza nguvu. Ikiwa ni dakika ya 75 sasa.

Bocco, Mao waomba radhi Azam kuchemsha Mapinduzi Cup


http://cecafafootball.org/wp-content/uploads/2014/03/john-bocco.jpg
John Bocco
Kikosi cha Azam kilichotolewa Mapinduzi Cup jioni ya leo visiwani Zanzibar

NAHODHA wa Azam, John Bocco 'Adebayor' amewaomba radhi mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo kwa matokeo mabaya ambayo timu hiyo imeyapata kwa siku za karibuni.
Kupitia akauti yake ya Facebook, Bocco amekiri Azam imekuwa kimeo kwa siku za karibuni na kukiri kwamba watajirejkebisha na kubwa ni kuwamba radhi wote waliokwazwa na matokeo ya timu yao ambayo jioni ya leo iling;olewa rasmi kwenye michunoa ya Kombe la Mapinduzi kwa kucharazwa mabao 2-1 na Mafunzo ya Zanzibar.
Ujumbe wa Bocco ndio huu, usome mwenyewe;
"Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi mashabiki wote wa Azam Fc kwa performance mbaya tulioonyesha kwenye mashindano ya Mapinduzi na mechi mbili za Ligi kabla ya kuja huku, matokeo ni sehemu ya mchezo inakubalika, lakin kitu kinacho angaliwa ni unapataje matokeo yawe mazuri au mabaya, tumepata matokeo mabaya kutoka kwenye performance mbaya zaidi kuwahi kuiona katika timu yetu tangu nilipoanza kucheza hadi sasa hivi, hivo tunawaomba radhi mashabiki wetu wote na kuwaaidi tutajituma na kupigania club yetu kwa moyo wetu wote."

Kadhalika naye Himid Mao aliomba radhi kama ujumbe wake unavyosomeka;
Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi mashabiki wote wa Azam Fc kwa performance mbaya tulioonyesha kwenye mashindano ya Mapinduzi na mechi mbili za Ligi kabla ya kuja huku, matokeo ni sehemu ya mchezo inakubalika, lakin kitu kinacho angaliwa ni unapataje matokeo yawe mazuri au mabaya, tumepata matokeo mabaya kutoka kwenye performance mbaya zaidi kuwahi kuiona katika timu yetu tangu nilipoanza kucheza hadi sasa hivi, nasikia aibu sana tena zaidi ya sana sina njia ya kuelezea ni kiasi gani najiskia vibaya na aibu naa mini na wachezaji wenzangu wanajiskia vibaya kama nnavyo jiskia mimi.....
I will work as harder as i can to make things better for me & my team
Samahani kwa mara nyingine tena,
Usiku Mwema

Kipidi cha pili Yanga v Mtibwa kimeanza

Kipindi cha kimeshaanza na timu zote zimeanza kwa kasi kusaka bao la pili. Pambano ni gumu  kwa timu zote, kila moja ikishambulia lango la mwenzake, lakini milango bado haijafunguka tena.


Nyota yaanza kumuwakia Samatta mapema...!

Mbwana Samatta (kushoto) alipokuwa akifanya majaribio CSKA Moscow
MANENO ya Wahenga huwa hayapotei. Wanasema dalili njema uanza asubuhi. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta ameanza kuwakiwa taa ya kijani katika tuzo za Afrika baada ya kutajwa miongoni mwa nyota wa kikosi cha wachezaji 11 Bora wa Caf 2015.
Samatta yupo Nigeria muda huu kwa ajili ya tuzo za Wachezaji Bora wa Afrika 2015 Glo Africa Awards 2015 zinazofanyika katika mji wa Abuja ametajwa kwenye kikosi hicho akiwa na wakali wengine wa dunia akiwa Mfungaji kinara wa mabao wa Bundesliga, Pierre-Emerick Aubameyang.
Wengine waliopo kwenye kikosi hicho ni kipa Robert Kidiaba, Serge Aurier, Aymen Abdennour, Mohammed Meftah, Andre Ayew, Yaya Toure, Sadio Mane, Yacine Brahimi, Aubameyang na Baghdad Bounedjah.
Huenda kwa mara ya kwanza Tanzania tukaandika historia kwa mwanasoka huyo kunyakua tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Ni Mapumziko matokeo ni bao 1-1

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/Kichuya.png
Muuaji wa Mtiobwa, Shiza Kichuya
Mfungaji wa Yanga, Issofou Boubacar 'Diego'
YANGA na Azam zinaenda mapumziko matokeo yakiwa bao 1-1. Wachezaji wanaenda kupewa mawaidha toka kwa makocha wao, kabla ya kurudi uwanjani kwa ngwe ya pili

Yanga, Mtibwa ngoma nzito Amaan

Mtibwa
Yanga
PAMBANO la timu za Mtibwa Sugar na Yanga bado ngoma nzito kwani mpaka sasa dakika chache kabla ya mapumziko, matokeo ni sare ya 1-1.
Mtibwa walikuwa wa kwanza kuandika bao dakika ya 10 kupitia kwa chipukizi, Shiza Kichuya akimalizia pasi na Vincent Barnabas kabla ya Yanga kuchomboa dakika ya 41 kwa mkwaju wa kiufundi uliofungwa na Issofou Boubacar baada ya Donald Ngoma kuchezewa vibaya na kuwa faulo ambapo Mniger huyo alimtungua kipa Said Mohammed 'Nduda'.
Kabla ya mabao hayo timu zote zilipoteza nafasi nyingi za wazi, huku Yanga ikionekana kuzinduka baada ya kutunguliwa kwa kipa wao Deogratius Munishi 'Dida' ambaye katika mechi sita za nyuma alikuwa hajaruhusu bao kabla ya Azam 'kumtengua udhu' katika sare ya 1-1.

AZAM HADI AIBU, YATUPWA MAPINDUZI CUP

*YANGA, MTIBWA HAOO NUSU FAINALI

AZAM aibu tupu! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mabingwa hao wa Kombe la Kagame  kuondoshwa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kufungwa mabao 2-1 na Mafunzo ya Zanzibar katika mchezo wa mwisho wa kundi B.
Kipigo hicho kilichopatikana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar imeifanya Azam kumaliza ikishika mkia wa kundi hilo na kuziacha Yanga na Mtibwa zitakazocheza usiku wa leo zikitinga nusu fainali kilaini na kusubiri tu kujua ipi itakuwa ya kwanza na nyingine ya pili.
Mafunzo ambayo haikupewa nafasi yoyote kwenye michuano hiyio na hasa kundi hilo la kifo, imeshika nafasi ya tatu ikiwa na pointi tatu, ingawa nayo imeaga michuano hiyo ya mwaka 2016.
Azam walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Kipre Tchetche katika dakika ya 21 kabla ya Mafunzo kurejesha bao hilo dakika ya 35 Rashid Abdallah na kufanya hadi mapumziko matokeo yalikuwa 1-1.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko ya wachezaji, lakini hakukuwa na jipya mpaka kwenye dakika ya majeruhi wakati mpira wa faulo wa Sadick Rajabu ulipotinga wavuni ukimuacha kipa mkongwe, Ivo Mapunda akiwa hana la kufanya langoni mwake.
Hicho ni kipigo cha kwanza kwa Azam kwa msimu huu, kwani ilikuwa haijafungwa katika mechi zake 13 za Ligi Kuu Bara na hata kwenye michuano hiyo ya Mapinduzi kwani ililazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Mtibwa na Yanga.
Msimamo
Kundi A
                 P  W  D L  F A Pts
Simba        2   1  1  0 3 2  4
JKU            2   1  0  1 4 3  3
URA           2   1  0  1 3 2  3
Jamhuri      2   0  1  1 2 5  1

Kundi B
                 P  W  D L F A Pts
Yanga        2   1  1  0 4  1  4
Mtibwa       2   1  1  0 2  1  4
Mafunzo     3   1  0  2 2  5  3
Azam         3   0  2  1  3 4  2

Wafungaji:
2-Donald Ngoma (Yanga)
   Awadh Juma (Simba)
   Villa Oromuchan (URA)
   Mohammed Abdallah (JKU)
    Kipre Tchetche (Azam)
1-Paul Nonga (Yanga)
  Hussein Javu (Mtibwa)
  John Bocco (Azam)
  Oscar Aggaba (URA)
  Emmanuel Martin (JKU)
  Said Bahanuzi (Mtibwa)
  Vincent Bossou (Yanga)
  Mwalimu Khalfan (Jamhuri)
  Ammy Bangaseka (Jamhuri)
  Nassor Juma             (JKU)
  Ibrahim Ajib             (Simba)
  Rashid   Abdallah (Mafunzo)
  Sadick Rajabu     (Mafunzo)

UTAMU WA LIGI DARAJA LA KWANZA UMEKAA HIVI!

Benchi la Ufundi la Africans Lyon

Wachezaji wa Akiba wa Ashanti Utd
LIGI Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) inatarajiwa kuingia kwenye ngwe nyingine wikiendi hii kwa mkichezo kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti nchini.
Timu za Ruvu Shooting, Oljoro JKT na Ashanti United zimeonyesha dhamira ya kurejea tena Ligi Kuu
kutokana na kuongoza kwenye makundi yao.
MICHARAZO inakuletea ratiba ya mechi zilizosalia za ligi hiyo ambayo inashirikisha jumla ya 24 zinazowania nafasi tatu za kupanda kwa ajili ya Ligi Kuu msimu wa 2016-2017. Sambamba na hilo pia unaweza kuchungulia msimamo wake kujua ligi hiyo muelekeo wake ukoje kwa timu shiriki, ingawa ndio kwanza imeanza ngwe ya duru la pili wiki mbili zilizopita.

Kundi A:
African Lyon FC (Dar es Salaam), Ashanti United SC (Dar es Salaam), Friends Rangers FC (Dar es Salaam),

Kiluvya United FC (Pwani), Kinondoni Municipal Council FC (Dar es Salaam), Mji Mkuu FC (Dodoma),

Polisi Dar es Salaam na Polisi Dodoma.

Kundi B:
Burkina Faso FC (Morogoro), Kimondo SC (Mbeya), Kurugenzi Mafinga FC (Iringa), Lipuli FC (Iringa),

Njombe Mji FC (Njombe), Polisi Morogoro na Ruvu Shooting (Pwani).

Kundi C:
Geita Gold SC (Geita), JKT Kanembwa FC (Kigoma), JKT Oljoro (Arusha), Mbao FC (Mwanza), Panone FC

(Kilimanjaro), Polisi Mara, Polisi Tabora na Rhino Rangers (Tabora).

Msimamo Kundi A
                                   P W  D  L   F   A  Pts
Ashanti Utd                  9  5  3  1   13  5  18
Kiluvya Rangers            9  4  4  1   9   4  16
Africans Lyon                9  4  2  2   10 6  14 
Friends Rangers            9  2  5  1   9   4  14
KMC FC                        9  3  3  3   6   7  12
Polisi Dar                      9  2  5  2   5   6  11
CDA                             9   2  2  5   7  12  8
Polisi Dom                     9  1  0  8  4   18  3

Msimamo Kundi B
                                    P  W  D  L   F  A  Pts
Ruvu Shooting              9   7   1  1   21 5  22
Njombe Mji                   9   5   1  3   10 8  16
Kurugenzi                     9   4   2  3   10 9  14
JKT Mlale                      9   3   4  2   10 7   13
Polisi Moro                    9   3   2  4   8  11  11
Lipuli Fc                        9   2   4  3   6  11 10
Kimondo                       9   3   1  5   5  12 10
Burkina Faso                 9   0   3  6   6  13  3

Msimamo Kundi C
                              P W  D  L  F   A  Pts
Oljoro JKT               9   5   3  1  9   7   18
Polisi Tabora            9   5   2  2  12  4  17
Geita Gold               9   4   4  1  13  6  16
Mbao FC                  9   3   3  3  11  15  12
Panone                   9   3   2   4  10 8  11
Rhino Rangers         9   1   6   2  4  7   9
Polisi Mara               9   1   5   3  6  9   8
JKT Kanembwa        9  0  3   6   4 13   3

Ratiba
Jan 9, 2016
Panone FC     v     JKT Kanembwa    
Polisi Mara     v     JKT Oljoro    
Rhino Rangers     v     Geita Gold FC    
Mbao FC       v     Polisi Tabora    
Mji Mkuu     v     Ashanti United    
Kiluvya United     v     Polisi Dar    
African Lyon     v     Friends Rangers    
Kiluvya United     v     Polisi Dar    
Polisi Morogoro     v     Lipuli FC                      
JKT Mlale     v     Kimondo FC    
Kurugenzi FC     v     Ruvu Shooting    
Njombe Mji     v     Burkinafaso FC    

Jan 16, 2016
Polisi Dodoma     v     KMC FC                      
Mji Mkuu     v     African Lyon    
Polisi Dar     v     Ashanti United    
KMC FC                       v     Kiluvya United    
Polisi Dodoma     v     Friends Rangers    
Njombe Mji     v     Kimondo FC    
Lipuli FC                       v     Kurugenzi FC    
JKT Mlale     v     Polisi Morogoro    
Rhino Rangers     v     JKT Kanembwa    
Mbao FC                       v     JKT Oljoro    
Panone FC     v     Geita Gold FC    
Polisi Mara     v     Polisi Tabora    

Jan 17, 2016
Ruvu Shooting     v     Burkina Faso

Jan 30, 2016
Polisi Morogoro     v     Kimondo FC    
Kurugenzi FC     v     Burkinafaso FC    
Lipuli FC        v     Ruvu Shooting    
Panone FC     v     Mbao FC      
Polisi Mara     v     Rhino Rangers    
Polisi Tabora     v     Geita Gold FC    

Feb 5, 2016
Polisi Dar     v     Mji Mkuu    
Ashanti United     v     Polisi Dodoma    

Feb 6, 2016
Kiluvya United     v     Polisi Dodoma    
Friends Rangers     v     Mji Mkuu    
Polisi Morogoro     v     Kurugenzi FC    
Kimondo FC     v     Burkinafaso FC    
Ruvu Shooting     v     Njombe Mji    
Lipuli FC                       v     JKT Mlale    
JKT Kanembwa     v     Mbao FC                      
Geita Gold FC     v     Polisi Mara    
JKT Oljoro     v     Rhino Rangers    
Polisi Tabora     v     Panone FC    

Feb 7, 2016
African Lyon     v     Kiluvya United    
KMC FC                       v     Friends Rangers    
Friends Rangers     v     Mji Mkuu    

Feb 13, 2016
Mji Mkuu     v     Ashanti United
Kiluvya United     v     Polisi Dar    
African Lyon     v     Friends Rangers    
Polisi Dodoma     v     KMC FC                      
Polisi Morogoro     v     Lipuli FC                      
JKT Mlale     v     Kimondo FC    
Kurugenzi FC     v     Ruvu Shooting    
Njombe Mji     v     Burkinafaso FC    
Panone FC     v     JKT Kanembwa    
Polisi Mara     v     JKT Oljoro    
Rhino Rangers     v     Geita Gold FC    
Mbao FC           v     Polisi Tabora    

Feb 20, 2016
Mji Mkuu     v     African Lyon
Polisi Dar     v     Ashanti United
KMC FC                      v     Kiluvya United
Polisi Dodoma     v     Friends Rangers
Njombe Mji     v     Kimondo FC    
Lipuli FC        v     Kurugenzi FC    
JKT Mlale     v     Polisi Morogoro    
Rhino Rangers     v     JKT Kanembwa    
Mbao FC      v     JKT Oljoro    
Panone FC     v     Geita Gold FC    
Polisi Mara     v     Polisi Tabora    

Feb 21, 2016
Ruvu Shooting     v     Burkina Faso FC

Feb 27, 2016
Polisi Dodoma     v     African Lyon
Kiluvya United     v     Mji Mkuu
Friends Rangers     v     Ashanti United
Polisi Dar     v     KMC FC       
Polisi Morogoro     v     Kimondo FC    
Kurugenzi FC     v     Burkinafaso FC    
JKT Mlale     v     Njombe Mji    
Lipuli FC       v     Ruvu Shooting    
Panone FC     v     Mbao FC     
Polisi Mara     v     Rhino Rangers    
Polisi Tabora     v     Geita Gold FC    
JKT Oljoro     v     JKT Kanembwa    

Mar 5,2016
African Lyon     v     Polisi Dar
Ashanti United     v     KMC FC   
Polisi Morogoro     v     Njombe Mji
Kurugenzi FC     v     JKT Mlale    
Burkinafaso FC     v     Lipuli FC      
Kimondo FC     v     Ruvu Shooting    
Rhino Rangers     v     Mbao FC     
Polisi Mara     v     Panone FC    
Geita Gold FC     v     JKT Oljoro    
JKT Kanembwa     v     Polisi Tabora    

Mar 12, 2016
Polisi Dar     v     Polisi Dodoma    
Mji Mkuu     v     KMC FC                      
African Lyon     v     Ashanti United    
Friends Rangers     v     Kiluvya United    
Mbao FC      v     Polisi Mara    
Polisi Tabora     v     JKT Oljoro    
JKT Kanembwa     v     Geita Gold FC    
Rhino Rangers     v     Panone FC    

Mar 13, 2016
Kimondo FC     v     Kurugenzi FC    
Njombe Mji     v     Lipuli FC      
Ruvu Shooting     v     Polisi Morogoro    
Burkinafaso FC     v     JKT Mlale    

Liverpool kuingia sokoni kusaka vifaa vipya

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/story_large/public/thumbnails/image/2015/10/31/14/CSpmUSYVAAAD4IX.jpg
Jurgen Klopp
HANA Ujanja. Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amekiri atalazimika kuingia sokoni ili kusajili wachezaji wapya kutokanana matatizo ya majeruhi kuzidi kuiandamana timu yake iliyopita ushindi juzi wa mkondo wa kwanza wa Nusu fainali ya michuano ya Kombe la Ligi (Capital One).
Liverpool iliikwanyua Stoke City kwa bao 1-0, huku nyota wake Philippe Coutinho na Dijan Lovren wakitolewa nje kutokana na majeraha ya msuli ya paja na Kolo Toure naye alimaliza mchezo huo akionekana kuwa na tatizo kama hilo.
Mara kadhaa Klopp amekuwa akidai kuwa hatanunua mchezaji mpya katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo. Lakini kutokana na majeruhi kuzidi kuongezeka, kocha huyo amefichua kuwa, anadhani anaweza kulazimika kuongeza nguvu katika kikosi chake.
Kuumia kwa Toure na Lovren kunaifanya Liverpool kukosa beki wa kati aliye fiti kwani Martin Skrtel na Mamadou Sakho nao pia ni majeruhi

Rafa Benitez hana kinyogo na Real Madrid

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01682/SNF0108A---_1682580a.jpg
Kocha Rafa Benitez
LICHA ya kumtimua kazi, Meneja wa zamani wa Real Madrid, Rafael Benitez ametoa ya moyoni kwa kuishukuru klabu hiyo kwa kumpa nafasi na kumtakia kila la kheri mrithi wake Zinedine Zidane. 
Benitez alitimuliwa Jumatatu  ikiwa ni miezi sba tu tangu alipokabidhiwa timu hiyo na nafasi yake kuchukua nguli wa klabu hiyo Zidane ambaye alikuwa akikinoa kikosi B cha Castilla. 
Kuanza kampeni za msimu huu kwa kusuasua kikiwemo na kipigo cha mabao 4-0 kutoka mahasimu wao Barcelona kulichangia kwa kiasi kikubwa kutimuliwa kwa Benitez, huku mgomo baridi katika vyumba vya kubadilishia nguo nao ukitajwa kuchangia pia. 
Lakini katika taarifa yake aliyotoa katika matandao wake, Benitez amewahakikishia kuwa hana kinyongo chochote kufuatia kutimuliwa kwake.  
Kocha huyo amesema imekuwa ni heshima kubwa kwake kupata nafasi ya kuinoa klabu hiyo hivyo anawashukuru viongozi, wafanyakazi, wachezaji na mashabiki kwa kumuunga kwao mkono katika kipindi chote alichokuwepo Santiago Bernabeu.
Chini ya Benitez, Real Madrid ilishindwa kupata ushindi katika mechi nane, saba zikiwa za La Liga na moja ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na sare ya 2-2 dhidi ya Valencia ilikuwa tiketi yake ya kutimuliwa klabuni hapo.

Tanzania yapanda nafasi 6 Fifa, Uganda noma!

Wachezaji wa Taifa Stars katika moja ya mechi zao za kimataifa
TANZANIA imepanda kwa nafasi sita kwenye msimamo wa Orodha ya Viwango vya Soka vya Dunia, ikishika nafasi ya 126 kutoka ile ya 132 iliyoshikilia Desemba mwaka jana.
Kwa mujibu wa orodha mpya iliyotolewa leo Alhamisi, Uganda imeweka rekodi ya kushika nafasi ya 62 ikiwa nafasi ya juu zaidi kuwahi kushikwa na taifa hilo la Afrika Mashariki ikipanda nafasi moja juu. Desemba ilikuwa nafasi ya 63, huku Rwanda, Kenya, Burundi na Ethiopia zikiifuata nchi hiyo katika orodha hiyo kwa nchi za ukanda huo wa Afrika Mashariki.
Ivory Coast, Algeria zimeendelea kukomaa kwenye nafasi zao mbili za juu sawa na ilivyo kwa Ghana na Cape Verde kwa upande wa Afrika zikishika nafasi ya 19, 28, 33 na 39 duniani, huku Ubelgiji anapotaka kwenda kucheza soka la kulipwa nyota wa Afrika na Tanzania, Mbwana Samatta ikiendelea kuongoza orodha hiyo ya ubora dunia wakifuatiwa na Argentina, Hispania na Ujerumani katika nafasi nne Bora.

Top 10 ya Dunia:

1. Ubelgiji
2. Argentina
3 Hispania
4. Ujerumani
5. Chile
6. Brazili
7.Ureno
8. Colombia
9.England
10. Austria

Top 10 ya Afrika:

1. Ivory Coast
2. Algeria
3. Ghana
4. Cape Verde
5. Tunisia
6. Senegal
7. Congo
8. Guinea
9. Cameroon
10. Misri

Top 10 ya Cecafa:

1. Uganda
2. Rwanda
3. Kenya
4. Burundi
5. Ethiopia
6. Tanzania
7. Sudan
8. Sudan Kusini
9. Djibout
10. Eritrea