STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 7, 2016

Liverpool kuingia sokoni kusaka vifaa vipya

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/story_large/public/thumbnails/image/2015/10/31/14/CSpmUSYVAAAD4IX.jpg
Jurgen Klopp
HANA Ujanja. Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amekiri atalazimika kuingia sokoni ili kusajili wachezaji wapya kutokanana matatizo ya majeruhi kuzidi kuiandamana timu yake iliyopita ushindi juzi wa mkondo wa kwanza wa Nusu fainali ya michuano ya Kombe la Ligi (Capital One).
Liverpool iliikwanyua Stoke City kwa bao 1-0, huku nyota wake Philippe Coutinho na Dijan Lovren wakitolewa nje kutokana na majeraha ya msuli ya paja na Kolo Toure naye alimaliza mchezo huo akionekana kuwa na tatizo kama hilo.
Mara kadhaa Klopp amekuwa akidai kuwa hatanunua mchezaji mpya katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo. Lakini kutokana na majeruhi kuzidi kuongezeka, kocha huyo amefichua kuwa, anadhani anaweza kulazimika kuongeza nguvu katika kikosi chake.
Kuumia kwa Toure na Lovren kunaifanya Liverpool kukosa beki wa kati aliye fiti kwani Martin Skrtel na Mamadou Sakho nao pia ni majeruhi

No comments:

Post a Comment