![]() |
| Jerome Boateng |
![]() |
| Alexander Gauland aliyetoa kauli za kibaguzi dhidi ya Jerome Boateng |
Gauland alikaririwa mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa asingependa kuwa rafiki au hata jirani na nyota huyo wa Bayern Munich ambaye ana asili Ghana.
Kauli hiyo ilizua mjadala mkubwa huku ikipondwa vikali na watu mbalimbali akiwemo Afisa Mkuu wa Ligi ya Soka ya Ujerumani-DFL aliyedai kuwa kauli hiyo mbaya na isiyovumilika.
Msemaji wa Kansela Merkel amesema 'bosi' wake amesikitishwa sana na kauli hiyo ikizingatiwa kuwa imetoka kwa mwanasiasa huyo anayeheshimika.
Boateng akihojiwa kuhusiana na suala hilo alisema amefarijika mno kuona watu mbalimbali wanavyopingana na kauli hiyo akiwemo kansela Merkel na kuongeza kuwa vita vya kupambana na ubaguzi wa rangi bao haijaisha.


LAZIMA iwashike. England imetangaza kikosi chake cha wachezaji 23 kwa ajili ya michuano ya Fainali za UEFA Euro 2016, huku chipukizi wa Manchester Utd, Marcus Rashford akijumuishwa katika kikosi hicho.
SIJUI ni mikosi au basi tu. Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Low amemuacha mshambuliaji wa Borussia Dortmund Marco Reus katika kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya michuano ya Euro 2016.
KAKATWA. Beki wa zamani wa Arsenal, Philippe Senderos ambaye amekuwa akihaha kurejea katika kiwango chake katika misimu ya karibuni, ameachwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Uswisi kwa ajili ya michuano ya Euro 2016.
WAKATI klabu nyingine zikienda likizo kwa ajili ya mapumziko ya Ligi Kuu Bara, Mbeya City haijalala kwani inatarajiwa kufanya ziara ya kisoka Malawi.