STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 8, 2013

Omar Omar mkali wa Mchiriku afariki dunia Dar

MSANII  nyota wa miondoko ya Mnanda a.k.a Mchiriku, Omari Omar amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Habari zilizoifikia MICHARAZO, asubuhii zinasema kuwa, Omar Omar aliyetamba na nyimbo mbalimbali ukiwemo ule maarufu wa 'Kupata ni Majaliwa' alifariki nyumbani kwao Temeke, saa chache baada ya kurejeshwa toka hospitali ya temeke alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.
Taarifa hizo zinasema kuwa mara baada ya kurejea nyumbani, msanii huyo alizidiwa na hatimaye kufariki na kwamba msiba wake upo nyumbani kwao Temeke Mikoroshini kwa ajili ya mipango ya mazishi.
Msiba wa msanii huo umekuja siku chache baada ya tasnia ya sanaa na burudani kumpoteza Juma Kilowoko 'Sajuki' msanii nyota wa filamu aliyefariki pia kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya muda mrefu.
MICHARAZO inawamuombea kila la heri Omar Omar na wengine waliotangulia mbele ya haki mapumziko mema katika safari yao ya Ahera. Innallillah Waina Illah Rajiun.
Taarifa zaidi tutakuwa tunawaletea kujua mkali huyo wa mduara aliyewafanya wasanii wengine kufuata mkondo wake akiwemo Dogo Mfaume, Ferouz, Easy Man na wengine.

Mayweather Jr, kuvaana na Guerrero Mei 4

BONDIA Floyd Mayweather Jr anatarajia kupanda jukwaani katika ukumbi wa MGM Grand, Las Vegas, Nevada, USA kuwania taji la WBC welterweight title May 4 ,2013 kuzipiga na Robert Guerrero bondia huyo ambaye ajawai kupigwa tangia angie katika uwanja wa masumbwi ya kulipwa tarehe 11-10-1996 bondia huyo alichezo mpambano wake wa mwisho May 5 mwaka jana na kutumikia kifungo cha Miezi mitatu kwa kosa la kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake mama watoto wake kwa sasa yupo katika maandalizi ya mpambano huo wa tarehe hiyo katika mchezo wake wa mwisho aliocheza na Miguel Cotto alipata ushindi mwembamba kwa kuibuka kumtwanga kwa point
www.superdboxingcoach.blogspot.com    BONDIA Floyd Mayweather Jr  anatarajia kupanda jukwaani katika ukumbi wa MGM Grand, Las Vegas, Nevada, USA kuwania taji la    WBC welterweight title May 4 ,2013 kuzipiga na Robert     Guerrero bondia huyo ambaye ajawai kupigwa tangia angie katika uwanja wa masumbwi ya kulipwa  tarehe 11-10-1996 bondia huyo alichezo mpambano wake wa mwisho May 5 mwaka jana na kutumikia kifungo cha Miezi mitatu kwa kosa la kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake mama watoto wake kwa sasa yupo katika maandalizi ya mpambano huo wa tarehe hiyo katika mchezo wake wa mwisho aliocheza na Miguel Cotto alipata ushindi mwembamba kwa kuibuka kumtwanga kwa point

LIONEL MESSI TENA MWANASOKA BORA WA DUNIA

Lionel Messi akifurahi baada ya kupokea tuzo yake ya nne mfululizo ya Ballon d'Or ya kwenye Ukumbi wa Convention Centre mjini Zurich Uswisi jana.
Lionel Messi akiwa kwenye tuzo za FIFA jana
Ronaldo, Iniesta na Messi wakiwa kwenye tuzo.
Kikosi XI cha FIFA kilichotangazwa jana. Kutoka kushoto mstari wa nyuma Cristiano Ronaldo, Marcelo, Sergio Ramos, Gerard Pique, Dani Alves, Iker Casillas. Mstari wa mbele kutoka kushoto: Radamel Falcao, Lionel Messi, Andres Iniesta, Xavi Hernandez na Xabi Alonso
Winga wa Fenerbahce, raia wa Slovakia, Miroslav Stoch akishukuru kwa tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka wakati wa sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.
Vicente del Bosque akishukuru baada ya kupokea tuzo ya Kocha Bora wa Dunia wa Mwaka 2012
Mwanasoka Bora wa Dunia wa zamani, Fabio Cannavaro wa Italia akionyesha jina la mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa Mwaka 2012, Lione Messi
Straika wa timu ya taifa ya Marekani, Abby Wambach akishukuru baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike wa Dunia

Mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama (kushoto) na mchezaji wa zamani wa Uholanzi, Ruud Gullit wakati wa kukabidhi tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka.

Mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama akisoma jina la mshindi wa tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka.

Fuleco, kikatuni cha fainali za Kombe la Dunia 2014 za nchini Brazil kikimkumbatia mwanasoka bora wa zamani Ronaldo stejini wakati wa sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.

Kocha wa timu ya taifa ya Brazi, Luiz Felipe Scolari na mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama wakipozi kwa picha

Straika wa Real Madrid, Mreno Cristiano Ronaldo na rafikiye wa kike Irina Shayk wakiingia kwenye sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.

Rais wa FIFA, Joseph Blatter akiambatana na muigizaji wa Kirafansa, Gerard Depardieu wakati akiwasili kabla ya kuanza kwa kwenye sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.
Waongozaji wa sherehe ya tuzo za FIFA Ballon d'Or, Ruud Gullit (kushoto) na Kay Murray wakiwa mzigoni

NYOTA wa Barcelona, Lionel Messi (25) jana aliweka rekodi ya kipekee ya kuwa mwanasoka wa kwanza duniani kutwaa tuzo ya Ballon d'Or ya Mwanasoka Bora wa Dunia kwa miaka minne mfululizo baada ya kuwashinda wapinzani wake Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Andres Iniesta wa Barcelona.
Muargentina huyo amekuwa mtu wa kwanza katika historia ya miaka 61 ya tuzo hiyo kuibeba mara nne mfululizo.
Johan Cruyff (1971, 1973, 1974) na Marco Van Basten (1988, 1989, 1992) wa Uholanzi, na Michel Platini wa Ufaransa walishinda tuzo ya Ballon d'Or mara tatu.
Mwanadada Abby Wambach wa Marekani alishinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike, wakati tuzo ya kocha bora wa kiume ilienda kwa Vicente Del Bosque wa timu ya taifa ya Hispania baada ya kuwashinda, Jose Mourinho wa Real Madrid ambaye alishasema mapema kwamba hatahudhuria sherehe hizo nchini Uswisi na Pep Guardiola.
Tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka
ilienda kwa winga wa Fenerbahce, raia wa Slovakia, Miroslav Stoch ambaye alifunga goli lake kwa kuunganisha moja kwa moja bila ya kutua chini mpira wa kona uliomfikia akiwa nje ya boksi. Stoch aliwaangusha Radamel Falcao aliyefunga goli la 'tik-taka' na Neymar aliyefunga goli katika mazingira magumu.
Kikosi cha wachezaji bora "First Eleven" wa dunia chote kimeundwa na nyota wanaocheza katika Ligi Kuu ya Hispania, huku Radamel Falcao pekee akitokea nje ya Barcelona na Real Madrid.
Real Madrid na Barcelona zimetoa wachezaji watano kila moja.

Kikosi Bora cha Dunia XI cha FIFA kilichotangazwa jana ni:

Kipa

Iker Casillas
Mabeki
Dani Alves, Marcelo, Sergio Ramos na Gerard Pique
Viungo
Xabi Alonso, Xavi Hernandez na Andres Iniesta
Washambuliaji
Cristiano Ronaldo, Radamel Falcao na Lionel Messi