STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, October 23, 2013

Yanga 'yaua' Taifa, Mnyama abanwa Tanga, Kiiza hashikiki


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imesahihisha makosa yake leo kwa kuicharaza Rhino Rangers ya Tabora kwa mabao 3-0 wakati Simba ikilazimisha suluhu jijini Tanga dhidi ya wenyeji wao Coastal Union.
Mabao mawili ya Hamis Kiiza kila moja katika kipindi na jingine la Frank Dumayo yalitosha kuwapa nafuu vijana na Ernie Brandts ambao Jumapili walishindwa kulinda ushindi wao wa mabao 3-0 na kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na watani zao Simba.
Kiiza akifunga bao la kwanza dakika ya 12 kwa krosi safi ya Simon Msuvah, goli lililodumu hadi kipindi cha kwanza kilipoisha.
Kipindi cha pili Yanga ilionekana kuzidisha mashambulizi dhidi ya wageni hao wa Ligi Kuu na kuongeza bao la pili dakika ya 73 kupitia Frank Domayo kabla ya Kiiza kurudi tena nyavuni dakika ya 81 na kuipa Yanga pointi tatu muhimu zilizowafanya wafikishe pointi 19.
Hata hivyo ushindi huo haukuisaidia Yanga kutoka nafasi ya nne kwani watani zao Simba waliongeza pointi moja wakiwa uwanja wa Mkwakwani Tanga baada ya kutoka suluhu na Coastal Union na kufikisha pointi 20 zilizowarejesha kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.
Simba imelingana pointi na Azam na Mbeya City, lakini Wekundu wa Msimbazi wana uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa na hivyo kurejea katika uongozi ikisubiri pambano lake la Jumapili dhidi ya Azam kwenye mfululizo wa ligi hiyo.
Katika pambano la Yanga na Rhino Brandts alipangua kikosi chake kwa kumpanga kipa Deo Munishi Dida, huku Ally Mustafa Barthez, Athumani Chuji na Nadir Cannavaro wakiwa nje ya dimba.

SHAMBA LINAUZWA

LIPO KISANGA KISARAWE MBELE YA KIWANDA CHA SIMENTI.
UKUBWA NI EKARI MOJA KASORO KIDOGO.
BEI SH.MILIONI 6 (MAELEWANO YAPO)
LIPO JIRANI NA BARABARA LINA MAZAO MBALIMBALI
KAMA MAFENESI, MACHUNGWA, MACHENZA NA MITI YA MINAZI.

WASILIANA KWA 0655 006971 AU 0755 006970
EMAIL: mkatedaniel@gmail.com

Arsenal yafa nyumbani, Chelsea yaua, Messi arejea na sare Barca

Roberto Lewandowski
 
Leveling up: Olivier Giroud celebrates making it 1-1
Giroud akishangilia bao lao
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Arsenal usiku wa kumkia leo imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kunyukwa mabao 2-1 na Borussia Dotmund katika mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bao la dakika za lala salama la Robert Lewandowski lilitosha kuizima Arsenal ilikuw aimeamini imambulia sare na wanafainali hao wa ligi ya msimu uliopita.
Henrikh Mkhitaryan aliifungia bao la kuongoza Borussia Dortmund kabla ya Olivier Giroud kusawazisha na katika dakika ya 80 Lewandowski akaiua Arsenal iliyokuwa dimba lake la nyumbani la Emirates.

Katika mapambano mengine, Chelsea iliifumua Schalke 04 ya Ujerumani kwa mabao 3-0, mshambuliaji Fernando Torres akitupia mawili na Eden Hazard moja, huku Lionel Messi alirejea uwanjani kwa kasi baada ya kuifungia Barcelona bao lililoipa sare ya ugenini dhidi ya Ac Milan baada ya kufungana bao 1-1.
Robinho alitangulia kuwafungia wenyeji bao dakika ya tisa na Messi kusawazisha dakika ya 24 baada ya kumalizia pasi ya Iniesta.
Nayo Steaua Bucuresti imetoka 1 - 1 na  Basel, Olympique Marseille imefungwa 2-1 na Napoli, Porto ikalala 1-0 mbele ya Zenit, Austria Wien imefungwa 3-0 na Atletico Madrid na Celtic imeshinda 2 - 1 dhidi ya Ajax.
Michuano hiyo itaendelea tena leo kwa michezo mingine nane, ambapo machoi yanaelekezwa katika pambano kati ya Real Madrid ya akina Cristiano Ronaldo na Gareth Bale watakaoikabili Juventus ya Carlos Tevez.