STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 7, 2014

Chelsea vs Stoke City, Arsena vs Covenrry City FA Cup

LONDON, England
IKIWA katika moto mkali vinara wa Ligi Kuu ya England Arsenal itawakabili Coventry City inayoshiriki Ligi Daraja la pili katika raundi ya nne ya Kombe la FA, huku Chelsea wakipangiwa kuvaana na Stoke City.
Arsenal iliwatoa  mahasimu wao wa mji wa London, Tottenham Jumamosi  na sasa itaavana na Coventry  na kutoa tumaini kwa timu hiyo kupenya kirahisi baada ya kulitwaa taji hilo mara ya mwisho mwaka 2005.
Mwkaa jana katika michuano hiyo Arsenal ilitolewa kwenye raundi ya tano na Blackburn Rovers na hivyo ni nafasi yao ya kuvuka hatua hiyo kuendea mafanikio ya mwaka 2005 ilipotwaa taji hilo, huku pia ikiwa katika mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu iliyopata kwa mara ya mwisho zaidi ya misimu mitano iliyopita.
Chelsea watawakaribisha Stoke, wakati Manchester City watacheza dhidi ya Bristol City ama Watford kama watawang'oa Blackburn katika mechi yao ya marudiano kwenye Uwanja wa Etihad baada ya kutoka sare ya 1-1 Jumamosi ugenini.
Mechi za raundi ya nne zitapigwa Januari 25 na 26.
Zawadi ya Swansea kwa kuwatoa Manchester United kwenye Uwanja wa Old Trafford juzi ni safari ya ugenini dhidi ya timu ya daraja la kwanza ya Birmingham City, Bristol Rovers ya daraja la tatu ama Crawley ya daraja la kwanza - kwani timu hizo mbili za mwisho hazijacheza mechi yao ya marudiano iliyoahirishwa.
Mabingwa watetezi Wigan watawakaribisha Crystal Palace kama watawafunga MK Dons katika mechi yao ya marudiano baada ya timu hizo mbili kutoka sare ya 3-3 Jumamosi.
Kikosi cha kocha Roberto Martinez cha Everton kitaenda kuikabili timu ya daraja la pili ya Stevenage, wakati Cardiff ya kocha Ole Gunnar Solskjaer itasafiri kwenda kucheza na timu ya daraja la kwanza ya Bolton Wanderers.
Liverpool, ambao waliifunga timu ya daraja la pili Oldham 2-0 Jumapili, watasafiri kuwakabili kati ya timu ya daraja la kwanza ya Bournemouth ya daraja la tatu ya Burton.
Hull City watasafiri kuivaa timu ya daraja la tatu ya Southend, ambayo inafundishwa na kocha wa zamani wa Hull, Phil Brown.
Timu mbili za "mchangani" bado zimo katika michuano hiyo, lakini zitahitaji kushinda mechi zao za marudiano za raundi ya tatu ili kuingia raundi ya nne.

RATIBA RAUNDI YA NNE:
Sunderland v Kidderminster or Peterborough
Bolton v Cardiff
Southampton v Yeovil
Huddersfield v Charlton or Oxford
Port Vale or Plymouth v Brighton
Nottingham Forest v Ipswich or Preston
Southend v Hull
Arsenal v Coventry
Stevenage v Everton
Wigan or MK Dons v Crystal Palace
Chelsea v Stoke
Blackburn or Manchester City v Bristol City or Watford
Bournemouth or Burton v Liverpool
Birmingham, Bristol Rovers or Crawley v Swansea
Sheffield United v Norwich or Fulham

Hivi ndivyo Waziri Mgimwa alivyozikwa mjini Iringa

Familia yake katika salamu za mwisho kabla kaburi lake halijafukiwa.
MAISHA katika uso wa dunia ya aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mbunge wa Jimbo la Kalenga, Dk William Mgimwa yamehitimishwa jana kijijini kwake Magunga wilayani Iringa mkoani Iringa.

Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda waliongoza watu wanaokadiriwa kuwa 10,000 kuupumzisha mwili wa Dk Mgimwa katika nyumba yake ya milele.

Pamoja na Rais na Waziri Mkuu, mawaziri mbalimbali, wabunge, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, watendaji wa wizara, na viongozi wa CCM na vyama vya upinzani walihudhuria mazishi hayo.
Rais Kikwete na wasaidi wake

Akiendesha ibada ya kumuombea marehemu, Msaidizi wa Makamu wa Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Songea, Julius Kangalawe aliomba Mungu awajalie na awape maisha marefu wanasiasa wanaohangaikia masikini.

“Siku hizi hakuna udugu, wenye nacho wanataka kuendelea kuwa nacho, watu wanaogopana, udugu umechakachuliwa na masikini wanaendelea kuwa masikini,” alisema.

Tofauti na viongozi wengi, alimsifu Dk Mgimwa kwa kuwa mnyenyekevu, mpenda watu na aliyetumia akili zake nyingi alizokuwa nazo kwa maendeleo ya watu.
 
Julius Kangalawe
“Umati huu mkubwa wa watu unadhihirisha jinsi Dk Mgimwa alivyokonga nyoyo za watu;inaonesha jinsi alivyokuwa mpenda haki, leo amepumzishwa katika nyumba yake hii, kesho hatujui nani atamfuata, lakini watakaomfuata wapo hapa hapa,” alisema.

Alimuomba Mungu awajalie watanzania wawe na siasa bora inayojali masikini kwa kuwa hiyo ndiyo njia ya kuwafananisha binadamu.
 
waombolezaji
“Leo hii wanasiasa  wanaingia katika ofisi zao baada ya kuomba Mungu kwa kutumia vitabu vitakatifu, lakini wengi wao ni waongo; wanatumia maandiko matakatifu kufanya udanganyifu, wakishakula kiapo, na vitabu vya Mungu wanatupa,” alisema.

Alisema pamoja na kiu kubwa waliyonayo watanzania ya kupata Katiba mpya, haiwezi kuwasaidia kwasababu bila Mungu hakuna linalowezekana.
 
Mwili wake ukipelekwa katika nyumba yake ya milele
“Hata katiba hiyo iwe nzuri kiasi gani, majambazi wataendelea kuwa majambazi, mafisadi vivyo hivyo na masikini wataendelea kudhulumia haki zao, kwasababu hakuna upendo wa Mungu,” alisema.

Alisema Katiba pekee inayoweza kumaliza matatizo ya watanzania ni zile sheria zilizoandikwa na Mwenyezi Mungu kwani ndizo zenye uwezo wa kubadili maisha.

Akitoa salamu za serikali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema afya ya Dk Mgimwa ilianza kuteteleka alipokuwa kikazi Marekeni mwishoni mwa mwaka jana.

“Serikali iliamua kumpeleka Afrika Kusini kwa matibabu, hata hivyo Mungu alimpenda zaidi na akayachukua maisha yake,” alisema.



Alisema Dk Mgimwa alikuwa mchapa kazi aliyeonesha muelekeo wa kuituliza serikali katika nafasi nyeti ya Waziri wa fedha.

“Serikalini tulianza kutulia, tukiamini wizara imepata mtu; kazi tuliyonayo ni kuenzi tunu alizokuwa nazo. Alikuwa mchapa kazi mwenye akili nyingi,” alisema.

Mwakilishi wa kambi ya Upinzani Bungeni, Mchungaji Peter Msigwa (MB) alisema taifa lilikuwa linamuhitaji Dk Mgimwa kwani alionesha tofauti kubwa na wazee wengine kwa kujali maendeleo ya watu.
 
“Alikuwa makini bungeni, aliacha itikadi za vyama alipokuwa akitekeleza majukumu yake, na mara kadhaa alikuwa akichukua hoja za wapinzani na kuzifanyia kazi,” Mchungaji Msigwa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini alisema.

Alisema binadamu hawajaumbwa ili kuleta matatizo kwa wengine na ndio maana thamani ya utu wao huhesabiwa kwa haki wanayotenda kama alivyokuwa Dk Mgimwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Christine Ishengoma alimkumba Dk Mgimwa kwa uchapi kazi wake huku akiwasilisha rambirambi ya Sh Milioni 5 kwa familia ya marehemu.

Akitoa shukrani za familia, mtoto wa Dk Mgimwa, Godfrey Mgimwa alizitaja kazi nyingi zilizkuwa zikitekelezwa na baba yake katika jimbo lake la Kalenga na kuiomba serikali kuziendeleza.

Kazi hizo ni pamoja na kusomesha watoto yatima, ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari, ujenzi wa miundombinu na mawasiliano, misaada kwa vikundi vya ujasriamali, na mkazo katika huduma za jamii ikiwemo afya, kilimo, na maji.
 
wafanyakazi wa wizara yake wakiweka mashada katika kaburi lake
Alisema siku kumi kabla ya kifo cha baba yake, alimwambia ameandaa mabati 120 anayotaka kuyagawa katika maeneo mbalimbali jimboni mwaka kwa lengo la kusukuma maendeleo.

Alimpongeza Rais Kikwete kwa upendo na ushirikiano aliotoa kwa familia yao katika kipindi chote ambacho baba yao alikuwa mgonjwa hadi kifo chake.

“Rais alionesha uzalendo na upendo wa hali ya juu kwani alimtembelea baba mara mbili akiwa amelazwa hospitalini,” alisema.

wawakilishi taasisi za fedha
Pamoja na Rais na Waziri Mkuu, mawaziri mbalimbali, wabunge, wakuu wa mikoa, watendaji wa wizara, na viongozi wa CCM walihudhuria mazishi hayo.
wakuu wa wilaya na mikoa
Joseph Mungai akiwakilisha wazee