STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 27, 2010

DC mikononi mwa Takukuru *Anawania ubunge viti maalum *Akamatwa na wapambe wake, fedha gesti

MKUU wa Wilaya ya Kasulu, Betty Machangu, ni miongoni mwa mavuno mapya ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) katika operesheni ya kukamata wagombea ubunge wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kugawa fedha.

Machangu alikamatwa juzi na maofisa wa Takukuru mkoani Kilimanjaro pamoja na vigogo wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) wa mkoani wa Kilimanjaro
na wa Wilaya ya Moshi Vijijini.

Mkuu huyo wa wilaya ambaye amejitosa kwenye kinyang’anyiro cha kusaka ubunge kupitia viti maalum mkoani Kilimanajro, alikamata na kuhojiwa kisha kuachiwa.

Machangu anadaiwa kutoa rushwa kwa wajumbe wa UWT mkoa ili wamchague.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Kilimanjaro, Alexander Budigila, aliwataja
watuhumiwa wengine kuwa ni Katibu wa UWT mkoa, Mariam Kaaya, Katibu wa
UWT wilaya ya Moshi, Hadija Ramadhani, mfanyabiashara wa Moshi
mjini, Hawa Sultani na dereva wa gari alilokuwa wakitumia, Swalehe
Twalibu.

Alisema Takukuru ilipokea taarifa kutoka kwa raia mwema za kuwepo vitendo vya rushwa katika nyumba ya kulala wageni ya Safari Resort, ambapo walikuwa wakigawa rushwa ya fedha na vitu kwa wajumbe kwa kila mmoja kuingia mmoja mmoja kuanzia majira ya saa 8:30 mchana.

Tarifa hiyo ilionyesha kuwa mgombea huyo na wafuasi wake walikuwa wakigawa fedha kiasi cha Sh. 100,000 na 50,000, kanga, asali na vipeperushi na kadi za wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT mkoa.

“Tuliizingira nyumba hiyo kuanzia majira ya saa nane hadi saa 10 ndipo tulipoingia ndani na kuwataka kufungua chumba namba 24 ambako
mgombea huyo na viongozi hao walikuwa wamejifungia huku dereva wa gari
lenye namba za usajili T 688 APQ aina ya Mitsubishi ambaye alikuwa anaimarisha ulinzi kwa kila anayefika,” alisema

Alisema walikaa kimya hadi saa 1:30 bila kufungua na ndipo maafisa wa
Takukuru walipojitambulisha na kugonga mlango kwa nguvu zaidi na
majira ya saa 2:15 usiku, ambapo ndipo walifanikiwa kuingia ndani na
kuwakuta watu wanne.

Alisema baada ya upekuzi walikuta Sh. 400,000 kwenye pochi ya katibu wa UWT, pea nne za vitenge, vipeperushi vya kumnadi mgombea
huyo, kadi za wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT mkoa ambazo zilitumbukizwa
kwenye chombo cha kuingiza maji chooni (tanki la chooni).

Alisema pia walikamata Sh.100,000 zikiwa kwenye pochi ya mgombea huyo, ambazo ziliwekwa kwenye bahasha na kuandikwa majina, lakini baada ya kuhisi watakamatwa walizitoa kwenye bahasha na
kuzichanachana na kisha kuzitupa chini ya uvungu wa kitanda.

Budigila alisema pia kwenye pochi ya katibu huyo walikuta vipeperushi
vya mgombea mwingine Regina Chonjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa UWT mkoa na walifanikiwa kulikamata gari hilo ambalo ni mali ya mgombea huyo.

Machangu akizungumza na wanahabari alisema kuwa majira ya saa 10 ndio
alikwenda kwenye baa hiyo kwa lengo la kupata chakula cha mchana na kwamba baada ya kufika alitafuta mahali penye utulivu, ili azungumze
na viongozi na msaidizi wake kabla ya kwenda kwenye mkutano wa kampeni.

Alisema walikosa pa kukaa na kumua kwenda kukaa chumbani na hakukua na
rushwa yoyote iliyotolewa kwa kuwa kila mmoja alikuja na mkoba wake na
hata kama angetaka kutoa rushwa angewafuata majumbani mwao.


Takukuru yashikiria saba

Wakati huo huo, Takukuru inawashikilia na kuwahoji watu saba waliodaiwa kuwa mabalozi, wajumbe wa vijiji na makatibu wa CCM katika kata ya Shirimatunda ambao wanadaiwa walikuwa wakila na kunywa na mgombea
udiwani mmoja.

Habari zinasema baada ya maafisa wa Takukuru kufika watu hao walikimbia akiwemo mgombea huyo na kwamba walifanikiwa kuwakamata watu hao kati
ya 30 waliokuwa wamekaa na mgombea huyo wakiwa na kikao cha kushawishi
mgombea huyo kupitishwa.

Kamanda wa Takukuru mkoani hapa alisema uchunguzi wa kina wa matukio hayo yote unaendelea na baada ya kukamilika watafikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria.

Dodoma wataka
matokeo yafutwe

Baadhi ya wagombea udiwani wa Viti Maalum kupitia UWT katika Wilaya ya Dodoma Mjini, wametaka matokeo yafutwe na uchaguzi urudiwe kutokana na uchaguzi huo kutofanyika kwa haki.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi ya CCM mkoa, mmoja wa wagombea hao, Catherine Mbiligwa, alisema uchaguzi huo haukuwa wa huru na haki kutokana na mmoja wa wasimamizi uchaguzi (jina tunalo) kutoa kauli za matusi kwa wagombea na wajumbe waliokuwepo kwenye uchaguzi huo.

Alisema moja ya sababu za kuomba uchaguzi huo kurudiwa ni kutokana na wagombea hao kutopata nafasi ya kuhesabu kura zao wala kuweka mawakala wao.

“Tulipojaribu kumuomba tuweke mawakala wetu kama haki yetu, tulifukuzwa kama mbwa na askari pamoja na katibu wa UWT wakishirikiana na msimamizi wa uchaguzi,” alisema.

Aidha, mgombea huyo alisema wakati wa kupiga kura pia hapakuwa na masanduku ya kutosha ya kuwekea kura, badala yake kura nyingine zililazimika kufungwa kwenye kanga za wajumbe.

Mgombea mwingine, Mwajuma Yame, alisema mbali na kutotendewa haki katika uchaguzi huo, pia hapakuwapo na uwiano wa nafasi za viti maalum kwa kila tarafa.

“Kila tarafa inatakiwa kuwa na madiwani watatu wa viti maalum, lakini tarafa zingine zina kata chache tofauti na Dodoma Mjini ambapo kuna kata takribani 20, lakini nafasi za viti maalum ni nne tu…Tunaomba uwiano,” alisema.

Akampeni harusini

Mgombea udiwani anaye maliza mda wake katika Kata ya Tambukareli Manispaa ya Dodoma, Edward Lamali, amejikuta akifanya kampeni katika ukumbi wa harusi.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Hall Cross, ambapo diwani huyo aliteuliwa na ndugu kutambulisha wageni pamoja na kuwapa nasaha maharusi katika maisha yao ya ndoa.

Diwani huyo alitoa utambulisho huo kama alivyoagizwa, lakini kabla ya kuhitimisha alianza kupiga kampeni kwa kuwataka wageni waalikwa kumpigia kura za maoni wakati utakapowadia.

Aliwaomba wamchague kwa mara nyingine ili aendelee kuyamalizia mambo ambayo alikuwa ameshaanza kuyatekeleza kwa kipindi kilichopita.

Mwangunga akumbana na Loliondo jimboni Ubungo
Mgombea wa ubunge Jimbo la Ubungo, Shamsa Mwangunga, amezidi kubanwa na wanachama baada ya kuambiwa kuwa kama alishindwa kuwasaidia Wamasai wa Loliondo mkoani Arusha wasinyang'anywe ardhi na mwekezaji, atawezaje kutatua kero zinazowakabili wananchi wa Mabibo, jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wanachama wa CCM alimbana mgombea Mwangunga ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii kwenye mkutano wa kujinadi wagombea uliofanyika Mabibo na kukutanisha matawi manne.

“Ukiwa kama Waziri wa Maliasili na Utalii ulishindwa kuwasaidia wafugaji hao ambao serikali ilidai kuwa waliingia eneo la hifadhi ya Taifa je, utaweza kutusaidia sisi?” alihoji mwanachama huyo.

Baada ya kuulizwa swali hilo, Mwangunga alishangaa kisha alimjibu kuwa wafugaji hao ndiyo waliovunja sheria na kuingia eneo la hifadhi hivyo serikali iliwaondoa kwa kuzingatia sheria.

Hata hivyo, mwanachama huyo alionekana kutoridhika na jibu hilo ingawa alilikubali na kukaa chini ili kumpa mwenzake aendelee kuuliza
swali lingine.

Maghari ya kifahari yatumika

Wakati huo huo, wagombea wa CCM wamezidi kuonyeshana ufahari wa kuwa na magari ya gharama wakati wa kampeni zao zinazoendelea maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam licha ya chama chao kuwataka wasitumie vyombo hivyo na badala yake wapande basi moja.

Baadhi ya magari hayo yaliyoonekana kuvinjari maeneo ya mikutano ni yenye namba za usajili, T 626 AEX aina ya Toyota Land Cruiser Prado, T 780 AZJ aina ya Nissan Patrol na T257 AQT Toyota Land Cruiser VX ambayo yalikuwa yakitumiwa na wagombea katika jimbo la Segerea.

Katika jimbo la Ubungo nalo, Mwangunga alionekana akiwa ndani ya gari lake aina ya Land Cruiser huku wagombea wenzake wakiwa kwenye basi la pamoja kama chama kilivyowataka kufanya.

Akizungumza na NIPASHE siku ya kwanza ya kuanza kampeni hizo, Katibu Msaidizi wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Abihudi Shilla, alisema wagombea wote hawaruhusiwi kutumia magari yao wala kuvaa suti au nguo nyingine tofauti na zile za chama.

Alisema chama kimeweka utaratibu huo ili wagombea wote waonekane wapo sawa kwa wanachama badala ya kila mmoja kufanya mbwembwe za kila aina ili kuwakoga wanachama.

Shy-Rose aibuka
na staili mpya

Mchakato wa kura za maoni kwa wagombea wa CCM Jimbo la Kinondoni umeendelea kuwa na vituko na moja ya matukio na vituko hivyo ni mmoja wa wagombea kutembea kwa gwaride mbele ya wanachama na kuwapigia magoti kuomba kura.

Mgombea huyo, Shy-Rose Bhanji, jana alitumia staili hiyo katika ukumbi wa DDC Magomeni Kondoa alipokuwa akiomba kura kutoka kwa wanaCCM wakazi wa Kata ya Ndugumbi.

Bhanji alitembea kwa gwaride wakati wa kujitambulisha na kupiga magoti kabla ya kuondoka kwa gwaride na kushangiliwa kwa makofi mengi.

Akijibu swali aliloulizwa la jinsi gani ataweza kupambana na dawa za kulevya na kitu gani alichowafanyia vijana kichama, Bhanji alisema kuwa atatetea kero mbalimbali ikiwemo ya kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana, kusaidia wajane kwa kuunda vikundi vya maendeleo.


Kigamboni wazozana

Kampeni katika Jimbo la Kigamboni jana zilikumbwa na mzozo baada wagombea ubunge kutaka kuwabana makatibu wa matawi na wanachama wao kususia kikao cha kampeni.

Matukio hayo yametokea katika mikutano ya katika Kata za Kibada na Mjimwema wakati wagombea hao walipokwenda kujinadi kwa wanachama.

Katika kata ya Kibada, wagombea ubunge walifika katika eneo la mkutano majira ya saa 4:00 asubuhi, lakini walijikuta wakiwa peke yao bila ya kupokewa na wenyeji, baada ya viongozi na wanachama kutokuwepo eneo hilo.

Kutokana na hali hiyo, baadhi walionekana kuja juu wakidai kuna dalili ya kuchezewa rafu, kwa sababu haiwezekani wasione hata mwanachama mmoja akiwa eneo la mkutano.

Juhudi za kusubiri wapiga kura ziligonga ukuta, baada ya mratibu wa kampeni hizo, Jimbo la Kigamboni, Sophia Kinega, kuwaagiza wagombea hao kujinadi mbele ya wanachama 50 pekee kati ya wapigakura 1,500 waliotakiwa kuwepo kwenye mkutano huo.

Akielezea tukio hilo, Mratibu huyo alisema hali hiyo ilisababishwa na makatibu wa matawi kususia kutoa taarifa kwa wanachama wao kwa sababu zisizoeleweka.

“Kwa kweli ni hali ya kusikitisha, nimewasiliana na katibu wa kata, lakini ameniambia makatibu wa matawi wamesusa na ndio maana hata wanachama hawakufika, jambo hili ni baya na ni lazima nilifikishe mbele,” alisema Kinega.

Mjumbe mmoja aliyejitaja kwa jina la Mohamed Namwogo, alisema kwa ujumla taarifa ya kuwepo kwa mkutano huo waliipata usiku na kusababisha wengi wao kushindwa kufika.


Nusura wapigane mkutanoni

Katika hatua nyingine, wagombea watatu nusura wapigane ngumi kwa madai kuwa mgombea mmoja alikuwa akieneza maneno yanayohusiana na ubaguzi wa kikabila.

Wagombea hao, John Kibaso na Magige Kiboko walimtuhumu Kazimbaya Makwega kwa kueneza maneno yanaoonyesha ishara ya kuwatenga kwa sababu wao wanatoka Mkoa wa Mara.

Tukio hilo lilitokea katika kituo cha Kata ya Mjimwema kabla ya kuanza kwa mkutano, ambapo wagombea hao walionekana kupandwa na hasira na kutishia kumtwanga ngumi kwa maelezo kuwa wamechoshwa na maneno yake.

“Haiwezekani bwana kila akisema utamsikia huyu mtu wa Musoma, sasa u-Musoma wetu unakuja vipi hapa, usitubabaishe bwana,” alisema Kibaso kwa hasira na kumfuata Makwega sehemu aliyokuwa amesimama.

Baada ya kuona hali imekuwa mbaya, baadhi ya wagombea waliingilia kati na kuwaingiza ndani ya gari wagombea hao na kuwasihi wapunguze jazba kwani wote ni wamoja.

Hata hivyo, wagombea wote walijinadi mbele ya wanachama na kuelezea mikakati na mipango yao ikiwa watachaguliwa.

Chanzo:GAZETI LA NIPASHE

Rais wa Tandale aja na filamu ya Mbagala


=============================


KIBAO cha 'Kwetu Mbagala' kinachozidi kutamba nchini cha msanii Naseeb Abdul 'Diamond' a.k.a 'Rais wa Tandale' kinatarajiwa kutengenezewa filamu itakayopewa jina hilo hilo la 'Mbagala'.
Akizungumza na Blog hii, Diamond, alisema tayari ameshaanza maandalizi ya kufyatua filamu hiyo ambayo itawashirikisha wasanii nyota wa fani hiyo akiwemo Jacqueline Wolper.
Diamond alisema lengo la kutoa filamu hiyo ni kutaka kufafanua ukweli juu ya kibao chake ambacho kimekuwa kikilalamikiwa na baadhi ya wapenzi na mashabiki wa fani hiyo wakazi wa eneo hilo la jijini wakidai amewadhalilisha.
"Baada ya kibao changu cha 'Mbagala' kutamba, natarajia kuja na filamu yenye jina hilo ambayo itawashirikisha wasanii kadhaa nyota, akiwemo Wolper, mimi mwenyewe na wengineo ambao wataifanya iwe ya kiwango," alisema Diamond.
Aliongeza kuwa kutoka kwa filamu hiyo kutamaliza 'ubishi' juu ya ukweli kama kibao chake cha 'Mbagala' kilikuwa kinalenga kuwadhalilisha wakazi wa Mbagala au alitumia jina hilo kupata vina vya wimbo huo, ilihali alikuwa akilenga maskani yake ya Tandale alipokulia.
"Mengi yamesemwa juu ya kibao hiki, lakini itakapotoka filamu yake ndio watu watajua mimi sikuwa na nia mbaya ya kusanifu kitongoji hicho, ila nililazimika kutumia jina lake kufikisha ujumbe juu ya mkasa wa kimapenzi na eneo letu nililokulia la Tandale," alisema

RATIBA LIGI KUU YA VODACOM 2010-2011







IFUATAYO NI RATIBA YA LIGI KUU YA VODACOM, VPL- 2010-2011 ILIYOTOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA, TFF, AMBAYO INATARAJIWA KUANZA AGOSTI 21, MWAKA HUU;


JUMAMOSI, Agosti 21
African Lyon v Simba
Polisi Dodoma v Yanga
AFC v Azam
Majimaji v Mtibwa Sugar
Toto African v Ruvu Shooting
Kagera Sugar v JKT Ruvu

JUMAMOSI, Agosti 28
Majimaji v African Lyon
Polisi Dodoma v Mtibwa Sugar
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Toto African v JKT Ruvu

JUMAMOSI, Septemba 4
Polisi Dodoma v Toto African
JKT Ruvu v Majimaji
African Lyon v AFC

JUMAMOSI, Septemba 11
AFC v Yanga
Azam v Simba

JUMATANO, Septemba 15
Kagera Sugar v Azam
Mtibwa Sugar v Yanga
Simba v Ruvu Shooting

Jumamosi Septemba 18
Toto African v Azam
Yanga v Majimaji
Ruvu Shooting v AFC
Mtibwa Sugar v Kagera Sugar

JUMAPILI, Septemba 19
Simba v Polisi Dodoma

JUMATATU, Septemba 20
African Lyon v JKT Ruvu

JUMATANO, Septemba 22
Ruvu Shooting v POlisi Dodoma
Yanga v Kagera Sugar
Majimaji v AFC

ALHAMISI, Septemba 23
JKT Ruvu v Mtibwa Sugar

IJUMAA, Septemba 24
Azam v African Lyon

JUMAMOSI, Septemba 25
Simba v Toto African
Majimaji v Polisi Dodoma

JUMAPILI, Septemba 26
Yanga v Ruvu Shooting

JUMATATU, Septemba 27
African Lyon v Kagera Sugar
AFC v Toto African

JUMANNE, Septemba 28
Azam v JKT Ruvu

JUMATANO, Septemba 29
Mtibwa Sugar v Simba

JUMAMOSI, Oktoba 2
Mtibwa Sugar v Toto African
Ruvu Shooting v African Lyon
Kagera Sugar v Polisi Dodoma
AFC v JKT Ruvu
Majimaji v Azam

JUMAMOSI, Oktoba 16
Simba v Yanga

JUMATANO, Oktoba 20
Simba v AFC
Mtibwa Sugar v Azam
Polisi Dodoma v African Lyon
Toto African v Kagera Sugar
Ruvu Shooting v Majimaji

ALHAMISI, Oktoba 21
JKT Ruvu v Yanga

JUMAMOSI, Oktoba 23
JKT Ruvu v Simba
Ruvu Shooting v Mtibwa Sugar
AFC v Polisi Dodoma
Toto African v African Lyon

JUMAPILI, Oktoba 24
Azam v Yanga
Kagera Sugar v Majimaji

JUMATANO, Oktoba 27
Toto African v Majimaji
Mtibwa Sugar v AFC
Yanga v African Lyon
Polisi Dodoma v Azam
Kagera Sugar v Simba

ALHAMISI, Oktoba 28
JKT Ruvu v Ruvu Shooting

IJUMAA, Oktoba 29
African Lyon v Mtibwa Sugar

JUMAMOSI, Oktoba 30
Azam v Ruvu Shooting

JUMAPILI, Novemba 7
Polisi Dodoma v JKT Ruvu
AFC v Kagera Sugar
Majimaji v Simba
Yanga v Toto

2011
JUMAMOSI, Januari 15
Azam v Kagera Sugar
Toto African v Polisi Dodoma
Majimaji v JKT Ruvu
AFC v African Lyon
Ruvu Shooting v Simba

JUMAPILI, Januari 16
Yanga v Mtibwa Sugar

JUMANNE, Januari 18
Simba v Azam

JUMATANO, Januari 19
Mtibwa Sugar v Polisi Dodoma
Ruvu Shooting v Kagera Sugar

ALHAMISI, Januari 20
African Lyon v Majimaji

IJUMAA, Januari 21
Yanga v AFC
JKT Ruvu v Toto African

JUMAMOSI, Januari 22
Yanga v Polisi Dodoma

JUMAPILI, Januari 23
Simba v African Lyon

JUMATATU, Januari 24
Azam v AFC

JUMATANO, Januari 26
Ruvu Shooting v Toto African
Mtibwa Sugar v Majimaji
JKT Ruvu v Kagera Sugar

JUMATANO, Februari 2
Azam v Toto African

JUMAMOSI, Februari 5
Majimaji v Yanga
Kagera Sugar v Mtibwa Sugar
AFC v Ruvu Shooting
Polisi Dodoma v Simba
JKT Ruvu v African Lyon

JUMAPILI, Februari 13
AFC v Majimaji
Mtibwa Sugar v JKT Ruvu
Polisi Dodoma v Ruvu Shooting

JUMATANO, Februari 16
African Lyon v Azam
Toto African v Simba
Kagera Sugar v Yanga

JUMAPILI, Februari 20
Kagera Sugar v African Lyon
Toto African v AFC
Polisi Dodoma v Majimaji
JKT Ruvu v Azam

JUMATANO, Februari 23
Toto African v Mtibwa Sugar
African Lyon v Ruvu Shooting
Polisi Dodoma v Kagera Sugar

JUMAPILI, Februari 27
Simba v Mtibwa Sugar

JUMATATU, Februari 28
Ruvu Shooting v Yanga

JUMANNE, Machi 1
JKT Ruvu v Ruvu Shooting

JUMATANO, Machi 2
Azam v Majimaji

JUMAMOSI, Machi 5
Yanga v Simba

JUMATANO, Machi 9
Kagera Sugar v Toto African
African Lyon v Polisi Dodoma
Majimaji v Ruvu Shooting

JUMAMOSI, Machi 12
AFC v Simba
Yanga JKT Ruvu

JUMAPILI, Machi 13
Azam v Mtibwa Sugar

JUMATANO, Machi 16
African Lyon v Toto African
Polisi Dodoma v AFC
Majimaji v Kagera Sugar
Mtibwa Sugar v Ruvu Shooting

JUMAMOSI, Machi 19
Majimaji v Toto African

JUMAPILI, Machi 27
Simba v Kagera Sugar

JUMATANO, Machi 30
Yanga v Azam
Ruvu Shooting v JKT Ruvu
AFC v Mtibwa Sugar

JUMAPILI, Aprili 2
Simba v JKT Ruvu

JUMATATU, Aprili 3
African Lyon v Yanga

ALHAMISI, APrili 7
Azam v Polisi Dodoma

JUMAMOSI, Aprili 9
JKT Ruvu v Polisi Dodoma

JUMAPILI, Aprili 10
Mtibwa SUgar v African Lyon
Kagera Sugar v AFC
Toto African v Yanga
Ruvu Shooting v Azam
Simba v Majimaji

Wanamichezo wauota ubunge 2010

MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Ismail Rage anaongoza orodha ya wanamichezo waliojitosa kwenye mchakato wa kuwania kuteuliwa kuwa wagombea na viti vya ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 31.
Rage anawania jimbo la Tabora Mjini kwa tiketi ya CCM, ambalo linashikiliwa kwa sasa na Juma Kaboyoga ambaye anakitetea kiti hicho.
Wanamichezo wengine wanaotaka ubunge ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mchezo Netiboli, CHANETA, Shy Rose Bhanji anayewania Jimbo la Kinondoni, Seneta wa zamani wa Yanga, Nasor Duduma na Mwenyekiti aliyemaliza muda wake katika klabu hiyo Imani Madega wao wamejitosa kwenye mbio hizo wakiwania Jimbo la Chalinze.
Wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Frrdirick Mwakalebela, aliyejitosa jimbo la Iringa Mjini, mkimbiaji bingwa wa zamani, John Bura aliyejitosa Jimbo la Karatu, Mkurugenzi wa Simba, Aziz Aboud aliyeomba katika jimbi la Morogoro Mjini.
Phares Magese, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Kikapu nchini, TBF, aliyejitosa Jimbo la Kigamboni.
Pia katika kinyang'anyiro hicho cha mbio za siasa, Mtangazaji wa Mtangazaji wa Channel Ten, Cyprian Msiba amejitosa Jimbo la Mwibara.
Majina ya wagombea wateule wa viti vya ubunge ndani ya CCM yanatarajiwa kutangazwa Agosti 1 baada ya kukamilika kwa kura za maoni za wanachama wa chama hicho.

Cheka amlaumu meneja wake

BINGWA wa dunia wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na mashirikisho ya ICB na UBO Francis Cheka amemlaumu meneja wake Juma Ndambile kwa kushindwa kumuandalia mapambano. Aidha, amedai anajuta kuingia nae mkataba ambao "unamfunga" bila faida.
Akizungumza na Micharazo, Cheka alisema katika kipindi cha mwaka mmoja alioingia mkataba na meneja huyo, ameshakosa michezo kadhaa ikiwemo pambano la kimataifa lililokuwa lifanyike Uingereza pamoja na mengine ya ndani.
Cheka, alisema hajui ni kwa nini meneja huyo anashindwa kumsaidia katika hilo wakati anatambua kuishi kwake kunategemea ngumi.
"Kwa kweli huwa najuta kwa nini niliingia mkataba na meneja huyu kwa jinsi anavyonizibia riziki zangu wakati hanitafutii mapambano ya kuniwezesha kuingiza fedha na pia kupima kiwango changu," alisema Cheka.
Aliongeza kuwa hata suala la malipo ya mishahara aliyokubaliana naye imekuwa ikilegalega na kusisitiza huenda asiongeze mkataba mpya na meneja huyo mara mkataba wa sasa utakapomaliza Desemba mwaka huu.
Hata hivyo Ndambile alisema madai ya Cheka ni ya "kitoto" kwa sababu yeye ni meneja na sio promota.
Wakati akiingia mkataba na bondia huyo alimlipa mishahara ya muda wa miezi sita pamoja na fedha nyingine za ziada kwa ajili ya dharura, alisema Ndambile.
Aliasema alimlipa mishahara ya miezi sita ambayo ni shilingi milioni 1.2 na kumpa dola za kimarekani 1,500 za maandalizi ya michezo atakayoipata na hivyo kushangazwa na tuhuma kwamba anamzungumza kumlipa chake.
"Anachokisema ni utoto, mimi sio promota ni meneja wake na unajua kazi za umeneja, hivyo sijui anataka nimfanyie nini," alisema Ndambile.
"Pia amekuwa akipata mapambano kibao, lakini amekuwa akiyakwepa kiasi cha kuwakera hata wadhamini waliojitolea kwa ajili yake."
Alisema bado anaendelea kumtambua Cheka kama bondia wake na ataendelea kumsimamia atakapopata mapambano kama mkataba unavyojieleza.

Friday, July 23, 2010

Mtoto wa Balozi Chokala ajitosa kumrithi Kimbisa



MTOTO wa Balozi Mstaafu Patrick Chokala, Simon Mashiku Chokala (28), amejitokeza kuchukua fomu za udiwani katika Kata ya Kivukoni kwa lengo la kumrithi Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa aliyekuwa diwani wa kata hiyo aliyeamua kujiweka kando.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya kurejesha fomu ofisi ya CCM kata ya Kivukoni, Chokala alisema lengo la kutaka kuongoza kata hiyo yenye ofisi ya Rais (Ikulu), ni kutaka kubadilisha mazingira ya kata hiyo.
"Kama kijana nimeamua kuchukua fomu ya udiwani ili niweze kuiweka kata hii katika mazingira ya kisasa zaidi...Ikulu ipo katika kata hii hata wageni wengi wa nchi lazima waje hapa, hivyo nimejipanga kuiweka sawa," alisema Chokala.
Alisema pamoja na Meya Kimbisa kuifanyia makubwa kata hiyo, bado anahitaji kuifikisha mbali zaidi kwa sasa.
Chokala ambaye baba yake akiwa Balozi nchini Urusi mwaka 2005, alijitokeza kuwania urais kupitia CCM, lakini alijitoa katika kura za maoni.
Akizungumzia taaluma yake, Chokala alisema alimaliza elimu ya msingi katika Bunge jijini Dar na kisha kupata elimu ya sekondari nchini Kenya kabla ya kuchukua digrii ya biashara nchini Urusi.
Aidha, alichukua mafunzo ya kompyuta nchini Urusi wakati baba yake, Balozi Chokala akiiwakilisha nchi huko.
Chokala anachuana na wagombea wengine waliojitokeza kuwania kiti hicho akiwemo Mbunge wa Afrika Mashariki, Didas Masaburi.
Meya Kimbisa ameamua kuwaachia vijana kuchukua fomu kuwania nafasi hiyo kwa madai anakwenda katika jimbo moja mkoani Dodoma kuwania Ubunge kupitia chama tawala.

Mwisho

Monday, July 19, 2010

Rage aupongeza uongozi mpya wa Yanga, amwagia sifa Nchunga



MWENYEKITI wa klabu ya soka ya Simba, Ismail Aden Rage, ameupongeza uongozi mpya wa watani zao Yanga na kumwagia sifa binafsi mwenyekiti mpya wa klabu hiyo, Lloyd Nchunga, akidai ni mchapakazi na muadilifu.
Akizungumza na Micharazo kwa njia ya simu kutoka Tabora, Rage alisema amefurahishwa mno na umakini wa wanachama wa Yanga wa kumchagua Nchunga na Davis Mosha kuwa viongozi wao kwa madai ni watu makini na watakayoiletea mabadiliko klabu yao.
Rage alisema binafsi anamfahamu Nchunga kutokana na kuwahi kufanya naye kazi na kumtaja kama kiongozi mchapakazi na muadilifu.
"Nawapongeza wana Yanga kwa umakini wao wa kumchagua Lloyd Nchunga kuwa mwenyekiti wao, namfahamu ni muadilifu na mchapakazi na naamini ataendeleza mauhusiano mema baina ya klabu zetu mbili za Simba na Yanga," alisema Rage.
Rage alisema Simba na Yanga ni watani wa jadi na sio maadui na hivyo kuingia madarakani kwa Nchunga na Davis Mosha pamoja wengine waliochagulia watalichukulia jambo hilo hivyo na kujenga umoja na mshikamano kwa lengo la kuendeleza soka la Tanzania.
Nchunga, alichaguliwa kuwa mwenyekiti baada ya kuwabwaga wagombea wenzake watatu, Abeid Abeid, Mbaraka Igangula na Edger Chibula, huku Francis Kifukwe akijiondoa wakati wa kujinadi, wakati Mosha alishinda umakamu mwenyekiti kwa kumshinda Constatine Maligo,.
Uchaguzi huo wa Yanga ulifanyika juzi kwenye uwanja wa PTA, Sabasaba Dar es Salaam, ambapo wagombea wengine nane kati ya 28 akiwemo Ally Mayay walichaguliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo.

M

Rage achukua na kurudisha fomu Tabora Mjini





MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Tabora, Ismail Aden Rage, mapema leo asubuhi amekuwa mtu wa kwanza kuchukua na kurudisha fomu ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Tabora Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi.
Akizungumza kwa simu kutoka Tabora, Rage, alisema alichukua fomu hiyo ya kuwania kiti hicho kinachoshikiliwa na Juma Siraju Kaboyoga majira ya saa 2;55 asubuhi na kuijaza kabla ya kuirudisha saa 5:30.
Rage alisema kuwa alikuwa ni mtu wa kwanza kujitokeza kuchukua fomu hiyo na pia amekuwa wa kwanza kuirudisha na matumaini yake ni kuibuka mshindi katika uteuzi wa CCM ili aweze kushiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 31.
"Nimekuwa mtu wa kwanza kuchukua na kurudisha fomu ya kuwania Ubunge Jimbo la Tabora Mjini, nikichukua muda wa saa tatu kuchukua na kurudisha fomu hiyo na tumaini langu kama ilivyokuwa uchaguzi wa mwaka 2000, naamini nitashinda," alisema Rage.
Katika uchaguzi huo wa mwaka 2000, Rage aliwania uteuzi wa CCM katika jimbo hilo na kuibuka na ushindi wa kishindo, lakini utaratibu wa chama chake uliliengua jina lake na kumpitisha aliyekuwa mshindi wa pili, Henry Mgombelo aliyekuja kuibuka mshindi wa kiti hicho.
Rage alisema ni yake ya kujitosa katika jimbo hilo ni kuipeperusha bendera ya CCM dhidi ya wapinzani na pia kutaka ridhaa ya wananchi ili awatumikie kama ambavyo amekuwa akijitolea kwa hali na mali kwao hata kabla ya kuwa mbunge.
Alisema kwa vile katiba ya nchi na demokrasia ndani ya chama chake inamruhusu yeyote kuwania uongozi naye haoni sababu ya kujiweka nyuma na haswa kusukumwa kwake na nia ya dhati ya kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo hilo.
Rage aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Wazazi-Tabora mwaka 2004 na kukitetea kjiti chake tena mwaka jana, alisema anaamini chama chake kitampa ridhaa ya kuongoza na wananchi wa Tabora Mjini hawatamuangusha Oktoba mwaka huu.
Mtetezi wa kiti hicho cha Ubunge wa Jimbo la Tabora, Juma Kaboyoga, ndiye aliyekuwa mtu wa pili kuchukua fomu majira ya saa 5:40, ingawa haikufahamika kama aliwahi kurejesha au la.

Mwisho

Wawili waiacha bendi ya Kalunde



Wanamuziki wawili wa bendi ya Kalunde ambayo iko chini ya ukurugenzi wa Deo Mwanambilimbi, wameondoka kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kufanya shughuli za muziki
Akizungumza na Micharazo, mkurugeni huyo aliwataja wanamuziki hao kuwa ni mwimbaji Sarafina Mshindo aliyetimikia Marekani na Bonny Kamplobo (solo) ambaye amekwenda Thailand.
Mwanambilimbi alisema wanamuziki hao wameondoka baada ya kupata baraka za uongozi wa bendi na kwamba watakapomaliza mikataba yao huko waliko watarudi kuendelea kazi katika bendi hiyo.
"Sarafina anaweza kukaa Marekani kwa muda mrefu, kutokana na mkataba alioupata, lakini Kamplobo
atarudi baada ya mwezi mmoja ujao kwani atakuwa anamaliza mkataba," alisema Mwanambilimbi.
Aliongeza kuwa Kamplobo amechukuliwa na Kanku Kelly ambaye kwa sasa wanafanya naye kazi ya muziki huko Thailand na kwamba ana uhakika mkataba ukiisha atarudi Kalunde.
Alifafanua kuwa wanamuziki hao wameondoka wakati bendi hiyo ikikamilisha albamu ya kwanza ya
'Hilda' ambayo baadhi ya nyimbo zake ni 'Itumbangwewe', 'Fikiria' na 'Umenigusa Nikakugusa'.
"Hii ndio albamu ya kwanza ya bendi ya Kalunde ingawa watu wengi huwa wanadhani kwamba Uchona ni albamu ya bendi, lakini ukweli ni kwamba bendi ilianzishwa wakati albamu hii ipo tayari mitaani," alisema.
Mwanambilimbi alizitaja baadhi ya nyimbo za albamu hiyo ambazo pia zimesaidia kuiweka juu bendi hiyo kuwa ni 'Siwezi Sema', 'Mwana Mpotevu', 'Chekacheka', 'Masikitiko' na 'Anitha'.
Bendi hiyo imekuwa ikitoa burudani kila Ijumaa katika ukumbi wa New Africa Hotel na kisha humalizia shughuli za burudani Jumapili, katika ukumbi wa Giraffe Ocean View, Mbezi Beach.

Pentagon, Shikito hawarudi Levent

WAIMBAJI wawili nyota wa bendi ya Extra Bongo 'Next Level', Athanas Thomas 'Shikito' na Ramadhan Mhoza 'Pentagon', wamesema kuwa hawana mpango wa kurejea katika bendi yao ya zamani.
Kabla ya kujiunga na Extra Bongo, waimbaji hao walikuwa kwenye bendi ya Levet Musica ya mjini Morogoro ambayo mwenzao Suzuki waliyekuwa naye Extra Bongo ameamua kurejea Levent.
Waimbaji hao wamemwambia mkurugenzi wao Ally Choki kuwa hawawezi kurudi Levent kwa sababu wana imani na uongozi wa Extra Bongo na hamu ya kuona mchango wao unasaidia bendi hiyo kusonga mbele.
Kauli ya waimbaji hao vijana imekuja wakati Extra Bongo leo ikitarajiwa kutua mjiji Morogoro kwa ajili ya onyesho moja linalofanyika katika ukumbi wa Savoy mjini humo.
Wakizungumza jijini Dar es Salaam, 'Pentagon' na 'Shikito' walisema kuwa sasa hawaoni kama kuna sababu ya wao kurudi tena Levent wakati mambo ndani ya Extra Bongo yakianza kunoga.
"Wakati mwingine kuhama kutoka bendi moja hadi nyingine ni kunamnyima mwanamuziki uzoefu, mimi na mwenzangu tumeamua kubaki Extra Bongo hadi kieleweke," alisema 'Shikito'.
Kwa upande wake 'Pentagon' alisema uongozi wa Extra Bongo hauna sababu ya kuwa na shaka juu yao kwamba huenda wakabaki Morogoro baada ya onyesho lao la leo.
Akizungumzia kauli hiyo, Ally Choki alisema yeye na viongozi wenzake wameipokea kwa moyo mkunjufu akisema kuwa safari ya mafanikio daima haikosi vikwazo wakati mwingine vya kuvunja moyo.
"Kwa kweli ni kauli ya kutia moyo, mimi pia nawaamini na kuwategemea sana wanamuziki wangu, natamani tuwe pamoja daima ili tufanikiwe kuivusha na kuifikisha mbali bendi yetu," alisema.

Dady, J-Mupa wote pamoja



WASANII wanaokuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya ambao kila mmoja anatamba na kibao chake, Leonard Fidelis 'Dady' na Juma Mussa 'J-Mupa' wanajiandaa kutoa albamu ya pamoja ya nyimbo 16.
Wakizungumza na Micharazo, wasanii hao, walisema albamu hiyo ya pamoja itakuwa na mchanganyiko wa miondoko tofauti ya R&B, Ragga na Hip Hop.
Dady anayetamba na kibao cha 'Ni Gani', alisema ana uhakika hiyo ya pamoja itawaweka kwenye matawi ya juu, kutokana na ukweli kwamba muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kutoka bila mafanikio.
Lakini sasa wameangukia mikononi mwa meneja wao mpya waliyemtaja kwa jina la Nassa na kwamba wana imani atasaidia kuhakikisha wanatoka upya na tena kwa kishindo.
"Baada ya kusota kitambo, hatimaye nimeachia kazi mpya iitwayo Ni Gani, huku nikiwa katika maandalizi ya kutoa albamu pamoja na mshirika wangu, J-Mupa, tutakayeshea nyimbo 16," alisema.
Dady alisema baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo ya pamoja ni kibao chao cha pamoja walichokitoa mwaka 2006 cha 'Uvumilivu', 'Upungufu', 'Inatosha', 'Rudi', 'Ni Gani', 'Namsaka' na nyinginezo.
Kwa upande wake J Mupa, anayetamba na 'Mzuri Yupi', alisema albamu yao hiyo huenda ikaleta mapinduzi kutokana na jinsi wanavyoumiza kichwa kuiandaa.
"Ni albamu bab' kubwa muhimu ni wapenzi na mashabiki kutupa sapoti ya kutosha ili tufanikiwe kutoka na kuwapa burudani murua," alisema J-Mupa ambaye pia hujihusisha na masuala ya filamu.

Diamond yaja na Power 2010


Diamond Musica yaja na Power 2010

BENDI ya Diamond Musica 'Vijana Classic', imeachana na mipango ya maandalizi ya kuzindua albamu ya pili ya 'Mapenzi Kitu Gani', badala yake sasa imeelekeza nguvu katika kuandaa albamu ya tatu.
Mkurugenzi msaidizi wa bendi hiyo Perfect Kagisa, ameliambia Micharazo Mitupu kuwa kwa vile nyimbo zao albamu ya pili zilishasikika sana redioni, kwenye televisheni na katika kumbi mbalimbali, haina haja kuizindua.
"Tumeamua kuandaa albamu nyingine kwa sababu pia bendi yetu ilifanya mabadiliko kwa kuleta wanamuziki wapya, ndipo tukaona kuwa tuanze pia na vitu vipya," alisema Kagisa.
Kagisa alizitaja baadhi ya nyimbo ambazo bendi hiyo imezikamilisha kwa ajili ya albamu ya tatu kuwa ni 'Power 2010', 'Kovu', 'Supu ya Kongolo' na 'Abdulkarim'.
Alisema wanamuziki wa bendi hiyo wanajiandaa kushuti video ya wimbo wa 'Power 2010' na kwamba kazi hiyo ya kushuti itafanyika wiki ijayo ili uanze kurushwa kwenye vituo mbalimbali vya televisheni.
"Hii intro ya Diamond Musica, ndio maana tumeamua kuanza nayo na kisha nyimbo nyingine zitafuata katika mpangilio wetu wa kurekodi nyimbo za albamu ya tatu," alisema.
Diamond Musica ilitua jijini Dar es Salaam zaidi ya miaka mitatu iliyopita ikitokea Zimbabwe ikiwa na albamu ya kwanza iliyopewa jina la 'Swali' ambayo hata hivyo, haikuitambulisha vyema bendi hiyo.
Baada ya hapo wanamuziki walikuna vichwa na kuibuka na albamu ya pili ya 'Mapenzi Kitu Gani' na kuifanya uanze kukwea matawi ya juu, lakini hadi sasa albamu hiyo haijazinduliwa.
Hata hivyo, mkurugenzi huyo alisema kuwa licha ya kuandaa albamu nyingine, zile za albamu ya pili zitaendelea kupigwa kwenye kumbi za burudani na kuuzwa madukani kama kawaida.

Ndumbaro bado alia na Boban



WAKALA wa kimataifa wa wachezaji anayetambuliwa na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Damas Ndumbaro, amezidi kulia na kiungo Harun Moshi 'Boban' akidai mchezaji huyo ana desturi ya kutoheshimu mikataba kama alivyofanya kwa kuitosa klabu ya GIF ya Sweden.
Akihojiwa na kituo kimoja cha redio, Ndumbaro alisema pamoja na Boban kujitetea kuwa kilichomkimbiza Sweden ni kukiukwa kwa mkataba baina yake na klabu hiyo, lakini ukweli ni kwamba inaonekana suala la kutoheshimu ni kawaida ya kiungo huyo mahiri.
Ndumbaro alisema kwa kumbukumbu zake kutaka kuvunja mkataba dhidi ya GIF ni mara ya tatu kwa Boban, kwani alishawahi kufanya hivyo pia alipoenda kucheza soka la kulipwa Arabuni na pia Ethiopia.
"Hili sio jambo la bahati mbaya ni wazi ni Boban ana kawaida ya kutoheshimu mikataba kwani alishawahi kuvunja alipoenda Arabuni na kuiponza klabu yake ya Simba kulipa gharama za huvunjwaji huo wa mkataba huo, pia alifanya hivyo alipokuwa Ethiopia," alisema Ndumbaro.
Wakala huyo alisema dai kwamba labda Boban hakuuelewa mkataba huo wa miaka miwili si sahihi kwa vile alisimamiwa na mwakilishi wa Academy yake anayezungumza kiswahili na ndipo aliposaini na kuanza kuitumia klabu hiyo.
Ndumbaro alisema pengine yale mazoea na kuwakosa 'washkaji' zake wa vijiweni kama anavyokuwa nchini ndio kilichochangia kiungo huyo kurejea nchini ghafla, ingawa Boban alinukuliwa akisema kuwa malipo kiduchu ndicho kilichomrejesha Bongo.

Mwisho

Boban awagawa wadau wa soka nchini



UAMUZI wa kiungo nyota wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Harun Moshi 'Boban' kuamua kurejea nchini kwa kuvunja mkataba na klabu yake ya GIF ya Sweden umewagawa wapenzi na wadau wa soka nchini baadhi wakimuunga mkono wengine wakimshangaa.
Baadhi ya wadau wamedai kitendo cha Boban kurejea ghafla nchini na kuiacha timu yake ya GIF ni kuonyesha jinsi wachezaji wa Kitanzania wavumilivu au kuwa tayari kucheza soka la kulipwa kama wenzao wa mataifa mengine.
Mmoja wa wajumbe wa kamati ya fedha ya klabu ya Simba Onesmo Wazir 'Ticotico'alisema hata kama kulikuwa na matatizo yaliyomkera Boban alipaswa kuzungumza na wakala wake kuona namna ya kutatua ikiwemo kuhamishwa klabu nyingine ya nje kuliko kurejea nchini.
"Unajua nafasi ya kucheza soka la kulipwa nje huja kwa nadra sana na ilipaswa Boban kutumia nafasi hiyo kuangalia mbele katika kipaji chake badala ya kukimbilia kurejea nchini ili kuendelea kuchedza soka la sifa kwa klabu za Simba na Yanga," Ticotico alisema.
Hata hivyo Kocha Mkuu wa timu ya TMK United, Kennedy Mwaisabula, alisema binafsi haoni sababu ya Boban kulaumiwa, iwapo hakuona faida ya kuendelea kucheza soka la kulipwa katika klabu hiyo ya Sweden kutokana na kuonyesha hakuufahamu vema mkataba wake.
Mwaisabula alisema huenda wakala wake, Damas Ndumbaro hakuwa muwazi kwa kiungo huyo na yeye alipoona mambo yapo ovyo hakuona sababu ya kuendelea kuwepo huko, huku akisema uamuzi wa kurejea nchini kucheza soka sio wa ajabu kwani ni suala lake binafsi.
"Sioni sababu ya kumshutumu na kumdhalilisha Boban, kurudi kwake ni sahihi na hasa baada ya kukaa nae kwa saa zima na kuzungumza nae akieleza kila kitu na sio kweli kama kaikimbia baridi au kuwakumbuka washkaji zake," alisema Mwaisabula.
Kocha huyo aliyewahi kuzinoa Yanga na Bandari Mtwara, alisema huenda Boban ameona soka la Bongo linalipa kuliko huko Sweden kwani kabla hajaenda huko tayari alishakuwa na uwezo wa kiuchumi akimiliki nyumba na gari la kisasa.
Mwaisabula alisema pia Boban hatakuwa mchezaji wa kwanza kucheza soka la nyumbani badala ya nje ya nchi akiwataja, Tresot Mputu wa DR Congo, Mohammed Abutrika wa Misri aliodai pamoja na uwezo wa kisoka hawajahi kuwaza au kwenda kucheza soka la kulipwa licha ya kuwindwa na klabu mbalimbali maarufu za Ulaya.

Mwisho

Njoroge apigiwa ramli Jangwani



HATMA na uwepo wa beki wa kimataifa wa Yanga, Mkenya John Njoroge ndani ya klabu hiyo bado haieleweki, kutokana na uongozi wa klabu hiyo kudai unasubiri maamuzi ya kocha wao, Kostadin Papic
Njoroge aliyetua Yanga akitokea Tusker ya Kenya, kwenye usajili wa dirisha dogo msimu uliopita, amekuwa akitajwa ataachwa ili kutoa nafasi ya kusajiliwa kwa kipa Mserbia, Ivan Knezevic kutekeleza kanuni mpya ya usajili inayosisitizwa na Shirikisho la Soka nchini, TFF.
Kanuni hiyo ya usajili inaelekeza klabu zote za ligi kuu kusajili wachezaji wa kigeni wasiozidi watano, kitu ambacho ndicho kinachomchanganya kocha wa Yanga, kuamua nani abaki na nani aondoke klabuni hapo.
Msemaji wa Yanga, Louis Sendeu aliliambia Micharazo kuwa, pamoja na kwamba usajili wao unaelekea kukamilika vema, lakini hadi sasa haijafahamika nani na nani katika wachezaji wageni watakaokuwa kwenye kikosi hicho hadi kocha wao atakapoamua.
Sendeu alisema kutokana na hilo, ndio maana inakuwa vigumu kwao kuweka bayana kama itamuacha Njoroge au la ambaye ilielezwa awali angeungana na mastaa wengine wa kigeni waliotupiwa virago katika timu hiyo.
"Aisee ni vigumu kuweka bayana juu ya hatma ya Njoroge, tunasubiri suala hilo liamuliwe na kocha na nasisitiza kuwa lolote linaweza kutokea katika usajili huo mpya wa timu yetu ambao utatangazwa wakati wowote kuanzia sasa baada ya kukamilika," alisema Sendeu.
Tayari uongozi wa Yanga umejinasibu kuwasainisha wachezaji wanne kutoka Ghana, kipa Yew Berko, mlinzi, Isaac Bokye, kiungo Ernest Boake na mshambuliaji Kenneth Asamoah, huku ikidaiwa kukaribia kumalizana na kipa Knezevic aliyetua wiki iliyopita kwa majaribio.
Iwapo kipa huyo atasajiliwa ili kuziba nafasi ya Obren Curcovic basi ni lazima kati ya Waghana wanne au Njoroge, mgeni pekee aliyebakishwa kikosi kilichopita mmojawao jina lake likatwe.
Yanga inayoendelea na mazoezi yao katika uwanja wa Uhuru, imedaiwa tayari imewanasa Nsa Job, Yahya Tumbo, George Minja, Chacha Marwa, Stephano Mwasika, Omega Sunday na Salum Telela kwa ajili ya kikosi kipya kuungana na nyota wengine walisalia msimu uliopita.

Mwisho

Diamond kutangaza utalii wa ndani



MSHINDI wa tuzo tatu za muziki nchini na Balozi wa Malaria, Naseeb Abdul 'Diamond' ameingia makubaliano ya mwaka mmoja na waandaaji wa shindano la Miss Utalii Tanzania kwa nia ya kuhamasisha utalii wa ndani sambamba na kuendelezxa vita dhidi ya malaria.
Habari zilizopatikana jijini na kuthibitishwa na Rais wa Miss Utalii, Gideon Chipungahelo, zinasema lengo la kamati hiyo kumshirikisha Diamond ni kuunganisha nguvu za sanaa ya muziki na urembo wa kitalii katika kuunga mkono juhudi za serikali za kukuza sekta ya utalii na utamaduni pia vita dhidi ya ugonjwa hatari wa malaria nchini na Africa kwa jumla.
Katika makubaliano ya awali kati ya wawili hao ni kwamba Diamond atafanya ziara ndefu maalum ya uhamasishaji itakayofahamika kwa jina la Diamond Tanzania Kamwambie Tour-Malaria Inaua Utalii ni Maisha'.
Pia msanii huyo aliyengara kwenye tuzo za Kilimanjaro Music Awards-2010, atatunga kibao maalum kwa ajili ya Miss Utalii Tanzania 2010 ambao ataimba na kurekodi pamoja na warembo wote wa Miss Utalii Tanzania wanaoshiriki fainali za mwaka 2010.
Kibao hicho ndicho kitakachotumika katika fainali za shindano hilo zitakazofanyika Septemba mwaka huu kwa kushirikisha jumla ya warembo 60 toka kanda na mikoa mbalimbali.
Washindi wa fainali hizo za Taifa watawakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya Dunia na ya kimataifa 2010 na 2011 yakiwemo ya Miss Heritage World 2011,Miss Tourism University World 2011,Miss Globe International 2010,Miss United Nation 2010,Miss Tourism World 2010 na Miss University africa 2011.
Rais wa Miss Utalii alithibitisha kuwepo kwa makubaliano hayo na Diamond, ingawa msanii huyo mwenyewe hakuweza kupatikana kufafanua juu ya suala hilo.

Mwisho

Mabingwa Ngumi EA kusakwa wiki ijayo





TIMU mbili za taifa za mchezo wa ngumi wa ridhaa zinatarajiwa kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya ngumi ya Mabingwa wa Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati itakayofanyika jijini Arusha kuanzia Julai 26 mwaka huu.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Mashanga Makore, alisema, Tanzania kama mwenyeji wa michuano hiyo itawakilishwa na timu mbili zilizopewa majina ya Tanzania A na B zitakazokuwa na wachezaji karibu 39.
Makore alisema timu ya taifa A itakuwa na wachezaji 19 wakati ile ya pili yaani Taifa B itakuwa na mabondia 20.
"Kutokana na uwenyeji wetu wa michuano ya ngumi ya Mabingwa wa Mabingwa wa nchi za Afrika Mashariki na Kati, tunatarajiwa kuwakilishwa na timu mbili na tayari timu hizo zimeshaanza mazoezi tangu wiki iliyopiuta kujiandaa na michuano hiyo," alisema Makore.
Makore alisema mazoezi ya timu hizo yanaendelea chini ya makocha wazawa, ambao wanawasiliana kila mara na kocha mkuu wa timu hizo, Mcuba Geovanis Hultado ambaye yupo mapumziko nchini kwao.
Katibu huyo alisema imani ya BFT ni kuona Tanzania inafanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo, ikizingatiwa kuwa wao ni wenyeji na pia itawakilishwa na timu nyingi tofauti na wapinzani wao.
Kuhusu maandalizi ya michuano hiyo, Makore alisema yanaendelea vema ikiwemo timu zote tano za Afika Mashariki kuthibitisha ambazo ni wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.


Mwisho

Nukuu kali za kukumbukwa Kombe la Dunia 2010





JOHANNESBURG, Afrika Kusini
MAKOCHA na wachezaji wamekuwa wakizungumzwa mara kwa mara, si kwa sababu ya viwango vyao uwanjani pekee, bali pia kwa sababu ya kauli zao za nje ya uwanja. Zifuatazo ni nukuu kali za kukumbukwa zilizowahi kutolewa nao wakati wa michuano ya mwezi mmoja ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini.

Milovan Rajevac
* "Nyie watu, hebu tumieni akili. Yeye si shujaa, yeye ni muongo mkubwa. Ni mkono gani wa Mungu? Ule ni mkono wa shetani," kocha wa Ghana, Mserbia Milovan Rajevac, alisema kuhusy mshambuliaji wa Uruguay, Luis Suarez, ambaye alizuia kwa mikono mpira uliokuwa ukivuka mstari wa goli katika dakika ya mwisho ya muda wa nyongeza kwenye mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Dunia.
‘Mkono wa shetani’ wa Suarez uliinyima Ghana nafasi ya kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kufuzu kwa nusu fainali ya Kombe la Dunia.


Patrice Evra
* "Tunajihisi kama taifa dogo la mchezo wa soka na hili linaumiza. Hakuna cha kuelezea zaidi ya kusema kwamba hili ni balaa," nahodha wa Ufaransa, Patrice Evra, akielezea kwa uwazi hitimisho la kiwango chao kibovu katika fainali zilizomalizika za Kombe la Dunia 2010. Ufaransa, sio tu ilimaliza ikiwa mkiani katika kundi ambalo ilitarajiwa kuwa kinaea, lakini pia ilikumbwa na kashfa ya wachezaji wake kugomea mazoezi kufuatia kutimuliwa kikosini kwa mshambuliaji Nicolas Anelka.

Jean-Louis Valentin
* "Hawataki kufanya mazoezi, ni kashfa. Najiuzulu, naachoa ngazi kwenye shirikisho. Hapa sina zaidi cha kufanya. Narudi zangu Paris," Mkurugenzi wa timu ya Ufaransa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Soka la Ufaransa, Jean-Louis Valentin, alisema baada ya wachezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa kugomea mazoezi kufuatia kutimuliwa kikosini kwa Anelka.

Diego Maradona
* "Hii ilikuwa ni (kama) ngumi kutoka kwa Muhammad Ali. Sikuwa na nguvu yoyote ile. Siku niliyostaafu soka ingeweza kufanana na hii, lakini hii ya leo ni mbaya zaidi," Maradona alisema baada ya Argentina kupata kipigo kikali cha 4-0 kutoka kwa Ujerumani, kipigo kibaya zaidi kwao katika fainali za Kombe la Dunia tangu waliposhindiliwa kwa magoli 6-1 katika mechi ya michuano hiyo dhidi ya Czechoslovakia mwaka 1958.

Dunga
* "Siku zote tunatakiwa kushinda, lakini hata tunaposhinda, hawatufurahii kwa madai kwamba hatuchezi soka la kuvutia. Tukicheza soka la kuvutia, hawafurahi kwa sababu hatushindi kwa magoli mengi kama sita au saba hivi. Tukishinda kwa magoli sita au saba, wanaibuka tena na kusema wapinzani wetu ni dhaifu," alisema kocha wa Brazil, Dunga, akidai kwamba hata siku moja, vyombo vya habari huwa haviridhiki.

Gennaro Gattuso
* "Miaka minne iliyopita tuliheshimiwa kwa kuwa mabingwa, leo hii tunacheza hovyo kama mabeberu ya mbuzi vile," kiungo wa Italia, Gennaro Gattuso, alisema katika tathmini isiyo ya kawaida ya kujishutumu binafsi kwa kiwango cha hivyo kiichoonyeshwa na timu yao iliyokuwa ikitetea ubingwa wa fainali za Kombe la Dunia na kumaliza ikiwa mkiani katika Kundi lao.

Howard Webb
* "Anashindwa hata kuwaongoza watoto wake mwenyewe. Sijui anamudu vipi jukumu la kuongoza mchezo wa soka uwanjani," mke wa refa aliyechezesha mechi ya fainali ya Kombe la Dunia, Howard Webb, alisema kabla ya mechi hiyo ya fainali iliyozikutanisha timu za mataifa ya Hispania na Uholanzi.

Cristiano Ronaldo
* "Maholi, kama gwiji mmoja wa soka alivyowahi kuniambia, huwa yanafuatana ... wakati mwingine, kadri unavyojaribu kuhaha ili ufunge, hayaji, na wakati yanapokuja, yanakuja mengi kwa wakati mmoja," alisema mchezaji wa bei mbaya zaidi duniani, Cristiano Ronaldo wa Ureno, kuelekea mechi yao ufunguzi ya hatua ya makundi ya Kombe la Dunia. Kiwango cha Ronaldo katika michuano hiyo ya Kombe la Dunia kilikuwa cha hovyo, huku mshambuliaji huyo akifunga goli moja pekee.

Roger Milla
* "Kwa hakika hakuna anayeweza kucheza kama mimi! Mauno yangu yalikuwa ya kwanza, tena ya ubunifu kabisa. Unahitaji kunengua kiasili, kuchezesha nyonga. Yote ni kuhusiana na uasili wa mguso binafsi, na inatakiwa uwe na mshawasha kutoka moyoni, iwe ni kitu chako mwenyewe. Na hakika, vilevile unapaswa kufunga goli kwanza, usisahau jambo hilo!" alisema Roger Milla kuhusiana na ushangiliaji wake wa goli kwa kukata viuno.
Mauno ya Milla kwenye kibendera cha kona kila mara alipofunga goli yalikuwa maarufu kama magoli yake aliyoifungia Cameroon wakati nchi hiyo ilipotinga robo fainali za Kombe la Dunia mwaka 1990.

England v Ujerumani
* "England walianzisha soka, lakini Ujerumani wanashinda soka", ulisema utani wa zamani uliotumika wakati wa fainali za Kombe la Dunia kuelezea ushindi wa kishindo wa Ujerumani wa 4-1 dhidi ya mahasimu wao wa jadi katika hatua ya 16-Bora ya Kombe la Dunia.

Sepp Blatter
"Itakuwa ni upuuzi kutolifungua tena jalada la mapendekezo ya kutaka kutumiwa kwa teknolojia ya goli," alisema Rais wa FIFA, Sepp Blatter, baada ya makosa ya marefa kuwagharimu England na Mexico.


Felipe Melo
* "Mimi ni mzoefu wa kupenda. Watu wanaweza kufikiri kuwa kuwa nina sura mbaya, lakini ninapenda kutuma kadi na maua kwa mke wangu na ninapenda pia kutumiwa," beki mpambanaji wa Brazil, Felipe Melo, akisema kuwa yeye si mtu mbaya ‘kiivyo’.

Oscar Tabarez
* "Soka ni kama blanketi fupi, ama litatosha kukufunika kichwani au miguuni," kocha wa Uruguay, Oscar Tabarez, alisema kuhusiana na udhaifu wa mabeki wa Korea Kusini kabla ya mechi yao ya hatua ya mtoano ambayo Uruguay walishinda dhidi ya Waasia hao.

Carlos Marchena
* "Sawa, ni pweza," alisema beki wa Hispania, Carlos Marchena, katika muonekano wa kukasirika wakati alipotakiwa kuelezea maoni yake kuhusiana na utabiri wa pweza uliodai kwamba Hispania watashinda katika mechi yao ya fainali dhidi ya Uholanzi. Pweza huyo maarufu alitabiri kwa usahihi matokeo ya mechi zote saba za Ujerumani wakati wa fainali za Kombe la Dunia.

Felipe Melo
* "Najua kwamba wakati mwingine huwa napitiliza. Ni jambo ambalo huwa nalifikiria muda wote na ninajua kwamba hili ni jambo linalohofiwa na Wabrazili wote. Baba yangu siku zote amekuwa akinisisitiza kuhusu jambo hili, haachi kunikumbusha," alisema kiungo wa Brazili, Felipe Melo, kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia, kuhusiana na umuhimu wa yeye kuepuka kadi nyekundu. Hata hivyo, alitolewa uwanjani katika mechi yao ya robo fainali dhidi ya Uholanzi kwa kumkanyaga mpinzani wake.

Dunga
* "Wakati wakionyesha vipande vya picha za video za fainali za mwaka 1970, unachoona ni sehemu nzuri tu. Kuanzia mwaka mwaka 1958, wanaonyesha vipande vya sehemu nzuri tu, na kuanzia mwaka 1962, pia wanaonyesha vipande vya sehemu nzuri tu. Kama tukichukua vilevile vipande vya sehemu nzuri tu za timu ya Brazil ya sasa, mashabiki wataamini kwamba ndio timu bora kabisa. Lakini leo hii, wanaonyesha vipande vingi vya picha za matukio mabaya kama ilivyo kwa matukio mazuri." Dunga akilalamikia kumbukumbu za timu ya Brazil ya mwaka 1970 na kudai kwamba haikuwa timu nmzuri sana kama inavyoonyeshwa kwenye televisheni.


Marcelo Bielsa
* "Wote tunajifunza kutokana na makosa tunayofanya na kutoka kwenye makosa tuliyoyashuhudia yakifanywa na watu wengine, na kujaribu kuepuka kuyarudia. Huu ni mchakato wa kufanya makosa na kuepuka kuyarudia tena, kuona namna wengine wanavyofanya makosa ili kuyaepuka makosa kama hayo, ni mchakato ambao hausimami, na hauwezi kupimika." kocha asiyetabirika wa Chile, Marcelo Bielsa, akizungumzia umuhimu wa kujifunza kutokana na makosa.
--------------

Diego Forlan: Shujaa wa Uruguay WOZA 2010








PENGINE maamuzi yake ya kuachana na mchezo wa tenisi alioupenda utotoni na kuucheza hadi akiwa na miaka 14 na kisha kufuata nyayo za baba na babu yake katika soka, hayakuwa ya kimakosa kutokana na mafanikio anayoyapata kwa sasa katika mchezo huo.
Forlan anayeichezea klabu ya Atletico Madrid ya Hispania na anayetajwa kama mmoja wa washambuliaji wanaotisha zaidi duniani, mbali na mafanikio mengi anayojivunia, kubwa ni kung'ara kwake katika fainali za Kombe la Dunia zilizomalizika wiki iliyopita nchini Afrika Kusini.
Katika fainali hizo za pili kwake, Forlan kwa juhudi binafsi, aliifikisha timu yake katika hatua ya nusu fainali ikiwa ni rekodi baada ya miaka 40 kupita tangu Uruguay, mabingwa wa kwanza wa michuano hiyo iliyoanzishwa mwaka 1930, kucheza nusu fainali kwa mara ya mwisho mwaka 1970.
Kuifikisha Uruguay hatua hiyo, kumemfanya Forlan aweke historia na kumfunika baba yake mzazi, Pablo Justo Forlan Lamarque, aliyekuwa akicheza kama beki aliyewahi kuiwakilisha nchini hiyo katika fainali mbili za Kombe la Dunia mwaka 1966 na 1974.
Amemfunika pia babu yake, Juan Carlos Corazo, aliyewahi kung'ara katika klabu ya Independiente ya Argentina na kuwahi kuinoa timu ya taifa ya Chile mwaka 1962.
Forlan aliibeba kwa kila hali Uruguay katika WOZA 2010, akicheza kwa kujituma na kuifungia mabao muhimu ambayo mwishowe yalimfanya kuwa miongoni mwa wafungaji bora wa michuano hiyo na kunyakua tuzo ya 'Adidas Golden Ball' ya Mchezaji Bora wa Kombe la Dunia 2010.
Nyota huyo alinyakua tuzo hiyo akiwazidi kete nyota wanne, Wesley Sneijder-Uholanzi, David Villa-Hispania, Thomas Muller Ujerumani na Gonzalo Higuain wa Argentina.
Kwa takwimu za waliopiga mashuti mengi langoni katika WOZA, Forlan aliyenyakua tuzo mbili tofauti za Mfungaji Bora Ligi ya Hispania na Ulaya kwa msimu ya 2004-2005 na 2008-2009, amelingana na Villa wakipiga mashuti 32 kila mmoja nyuma ya Asamoah Gyan wa Ghana aliyekuwa kinara.
Mafanikio ya Forlan aliyeanza kuichezea Uruguay tangu mwaka 2002, akifikisha jumla ya mechi 69 na kuifungia mabao 29, yamekuja katika michuano hiyo ya Dunia ikiwa ni miezi michache tangu alipotoka kuisaidia klabu ya Atletico Madrid kutwaa la ubingwa wa Ligi ya Europa, jina jipya la michuano ambayo ni maarufu zaidi nchini kama "UEFA ndogo".
Nyota huyo aliifungia mabao muhimu Atletico katika michuano hiyo mikubwa ya pili nyuma ya Ligi ya Mabingwa barani humo na kuifikisha fainali, ambako yeye mwenyewe "aliinyonga" Fulham ya England na kuipa ubingwa klabu hiyo ya Hispania.

FORLAN NI NANI?
Forlan ambaye majina yake kamili ni Diego Martin Forlan Corazo, alizaliwa Mei 19, 1979 mjini Montevideo, Uruguay na utotoni alipenda mno mchezo wa tenisi, ingawa pia alijihusisha na soka katika klabu za vijana za Penarol na Danubio za nchini mwake.
Inadaiwa alijikita zaidi katika soka baada ya ajali mbaya iliyompata dada yake Alejandra Forlan, iliyomfanya apooze mwili na kumpoteza mchumba wake na ndipo aliponyakuliwa na Independiete ya Argentina, ambapo alianza kwa kuchezea kikosi cha vijana kabla ya kupandishwa kwenye timu ya wakubwa mwaka 1998 hadi Januari 2002 aliposajiliwa na klabu ya Manchester United ya England kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 6.9 (sawa na Sh. Bilioni 15.5).
Manchester ilimnyakua Forlan kwa lengo la kwenda kuziba nafasi ya Andy Cole, lakini ilimchukua miezi nane kufunga goli lake la kwanza katika klabu hiyo katika mechi ya ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Maccabi Haifa ya Israel katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Kutokana na kushindwa kufanya vema katika misimu yake miwili ndani ya Old Trafford, aliotwaa nao taji la Ligi Kuu ya England 2002-2003, Kombe la FA 2003-2004 na Ngao ya Hisani 2003, Forlan aliuzwa kwa klabu ya Villarreal ya Hispania Agosti 21, 2004.
Kuondoka kwake Manchester kulitoa fursa kwa nyota wa sasa wa England, Wayne Rooney kutua akitokea klabu aliyolelewa ya Everton.
Katika msimu wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya Hispania, Forlan alifunga magoli 25 na kuisaidia kuiingiza Villareal kwa mara ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku mwenyewe akinyakua tuzo ya Mfungaji Bora wa la Liga iitwayo 'Pichichi' na ile ya Mfungaji Bora wa Ulaya, akilingana na Thiery Henry (aliyekuwa Arsenal wakati huo).
Aliendelea kuipa mafanikio timu yake hiyo kabla ya mwaka 2007 kutua katika klabu ya Atletico Madrid ambapo aliifungia mabao 32 katika mechi 33 alizoichezea na kunyakua tena tuzo ya Pichichi na ile ya Ulaya kwa mara ya pili msimu wa 2008-2009.
Kunyakua tuzo ya Mfungaji Bora wa Hispania na Ulaya akiwa na klabu mbili tofauti za La Liga, kulimfanya kuwa mchezaji wa kwanza tangu Ronaldo aliyefanya hivyo katika msimu wa mwaka 1996-97 akiwa na Barcelona, kisha 2003-2004 akiwa na kikosi cha Real Madrid.
Msimu uliopita mkali huyo alishika nafasi ya tano ya ufungaji mabao ya ligi ya Hispania akiwa na mabao mabao 18, akizidiwa mabao 16 na aliyekuwa kinara, Lionel Messi wa Barcelona.
Hata hivyo, ufungaji wake wa magoli muhimu uliibeba Atletico Madrid iliyonyakua ubingwa wa Ligi ya Europa baada ya kuilaza Fulham ya England, ikiwa ni baada ya kusaidia kuingoa Liverpool.
Kuhusu maisha yake binafsi, Forlan anayefahamika kama 'Cachavacha' na aliyemiliki mfuko maalum wa kusaidia wahanga wa ajali kama njia ya kumuenzi dada yake Alejandra Forlan, anaishi na mwanamtindo maarufu wa Argentina, Zaira Nara.

DONDOO MUHIMU
* Alisajili wa Atletico Madrid 2007 kwa ajili ya kuziba pengo la Fernando Torres, aliyehamia Liverpool.
* Alitwaa tuzo yake ya pili ya Kiatu cha Dhahabu kwa kuwa Mfungaji Bora wa Ulaya katika msimu wa 2008/09 kutokana na kuwa na magoli 32 ya ligi kuu, ambapo 12 kati ya hayo aliyafunga katika mechi nane za mwisho za msimu na kumpiku mshmabuliaji wa Barcelona kwa wakati huo, Samuel Eto'o.
* Alikuwa katika kiwango cha juu katika Ligi ya Europo msimu uliopita na kuisaidia Atletico kutwaa ubingwa wao wa kwanza Ulaya katika miaka 48.
* Alifunga magoli yote mawili ya Atletico katika ushindi wa 2-1 wa fainali ya Ligi ya Europa dhidi ya klabu ya Fulham mjini Hamburg.

Matumla adundwa na Maugo, astaafu ngumi






BINGWA wa zamani wa Dunia wa ngumi za kulipwa, Rashid Matumla 'Snake Boy' jana alipigwa kwa pointi na Mada Maugo na kutangaza kustaafu kuendelea kupigana na ulingoni na badala yake kugeukia kazi ya ukocha.
Pambano hilo lililoandaliwa na Oganizesheni ya Ngumi za Kulipwa nchini, TPBO, lilifanyika kwenye ukumbi wa PTA, Sabasaba Dar es Salaam kwa nia ya kumaliza ubishi baina ya wawili hao waliokuwa wakitambiana kwa muda mrefu.
Matumla ambaye alishawahi kutangaza kuacha ngumi baada ya kupigwa kwa mara nyingine na Francis Cheka 'SMG', alishindwa kuhimili vishindo vya Maugo, ingawa alimudu hadi mwisho wa mchezo huo uliokuwa wa raundi 10 uzito wa kilo 72.
Mara baada ya kumalizika kwa pambano hilo lililotanguliwa na michezo kadshaa ya utangulizi, Snake Boy, alitangaza kuwa huo ndio mchezo wake wa mwisho kupanda ulingoni na kwamba anaamini 'ameshazeeka' na kusema atageukia ukocha ili kuwarithisha vijana ujuzi wake wa mchezo huo uliompa sifa kubwa ndani na nje ya nchi.
Kutokana na ushindi huo wa pointi, Mada Maugo sasa anaweza kupigana na Cheka, ambaye alishatangaza kama bondia huyo atashinda basi atakuwa radhi kupigana nae au la yeye (Cheka) atamtafuta Karama Nyalawila ili kumaliza ubishi baada ya wawili hao yaani Maugo na Nyalawila kutamba kuwa ndio pekee wanaoweza kumsimamisha Cheka.

Nchunga amrithi Madega Yanga, Mosha aula...!







MWANASHERIA, Lloyd Nchunga amefanikiwa kuibuka kidedea na kumrithi aliyekuwa mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega katika kiti hicho baada ya kuibuka kidedea katika uchaguzi mkuu wa Yanga uliokesha ukifanyika kwenye ukumbi wa PTA, Sabasaba, jijini Dar.
Nchunga, anayeendesha kampuni ya uwakili, aliibuka kidedea kwa kuwabwaga wagombea watatu aliokuwa anachuana nao baada ya Francis Kifukwe 'kuchomoa' mapema kwa kile alichodai kuwa kulikuwa na mizengwe ambayo anaamini ingemuangusha katika uchaguzi huo.
Mshindi huyo aliyekuwa akipewa nafasi kubwa katika uchaguzi huo na kuwa tishio la Kifukwe, aliwashinda Abeid Abeid 'Falcon', Edger Chibura na Mbaraka Igangula, ambaye huenda asiamini kama pamoja na kujitangaza kwa mabango barabarani bado kapigwa chini.
Kwenye nafasi ya makamu mwenyekiti, nafasi iliyokuwa wazi kwa muda mrefu tangu kufariki kwa aliyekuwa akiishikilia, Marehemu Rashid Ngozoma Matunda, ilienda kwa mfanyabiashara maarufu wa mafuta, Davis Mosha aliyemuangusha Constatine Maligo.
Kura za nafasi nane za Wajumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo zilikuwa bado zikiendelea kuhesabiwa hadi muda huu, ingawa kuna baadhi ya waliokuwa wakipewa nafasio ya kuibuka kidedea kama Ally mayai Tembele, Mohammed Bhinda na wengine.

Saturday, July 10, 2010

Shujaa Namba 1 wa Hispania aotae ubingwa





BAO lake lililoizamisha waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia, Carles Puyol, limempa ushujaa wa kipekee katika nchi yake ya Hispania.
Beki huyo anayekipiga Barcelona alijinyakulia ushujaa bila kutegemewa katika ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ujerumani wa nusufainali ya Kombe la Dunia katikati ya wiki katika timu ambayo imejaa vipaji kama David Villa na Andres Iniesta.
Saa zikiwa zinayoyoma kuelekea muda wa nyongeza katika mechi yenye ushindani mkali, beki huyo mwenye nywele zilizovurugika wakati wote alipiga kichwa cha nguvu kilichoishia nyavuni katika dakika ya 73 na kuwaingiza mabingwa wa Ulaya hao katika mtanange wa kukata na shoka kesho Jumapili dhidi ya Uholanzi.
Lilikuwa bao la tatu la timu ya taifa la mchezaji huyo mwenye miaka 32 aliyekuwa akicheza mechi ya 89 ya kimataifa na liliingiza Hispania fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.
"Puyol 'shark' ametuingiza fainali," mchezaji mwenzake katika klabu ya Barcelona David Villa, ambaye ni mfungaji mwenza anayeongoza katika fainali hizi za Afrika Kusini akiwa na mabao matano, aliwaambia waandishi wa habari akiwa ni mwenye furaha.
Uchezaji wa kuwepo kila mahali wa Puyol katika mchezo huo ulikuwa "maridadi", Villa alisema wakati kiungo Xabi Alonso alisema zaidi: "Tulijenga kambi nje ya eneo lao la hatari kwa dakika kama 10 hivi lakini hatukufunga mpaka Puyol alipochupa kama mkizi na kufunga."
Waziri mkuu wa Hispania Jose Luis Rodriguez Zapatero, ambaye ni shabiki wa Barcelona, alichangia sifa kwa beki huyo, alipoiambia redio ya Hispania: "Si kuruka kule mwanangu, bonge la kichwa cha Puyol! Ni bonge la mchezaji."
Kocha wa Ujerumani Joachim Loew aliiponda timu yake kwa kushindwa kumchunga Puyol aliyeingia kwenye eneo la hatari akikimbia peke yake lakini akasifu "nguvu nyingi" na "kujituma kulikopitiliza" alikoonyesha.

INASTAHILI
Puyol anaamini kuwa 'Furia Roja' imeingia fainali ya Kombe la Dunia kwasababu inastahili na anaisubiri kwa hamu mechi ya kesho Jumapili dhidi ya Uholanzi.
Mabingwa hao wa Ulaya wataikabili 'Oranje' kwenye Uwanja wa Soccer City jijini Johannesburg, na Puyol anajivunia mafanikio ya timu yake mpaka sasa na anadai hakuna anayeweza kusema hawastahili kucheza fainali hiyo.
"Tupo tunapostahili kuwa," Puyol alisema, kwa mujibu wa gazeti la michezo la kila siku la Hispania la Marca. "Timu nzima ina usongo na mechi ijayo na inataka kufanya kitu kikubwa.
"Mechi dhidi ya Uholanzi itakuwa ngumu mno. Ni timu mbili zilizosheheni vipaji na zitakazocheza kufa na kupona kutwaa ubingwa.
"Mechi ya fainali siku zote huwa ni 50/50. Mwanzoni tulikuwa pia tukipewa nafasi kubwa lakini baada ya kufungwa na Uswisi, ikawa balaa."
Alipoulizwa kama mechi ya kesho itakuwa ya mwisho kwake ya kimataifa, Puyol alisema, "Kilichopo mbele ni kitu kizuri sana, baada ya hapo patakuwa na muda wa kufanya tathimini. Sijachukua uamuzi wowote mpaka sasa."

Friday, July 9, 2010

Katibu Mkuu TFF ang'atuka






KATIBU mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela, amesema kwamba hataomba kuongeza mkataba mpya wa kuendelea kulitumikia shirikisho hilo baada ya mkataba wake kumalizika mwezi ujao.
Mwakalebela sasa hivi ameelekeza nguvu zake katika kuwania ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini, mkoani Iringa kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na blog hii, Mwakalebela alisema kuwa amefikia maamuzi hayo baada ya kulitumikia shirikisho hilo kwa muda wa miaka minne na sasa anataka kuiachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine.
Mwakalebela alisema kuwa amepanga kuiandikia barua Kamati ya Utendaji ya TFF kuijulisha maamuzi yake ambayo inatarajia kukutana jijini Dar es Salaam Julai 17 kujadili mambo mbalimbali.
Mwakalebela alisema kuwa akiwa katika nafasi hiyo anajivunia kuona shirikisho linaendeshwa bila ya kuwa na migogoro baina yake na wanachama huku pia ukaguzi wa fedha ukifanyika kila mwaka na kupata cheti chenye alama ya juu.
Alisema pia wadhamini mbalimbali wamejitokeza kuisaidia timu ya taifa, Taifa Stars, na kufanikiwa kushiriki katika fainali za kwanza za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa Ndani (CHAN).
Aliongeza kwamba anajivunia akiliacha shirikisho hilo likiwa na kituo cha kulea wachezaji wenye vipaji, ambacho tayari matunda ya nyota wake yameanza kuonekana kwa kupata mialiko ya kwenda kufanya majaribio katika klabu za Ulaya na kugombaniwa na klabu kongwe za nchini.
Mwakalebela aliajiriwa katika nafasi hiyo mwaka 2006 baada ya kamati ya utendaji ya shirikisho hilo, kusitisha mkataba wa aliyekuwa katibu mkuu wa kwanza wa kuajiriwa, Ashery Gasabile, kutokana na kushindwa kumudu majukumu aliyopewa.
Wakati huo huo, habari kutoka Dodoma zinasema kuwa, wabunge mbalimbali jana, walimpongeza Mwakalebela kutokana na maamuzi yake ya kujitosa katika kinyang'anyiro cha kuwania ubunge.
Mwakalebela ambaye yuko Dodoma kufuatilia bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, iliyokuwa inawasilishwa jana, walimueleza kwamba waliridhishwa na utendaji wake TFF, nchi imefanikiwa kutangazika kimataifa ambapo ikiwemo kuileta timu ya Brazil.
Walimweleza kuwa wanamtakia mafanikio na watafurahi akirejea katika bunge hilo akiwa kama mbunge kamili na wabunge wengi ni wanamichezo na kwamba muda wote alipokuwa madarakani walifurahishwa na utendaji wake.

mwisho.

Wajerumani wataka pweza aliwe hadharani



BERLIN, Ujerumani
BAADHI ya mashabiki wa soka wa Ujerumani wametaka pweza Paul, ambaye amebashiri kiusahihi mechi zote sita za Ujerumani kwenye Kombe la Dunia ikiwemo ya kipigo kinachouma cha nusu fainali kutoka kwa Hispania juzi Jumatano, abanikwe na kuliwa hadharani.
Paul, pweza mwenye umri wa miaka miwili anayeishi katika 'ki-kontena' cha kioo nchini Ujerumani, amegeuka kuwa 'supastaa' wa dunia kutokana na uwezo wake wa kubashiri mshindi wa mechi zote sita za Ujerumani, ikiwemo ya kipigo cha hatua ya makundi walichopata kutoka kwa Serbia na kilichowaondoa kwenye nusu fainali kutoka kwa Hispania.
"Hakuna chakula kitamu kama pweza wa kubanika," alisema Dolores Lusch, shambiki wa Ujerumani anayefanya kazi katika duka la samaki la mjini Berlin. "Mkate katika 'slesi' ndogo nidogo na kisha mbanike kwa kummiminia juisi ya limau, ama mafuta ya olive. Ni mtamu ajabu!"
Wajerumani ambao kwa kawaida hawaamini nguvu za giza wamegeuka kuwa watu wanaoamini sana kuhusu nguzu za utabiri za pweza Paul. Nchi hiyo iliingia ganzi wakati pweza Paul alipoichagua Hispania kuwa ndiyo itakayoshinda mechi dhidi ya Ujerumani baada ya kupatia kuwa itashinda dhidi ya Argentina, England, Ghana na Australia.
Magazeti ya Ujerumani na tovuti yalichapisha mitazamo ya watu kuhusu nini wamfanye pweza Paul, ambapo wengi wamependekeza apikwe na aliwe.
"Mrushe kwenye kikaangio," liliandika gazeti la Berliner Kurier katika kichwa cha habari maarufu kilichoandikwa pia magazeti ya Die Welt, Sueddeutsche Zeitung, The Hamburger Abendblatt na mengineyo.
Utabiri wa pweza Paul umekuwa habari kubwa nchini Ujerumani na kwingineko duniani. Vituo vya televisheni vya Ujerumani vilikatisha ghafla matangazo Jumanne ili kuonyesha 'laivu' tukio la pweza Paul wakati alipokuwa kuwa akitabiri mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia baina ya Hispania na Ujerumani.
Leo, pweza Paul atatabiri mshindi wa mechi ya Jumamosi baina ya Ujerumani na Uruguay ya kusaka mshindi wa tatu pamoja na mshindi wa mechi ya fainali ya Kombe la Dunia itakayochezwa Jumapili baina ya Hispania na Uholanzi. Vituo vya televisheni vya Ujerumani, Hispania na Uholanzi vinapanga kurusha 'laivu' tukio hilo.
Pweza huyo, ambaye anaaminika kwa baadhi kuwa ndiye kiumbe mwenye akili sana, hupewa fursa ya kuchagua chakula kutoka katika 'vi-kontena' viwili tofauti vilivyotumbukizwa kwenye 'tenki' lake analoishi -- kimoja kikiwa na bendera ya Ujerumani na kingine kikiwa na bendera ya upinzani.
'Ki-kontena' ambacho pweza Paul atakifunua kwanza ndicho huaminika kuwa ndio utabiri wake wa mshindi.
Mvuto uliovikumba vyombo vya habari kuhusu utabiri wa pweza Paul nchini Ujerumani na nje umekuwa mkubwa sana na wachambuzi wameelezea hisia zao kwamba huenda kupatia kwa asilimia 100 kwa utabiri huo huenda kukaingiza imani za kishirikina miongoni mwa wachezaji.
Licha ya mitazamo ya kutaka pweza huyo abanikwe, msemaji wa hifadhi ya viumbe wa baharini ya Sea Life inayomlea pweza huyo, Tanja Munzig, amesema pweza Paul ataendelea kula maisha katika nyumba yake iliyopo mjini Oberhausen, Ujerumani.
"Hakuna lolote baya litakalotokea kwa pweza Paul," alisema mwanamama huyo. "Hakuna mtu anayemuombea baya. Pweza Paul ana rekodi nzuri."
Munzig aliongeza kuwa utabiri wa pweza Paul utaendelea, ambapo leo mchana anatarajiwa kutabiri pambano la fainali za Kombe la Dunia kati ya Spain na Uholanzi litakalofanyika siku ya Jumapili.

Wednesday, July 7, 2010

Forlan alicheza akiwa majeruhi-Kocha




CAPE TOWN, Afrika Kusini
NYOTA tegemeo wa timu ya taifa ya Uruguay, Diego Forlan, alicheza pambano la nusu fainali dhidi ya Uholanzi akiwa majeruhi na kumlazimisha kocha wake Oscar Tabarez, kumtoa nje kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Forlan aliyekaririwa jumanne iliyopita kwamba katu hawezi kurejea tena katika Ligi Kuu ya Uingereza na kufuta ndoto za meneja wa Tottenham Hotspur, Harry Redknapp kumnyakua, alimua tangu mwanzo wa mchezo huo.
"Tangu dakika ya kwanza Forlan alikuwa na tatizo. Aliumia na hakuweza kuendelea kucheza,"
"Alikuwa na maumivu na wakati wa mchezo tuliamua kuchukua maamuzi ya kumjaribu kumbadili na mchezaji mwingine" aliongeza Tabarez.
Hata hivyo kocha huyo alisema tatizo la mshambuliaji huyo anayeichezea Atletico Madrid ya Hispania, sio kubwa na huenda kesho akacheza kuipigania nchi yake katika pambano la kusaka mshindi wa tatu kati yao na mshindi kati ya Ujerumani na Hispania.
"Sio tatizo lake halikuwa kubwa, lakini hakuwa fiti kwa asilimia 100 kucheza hadi mwisho," alisema kocha huyo.
Forlan, mshambuliaji wa Atletico Madrid ya Hispania, alifunga bao maridadi wakati timu yake iliposhindwa mabao 3-2 na Uholanzi.
Mshambuliaji huyo alifunga bao hilo dakika moja kabla ya mapumziko kwa shuti kali la umbali ya mita 30 lililomshinda nguvu kipa wa Uholanzi, Maarten Stekelenburg.
Huenda kesho mchezaji huyo aliyeifungia timu hiyo mabao manne katika fainali hizo za WOZA 2010 akawemo katika pambano la kusaka mshindi wa tatu litakalochezwa kwenye mjini wa Port Elizabeth.

Sajuki: Mkali wa filamu anayeulilia mguu wa mkewe






NDOTO zake enzi akiibukia kwenye sanaa ilikuwa ni kuja kuwa mchekeshaji kutokana na kumzimia mno, msanii Athuman Amir 'King Majuto'.
Hata hivyo kupenda kwake kuangalia filamu za Sylvester Stallone 'Rambo' zilimfanya abadili upepo na kujikita kwenye uigizaji wa kawaida na kisha kujitumbukiza kwenye tasnia hiyo, ambapo leo ni mmoja wa nyota wa fani hiyo nchini.
Sajuki, ambaye majina yake kamili ni Juma Juma Issa Kilowoko, alisema hamu yake ya kufika mbali katika sanaa ya uigizaji ndiyo iliyomfanya apite kundi moja hadi jingine hadi kuangukia Kaole Sanaa, lililomtangaza vema kupitia michezo iliyokuwa ikirushwa na kituo cha runinga cha ITV.
Alisema mchezo wake wa kwanza ndani ya kundi hilo lililotoa nyota kibao wa filamu nchini ni Baragumu wa mwaka 2005 na kufuatia na michezo mingine hadi mwaka 2008 alipojitoa kundini na kujikita zaidi katika filamu, kazi yake ya kwanza ikiwa ni Revenge.
"Baada ya kupita makundi kadhaa tangu nikiwa mjini Songea nilipozaliwa, hatimaye nilitua Kaole Sanaa, lililoniivisha kabla ya kuachana nao kusaka masilahi zaidi na kujikita katika filamu," alisema.
Mbali na Revenge filamu zingine alizocheza Sajuki ni pamoja na Dhambi, Mboni Yangu, Two Brothers, Behind the Scene, Round, Shetani wa Pesa, Hero of the Church na nyinginezo.
Kwa sasa yupo mbioni kuachia kazi mbili binafsi za Vita na Briefcase zilizowashirikisha nyota kadhaa nchini akiwemo mshindi wa pili wa BBA, Mwisho Mwampamba.
Sajuki alisema fani ya filamu imemnufaisha kwa mambo mengi ikiwemo kimaisha, lakini kubwa ni kufanikiwa kumuoa mke mrembo na muigizaji mwenzake, Wastara Juma.
"Kufanikiwa kumpata Wastara na kumuoa kwangu ni jambo kubwa na la kuvutia mno kati ya mafanikio kibao niliyoyapata katika fani hii ya filamu nchini," alisema.
Mkali huyo, ambaye hupenda kucheza na watoto na shabiki wa muziki wa 'Quito', alisema kama kuna kitu kinachomkera katika sanaa hiyo ni tabia za 'Wauza Sura' wanaojiingiza kwenye skendo chafu zinazowachafua wasanii wote wa tasnia hiyo mbele ya jamii.
Alisema wasanii wenye kusaka umaarufu kwa lazima wanamnyima raha kwa vile jamii inadhani wasanii wote wana silka na tabia kama za wauza sura hao wanaojirahisi na kujidhalilisha.
Kuhusu rushwa ya ngono, Sajuki mtoto wa nne kati ya watano wa Mzee Juma Issa Kilowoko, alisema wanaojihusisha nao wanafanya hivyo kwa kujitakia kwa sababu hakuna anayelazimishwa kutoa mwili wake iwapo ana uwezo na kipaji kikubwa katika sanaa hiyo.
"Rushwa ya ngono kwa watoto wakike ni kujitakia kwa vile wana akili na ufahamu wa kujua athari za kufanya hivyo na watayarishaji wanaolazimisha hawafai na wanapaswa kuchukuliwa hatua kali za kisheria," alisema Sajuki.
Sajuki, aliyelifafanua jina lake hilo kuwa ni muunganisho wa jina la kaka yake mkubwa Salum, lake la Juma na lile la ukoo wao la Kilowoko, alisema hakuna kitu kinachomtia simanzi na kumsikitisha kama tukio la ajali ya pikipiki iliyompata akiwa na mkewe, Wastara Juma enzi wakiwa wachumba.
Nyota huyo mwenye mtoto mmoja wa kiume na anayeishukuru famili yake na Vincent Kigosi 'Ray' kwa kumfikisha hapo alipo, alisema ajali hiyo sio inayomuuma, ila kitendo cha kulazimika kuidhinisha fomu hospitalini ili Wastara akatwe mguu wake uliokuwa umeharibika kwa ajali hiyo.
"Kwa kweli kile kitendo cha kuidhinisha kukatwa kwa mguu kwa Wastara kinaniuma hadi leo, lakini sikuwa na jinsi ila kufanya hivyo ili kumuokoa," alisema Sajuki.
Hata hivyo alisema anajisikia fahari mno kuuoana na kisura huyo ambaye kwa sasa anao mguu wa bandia, kwa vile wamesaidia kuanzisha kampuni yao binafsi ya Wajey Films Production.
Mkali huyo alizaliwa miaka zaidi ya 25 iliyopita huko Songea na kusoma hadi elimu ya sekondari katika shule za Songea na Luwiko, alikoanza kuonyesha kipaji chake cha sanaa katika matamasha mbalimbali ya shule kabla ya kujitosa kwenye makundi.
Kwa sasa, Sajuki anayeitaka filamu ya Mboni Yangu kama picha kali kuliko zote alizowahi kuigiza, yupo mbioni kuachia kazi zake mbili binafsi za Vita na Briefcase zilizowashiriki wakali kadhaa na matarajio yake ni kujiendeleza zaidi ili kuleta mapinduzi katika tasnia ya filamu nchini.
.
Mwisho

Bileku Mpasi: Dansa na Rapa wa Empire Bakuba anayekumbukwa * Alifunika na kumtia kiwewe Papy Tax, akamuibua Kokoriko Tz *




KWA wapenzi wa muziki wanaweza kukumbuka kuwa, bendi ya Empire Bakuba ilianzishwa na watu watatu, marehemu Joseph Kabasele Yampanya 'Pepe Kalle', Papy Tex na Dilu Dilumona miaka ya 1970.
Lakini pamoja na bendi hiyo kuasisiwa na watatu hao na baadae kupewa nguvu na Jojo Ikoma, ni vigumu kutaja mafanikio yake bila kumhusisha Djouna Mumbafu 'Bikelu Mpasi' a.k.a Big One.
Bileku aliyezaliwa na kupewa majina ya wazazi wake ya Bileku Jean-Pierre Matonet, aliweza kuifanya Bakuba ie juu kinoma.
Pamoja na ukweli kuwa alichukuliwa na Pepe Kalle kama dansa na rapu wa bendi hiyo, Bileku Mpasi aliweza kupanda haraka na kuwa maarufu pengine hata waasisi wenyewe.
Kupanda kwake kwa mafanikio kulitokana na umahiri wake wa kucheza, kurapu na baadae kuimba kiasi kwamba marehemu Pepe Kalle alifikiria kumpa nafasi ya hisa zake katika bendi hiyo.
Marehemu Pepe Kalle alitokea kumpenda na kumuamini Bileku Mpasi kama alivyofanya marehemu Franco kwa marehemu Madilu Systems enzi za uhai wao walipokuwa pamoja bendi ya T.P OK Jazz.
Jitu hilo la Miraba Minne hakumpenda bure kijana huyo, bali ni kutokana na ukweli alikuwa akijituma na kuifanya Empire Bakuba iliyoanzishwa kutokana na jina la moja ya makabila ya nchini Zaire (DR Congo ya sasa) kufunika kwa sana enzi za uhai wake.
Kasi yake ya kucheza na kurapu kwa wakati mmoja ndiyo kwa sasa imekuwa ikiigwa na marapa mbalimbali wa makundi ya muziki wa Lingala kuanzia DR Congo, Congo Brazaville hadi Bongo.
Enzi zake mkali huyo alikuwa akichuana na wakali kama Robert Ekokota Wenda wa Wenge Musica BCBG kabla ya kuibuka wengine kadhaa waliofuata nyayo zao.
Wapo wengine wanaodai kuwa Bileku Mpasi ndiye muasisi wa Ma-Atalaku walioibua nchini Congo na kufanya muziki wa Lingala ama Bolingo kuchangamka mno isivyo kawaida.
Ukali wake na ushirikiano aliokuwa nao na mbilikimo Emorro na baadae Djuma Fatembo na Jully Bebe, kulimfanya Bileku kuzidi kuwa juu na hasa kwa rafu zake matata katika albamu mbalimbali.
Ingawa hakuna taarifa kamili juu ya historia kamili ya mkali huyo ambaye kwa sasa ana kundi lake binafsi la Orchestra Big One, akitamba na albamu ya Tonnerre de Brest yenye kibao cha 6600 Volts, inadaiwa alizaliwa miaka zaidi ya 40 iliyopita.
Shughuli zake za muziki alizianza katika mji wa Kalemi kabla ya kuibukia Kishansa miaka ya mwishoni ya 1970.
Mwanzoni mwa miaka ya 1980 alikuwa akifanya shughuli zake katika bendi ndogondogo kama mnenguaji kabla ya kuchukuliwa na Pepe Kalle na kuwa dansa na rapa wao.
Hata hivyo kutokana na kuonyesha kipaji kikubwa katika uimbaji, Pepe Kalle akishirikiana na mtunzi mahiri wa Empire Bakuba enzi za uhai wake, Papy Tex walimpika kuwa muimbaji mkali.
Hata hivyo ukali wake na kuwafunika wawili kati ya waasisi wa kundi hilo, inaelezwa kuwa kulimsababishia rapa huyo 'kuunda' bifu kali na Papy Tex.
Ndio maana mara baada ya kifo cha marehemu Pepe Kalle Novemba mwaka 1998, kulitokea mtafaruku kama ule wa TP OK Jazz baada ya kifo cha Franco juu ya mustakabali wa bendi hiyo na Madilu.
Ilidaiwa kuwa wanamuziki waliosalia katika bendi hiyo walikuwa na nia ya kuiendeleza Empire Bakuba, ila waasisi na waliokuwa wamiliki wake, Dilumona na Papy walianzisha zengwe baada ya kufahamika Bileku amepewa usimamizi wa hisa za Pepe Kalle.
Yeye na Gode Lufombo waliamua kujiondoa na kuiacha Bakuba mikononi mwa mwenye nayo na kwenda kujiunga na kundi la Delta Force, ambalo lilikuwepo hata kabla ya kifo cha Pepe Kalle.
Delta Force alikaa nao kwa muda tngu mwaka 1999 hadi 2002 kabla ya kuamua kujiondoa na kuwa msanii wa kujitegemea na kufanikiwa kufyatua albamu yae ya kwanza ya Tonnerre de Brest.
Albamu hiyo ilikuwa na kibao matata cha 6600 Volts, ilitolewa mwaka 2004 na kumfikisha Bileku kwenye Fainali za Tuzo za Muziki za Afrika za Kora (Kora Music Award) za mwaka huo kupitia kibao hicho, ingawa hakufanikiwa kubeba tuzo yoyote.
Miongoni mwa vibao vya albamu hiyo iliyompa mafanikio makubwa kabla ya mkali huyo kujiundia Orchestra Big One inayotamba na albamu nyingine mpya ya mwaka jana ni pamoja na 100% TVA, 6600 Volts na Cupidon Brisé.
Vibao vingine ni pamoja na Fin Du Match, Karachiga, Nez a Nez, Mihona, Onze, Respect Pepe Kalle, Tatou na Tonnerre De Brest.
Bileku anayekumbukwa na Watanzania kwa kuchangia kuibua vipaji vya madansa wa Kitanzania kama akina Kokoriko aliyeshabihiana nae, Marehemu Maxi Prest, Mrisho Mpasi na wengine ndani ya bendi yake anaimba pamoja na mdogo wa marehemu Pepe Kalle.
Mdogo huyo wa marehemu Pepe Kalle, Ally Kale amefanana mno kisauti na marehemu kaka yake kiasi ukisikiliza nyimbo za kundi hilo unaweza kudhani 'Tembo wa Afrika' amefufuka.