STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Rage aupongeza uongozi mpya wa Yanga, amwagia sifa Nchunga



MWENYEKITI wa klabu ya soka ya Simba, Ismail Aden Rage, ameupongeza uongozi mpya wa watani zao Yanga na kumwagia sifa binafsi mwenyekiti mpya wa klabu hiyo, Lloyd Nchunga, akidai ni mchapakazi na muadilifu.
Akizungumza na Micharazo kwa njia ya simu kutoka Tabora, Rage alisema amefurahishwa mno na umakini wa wanachama wa Yanga wa kumchagua Nchunga na Davis Mosha kuwa viongozi wao kwa madai ni watu makini na watakayoiletea mabadiliko klabu yao.
Rage alisema binafsi anamfahamu Nchunga kutokana na kuwahi kufanya naye kazi na kumtaja kama kiongozi mchapakazi na muadilifu.
"Nawapongeza wana Yanga kwa umakini wao wa kumchagua Lloyd Nchunga kuwa mwenyekiti wao, namfahamu ni muadilifu na mchapakazi na naamini ataendeleza mauhusiano mema baina ya klabu zetu mbili za Simba na Yanga," alisema Rage.
Rage alisema Simba na Yanga ni watani wa jadi na sio maadui na hivyo kuingia madarakani kwa Nchunga na Davis Mosha pamoja wengine waliochagulia watalichukulia jambo hilo hivyo na kujenga umoja na mshikamano kwa lengo la kuendeleza soka la Tanzania.
Nchunga, alichaguliwa kuwa mwenyekiti baada ya kuwabwaga wagombea wenzake watatu, Abeid Abeid, Mbaraka Igangula na Edger Chibula, huku Francis Kifukwe akijiondoa wakati wa kujinadi, wakati Mosha alishinda umakamu mwenyekiti kwa kumshinda Constatine Maligo,.
Uchaguzi huo wa Yanga ulifanyika juzi kwenye uwanja wa PTA, Sabasaba Dar es Salaam, ambapo wagombea wengine nane kati ya 28 akiwemo Ally Mayay walichaguliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo.

M

No comments:

Post a Comment