STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Ndumbaro bado alia na Boban



WAKALA wa kimataifa wa wachezaji anayetambuliwa na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Damas Ndumbaro, amezidi kulia na kiungo Harun Moshi 'Boban' akidai mchezaji huyo ana desturi ya kutoheshimu mikataba kama alivyofanya kwa kuitosa klabu ya GIF ya Sweden.
Akihojiwa na kituo kimoja cha redio, Ndumbaro alisema pamoja na Boban kujitetea kuwa kilichomkimbiza Sweden ni kukiukwa kwa mkataba baina yake na klabu hiyo, lakini ukweli ni kwamba inaonekana suala la kutoheshimu ni kawaida ya kiungo huyo mahiri.
Ndumbaro alisema kwa kumbukumbu zake kutaka kuvunja mkataba dhidi ya GIF ni mara ya tatu kwa Boban, kwani alishawahi kufanya hivyo pia alipoenda kucheza soka la kulipwa Arabuni na pia Ethiopia.
"Hili sio jambo la bahati mbaya ni wazi ni Boban ana kawaida ya kutoheshimu mikataba kwani alishawahi kuvunja alipoenda Arabuni na kuiponza klabu yake ya Simba kulipa gharama za huvunjwaji huo wa mkataba huo, pia alifanya hivyo alipokuwa Ethiopia," alisema Ndumbaro.
Wakala huyo alisema dai kwamba labda Boban hakuuelewa mkataba huo wa miaka miwili si sahihi kwa vile alisimamiwa na mwakilishi wa Academy yake anayezungumza kiswahili na ndipo aliposaini na kuanza kuitumia klabu hiyo.
Ndumbaro alisema pengine yale mazoea na kuwakosa 'washkaji' zake wa vijiweni kama anavyokuwa nchini ndio kilichochangia kiungo huyo kurejea nchini ghafla, ingawa Boban alinukuliwa akisema kuwa malipo kiduchu ndicho kilichomrejesha Bongo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment