STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 12, 2017

Dude linaamshwa Champion League, nani kucheka?




Picha tofauti zikionyesha Juventus wakipasha kwenye Uwanja wa Nou Camp kabla ya leo usiku uliamsha dude dhidi ya Barcelona
BARCELONA, Spain
KAZI imeanza kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati mechi za makundi kwa msimu huu wa 2017-2018 ukianza rasmi usiku wa leo kwa kushuhudiwa mechi nane, lakini macho na masikio yakielekezwa Nou Camp, wakati Kibibi Kizee cha Turin, Juventus itakapoifuata Barcelona katika mechi iliyovuta mashabiki wengi wa michuano hiyo.
Juventus imeenda Hispania ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wa fainali zilizopita dhidi ya mahasimu wa Barcelona, Real Madrid, lakini wakijivunia rekodi ya kuanza Ligi Kuu ya Italia Serie A ikishinda mechi zao tatu zote na kufunga mabao 10 na kukaa kileleni ikizizidi ujanja Napoli na Inter Milan kwa tofauti na uwiano wa mabao.
Kikosi hicho cha Juve kilifanya mazoezi jana kwenye Uwanja wa Nou Camp kikiwa na nyota wake wote wakiwamo wakali kinara wa mabao Paul Dyabala, Gonzalo Higuain na Mario Mandzukic.
Wenyeji wataendelea kumtegemea zaidi nyota wao Lionel Messi na Luis Suarez kuweza kulinda heshima yao katika michuano hiyo baada ya msimu uliopita kukwamia njiani kwa aibu.
Mbali na mechi hiyo, pia leo kuna gemu kali yenye mvuto Manchester United waliorejea kwenye michuano hiyo kwa mlango wa uwani itakuwa nyumbani kukabiliana na Basel, huku Chelsea wakicheza na Qarabag, PSG ikiwa na wachezaji ngali zaidi kwa sasa duniani Neymar na Kylian Mbappe watakuwa ugenini nchini Scotland kuvaana na Celtic.

RATIBA KAMILI  LIGI YA MABINGWA ULAYA
Leo, Jumanne
Celtic v PSG         (Saa 3:45 usiku)
Benfica v CSKA Moskva (Saa 3:45 usiku)
Man United v Basel         (Saa 3:45 usiku)
Olympiakos v Sporting CP         (Saa 3:45 usiku)
Bayern Munichv Anderlecht (Saa 3:45 usiku)
Roma v At.Madrid         (Saa 3:45 usiku)
Chelsea v Qarabag (Saa 3:45 usiku)
Barcelona v Juventus (Saa 3:45 usiku)

Kesho Jumatano
Maribor v Spartak Moskva (Saa 3:45 usiku)
Tottenham v B.Dortmund         (Saa 3:45 usiku)
RB Leipzig v Monaco (Saa 3:45 usiku)
Feyenoord v Man City         (Saa 3:45 usiku)
Shakhtar v Napoli         (Saa 3:45 usiku)
Liverpool v Sevilla         (Saa 3:45 usiku)
Porto v Besiktas (Saa 3:45 usiku)
Real Madrid v APOEL (Saa 3:45 usiku)


EUROPA LEAGUE
Alhamis, Septemba 14,  2017
Young Boys v Partizan (Saa 2:00 usiku)
Atalanta v Everton (Saa 2:00 usiku)
Slavia Praha v Maccabi Tel Aviv(Saa 2:00 usiku)
Dynamo Kyiv v Skënderbeu Korçë(Saa 2:00 usiku)0
Hoffenheim v Sporting Braga (Saa 2:00 usiku)
Apollon v Lyon         (Saa 2:00 usiku)
Zlín         v Sheriff   (Saa 2:00 usiku)
Rijeka v AEK Athens (Saa 2:00 usiku)
Istanbul Basaksehir v Ludogorets (Saa 2:00 usiku)
København v L'tiv Moskva (Saa 2:00 usiku)
Austria Wien v Milan          (Saa 2:00 usiku)
Villarreal v Astana         (Saa 2:00 usiku)
Hapoel B.Sheva v Lugano (Saa 4:05 usiku)
Zorya v Östersunds FK (Saa 4:05 usiku)
Real Sociedad v Rosenborg         (Saa 4:05 usiku)
Vitesse v Lazio         (Saa 4:05 usiku)
Zulte-Waregemv Nice      (Saa 4:05 usiku)
Arsenal v Koöln         (Saa 4:05 usiku)
Marseille v Konyaspor         (Saa 4:05 usiku)
Vitoria Guimarães v Salzburg (Saa 4:05 usiku)
Crvena Zvezda v BATE (Saa 4:05 usiku)
Hertha BSC v At.Bilbao      (Saa 4:05 usiku)
Vardar v Zenit         (Saa 4:05 usiku)
FCSB v Viktoria Plzen (Saa 4:05 usiku)

Andre Ayew aitibulia Huddersfield akiibeba West Ham

Andre Ayew akiifungia West Ham bao la pili
 

Andre Ayew akishangilia bao lake

Obiang akishangilia bao lake 
LONDON, England
WEST Ham United usiku wa kuamkia leo walipata ushindi muhimu nyumbani baada ya kuichapa Huddersfield na kuitibulia rekodi yao ya kupototeza mchezo wowote tangu msimu huu wa Ligi Kuu England kuanza.
Straika Andre Ayew aliyetokea benchi alihusika na mabao yote mawili ya Wagonga Nyundo hao baada ya awali kumtengenezea bao Pedro Obiang katika ya 72 kabla ya mwenyewe kutumbukiza wavuni bao la pili dakika tano baadaye kwenye mchezo mkali uliopigwa Uwanja wa London.
Nyota huyo wa Ghana na mtoto wa Mwanasoka Bora wa zamani Afrika, Abedi Ayew Pele aliingia uwanjani dakika ya 64 kuchukua nafasi ya nyota wa zamani wa Manchester United, Javier Hernandez 'Chicharito' kabla ya kuibeba West iliyotoka kupoteza mechi yao dhidi ya NewCastle United waliowafumua mabao 3-0 ugenini.

Okwi awazidi ujanja Ngoma na Ajibu, Mtibwa yatikisa

Emmanuel Okwi akiwa na mpira wake baada ya kupiga hat trick dhidi ya Ruvu Shooting
Ibrahim Ajibu katika mazoezi ya Yanga

Donald Ngoma
Mtibwa Sugar
NA TARIQ JUNIOR
STRAIKA wa Simba, Emmanuel Okwi anayeichezea Simba amewazidi ujanja mastraika wa Yanga, Donald Ngoma na Ibrahim Ajibu, baada ya kusalia kileleni mwa orodha ya wafungaji akiwa na mabao manne, licha ya  nyota hao wa Jangwani kushuka dimbani kwa  dakika nyingi zaidi ya Mganda huyo.
Okwi ametumia dakika 90 tu kufunga mabao yake akicheza mchezo mmoja tu na kuukosa mchezao mmoja, lakini  Ngoma na Ajibu kila mmoja amecheza mechi mbili na kufunga bao moja kila mmojam, jambo lililowapa kiburi mashabiki wa Msimbazi kuwatambia wenzao wa Jangwani.
Mganda huyo aliyewahi kuichezea Yanga misimu mitatu iliyopita, aliukosa mchezo wa timu yake dhidi ya Azam Jumamosi iliyopita ulioisha kwa suluhu, lakini hilo halikumfanya ashindwe kukalia kiti cha uongozi wa wafungaji.
Okwi ambaye jana asubuhi alishindwa kuhudhuria mazoezi ya timu yake yaliyofanyika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam ili kujiandaa na mchezo wao ujao dhidi ya Mwadui Jumapili hii, alishindwa kuwahi mechi ya Azam kutokana na kuwa na timu yake ya taifa ya Uganda The Cranes iliyoenda kuvaana na Misri katika mechi ya makundi ya kuwania Fainali za Kombe la Dunia 2018.
Ngoma aliyeifungia Yanga bao la kusawazisha katika mchezo wa kwanza dhidi ya Lipuli na kutolewa katika kipindi cha pili kwenye mchezo dhidi ya Njombe Mji, bado hajarudi kwenye ubora wake tangu atoke kwenye majeraha ya muda mrefu yaliyomfanya ashindwe kuitumikia timu hiyo kwenye mechi za nusu wa msimu uliopita aliomaliza na mabao nane.
Ajibu aliyecheza dakika 180 za mechi mbili za Yanga za msimu huu, naye alifunga bao moja lililokuwa la pekee katika mchezo wao na Njombe Mji na kuzidi kuwapa kiburi Simba kuamini kuwa, licha ya Yanga kuwa na safu kali ya washambuliaji lakini jeshi la mtu mmoja, yaani Okwi ni funika bovu.
Okwi alifunga mabao manne katika mechi ya ufunguzi wa ligi dhidi yas Ruvu Shooting ambapo Simba walishinda mabao 7-0 na timu yake kushindwa kupata matokeo kwenye Uwanja wa Azam Complex dhidi ya Azam.
Mpaka sasa wachezaji 27 wamefanikiwa kufunga jumla ya mabao 32, huku Mohammed Rashid wa Prisons na Marcel Bonventure wa Majimaji wenye mabao mawili kila mmoja wakionekana kumkimbiza Okwi.
Mpaka sasa Ligi ikiwa imeshacheza mechi 16, Ruvu Shooting ndio klabu yenye ukuta mlaini baada ya kuruhusu mabao tisa na yenyewe kufunga bao moja tu, huku Chama la Wana Stand United ikiwa ndiyo timu pekee ambayo haijafanikiwa kufunga bao hata moja, licha ya yenyewe kuruhusu mabao mawili nyavuni mwao.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo nane, Ijumaa Azam itaikaribisha Kagera Sugar kabla ya Simba na Yanga kucheza katika miji ya Dar es Salaam na Ruvuma dhidi ya Mwadui na Majimaji, wakati vinara wa ligi hiyo, Mtibwa Sugar wenyewe wataendelea kuwa nyumbani kuwakaribisha Mbao FC iliyotoka kujeruhiwa mjini Dodoma na Singida United Jumapili iliyopita.

Msimamo Ligi Kuu Tanzania Bara 2017-2018 ulivyo kwa sasa
         P W D L F A PTS
1.Mtibwa  2 2 0 0 2 0 6
2.Simba    2 1 1 0 7 0 4
3.Prisons  2 1 1 0 4 3 4
4.Lipuli  2 1 1 0 2 1 4
5.Yanga  2 1 1 0 2 1 4
6.Azam  2 1 1 0 1 0 4
7.Singida  2 1 0 1 3 3 3
8.Mwadui 2 1 0 1 2 2 3
9.Mbao  2 1 0 1 2 2 3
10.Mbeya 2 1 0 1 1 1 3
11.Ndanda2 1 0 1 1 1 3
12.Majimaji2 0 1 1 2 3 1
13.Kagera2 0 1 1 1 2 1
14.Ruvu 2 0 1 1 1 8 1
15.Njombe2 0 0 2 1 3 0
16.Stand 2 0 0 2 0 2 0

WAFUNGAJI:
4 Emmanuel Okwi (Simba)
2 Marcel Boniventure (Majimaji)
Mohammed Rashid (Prisons)
1 Ibrahim Ajibu (Yanga)
Erasto Nyoni (Simba)
Juma Liuzio (Simba)
Shiza Kichuya (Simba)    
Donald Ngoma (Yanga)
Paul Nonga (Mwadui)
Yahaya Mohammed (Azam)
Salim Khamis (Mwadui)
Kenny Ally (Singida United)
Boniface Maganga (Mbao FC)
Hussein Javu (Mtibwa Sugar)
Eliud Ambukile (Mbeya City)
        Kassim Khamis (Prisons)
Nurdin Chona (Prisons)
Hassan Kapalata (Njombe Mji)
Seif Karihe (Lipuli)
Jerome Lambele (Lipuli)
Mudathir Yahya (Singida)
Michelle Katsvairo (Singida)
Seleman Kihimbwa (Mtibwa)
Habib Kayombo (Mbao)
Majid Bakar (Ndanda)
Raphael Kyara (Ruvu Shooting)

RATIBA WIKIENDI HII:
Ijumaa Sept 15, 2017
Azam v Kagera Sugar

Jumamosi Sept 16, 2017
Mtibwa Sugar v Mbao FC
Majimaji v Yanga
Prisons v Ndanda
Stand United v Singida United
Lipuli v Ruvu Shooting

Jumapili Sept 17, 2017
Simba v Mwadui
Mbeya City v Njombe Mji

MCL MAGAZETINI SEPTEMBA 12, 2017: LOWASSA AMFUATA LISSU NAIROBI

Thursday, April 13, 2017

Sanchez, Lukaku, Zlatan kuonyeshana kazi tuzo za PFA 2017

Lukaku

NYOTA wa Arsenal, Alexix Sanchez na yule wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, watachuana kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Chama cha Soka cha Wachezaji wa Kulipwa nchini England, (PFA)
Mbali na wakali hao wanaochuana kwa kufumania nyavu katika Ligi Kuu ya England (EPL), pia watakula sahani moja na nyota wengine akiwamo kinara wa mabao wa sasa wa ligi hiyo, Romelu Lukaku wa Everton.
Orodha kamili ya wawania tuzo hiyo ipo hivi;

Mchezaji Bora
Eden Hazard - Chelsea Zlatan Ibrahimovic - Manchester United
Harry Kane - Tottenham Hotspur
N'Golo Kante - Chelsea
Romelu Lukaku - Everton
Alexis Sanchez - Arsenal

Wachezaji Chipukizi

Dele Alli - Tottenham Hotspur
Harry Kane - Tottenham Hotspur
Michael Keane - Burnley
Romelu Lukaku - Everton
Jordan Pickford - Sunderland
Leroy Sane - Manchester City

Mchezaji Bora Wanawake

Lucy Bronze - Manchester City
Karen Carney - Chelsea
Jane Ross - Manchester City
Jill Scott - Manchester City
Caroline Weir - Liverpool
Ellen White - Birmingham City

Mchezaji Bora Chipukizi wa KikeMillie Bright - Chelsea
Jess Carter - Birmingham City
Nikita Parris - Manchester City
Georgia Stanway - Manchester City
Keira Walsh - Manchester City
Caroline Weir - Liverpool

Viongozi DRFA warejea tena DRFA

Almas Kasongo aliyetetea kiti cha Uenyekiti wa DRFA
Na Rahim Junior
SEHEMU kubwa ya uongozi uliokuwepo kwenye Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), akiwamo Mwenyekiti Almas Kasongo na Katibu Mkuu wake, Msanifu Kondo wamerejea madarakani baada ya kushinda kwenye uchaguzi uliofanyika leo.
Uchaguzi huo uliofanyika Hoteli ya Lamada, Ilala ilishuhudia Kasongo akitetea kiti chake mbele ya Peter Mhinzi na Emmanuel Kazimoto kwa kupata kura 12 dhidi ya 9 za Mhinzi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Temeke (TEFA).
Kondo akitetea kiti cha ukatibu Mkuu  akimbwaga Frank Mchaki na Ramadhani Nassib, huku Mhazini aliyeongoza kiti hicho kwa muda mrefu, Ally Hassan akibwaga na Ally Masoud, huku Mtanganzaji na mchambuzi mahiri wa soka nchini, Shafii Dauda akitwaa Ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF.
Wengine waliochaguliwa ni Salum Mwaking'inda aliyeshinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti, huku Michale Lupiana akishinda Uwakilishi wa Klabu na Amour Amour na Chichi Mwidege wakitwaa Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya chama hicho.

Yanga wawafuata Waalgeria kwa mafungu

MABINGWA wa Soka nchini, Yanga wameondoka nchini kwa mafungu kundi la kwanza likitimka jioni hii na jingine linatarajiwa kuondoka usiku huu ili kuwahi pambano lao la Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya MC Alger ya Algeria.
Kundi la kwanza lilitimka saa 10 likitumia ndege ya Shirika la Emirates Air likiwa na wakuu wa benchi la ufundi chini ya Kocha George Lwandamina sambamba na nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Hassan Kessy, Said Juma ‘Makapu’, Simon Msuva, Geoffrey Mwashiuya, Juma Mahadhi na straika Amissi Tambwe ambao watapitia Dubai.
Mbali na Lwandamina wengine wa benchi la ufundi waliopo kwenye kundi hilo ni Wasaidizi wake, Juma Mwambusi, Kocha wa mazoezi ya utimamu wa mwili, Noel Mwandila kutoka zambia na kocha wa makipa, Juma Pondamali.
Pia kundi hilo lina Meneja Hafidh Ally, Daktari Edward Bavu na Mchua Misuli, Jacob Onyango.
Kundi la pili litafuatia muda mchache ujao litaondoka kwa Ndege ya Shirika la Uturuki likiwa na wachezaji 13 na baadhi ya Maofisa wa timu hiyo likipitia Istanbul ambao ni makipa; Deogratius Munishi ‘Dida’ na Beno Kakolanya; mabeki; Juma Abdul,  Mwinyi Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’ na Kevin Yondan.
Pia wamo viungo ni Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Emmanuel Martin wakati mshambuliaji ni Donald ngoma. 
Wawakilishi hao walishinda mchezo wa awali jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kwa bao 1-0 hivyo inahitaji sare ama kutofungwa zaidi ya mabao 2-1 ili kutinga makundi na kuwang;oa wenyeji wao MC Alger.
Yanga haijawahi kuitoa timu yoyote ya Afrika Kaskazini wala kupata ushindi ugenini katika nchi hizo, zaidi ya sare mbili ilizopata mwaka 1992 dhidi ya Ismailia ya Misri waliotoka nao 1-1 sawa na ile ya 2008 dhidi ya Al Alkhdar ya Libya.
Kama Yanga itapenya hapo itafuzu makundi ya michuano hiyo na kuweka rekodi kwa mara ya pili mfululizo kwani mwaka jana ilipenya, ikiwa chini ya Kocha Hans Pluijm ambaye alitimuliwa na kutua Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu ujao.

Algeria yamteua Kocha Mkuu Mpya

CHAMA cha Soka cha Algeria, kimemteua Lucas Alcaraz kuwa Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya nchi hiyo maarufu kama Mbweha wa Jangwani, ikiwa ni mara ya nne kufanya hivyo katika kipindi cha miezi 13 iliyopita.
Alcaraz raia wa Hispania alitimuliwa Jumatatu iliyopita kama kocha wa Granada kufuatia klabu hiyo kusuasua kwenye La Liga ikiwa mkiani kwenye msimamo. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 anachukua nafasi ya Georges Leekens wa Ubelgiji ambaye alijiuzulu baada ya Algeria kuenguliwa katika hatua ya makundi ya michuano ya Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu.
Mechi ya kwanza ya mashindano kwa Alcaraz itakuwa dhidi ya Togo wakati Algeria watakapoanza kampeni zao za kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwaka 2019.

Mbeya City ikiibana Lyon, Pazi kama kawa

BAO la kipindi cha pili lililofungwa na Thomas Morris limeisaidia African Lyon kuepuka kipigo mbele ya Wakali wa Green Town, Mbeya City baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye pambano la Ligi Kuu Bara lililochezwa jioni ya leo Alhamisi.
Katika pambano hilo lililopigwa Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, Mbeya City itabidi ijilaumu kwa kushindwa kuibuka na ushindio baada ya kupoteza mkwaju wa penalti dakika ya 37 kabla ya zahoro Pazi kusahihisha makosa dakika tano baadaye kwa kuifungia timu hiyo bao la kuongoza.
Bao hilo lilikuwa la tano kwa winga huyo teleza ndani ya timu hiyo iliyomrejesha uwanjani baada ya kuwa nje ya karibu misimu miwili kwa tatizo la ITC iliyokuwa imenasa FC Lupopo ya DR Congo.
Uzembe uliofanywa na mabeki wa Mbeya City ulisaidia mkongwe Thomas Morris aliyewahi kutamba na Yanga na Moro United kufunga bao la kusawazisha na kuifanya Lyon kufikisha pointi 31 baada ya mechi 27.
City kwa sare hiyo imeifanya ifikishe pointi 32 sawa na Mwadui ila imebebwa kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, ikishika nafasi ya saba ikiwatoa wachimba madini hao wa Shinyanga ambao wanarudi nafasi ya 8.
Ligi hiyo itaendelea tena wikiendi hii kwa mechi sita ambapo nne zitachezwa Jumamosi ikiwamo ile inayosubiwa kwa hamu kubwa kati ya Toto Africans itakayoikaribisha Simba wanaoongoza msimamo wa ligi kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza na Jumapili zitapigwa mechi mbili tu.

Messi aichanganya Argentina adhabu ya FIFA


WAMEPAGAWA. Kitendo cha nyota wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limewatia wazimu Waargentina kiasi Chama cha Soka nchini humo (AFA) kuamua kujitosa kumtetea.
Rais wa AFA, Claudio Tapia amefunga safari mpaka Hispania ili kujadili kesi inayuomkabili Messi, ambaye ndiye tegemeo na tumaini la nchini hiyo katika mbio zake za kucheza Fainali za Kombe la Dunia 2018.
Tapia alisisitiza safari ya kwenda nchini Hispania ni mahsusi kwa ajili ya kwenda kujadili kesi ya Lionel Messi ya kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA na sio kwenda kuzungumza na Jorge Sampaoli au Diego Simeone kuhusiana na kibarua cha kuinoa nchi hiyo.
Messi alilimwa adhabu hiyo na FIFA baada ya kumtolea kauli chafu mwamuzi wakati wa ushindi wa bao 1-0 Argentina iliyopata dhidi ya Chile mwezi uliopita na kumfanya kukosa mchezo waliofungwa na Bolivia mabao 2-0 na nyingine tatu zijazo za kufuzu Kombe la Dunia.
Nyota huyo wa Barcelona anayo nafasi ya kukata rufani ya kutaka kupunguzwa kwa adhabu hiyo mwezi ujao kitu ambacho Tapia alitaka kwenda kujadili naye ana kwa ana.
Tapia alisema FIFA imemtaka Messi kupeleka shauri lake hilo la kufungiwa mechi nne baada ya mchezo wao dhidi ya Chile Alhamisi Mei 4 mwaka huu hivyo ilikuwa muhimu kwenda kujadiliana naye kuhusiana na hilo.
Mchezo ujao wa Argentina utakuwa ni ule wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Brazil utakaofanyika nchini Australia Juni mwaka huu huku mechi za kufuzu Kombe la Dunia zikitarajiwa kuendelea Agosti.

Mabao ya Barcelona yampa ulaji Dyabala Juventus

SAA chache baada ya kuitia aibu Barcelona katika mechi ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Straika wa Juventus, Paulo Dybala amesaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Italia ambao utamalizika mwaka 2022.
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 23 ameifungia Juventus mabao 16 msimu huu na kulikuwa na tetesi zikimuhusisha na kuondoka. Dybala alijiunga Juventus kwa kitita cha Pauni 23 milioni kutoka Palermo na kupewa mkataba wa miaka mitano Juni 2015 na kufanikiwa kushinda mataji mawili mwaka jana.
Dybala alisema siku zote amekuwa akitaka kufanikiwa kwenye kila kitu na anafahamu Juventus ndio mahali sahihi kuwepo kama anataka kushinda mataji. Dybala amefunga mabao 39 na kusaidia mengine 16 kwenye mechi 82 toka ajiunge na Juventus, ikiwa ni dadi kubwa zaidi ya mchezaji yeyote katika klabu kwa muda aliojiunga.

Sunday, January 15, 2017

Manchester City aibu tupu, wapigwa 4-0

Picha zote kwa hisani ya Mirror
AIBU tupu. MANCHESTER City jioni hii imekumbana na aibu kubwa baada ya kutandikwa mabao 4-0 na Everton kwenye uwanja wa Goodson Park, mjini Liverpool.
City inayonolewa na Kocha Pep Guardioala kwa kipigo hicho imesalia nafasi ya tano ya msimamo na ikiwa katika hati hati ya kuzidiwa maarifa na watani zao wa Jiji la Manchester, Man United iwapo itafanikiwa kuifunga Liverpool kwa idadi kubwa ya mabao, kwani zinaweza kulingana na kuzidiana uwiano wa mabao.
United ina pointi 39 na mabao 31 ya kufunga na kufungwa 19 wakati City kwa kipigo cha jioni hii imesaliwa na pointi 42 na mabao 41 ya kufunga na kufungwa 26, ikiwa na maana wana uwiano tofauti na mabao matatu tu mpaka sasa.
Mabao yaliyoiangamiza City leo ikiwa kiigo chao cha tano msimu huu yalitumbukizwa na Romelu Lukaku dakika ya 34, Kevin Mirallas dakika 47', Tom Davies dakia ya 79 na chipukizi Ademola Lookman aliyefunga dakika za nyingeza za mpambano huo mkali ambao umemfanya Guardiola kujikuta kwenye simanzi kubwa.
Muda mchache ujao Man United itakuwa wenyeji wa Liverpool kwenye Uwanja wa Old Trafford, kwenye mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu msimu huu timu hizo zilishindwa kutambiana kwa kutofungana. Mechi ilichezwa Oktoba 17, 2016.

Mbao, Lyon zashindwa kutambiana kesho zamu ya Toto v Prisons

Mbao FC
Lyon
Na Mwandishi Wetu
KLABU za Mbao FC na wageni wao African Lyon zimeshindwa kutambia kwenye mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Bara baada ya kutoka suluhu.
Timu hizo zimeshindwa kufunga kwenye mchezo uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kuzifanya zigawane pointi moja moja.
Kwa matokeo hayo zimezifanya timu hizo kuendelea kusalia katika nafasi zao walizokuwa kabla ya mchezo huo uliomalizika hivi punde.
Lyon imefikisha pointi 21 na Mbao imekusanya alama 20, lakini zimeshindwa kusogea katika maeneo waliyokuwapo.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumatatu kwa mchezo mmoja kati ya Toto African na Prisons jijini Mwanza na Jumanne Yanga itakuwa wageni wa Majimaji Songea na Jumatano Simba na Azam zitashuka viwanja tofauti vya mjini Morogoro na Dar es Salaam.
Simba itakuwa mgeni wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakati usiku wa saa 1 jioni, Azam itakuwa wenyeji wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.
Simba ndio vinara wa Ligi Kuu mpaka sasa ikiwa na pointi 44 baada ya kushuka uwanjani mara 18, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 40 na Kagera Sugar kushika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31 ikiiengua Azam iliyoshuka nafasi ya nne na pointi zao 30.

Msimamo wa Ligi Kuu Bara

                                P  W   D  L   F   A  Pts
1. Simba                   18 14  2   2  30  6  44
2. Yanga                   18  12  4   2  39  9  40
3. Kagera Sugar        19  9   4   6   21 18 31
4. Azam                    18  8   6   4  23  15 30
5. Mtibwa Sugar        18  8   6   4  22  19 30
6. Stand Utd             19  6   7   6  18  16  25
7. Mbeya City            18  6   6   6  16  16  24
8. Ruvu                    19   5   9   5  18  20  24
9. Prisons                 18   5   7   6  10  13  22
10.Mwadui                19   6   4   9  16  24  22
11.African Lyon         19   4   9   6  11  16  21
12.Mbao                   19   5   5   9  17  24  20
13.Ndanda                19  5   4  10  15  26  19
14.Majimaji               18  5   2  11  13  26  17
15.Toto Africans         18  4   4  10  11  20  16
16.JKT Ruvu              19  3   9   7   7   17   15

Wafungaji:   

9- Shiza Kichuya                             (Simba)
     Simon Msuva                             (Yanga)   
     Amissi Tambwe                         (Yanga)
8- Abdulrahman Mussa  (Ruvu Shooting)
    Mbaraka Yusuf              (Kagera Sugar)
7- Rashid Mandawa         (Mtibwa Sugar)
    Donald Ngoma                           (Yanga)
    John Bocco                               (Azam)
6- Mzamiru Yasin                           (Simba)
    Haruna Chanongo        (Mtibwa Sugar)
5- Omar Mponda                         (Ndanda)
    Obrey Chirwa                             (Yanga)
    Riffat Khamis                           (Ndanda)
    Victor Hangaya                        (Prisons)
    Rafael Daud                      (Mbeya City)
    Venance Joseph              (African Lyon)
4-Peter Mapunda                      (Majimaji)
    Kelvin Sabato                (Stand United) 
    Laudit Mavugo                          (Simba)
    Marcel Boniventure             (Majimaji)
    Boniface Maganga                     (Mbao)
    Deus Kaseke                              (Yanga)
    Shaaban Kisiga            (Ruvu Shooting)
    Mohammed Ibrahim 'MO'        (Simba)   
    Tito Okello                       (Mbeya City)
3- Hood Mayanja                (African Lyon)
    Ibrahim Ajib                               (Simba)
    Abdalla Mfuko                        (Mwadui)
    Subianka Lambert                   (Prisons)
    Ditram Nchimbi                (Mbeya City)
    Wazir Junior                    (Toto African)
    Issa Kanduru               (Ruvu Shooting)
    Ally Nassor 'Ufudu'       (Kagera Sugar)
    Kelvin Friday                 (Mtibwa Sugar)
    Mfanyeje                                 (Majimaji)
    Francisco Zukumbawira             (Azam)
    Shaaban Idd                                 (Azam)
    Jamal Mnyate                             (Simba)
   Jamal Soud                  (Toto Africans)
    Adeyum Saleh               (Stand United)
    Jacob Massawe             (Stand United)
2- Adam Kingwande          (Stand United)
    Samuel Kamuntu                  (JKT Ruvu)
    Vincent Philipo                            (Mbao)
    Mcha Khamis                               (Azam)
    Danny Mrwanda            (Kagera Sugar)
    Pastory Athanas           (Stand United)
    Paul Nonga                             (Mwadui)
    Fully Maganga           (Ruvu Shooting)        
    Themi Felix                  (Kagera Sugar)
    Mudathir Yahya                        (Azam)
    Atupele Green                    (JKT Ruvu)
    Jerry Tegete                          (Mwadui)
    Jamal  Mwambeleko               (Mbao)
    Vincent Barnabas     (Mtibwa Sugar)
    Adam Salamba            (Stand United)
    Jaffar Salum             (Mtibwa Sugar)

Mbaraka Yusuf aibeba Kagera Sugar kwa Ndanda FC

Kagera Sugar wakishangilia moja ya mabao yao ya Ligi Kuu Bara
Na Rahim Junior
MABAO mawili moja kila kipindi yamemfanya Mbaraka Yusuf wa Kagera Sugar kuwasogelea vinara wa mabao wa Ligi Kuu Bara, Simon Msuva, Amissi Tambwe wote wa Yanga na Shiza Kichuya wa Simba.
Yusuf aliyeisaidia Kagera kupata ushindi muhimu nyumbani wa mabao 2-0 dhidi ya Ndanda katika mechi iliyopigwa jana, amefikisha jumla ya mabao nane, moja pungufu na waliyonayo kina Msuva.
Straika huyo wa zamani wa Simba, amelingana sasa kwa ufungaji mabao nane na mkali mwingine wa Ruvu Shooting, Abdulrahman Mussa aliyeisawazishia timu yake juzi isiadhiriwe na JKT Ruvu katika mechi iliyoisha kwa sare ya 1-1.
Katika mechi nyingine ya jana Mwadui ikiwa ugenini Uwanja wa Kambarage, mjini Shinyanga ilikumbana na kipigo cha kushtukiza cha mabao 2-0 toka kwa Chama la Wana, Stand United.
Hicho kilikuwa kipigo cha kwanza kwa Mwadui mbele ya wapinzani wao hao wa jadi wa mkoa huo na kuwafanya isalie na pointi zao 22 katika nafasi ya 10, huku Stand ikichupa toka nafasi ya saba hadi ya sita kwa kufikisha pointi 25.
Mabao ya beki Adeyum Saleh dakika ya 16 na lingine la penalti la Nahodha Jacob Massawe dakika nne baadaye yaliyotosha kuipa Stand ushindi wake wa kwanza tangu ilipokimbiwa na kocha wake, Mfaransa Patrick Liewig.
Kabla ya ushindi huo Chama la Wana ilikuwa imecheza mechi 11 bila kupata ushindi wowote, huku mitatu kati ya hiyo ikiwa chini ya Kocha Mkuu mpya, Hemed Morocco, ambaye ni Kocha Msaidizi wa timu ya taifa, Taifa Stars.
Ligi hiyo jioni hii kuna mchezo mmoja unaoelekea ukingoni kati ya Mbao FC ya Mwanza dhidi ya African Lyon ya Dar es Salaam na kesho Toto Africans itaikaribisha Prisons Mbeya kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Carzola majanga matupu Arsenal, nje wiki 10 zaidi

MAJANGA. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anahofu kiungo wake nyota Santi Cazorla anaweza kukaa nje ya uwanja kwa wiki 10 zaidi kutokana na majeruhi ya kifundo cha mguu yanayomsumbua.
Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa nje ya uwanja toka Oktoba baada ya kucheza mechi 11 katika mashindano yote msimu huu. Lakini Cazorla mwenye umri wa miaka 32 sasa anategemewa kuendelea kukaa nje zaidi kutokana na majeruhi kupona taratibu kuliko ilivyotegemewa awali.
Wenger alisema Cazorla bado hajaanza hata kukimbia hivyo hadhani kama atarejea uwanjani hivi karibuni.

Imeelezwa huenda Wenger akafanya mpango wa kusajili mbadala wake.
Klabu hiyo jana Jumamosi ilivaana na Swansea City na kupata ushindi wa mabao 4-0 ugenini katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England.

PSG yaingia vita ya kumnasa Depay wa Man United

Memphis Depay
PSG nayo imoooo! Klabu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa, imedaiwa nayo kuingia kwenye mbio za kumwania winga wa Manchester United, Mholanzi Memphis Depay.
Meneja wa United Jose Mourinho tayari ameshamwambia winga huyo kutafuta timu nyingine, huku Everton na Olympique Lyon zote zikitajwa kumtaka.
PSG walikaribia kumsajili Depay kabla hajakwenda Old Trafford kwa kitita cha Pauni milioni 25 mwaka 2015, lakini sasa wanaonekana kumhitaji tena mchezaji huyo ambaye hajacheza katika kikosi cha United toka Novemba mwaka jana. United inataka kitita cha Paundi milioni 15 kwa Depay baada ya kukataa ofa ya Paundi milioni 10 iliyotolewa na Everton inayoshiriki Ligi Kuu ya England.

Breaking News: Mwili wa Amina kuletwa, kuagwa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu

HABARI zilizotufikia muda huu, zinasema kuwa mwili wa Mwandishi wa Habari wa Kampuni ya Uhuru Publications Limited, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Uhuru Wikiendi, Burudani na Mzalendo, Amina Athuman unatarajiwa kurejeshwa Dar es Salaam kesho asubuhi kwa boti kutoka Zanzibar. Msemaji wa Familia ya Marehemu, Athumani Kazukamwe, amesema jioni hii kuwa, mwili wa Amina utasafirishwa kutoka Zanzibar saa moja asubuhi kwa boti na unatarajiwa kuwasili Dar es Salaam kati ya saa tatu na saa nne asubuhi.
Kazukamwe, ambaye ni baba mkubwa wa mume wa marehemu, amesema mazishi ya Amina yamepangwa kufanyika keshokutwa Jumanne katika makaburi ya Soni, nje kidogo ya mji wa Tanga.
Amesema awali, upande wa mume wa marehemu ulitaka mazishi hayo yafanyike kesho Dar es Salaam, lakini baada ya majadiliano na familia ya marehemu, waliafikiana mazishi yakafanyika Tanga.
Kwa mujibu wa msemaji huyo wa familia ya marehemu, taratibu za kuuaga mwili wa Amina zitafanyika papo hapo bandarini na mara baada ya kumalizika, utasafirishwa kwa basi maalumu la kukodi kupelekwa Tanga.
Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL, Ramadhani Mkoma, amethibitisha mazishi ya marehemu Amina kufanyika Tanga.
Ramadhani amesema amepokea taarifa za kifo hicho kwa mshtuko mkubwa kwa sababu hakutarajia iwapo Amina angetangulia kuondoka duniani katika umri mdogo.
Amesema Amina ameacha pengo kubwa kwa sababu alikuwa mmoja wa wanahabari wa UPL waliokuwa wakifanyakazi kwa kujituma, aliipenda kazi yake na ilikuwa mwiko kwake kusukumwa kutimiza wajibu wake.
Amesema kazi aliyoifanya wakati wa michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambayo alitumwa kuandika habari zake, ni uthibitisha wa wazi wa utendaji mzuri aliokuwa nao.
Amesema hawana la kufanya isipokuwa kumshukuru Mungu kwa kuwa kila alipangalo, hakuna anayeweza kulipangua. Amewataka wafanyakazi wa UPL kumuenzi Amina kwa kuiga utendaji wake wa kazi.

Mwanariadha wa Tanzania, Alphonce Simbu ang'ara India Marathon

Simbu (wa pili kushoto) akipozi na washindani wake baada ya kutwaa nafasi ya kwanza wa Mbio za kimataifa za India Marathon 2017
Na Lasteck Alfred
MWANARIADHA wa kimataifa wa Tanzania, Alphonce Simbu, ameibuka mshindi kwenye mbio ndefu za Mumbai Marathon  2017, akifanikiwa kumpiku Mkenya Joshua Kipkorir na wakimbiaji wengine wazoefu kutoka mabara mbalimbali.
Mashindano hayo yajulikanayo kama Standard Chartered Mumbai Marathon huwa yanafanyika kila Jumapili ya tatu ya Januari katika jiji la Mumbai, India na yanaaminika kuwa ni mbio kubwa kabisa barani Asia kwa idadi ya washiriki.
Simbu, aliyedhaminiwa na kampuni ya Multichoice Tanzania, aliibuka mshindi kwa kutumia muda wa dakika 2:09:28 muda ambao ni mzuri sana kwa mbio za aina hiyo.
Akizungumzia ushindi wake, Simbu alisema ushindi huo umesababishwa na maandalizi mazuri aliyoyafanya.
Alisema anauchukulia ushindi huo kama changamoto kwa mashindano mengine makubwa na kwamba huo ni mwanzo tu. Amesisitiza kuwa ushindi huo sio wake pekee yake au Multichoice ambao ndio wathamini wake, bali ni ushindi wa Taifa zima.
Kwa upande wa Serikali,  Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Nape Nnauye alimpongeza kupitia kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akisema: "Tumefanikiwa tena, hongera Simbu, hongera RT (Chama cha Riadha Tanzania), asanteni Multichoice Tanzania kwa kumsapoti. Mungu ibariki Tanzania."
Kwa upande wake Mkuu wa Mahusiano wa Multichoice Tanzania, Johnson Mshana alisema Multichoice imefurahishwa sana na matokeo hayo na kwamba wataendela kumdhamini Simbu kwa mujibu wa makubaliano yao, ili kuhakikisha anaendelea kufanya vyema na kuliletea taifa sifa kubwa.
“Tulichukua jukumu la kumdhamini simbu katika mazoezi na maandalizi yake kwa kipindi cha mwaka mzima, kwani tunafahamu fika kuwa mazoezi na maandalizi ndiyo siri kubwa ya mafanikio katika mchezo wowote.
Alisema Mshana na kuongeza “Dhamira yetu kubwa ni kuinua vipaji na kulirejesha taifa letu kwenye ramani ya dunia katika ulingo wa michezo na burudani”
Katika mbio hizo, waigizaji maarufu wa Bollywood John Abraham and Neha Dhupia walikuwepo kuleta amsha amsha kwa washiriki. Alphonce anatarajiwa kurejea nyumbani leo Jumatatu.

Beki Mholanzi akichonganisha Chelsea na Man United

Beki Stefan De Vrij
LAZIMA kieleweke. Klabu za Chelsea na Manchester United zimedaiwa kuingia vitani kwa ajili ya kusaka saini ya beki wa Lazio, Stefan De Vrij.
Duru za kisoka zinasema kuwa, Chelsea imejipanga kupambana na Man United katika kipindi cha kiangazi kwa ajili ya kumwania beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi ambaye kwa muda mrefu amekuwa akiwindwa na Mashetani Wekundu.
Chelsea inadaiwa nao wako tayari kuingia katika kinyang’anyiro hicho, huku klabu yake ya Lazia imeondoa uwezekano wa kumuuza beki huyo katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
Hatua hiyo imetoa mwanya kwa klabu hiyo kuweka kitita cha Euro milioni 40 kwa timu itakayomhitaji majira ya kiangazi, ambapo klabu yoyote kati ya Man United ama Chelsea wakituliza kichwa inaweza kueleweka kwao kwa beki huyo.

Simanzi! Mwandishi Amina Athuman hatunaye, Malinzi amlilia

Amina Athuman enzi za uhai wake
Na Alfred Lucas
SIMANZI. Mwandishi wa habari wa michezo wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Amina Athuman amefariki dunia asubuhi ya leo Jumapili na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za rambirambi.
Malinzi ametuma salamu hizo kwa Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani kutokana na kifo hicho cha Amina, aliyekuwa visiwani Zanzibar kuripoti michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyomalizika juzi Ijumaa.
Katika salamu hizo ambazo pia zimeenda kwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto; Rais Malinzi ameelezea kushtushwa kwake kwa taarifa za kifo cha ghafla cha Amina.
“Niseme tu wazi kuwa tangu kuanza kwa michuano ya Mapinduzi, nimekuwa nikifuatilia taarifa mbalimbali zinazotolewa na wanahabari. Huwa pia sikosi magazeti ya Uhuru na Mzalendo na kuona byline (jina la mwandishi) ya Amina. Mpaka matokeo ya fainali zilizofanyika Januari 13, mwaka huu.
“Sasa asubuhi hii nimepata taarifa za kifo chake, ama kwa hakika zinasikitisha. Ni kifo cha ghafla, ninavyomfahamu binti huyo ni mchapakazi hodari na mfano uko wazi kwani katika hali ya ujauzito alikuwa hakosi kufuatilia habari,” amesema Rais Malinzi.
Kadhalika, Rais Malinzi ametuma salamu hizo za rambirambi kwa familia ya marehemu Amina, ndugu, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa mpendwa wao.
“Binafsi naona ni kama askari aliyefia vitani. Naweza kumwita ni shujaa, lakini ndivyo hivyo tena, huwezi kupingana na mipango ya Mungu, nimepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa, naomba wenzangu pia muwe na subira wakati huu mgumu ambao tasnia na Kampuni ya Uhuru Publications imepoteza mwanahabari mahiri.
Taarifa zinasema Amina alifariki dunia leo Jumapili Januari 15, 2017 akiwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Mnazimmoja, iliyoko Zanzibar mara baada ya kujifungua jana kwa mtoto ambaye pia alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Hadi mauti yanamkuta alikuwa Mwandishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo pamoja na gazeti la Burudani linalochapisha mahsusi habari za michezo na sanaa kabla ya hapo aliwahi pia kufanya kazi kampuni na Business Times Limited. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Amina Athuman Mahala Pema Peponi. Inna Lillah wa Innaa Ilaihi Rajaajiuun.

Friday, January 13, 2017

Msuva, Manula, Mwanjali noma sana Ma[pinduzi 2017


Add caption
Na Rahma White
SIMON Msuva amefanikiwa kunyakua tena tuzo ya Mfungaji Bora wa michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya mabao yake manne aliyofunga kwenye mechi mbili za awali za Yanga kushindwa kufikiwa na mchezaji yeyote.
Mwaka 2014 winga huyo alinyakua pia tuzo hiyo kwa idadi kama hiyo wakati Yanga ikiwa imeaga mashindano hatua ya robo fainali kwa kuchapwa bao 1-0 na JKU.
Kipa Aishi Manula wa Azam ambaye hakuruhusu wavu wake kuguswa hata mara moja kama alivyofanya kwenye michuano ya Kombe la Kagame mwaka 2015, alitangazwa kuwa Kipa Bora wa michuano ya mwaka huu ya Mapinduzi, huku beki wa Simba, Method Mwanjali akitwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa mashindano na Said Mohammed wa Taifa akitangazwa Mchezaji Bora Chipukizi.
Mwamuzi Mfaume Ali alitwaa tuzo ya Mwamuzi Bora na kila mmoja kati ya walionyakua tuzo hizo alitwaa kitiota cha Sh 1 milioni moja.
Tuzo hizo na zawadi kwa washindi wote wa michuano ya msimu huu wa 11 ya Kombe la Mapinduzi walikabidhiwa zawadi zao na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein aliyekuwa mgeni rasmi.
Azam ndio mabingwa wapya wa michuano hiyo iliyoanza Desemba 30 mwaka jana kwa kuilaza Simba kwa bao 1-0.

AZAM NDIO MABINGWA WAPYA WA KOMBE LA MAPINDUZI 2017

PAMBANO la fainali ya Kombe la Mapinduzi 2017 limeisha kwa Azam kutwaa taji kwa mara ya tatu bila kupoteza pambano lolote wala kufungwa bao hata moja baada ya usiku huu kuichapa Simba kwa bao 1-0.
Bao pekee la Azam liliwekwa kimiani dakika ya 13 na Himid Mao 'Ninja' na kuifanya Azam kuweka rekodi ya aina yake katika michuano hiyo ikifanikiwa kuzilaza Simba na Yanga kwa hatua tofauti na kubwa kutoruhusu bao lolote katika michuano hii ya 11 iliyochezwa Uwanja wa Amaan.
Azam ilionekana tangu mapema kuibana Simba ambayo ilicharuka dakika za mwishoni mwa washambuliaji wake Juma Liuzio, Pastory Athanas na Laudit Mavugo wakikosa mabao ya wazi.

Zimeongezwa dakika nne

ZIMEONGEZWA dakika nne kabla ya pambano la fainali tya Kombe la Mapinduzi 2017 kati ya Simba na Azam kumalizika na Azam inaelekea kuweka rekodi ya kutwaa taji lao la tatu katika fainali tatu ilizowahi kucheza katika michuano hiyo.
Kama itatwaa itakuwa inalingana na Simba ambayo ilikuwa imetwaa mataji matatu katika fainali zao tano za mwanzo kabla ya leo inayoelekea mwishoni. Azam 1 Simba 0.

Mudathir Yahya kabadili mchezo

KUINGIA kwa Mudathir Yahya kwa upande wa Azam kumefanya timu hiyo kubadilika kabisa, tofauti na kipindi cha pili kilipoanza ambapo Simba walitawala kwa sehemu kubwa ya mchezo na kuonekana kama itasawazisha bao. Bao bado 1-0 Azam ikiwa mbele.

Dakika ya 75 bado 1-0 Azam ikiongoza

DAKIKA ni ya 75 matokeo bao ni 1-0, Azam ikiongoza na timu zimefanya mabadiliko, Joseph Mahundi katoka kumpisha Frank Domayo, Mudathjiri Yahya kampokea Yahya Mohammed, huku Simba ikimtoa Mzamiru Yahya na kumuingiza Pastory Athanas. 

Pambano limeanza tena kule Amaan

PAMBANO la Simba na Azam, limeanza tena kwa ngwe ya dakika 45 za mwisho, matokeo yakiwa bado ni bao 1-0, azam wakiwa mbele.

Kocha Antonio Conte atwaa tuzo nyingine England

Kocha Conte

Zlatan na tuzo yake
KOCHA wa Chelsea, Mtaliano Antonio Conte ametwaa tuzo kwa mara nyingine ya kuwa Kocha Bora katika Ligi Kuu ya England kwa mwezi Desemba.
Hiyo ni tuzo ya tatu mfululizo ambayo Kocha hjuyo ameitwaa ikiwa ni rekodi katika ligi hiyo. Conte alipewa tuzo hiyo leo ikiwa ni mara ya tatu baada ya Oktoba na Novemba pia kuibeba.
Wakati huo huo, straika wa Man United, Zlatan Ibrahimovic amenyakua tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi huo wa Desemba mwaka jana.

Farid Mussa apata leseni, ila apelekwa timu B Hispania

Na Mahmoud Zubeiry
HATIMAYE winga chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Farid Malik Mussa amepewa leseni ya Mamlaka ya Shirikisho la Soka Hispania (RFEF) aanze kuchezea nchini humo na klabu yake, Deportivo Tenerife imempangia kuanza kuchezea kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 23.
Akizungumza na Bin Zubeiry Sports - Online leo kwa simu kutoka Tenerife, Farid amesema kwamba amepangiwa kuanza kuchezea kikosi cha U23 ili kupata uzoefu kabla ya kupandishwa kikosi cha kwanza kinachocheza Ligi Daraja la Kwanza nchini humo, maarufu kama Segunda.

Farid Mussa na mmoja ya wachezaji wenzake wa timu yake mpya
“Nimepatiwa leseni na tayari nimepelekewa Tenerife B ili nikapate uzoefu kwanza na Jumamosi (leo) natarajia kucheza mechi yangu ya kwanza dhidi ya timu inaitwa Vera,”alisema Farid.
Farid amejiunga na klabu hiyo ya Santa Cruz de Tenerife, Tenerife, visiwa vya Canary Desemba kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu kutoka Azam FC ya Dar es Salaam.
Azam FC imemtoa kwa mkopo Farid kwenda CD Tenerife kwa makubaliano maalum baada ya winga huyo kufuzu majaribio katika klabu hiyo Aprili mwaka jana alipokwenda na Mkurugenzi wa klabu yake, Yussuf Bakhresa.
Farid alitua Hispania Aprili 21 baada ya kuichezea Azam FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance mjini Tunis, Tunisia ikifungwa 3-0 na kutolewa kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya awali kushinda 2-1 Dar es Salaam.
Na ilimchukua wiki moja tu Farid kuwakuna kwa kipaji chake makocha wa Tenerife na kutaka kumnunua, lakini Azam ikakataa na kuamua kumtoa kwa mkopo.
Bin Zubeiry