STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 13, 2017

Farid Mussa apata leseni, ila apelekwa timu B Hispania

Na Mahmoud Zubeiry
HATIMAYE winga chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Farid Malik Mussa amepewa leseni ya Mamlaka ya Shirikisho la Soka Hispania (RFEF) aanze kuchezea nchini humo na klabu yake, Deportivo Tenerife imempangia kuanza kuchezea kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 23.
Akizungumza na Bin Zubeiry Sports - Online leo kwa simu kutoka Tenerife, Farid amesema kwamba amepangiwa kuanza kuchezea kikosi cha U23 ili kupata uzoefu kabla ya kupandishwa kikosi cha kwanza kinachocheza Ligi Daraja la Kwanza nchini humo, maarufu kama Segunda.

Farid Mussa na mmoja ya wachezaji wenzake wa timu yake mpya
“Nimepatiwa leseni na tayari nimepelekewa Tenerife B ili nikapate uzoefu kwanza na Jumamosi (leo) natarajia kucheza mechi yangu ya kwanza dhidi ya timu inaitwa Vera,”alisema Farid.
Farid amejiunga na klabu hiyo ya Santa Cruz de Tenerife, Tenerife, visiwa vya Canary Desemba kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu kutoka Azam FC ya Dar es Salaam.
Azam FC imemtoa kwa mkopo Farid kwenda CD Tenerife kwa makubaliano maalum baada ya winga huyo kufuzu majaribio katika klabu hiyo Aprili mwaka jana alipokwenda na Mkurugenzi wa klabu yake, Yussuf Bakhresa.
Farid alitua Hispania Aprili 21 baada ya kuichezea Azam FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance mjini Tunis, Tunisia ikifungwa 3-0 na kutolewa kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya awali kushinda 2-1 Dar es Salaam.
Na ilimchukua wiki moja tu Farid kuwakuna kwa kipaji chake makocha wa Tenerife na kutaka kumnunua, lakini Azam ikakataa na kuamua kumtoa kwa mkopo.
Bin Zubeiry

No comments:

Post a Comment