STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 13, 2017

Majembe ya Simba yatakayoivaa Azam usiku huu, Kazimoto ndani

Na Rahma Junior
KOCHA wa Simba amekitoa hadharani kikosi chake kitakachoivaa Azam muda mchache kwenye pambano la fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017 litakalochezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Sehemu kubwa ya kikosi hicho ni kile kile kilichoizamisha Yanga kwenye nusu fainali kwani golini yupo, Mghana Daniel Agyei kama kawa akilindwa na mabeki wa pembeni Janvier Bokungu na Mohammed Hussein 'Tshabalala' huku kati wakiwamo Abdi Banda na Method Mwanjali.
Jonas Mkude, Muzamir Yassin na James Kotei wakisimama kati, huku mshambuliaji akiwa Juma Liuzio 'Ndanda' na mawinga wakiwa ni Shiza Kichuya na Mkongwe, Mwinyi Kazimoto.


Akiba: Manyika Peter, Hamad Juma, Novaty Lufunga, Said Ndemla, Jamal MNyate, Pastory Athanas na Laudit Mavugo.

No comments:

Post a Comment