STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 13, 2017

Azam yaivaa Simba kuitemi, Himid Mao ndani, Domayo anasubiri

Kikosi cha Azam, hapo Domayo tu ndio yupo nje kumpisha Himis Mao 'Ninja'
Na Rahma White
MABINGWA wa Kombe la Kagame, Azam imemjumuisha kikosi Himid Mao 'Ninja', wakati wakijiandaa kuvaana na Simba muda mchache kwenye pambano la fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017 litakalochezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Sehemu kubwa ya kikosi hicho ni kile kile kilichoizamisha Yanga na Taifa Jang'ombe kwenye nusu fainali kwani golini atasimama Aishi Manula, akisaidiwa na Shomari Kapombe na Gadiel Michael, huku kati wakiwamo Aggrey Morris na Yakubu Mohammed, wakati kati kuna majembe kama Himid Mao na Shephan Kingue, huku pemeni wakicheza Salum Abubakar 'Sure Boy' na Joseph Mahundi wakati safu ya ushambuliaji itaongozwa na Nahodha, John Bocco 'Adebayopr' akisaidiana na Yahya Mohammed.

Akiba: Mwadini Ali, David Mwantika, Frank Domayo, Mudathir Yahya, Enock Atta-Agyei, Samuel Afful na Shaaban Idd.

No comments:

Post a Comment