STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Mazoezi ya Miss Kibaha 2013 yapamba moto


Mkufunzi wa Warembo wa Redd's Miss Kibaha Rehema Uzuwiya akizungumza na warembo hawo wakati wa mazoezi yao yanayo endelea katika ukumbi wa Vijana Kinondoni picha na www.burudan.blogspot.com

Warembo wa Redd's miss kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao

Warembo watakao wania taji la Redd's Miss Kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika ukumbi wa vijana Kinondoni Dar es salaam picha na www.burudan.blogspot.com

Kivumbi ya UEFA Ndogo ni leo, Chelsea kupenya kwa Basel

http://www.thenewstribe.com/wp-content/uploads/2013/04/Chelsea-vs-FC-Basel-1.jpg
Vita hii ya Basel na Chelsea inatarajiwa kujirtudia tena usiku wa leo kwenye UEFA League

IKIWA na faida ya ushindi wa mabao 2-1 iliyopata ugenini dhidi ya Basel ya Uswiss, Chalsea itawakaribisha wageni wao hao kwenye nusu fainali ya pili ya Ligi Ndogo ya Ulaya katika pambano litakalochezwa uwanja wa Stanford Bridge, jijini London.
Chelsea am,bayo inashuka dimbani ikiwa na furaha ya ushindi wa mabao 2-0 iliyopata dhidi ya Swansea City katika Ligi Kuu ya England itahitaji ushindi au sare yeyote kuweza kufuzu fainali za michuano hiyo zitakazofanyika Mei 15.
Kocha wa Chelsea, Rafa Benitez ameweka bayana wameweka akili zao kwa ajili ya pambano hilo wakiwa na tahadhari kubwa kutokana na wapinzani wao kutotabirika akikumbukia walivyowaondoa michuanoni Tottenham katika mechi ya robo fainali.
Benitez amenukuliwa akisema watashuka dimbani wakiwa na dhamira kuu ya kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi ya leo, lakini hawaipuuzii Waswisi hao ambao wametoka kupokea kichapo cha mabao 3-0 katika mechi ya ligi ya nyumbani kwao dhidi ya Luzern Jumapili iliyopita.
Naye kocha wa Basel Murat Yakin, amedai inahitgaji miujiza kidogo kuweza kuwaondosha Chelsea katika hatua hiyo ya nusu fainali na wao kutinga fainali.
Yakin alisema hata hivyo wachezaji wake wana ari kubwa na kujiamini kupita kiasi katika pambano hilo la leo dhidi ya kigogo kingine cha jiji la London baada ya awali kuiondosha Tottenham kwa mikwaju ya penati kufuatia kutoka sare ya mabao 4-4 katika mechi zote mbili.
Bila shaka ni suala la kusubiri kuona kama vijana wa darajani watatinga fainali ya pili mfululizo ya michuano ya Ulaya baada ya mwaka jana kucheza Ligi ya Mabingwa na kuiondosha patupu Bayern Munich waliotinga tena fainali hizo msimu huu baada ya jana kuing'oa kwa aibu Barcelona kwa mabao 7-0.
Pambano jingine la pili la nusu fainali ya marudiano usiku wa leo ni kati ya timu za Benfica na Fenerbache nchini Ureno.
Wenyeji hao walichezeas kichapo cha bao 1-0 ugenini nchini Uturuki wiki iliyopita, hivyo kuhitaji ushindi ili kuweka hai matumaini ya kucheza fainali hizo za UEFA Ndogo wiki mbili zijazo mjini Amsterdam, Uholanzi.

Redd's Miss Kigamboni 2013 kumekucha!

Somoe Ng'itu (wa pili toka kulia akiwa na wanahabari wenzake

FIFA yatengua uchaguzi wa TFF, kisa...!



Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limelitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuanza upya mchakato wa uchaguzi baada ya kubaini kasoro iliyotokana na ukosefu wa kutokuwepo vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.

FIFA ambayo ilituma ujumbe wake katikati ya mwezi uliopita kufanya utafiti kuhusu mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa TFF ambao ulisimamishwa baada ya baadhi ya wagombea kulalamika, imetaka uchaguzi ufanyike kabla ya tarehe 30 Oktoba 2013, lakini ukitanguliwa na mabadiliko ya katiba ambayo yatahusisha uundwaji wa vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.

Raiswa TFF, Leodegar Tenga aliwaambia waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa shirikisho hilo kuwa suala la Tanzania lilijadiliwa kwenye kikao cha Kamati ya Dharura ya FIFA kilichofanyika tarehe 28 Aprili 2013 na maamuzi yake kutumwa juzi kwa barua iliyosainiwa na KatibuMkuuwa FIFA, Jerome Valcke.

Baada ya kupokea barua hiyo, Rais wa TFF alifunga safari kwenda Dodoma jana kukutana na Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT). 

“Matarajio yetu sote yalikuwa kupokea majina ya waliopitishwa ili tufanye uchaguzi. Kinyume chake tumepokea maagizo hayo. Hata hivyo tumeona kuwa hili ni jambo la kheri kwa vile siyo tu haki itatendeka bali pia itaonekana imetendeka.” alisema Tenga, ambaye alishatangaza kuwa hatagombea tena urais baada ya kuliongoza Shirikisho kwa vipindi viwili vya miaka minne kila kimoja.

“Lengo letu ni kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa na uchaguzi kufanyika mapema iwezekanvyo kabla ya tarehe iliyotolewa. Yale mambo nayoweza kufanyika kwa pamoja yatafanyika ili tuharakishe utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na FIFA.”
Uchaguzi wa TFF ulipangwa kufanyik tarehe 23 na 24 Februari 2013 na ulikuwa ukielekea ukingoni, lakini baadhi ya wagombea walienguliwa katika hatua ya mwisho na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na ndipo walipo andika barua FIFA kuomba iingilie kati.

Rais Tenga alisema kuwa ujumbe wa FIFA ulikutana na pande zote zilizoathiriwa na mchakato wa uchaguzi na kwamba baada ya kukusanya taarifa hizo, maagizohayo ya FIFA sasa yatakuwa ni suluhisho la matatizo ya muda mrefu katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.

Katika barua hiyo, FIFA imeiagizaTFF:
1.   Kuunda vyombo sahihi (Kamati ya Maadili itakayokuwa na vyombo viwili ambavyo ni cha kutoa maamuzi ya awali na cha rufaa) ambavyo mamlaka yake yatakuwa ni kushughulikia masuala ya ukiukwaji wa maadili;
2.   Kufanya mabadiliko ya katiba kwa kuzingatia uundwaji wa vyombo hivyo;
3.   Kuanza upya kwa mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Utendaji kwa kufungua milango kwa wagombea ambao walishachukua fomu na wagombea wapya:
4.   Shughuli hiyo ikamilike ifikapo tarehe 30 Oktoba 2013.
Katika kutekeleza hayo, TFF inatakiwa iitishe Mkutano Mkuu wa Dharura kwa ajili ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya kuunda kamati hizo za maadili na Kanuni za Uchaguzi kabla ya kuendelea na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Kamati Mpya ya Utendaji.

Katika maoni yake FIFA imeeleza kuwa katika mchakato, Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliwaengua au kupitisha baadhi ya wagombea kwa kubaini kuwa walikiuka Ibara ya 9 (7) ya Kanuni za Uchaguzi na pia Ibaray a 29 (7) ya Katiba ya TFF ambavyo vinahusisha suala la kufungua kesi mahakamani, kufuja fedha za shirikisho na ukosefu wa uwajibikaji wa pamoja.

Hata hivyo, FIFA ilisema kuwa watu hao walitakiwa waadhibiwe kwanza na kamati husika (kamati za maadili) kabla ya kuenguliwa na kamati za uchaguzi za TFF.

“Kutokana na ukosefu wa kamati za maadili matokeo yake, mmoja wa wagombea amekuwa akienguliwa kwenye uchaguzi kila anapombea bila ya kujua adhabu yake ni ya muda gani,” inasema barua hiyo ya FIFA.

Rais Tenga ameagiza kuitishwa kwa kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kupokea maagizo ya FIFA na kupanga ratiba ya utekelezaji wake kwa lengo la kuhakikisha kuwa mchakato huu unatekelezwa mapema iwezekanavyo.


Shule 20 za Sekondari kuonyeshana ubabe Copa Coca Cola Ilala


JUMLA ya Shule 20 za Sekondari na Academia 10 za soka zinatarajiwa kuchuana katika mashindano ya Copa Coca Cola Wilaya ya Ilala yatakayoanza rasmi Mei 12 wilayani humo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Soka cha Ilala (IDFA) Daud Kanuti alisema timu hizo zitachuana kwenye viwanja vitatu tofauti vya Airwing-Ukonga, Shule ya Benjamini Mkapa, Ilala na Kinyerezi.
Alisema maandalizi ya michuano hiyo yanaendelea vyema ikiwamo kutolewa ratiba ya makundi ya timu hizo shiriki.
"Michuano yetu ya Coca Coca Cola Ilala inaanza rasmi Mei 12 mwaka huu kwa kushirikisha timu 20 za Shule za Sekondari na 10 za vituo vya kukuzia na kuendeleza soka, ambapo zitachuana katika viwanja vitatu tofauti,' alisema Kanuti.
Kanuti aliongeza wakati michuano hiyo ya Coca Coca ikianza Mei 12, Ligi Daraja la Tatu wilayani humo, itaanzaa kutimu vumbi lake Jumamosi Mei 4.
Alisema Ligi hiyo kuwaniwa bingwa wa Ilala na timu za kushiriki Ligi ya Kanda itashirikisha jumla ya timu 20 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.
Katibu huyo alisema tayari timu zote zimeshapewa ratiba ya michuano hiyo itakayochezwa pia kwenye viwanja vitatu tofauti vilivyopo wilayani humo.

Kaseba kuzipiga na Mkenya mwezi ujao

Japhet Kaseba

BINGWA wa Taifa wa Ngumi za Kulipwa wa uzani wa Kati anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), Japhet Kaseba anatarajiwa kupanda ulingoni mwezi ujao kupigana na bondia kutoka Kenya, Joseph Odhiambo Magudha katika pambano la kimataifa.
Pambano hilo litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi litaratibiwa na kampuni ya Bigright Promotion chini ya Ibrahim Kamwe.
Akizungumza na MICHARAZO Kamwe alisema pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 litafanyika mwezi ujao jijini Dar es Salaam katika ukumbi na tarehe itakayotangazwa baadaye.
"Kampuni yetu imeandaa pambano la kimataifa litakalomkutanisha Japhet Kaseba dhidi ya Mkenya Joseph Magudha litakalofanyika mwezi Juni na kusindikizwa na michezo nkadhaa ya utangulizi," alisema Kamwe.
Kamwe alisema pambano hilo ni fursa nzuri ya Kaseba kurejea kwenye ngumi za kimataifa baada ya kutamba nyumbani aklitokea kwenye mchezo wa Kick Boxing alipokuwa bingwa wa Afrika na Dunia.
Mratibu huyo alisema maandalizi ya pambano hilo na mengine ya utangulizi yameanza ikiwamo kuwasainisha mikataba mabondia hao kwa ajili ya michezo hiyo ya mwezi Juni.
Alisema mabondia watakaosindikiza pambano hilo la Kaseba na Mkenya ni pamoja na Kamanda wa makamanda atakayezipiga na Ibrahim Maokola, Juma Seleman dhidi ya Issa Omar, Juma Fundi dhidi ya Moro Best na Yohana Matyhayo atakaychpana na Mkenya Joseph Onyango.
Mara ya mwisho kwa Kaseba kupanda ulingoni ni Machi mwaka huu alipopigana na Maneno Osward katika pambano la marudiano la ubingwa wa taifa, ambapo kama ilivyokuwa pigano lao la mwaka jana, Kaseba aliibuka mshindi kwa pointi.

Ni fainali ya Wajerumani, Barca wapigwa tena nyumbani na Bayern

Arjen Robben akionyesha manjonjo ya ushindi

Aah hii aibu bana! Kipa wa Barcelona na beki wake wakiwa hoi

Wachezaji wa Bayern Munich wakipongeza baada ya kuisasambua Barcelona nyumbani kwao jana


Kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Gardiolla aliyetua Bayern Munich akishangilia ushindi wa timu yake mpya na Franky Ribbery


BARCELONA, Hispania
BAYERN Munich walitinga katika fainali ya kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya itakayokutanisha Wajerumani watupu wakati walipoisambaratisha Barcelona 3-0 kwenye Uwanja wa Nou Camp jana na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 7-0.
Mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu ya Ujerumani waliimaliza mechi mapema wiki iliyopita kwa ushindi wa 4-0 nchini Ujerumani na hapakuwa na namna ya kufufuka kwa Wahispania hao wakati Arjen Robben alipofunga goli la kuongoza dhidi ya kipa Victor Valdes katika dakika ya 49.
Kudhalilika kwa Barca kulikamilishwa mwishoni mwa mechi wakati Gerard Pique alipojifunga mwenyewe na Thomas Mueller, ambaye alifunga magoli mawili katika mechi yao ya kwanza, akapachika la tatu kwa kichwa.
Barca, kama Bayern ambao wanafukuzia taji la tano la Ulaya, wanategemea kipaji cha Lionel Messi, ambaye anarejea kutoka katika majeraha ya misuli ya nyuma ya paja na ambaye aliachwa benchi, lakini bila ya Mwanasoka Bora wa Dunia huyo hawakuwa na makali yoyote.
Bayern watacheza dhidi ya Borussia Dortmund katika mechi ya fainali kwenye Uwanja wa Wembley mjini London Mei 25 baada ya Dortmund kuitoa Real Madrid kwa jumla ya mabao 4-3 juzi Jumanne.

Cheka ni nouma amzima Mashali na kutibua rekodi yake ya kutopigika


Bondia Fransic Cheka Kushoto akipambani na Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Cheka Kushoto akimshambilia kwa makonde ya nguvu Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUTraundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' akishangilia ushindi uku akiwa amebebwa juu juu kama mkungu wa ndizi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Cosmas Cheka kushoto akipambana na Charles Mashali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba siku ya mei mosi Cheka alishinda kwa ponti mpambano huo Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' akimsindikiza wakati wa kupigana bondia Ibrahimu Class 'King class Mawe wakati wa mpambano wake na amos mwamakula
Bondia Amos Mwamakula kushoto na Ibrahimu Class 'King Class mawe' wakisubili matokeo ambapo class alishinda kwa point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Thomas Mashali kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Cheka katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT



Shomari kimbau akiwa na Cheka baada ya kumvisha ubingwa wa IBF Africa aliokuwa akiutetea
Kotoka kushoto ni Kocha wa mchezo wa ngumi Kimataifa Rajabu Mhamila 'Super D' mdau ambaye ajajulikana jina Mtaalishaji wa mpambano kati ya Fransic Cheka Vs Thomasi Mashali Adamu Tanaka 'Tunaluza' na MC wa mpambano huo COOL p
Rashidi Mhamila 'Ngade akiwa amepozi na Bad Boy wakati wa onesho hilo



BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa, Francis Cheka usiku wa kuamkia leo ameendeleza rekodi yake ya kuwapiga mabondia wenzake nchini baada ya kumtwanga kwa KO ya raundi ya 10 Thomas Mashali na kunyakua zawadi ya gari na kutetea taji lake la IBF-Afrika.
Cheka kwa kumpiga Mashali amefanikiwa kumvunjia rekodi mpinzani wake ya kutopigika nchini tangu ajitose kwenye ngumi hizo za kulipwa, ambapo kipigo cha jana kilikuwa cha kwanza kwake.
Mashali alikuwa na rekoidi ya kucheza mapambano 9 na kushinda nane na kutoka droo moja, lakini ukali wa ngumi za Cheka zilimfanya asalimu amri katika raundi hiyo ya 10 akiwa amebakisha mbili tu kumaliza mchezo huo uliokuwa wa raundi 12 la uzani wa Super Middle.
Ushindi huo wa Cheka umemfanya kuendeleza rekodi yake ya kuwapiga mabondia karibu wote nchini na kutowahi kupigwa katika ardhi ya Tanzania tangu mwaka 2008 akiwa amewachakaza karibu nyota wote nchini na Afrika Mashariki na Kati.
Cheka kwa kutetea taji lake sasa atapaswa kujiandaa kupambana tena na Mmalawi Chiotcha Chimwemwe aliyemtwanga kwa pointi walipoikutana katika pambano lililofanyika mjini Arusha ambapo alikuwa pia akitetea taji hilo alililotwaa kwa kumtwanga Mada Maugo, Aprili mwaka jana.