STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Shule 20 za Sekondari kuonyeshana ubabe Copa Coca Cola Ilala


JUMLA ya Shule 20 za Sekondari na Academia 10 za soka zinatarajiwa kuchuana katika mashindano ya Copa Coca Cola Wilaya ya Ilala yatakayoanza rasmi Mei 12 wilayani humo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Soka cha Ilala (IDFA) Daud Kanuti alisema timu hizo zitachuana kwenye viwanja vitatu tofauti vya Airwing-Ukonga, Shule ya Benjamini Mkapa, Ilala na Kinyerezi.
Alisema maandalizi ya michuano hiyo yanaendelea vyema ikiwamo kutolewa ratiba ya makundi ya timu hizo shiriki.
"Michuano yetu ya Coca Coca Cola Ilala inaanza rasmi Mei 12 mwaka huu kwa kushirikisha timu 20 za Shule za Sekondari na 10 za vituo vya kukuzia na kuendeleza soka, ambapo zitachuana katika viwanja vitatu tofauti,' alisema Kanuti.
Kanuti aliongeza wakati michuano hiyo ya Coca Coca ikianza Mei 12, Ligi Daraja la Tatu wilayani humo, itaanzaa kutimu vumbi lake Jumamosi Mei 4.
Alisema Ligi hiyo kuwaniwa bingwa wa Ilala na timu za kushiriki Ligi ya Kanda itashirikisha jumla ya timu 20 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.
Katibu huyo alisema tayari timu zote zimeshapewa ratiba ya michuano hiyo itakayochezwa pia kwenye viwanja vitatu tofauti vilivyopo wilayani humo.

No comments:

Post a Comment