STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Kaseba kuzipiga na Mkenya mwezi ujao

Japhet Kaseba

BINGWA wa Taifa wa Ngumi za Kulipwa wa uzani wa Kati anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), Japhet Kaseba anatarajiwa kupanda ulingoni mwezi ujao kupigana na bondia kutoka Kenya, Joseph Odhiambo Magudha katika pambano la kimataifa.
Pambano hilo litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi litaratibiwa na kampuni ya Bigright Promotion chini ya Ibrahim Kamwe.
Akizungumza na MICHARAZO Kamwe alisema pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 litafanyika mwezi ujao jijini Dar es Salaam katika ukumbi na tarehe itakayotangazwa baadaye.
"Kampuni yetu imeandaa pambano la kimataifa litakalomkutanisha Japhet Kaseba dhidi ya Mkenya Joseph Magudha litakalofanyika mwezi Juni na kusindikizwa na michezo nkadhaa ya utangulizi," alisema Kamwe.
Kamwe alisema pambano hilo ni fursa nzuri ya Kaseba kurejea kwenye ngumi za kimataifa baada ya kutamba nyumbani aklitokea kwenye mchezo wa Kick Boxing alipokuwa bingwa wa Afrika na Dunia.
Mratibu huyo alisema maandalizi ya pambano hilo na mengine ya utangulizi yameanza ikiwamo kuwasainisha mikataba mabondia hao kwa ajili ya michezo hiyo ya mwezi Juni.
Alisema mabondia watakaosindikiza pambano hilo la Kaseba na Mkenya ni pamoja na Kamanda wa makamanda atakayezipiga na Ibrahim Maokola, Juma Seleman dhidi ya Issa Omar, Juma Fundi dhidi ya Moro Best na Yohana Matyhayo atakaychpana na Mkenya Joseph Onyango.
Mara ya mwisho kwa Kaseba kupanda ulingoni ni Machi mwaka huu alipopigana na Maneno Osward katika pambano la marudiano la ubingwa wa taifa, ambapo kama ilivyokuwa pigano lao la mwaka jana, Kaseba aliibuka mshindi kwa pointi.

No comments:

Post a Comment