STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 30, 2013

Simba yaalika matawi kutoa maoni ya katiba yao


KLABU ya soka ya Simba imefungua milango kwa wanachama wake kuanza kutoa maoni na mapendekezo ya mchakato wa katiba yao ambapo kuanzia kesho wataanza kufanya hivyo kwa kupitia matawi yoao yaliyopo ndani na nje ya jijini la Dar.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa klabu hiyo, Ezekiel Kamwaga alisema kuwa zoezi hilo litachukua muda wa usiozidi siku 10 kwa kuwasilisha kwa Katibu Mkuu wao, Evodius Mtawala kabla ya kuja kufanyika kwa mkutano.

Ajali tena! Basi la 5 Alliance laua mmoja Lindi



Basi la 5 Alliance likiwa limeanguka katika ajali iliyopata leo
ABIRIA mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja amefariki dunia katika ajali ya basi la 5 Alliance na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Ajali hili inaelezwa imetokea eneo ya Nyamwage mkoa wa Lindi wakati bali basi hilo    lililokuwa likitokea Dar Es Salaam kuelekea Lindi limepinduka na kusababisha kifo cha abiria huyo na watu wengine waliokuwa ndani ya gari hilo kujeruhiwa. Taarifa kamili tunafuatilia na kuziweka hapa.

Msiba Tena! Mac 2 B afariki, Watuguru naye katangulia

TASNIA ya sanaa nchini imeendelea kupata pigo baada ya mcharaza gitaa Joseph Watuguru na Mac Maliki Simba 'Mac 2 B wamefariki dunia siku ya leo.

Watuguru alifariki  katika hospitali ya Amana wakati Mac 2 B aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, mtayarishaji wa muziki huo na Reggae kufariki leo asubuhi nyumbani kwao Yombo kwa Abiola.

Mac 2B aliyekuwa membaz wa kundi la Wateule alikuwa akisumbuliwa na miguu mpaka mauti yalipompata nyumbani kwao Yombo na anatarajiwa kuzikwa kesho asubuhi.

Naye Watuguru aliyewahi kutamba na bendi mbalimbali ikiwemo African Revolution 'Tamtam' na Mchinga Sound alifariki kutokana na kuugua muda mrefu na inaelezwa kuwa huenda naye akazikwa kesho.

MICHARAZO inatoa pole kwa wanafamilia, ndugu, jamaa na wadau wa sanaa kwa ujumla kwa misiba hiyo ambayo imekuja wakati tasnia hiyo ikiendelea kuomboleza vifo vya wasanii wengine waliotangulia mbele ya haki tangu mwaka jana.

Yanga yatoa taarifa juu ya mradi wa ujenzi wa uwanja wao


LEO tungependa kupitia kwenu kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi wetu wa Uwanja wa kisasa wa mpira katika Jiji la Jangwani kama itakavyojulikana

Mara ya mwisho tuliongea ama kuonana ilikuwa mwezi wa tatu wakati Ndugu zetu wa BCEG walipokabizi Concept design ama Usanifu wa awali na kuanzia sasa tutakuwa tunatoa taarifa za mara kwa mara kuhusu mradi huu. Wahenga walisema UKICHA KUSEMA HUTATENDA JAMBO lakini pia KUKAA KIMYA SANA kunajenga hisia mbaya na kutoa nafasi ya upotoshwaji wa habari.

Kwa kifupi napenda kuwakumbusha kuwa Makubalino ya Awali (Memorandum of Understanding) yalisainiwa 23 Novemba 2012. Pamoja na mengineyo YANGA inatakiwa:

· Kupata na kuwa na eneo la kutoshereza malengo ya mradi

· Kupata ushauri mzuri, michoro mizuri na mkandarasi mzuri wa mradi

· Kupata na kutenga fedha za kukamilisha usanifu na ujenzi wa mradi

Kwa upande wa BCEG wajibu wao ni kuwa na utaalamu na uzoefu wa kutosha. BCEG wameandaa na kukabidhi michoro ya usanifu wa awali kukidhi matakwa ya YANGA. YANGA tunatakiwa kutoa maoni yetu na na kuingia RASMI mkataba wa ujenzi.

Kutokana na kukua kwa Jiji la Dar es Salaam, na katika hali ya kutaka klabu iwe na vitega uchumi klabu imeonelea ni vyema kama ingekuwa na uwanja wa mpira wa karne ya sasa na baadaye ambao pamoja na mambo mengine utakuwa na mioundombinu ifuatayo:-

1. Uwanja wa mpira wenye viti 40,000

2. Hostel ya wachezaji na football academy ya vijana

3. Viwanja vya mazoezi

4. Uwanja wa kutosha kuegesha magari

5. ­­­­­Hoteli na sehemu ya makazi

6. Ukumbi wa mikutano

7. Sehemu ya maofisi, benki, zahanati (sports clinic)

8. Maduka, supermarket na sinema

9. Sehemu za kubarizi, kupumzikia (Recretional and Open spaces)

Mara baada ya azma yetu kukamilika eneo hili litaitwa “Jangwani City” na kufanya wakazi wa maeneo ya Jangwani na sehemu za jirani wasiende maeneo ya mbali kutafuta huduma muhimu za kijamii. Eneo hili litaboresha mandhari nzima ya Jangwani kwa kukuza mazingira na miundombinu. Hii itahusu pamoja na mambo mengine ujazaji udongo (tuta kubwa), upandaji miti, bustani za kubarizi, kuboresha mifereji ya majitaka na kudhibiti mafuriko ya eneo la Jangwani na hivyo kulipatia sura ya kibiashara na kitalii.

Ili kukamilisha azma ya kuwa na Jangwani City itakayo kuwa na miundombinu yote hiyo, Uongozi ulipeleka maombi ya eneo la nyongeza Manispaa ya Ilala na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa barua zenye kumbukumbu namba YASC/ARDHI/MWK/YM/46/2012 na YASC/ARDHI/MWK/YM/47/2012 za 12 Desemba 2012, na mpaka sasa bado maombi yetu hayajajibiwa.

Mwezi wa saba, Wadhamini/Uongozi wa YANGA walimwandikia Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuomba msaada wake kufanikisha maombi ya nyongeza ya kiwanja yaliyowasilishwa Manispaa ya Ilala na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Klabu ya Yanga ina kiwanja chenye ukubwa wa hekta 3.59 eneo la Jangwani. Kiwanja hiki kina hati miliki kwa miaka 99 toka mwaka 1972 na katika eneo hilo, klabu ilifanikiwa kujenga uwanja wa mpira wa Kaunda na Jengo la klabu la ghorofa tatu. Jengo hili lilijengwa kwa ufadhili mkubwa sana wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume (Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi) na michango ya wanachama na wapenzi wa klabu ambao kila siku wamekuwa wakiamini kuwa haba na haba hujaza kibaba.

Ndugu Wandishi wa habari kwa kifupi tumefikia hapo, zoezi la kutoa maoni yetu kuhusu michoro ya usanifu wa awali na kuingia rasmi mkataba wa ujenzi na BCEG limesimama, likisubiri majibu ya nyongeza la eneo. Ni matumaini yetu zoezi hili litakamilika hivi karibuni na kuendelea na mradi.

YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO
Dar es Salaam, 30 September 2013
Francis Mponjoli Kifukwe

Mrembo Miss Utalii Tanzania kupaa kesho kwenda Equatorial Guinea

Miss Utalii Tanzania 2013

MREMBO wa Miss Utalii Tanzania 2013, Khadija Mswaga anatarajiwa kuondoka nchini kesho kuelekea Equatorial Guinea kwa ajili ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kusaka mrembo wa Utalii Duniani 'Miss Tourism World 2013'.
Shindano hilo la urembo la dunia litafanyika katika nchi ya Equatorial Guinea ambapo warembo wa nchi 126 wanatarajiwa kuchuana kuwania taji hilo.
Rais wa Bodi ya Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo 'Chipps' aliiambia MICHARAZO kuwa mrembo huyo wa Tanzania ataondoka kesho Jumanne kwa ndege ya kampuni ya Ethiopia kuelekea nchini humo tayari kwa kinyang'anyiro kitakachofanyika Oktoba 12.
Chipungahelo alisema mwakilishi wao anaenda katika shindano hilo akiwa amebeba ujumbe wa kutangaza hifadhi ya taifa ya Ngorongoro Crater kama moja ya maajabu ya dunia Afrika.
Mrembo huyo alisema ameamua kubeba ujumbe huo kwa sababu ni hifadhi ya kipekee duniani ambayo pia inaelezewa ndiyo chimbuko la binadamu wa kwanza na sehemu pekee binadamu anaishi na wanyama kwa ushirikiano bila kudhuriana.
Mrembo huyo alisema ana imani kubwa ya kufanya vizuri katika shindano hilo ili kuifuta machozi Tanzania ambayo imekuwa na bahati mbaya ya kufanya vibaya katika kila shindano la kimataifa inayoshiriki duniani.