STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 30, 2013

Mabao 90 yatinga Ligi Kuu, Mrundi azidi kupepea Ashanti bado 'gonjwa'

Tambwe Amissi akishangilia moja ya mabao yake
JUMLA ya mabao 90 mpaka sasa yametinga wavuni wakati Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa raundi ya sita, huku Mrundi Tambwe Amissi akiendelea kuongoza orodha ya wafungaji Bora akiwa  magoli saba.
Tambwe alionmgeza bao jingine jana wakati Simba walipoizamisha JKT Ruvu kwa mabao 2-0 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa na kuwaacha mbali wachezaji wenzake wanaomfukukizia katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu.
Mfungaji Bora huyo wa Kagame Cup 2013, alifunga bao lake la saba katika mechi tatu mfululizo kwa mkwaju wa penati kabla ya Ramadhani Singano 'Messi' kuongeza la pili na kuifanya 'Mnyama' izidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 14 na mabao 15 ya kufunga na kufungwa manne.
Simba ikionekana kuwa na safu kali ya ushambuliaji, Ashanti imeendelea kuwa timu yenye ukuta mwepesi baada ya kuruhusu jumla ya mabao 14 huku yenyewe ikifunga mabao manne tu.
Matokeo ya mwishoni mwa wiki ya ligi hiyo imevuruga kabisa msimamo wa kwa baadhi ya timu kupanda nafasi za juu nyingine zikiporomoka, Kagera Sugar na Coastal Union zikichekelea huku, timu 'ndugu' za JKT Ruvu na Ruvu Shooting zikiporomoka katika msimamo huo.
Kagera iliyopata ushindi ugenini dhidi ya Rhino Rangers imekwea hadi nafasi ya pili nyuma ya Simba ikiwa na pinti 11, huku Coastal na Azam zilizoambulia sare jijini Mbeya zikikalia nafasi ya tatu zikiwa na pointi 10 kila moja, kisha kufuatiwa na Yanga, JKT Ruvu na Ruvu Shooting zikiwa nafasi ya nne na pointi zao 9.
Ashanti imeendelea kukalia mkiani ikiwa na pointi mbili tu baada ya jana kulazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Mtibwa Sugar ambayo Jumapili ijayo itashuka dimba la Taifa kuikabili Yanga mabingwa watetezi wa taji hilo.
Msimamo kamili wa ligi hiyo baadfa ya mechi za jana ni kama ifuatavyo;

                                  P  W  D  L    F  A  GD  PTS
1.  Simba                    6   4   2   0  15  4  11   14
2. Kagera Sugar         6   3   2   1   7   3    4   11
3. Azam                     6    2   4   0   9   6   3   10
4. Coastal Union        6    2   4   0   6   3   3   10
5. Yanga                    6    2   3   1  11  7   4   9
6. JKT Ruvu              6    3   0   3   6   4   2    9
7.  Ruvu Shooting      6    3   0   3   6   4   3    9
8.  Mbeya City          6   1   5   0   6   5   1    8
9.  Rhino Rangers      7   1   4   2   7   8   -1   7
10.Mtibwa Sugar       6   1  4   1   5   6    -1   7
11.Oljoro                   6   1   2   3   3   6   -3   5
12.Mgambo               6   1   2   3   2  10  -8   5
13.Prisons                  6   0   4   2   3    9   -6   4
14.Ashanti                  7   0   2   5   4  15 -11  2
 
Wafungaji Bora:

7- Tambwe Amisi (Simba)
3- Jerry Tegete , Didier Kavumbagu (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Kipre Tchetche (Azam), Peter Michael (Prisons)
2- Jonas Mkude (Simba), Jerry Santo, Haruna Moshi (Coastal Union), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Paul Nonga, Mwagani Yeya (Mbeya City), Hamis Kiiza (Yanga), Themi Felix (Kagera Sugar), Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla,(Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris,  John Bocco, Joseph Kimwaga (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally, Shaaban Nditti, (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Tumba Swedi, Paul Maono (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Godfrey Wambura, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa (Oljoro JKT)

Matokeo ya mechi zilizopita

Agosti 24, 2013Yanga vs Ashanti United (5-1)
Mtibwa Sugar vs Azam (1-1)
Oljoro JKT vs Coastal Union (0-2)
Mgambo JKT vs JKT Ruvu (0-2)
Rhino Rangers vs Simba (2-2)
Mbeya City vs Kagera Sugar (0-0)
Ruvu Shooting vs Prisons (3-0)

Agosti 28, 2013Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar (1-0)
Rhino Rangers vs Azam (0-2)
JKT Ruvu  vs Prisons (3-0)
Mbeya City vs Ruvu Shooting (2-1)
Mgambo  vs Ashanti United (1-0)
Oljoro JKT vs Simba (0-1)
Yanga  vs Coastal Union (1-1)

Sept 14, 2013Simba  vs Mtibwa (2-0)
Coastal Union  vs Prisons (0-0)
Ruvu Shooting va Mgambo JKT (1-0)
Oljoro JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Mbeya City  vs Yanga (1-1)
Kagera Sugar vs Azam (1-1)
Ashanti United  vs JKT Ruvu (0-1)

Sept 18, 2013Prisons vs Yanga (1-1)
Simba vs Mgambo JKT (6-0)
Kagera Sugar vs JKT Oljoro (2-1)
Azam  vs Ashanti United (1-1)
Coastal Union  vs Rhino Rangers (1-1)
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City (0-0)
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu (1-0)

Sept 21, 2013Mgambo JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Prisons vs Mtibwa Sugar (1-1)
Simba vs Mbeya City (2-2)
Kagera Sugar vs Ashanti United (3-0)

Sept 22, 2013JKT Ruvu vs Oljoro JKT (0-1)
Azam  vs Yanga (3-2)
Coastal Union v Ruvu Shooting (1-0)

Sept 25, 2013
Rhino Rangers vs Ashanti Utd (2-0)

Sept 28, 2013Yanga vs Ruvu Shooting (1-0)
Rhino Rangers v Kagera Sugar (0-1)
Mbeya City vs Coastal Union (1-1)
Mgambo JKT vs Oljoro JKT (0-0)

Sept 29,2013
Ashanti Utd vs Mtibwa Sugar (2-2)
JKT Ruvu vs Simba (0-2)
Prisons vs Azam (1-1)

Mechi zijazo katika ligi hiyo
Okt 05, 2013Ruvu Shooting vs Simba
JKT Ruvu vs Kagera Sugar
Coastal Union vs Azam
Oljoro JKT vs Mbeya City

Okt 06, 2013

Mgambo JKT vs Prisons
Yanga vs Mtibwa Sugar

No comments:

Post a Comment