STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 30, 2013

Rich Richie ana mbili kwa mpigo

Rich Richie
MUIGIZAJI nyota ambaye pia ni mtayarishaji na muongozaji wa filamu, Single Mtambalike 'Richie' yupo njia panda asijue ni filamu ipi kati ya mbili mpya alizozikamilisha kwa mkupuo aanze kuiingiza sokoni.
Filamu hiyo alizofyatua mkali huyo aliyeewahi kutamba na michezo ya runinga kupitia vituo vya televisheni vya ITV na CTN, ni 'Kitendawili' na 'Likizo Hii'.
Richie alisema hajui hadi sasa filamu ipi kati ya hizo aanze kuingiza sokoni kutokana na zote kuwa bomba kwa ujumbe wake na namna washiriki wake walivyozitendea haki.
"Kwa kweli nipo njia panda mpaka sasa sijui nianze na 'Kitendawili' au 'Likizo Hii' ambazo nimezikamilisha hivi karibuni na zote zimechezwa na wasanii nyota nchini," alisema Richie.
Aliwataja baadhi ya wasanii waliozishiriki filamu hizo ni pamoja na Mzee Majuto, Chuchu Hans, Maringo Saba, Baba Haji na wengine.

No comments:

Post a Comment