STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 16, 2014

Everton yafa nyumbani, Man City chupuchupu kwa Sunderland

Fernandinho
Fernandinho akiifungia City bao la kuongoza dhidi ya Sunderland
Jason Puncheon
Wachezaji wa Crystal Palace wakishangilia moja ya mabao yao wakati wakiizamisha Everton kwao
Manchester City's Samir Nasri scores his side's equaliser
Samir Nasir akiisawazishia Manchester City bao la pili dhidi ya Sunderland
Kevin Mirallas of Everton goes past Julian Speroni to score his side's second goal
Everton walipokuwa wakifurukuta kwa Crystal Palace na kuangukia pua usiku huu
Connor Wickham of Sunderland scores their first goal past Joe Hart of Manchester City
Sunderland wakiandika moja ya mabao yao langoni mw Manchester City usiku huu
TIMU ya Everton imeshindwa kurejea kwenye nafasi ya nne ya Ligi Kuu ya England baada ya kujikuta ikipokea kipigo cha mabao 3-2 kwenye uwanja wake wa nyumbani, huku Manchester City wakiponea chupuchupu kwa Sunderland na kulazimisha sare ya 2-2 nyumbani bila kutarajiwa.
Everton iliyoipisha Arsenal katika nafasi ya nne baada ya The Gunners kupata ushindi mnono jana wa mabao 3-1, ilishuktukizwa na Crystal Palace waliowafuata uwanja wa Godson Park kwa kufungwa bao  dakika ya 23 kupitia Jason Puncheon goli lililodumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa wageni kuandikisha bao la pili kupitia kwa Scott Dann dakika nne baada ya kuanza kwa kipindi hicho kabla ya Steven Naismith kuifungia Everton bao la kwanza la kufutia machozi dakika ya 61.
Wageni waliongeza bao la tatu dakika ya 73 kupitia kwa Cameron Jerome kabla ya Kevin Mirallas akaifungia wenyeji bao la pili la kufutia machozi dakika nne kabla ya mchezo huo kuisha.
Kwa matokeo hayo Everton amesaliwa nafasi ya tano na pointi 66, moja zaidi ya ilizonazo Arsenal huku wakiwa wamecheza mechi 33 kila mmoja, Crystal Palace wamechupa hadi nafasi ya 11 wakiwa na pointi 40.
Katika pambano jingine la mfululizo wa ligi hiyo, Manchestwer City ikiwa uwanja wa nyumbani ilishtukizwa na vibonde, Sunderland kwa kulazimishwa sare ya mabao 2-2.
Wenyeji walianza kuandika bao dakika ya pili lililofungwa na Fernandinho akimalizia kazi nzuri ya Kun Aguero.
Hata hivyo Sunderland wanaopigana kuepuka kushuka daraja ilirejesha bao hilo kupitia kwa Cannor Wickham katika dakika ya 73 kabla ya mchezaji huyo huyo kuongeza bao la pili lililowakata maini Manchester City katika harakati za kupunguza pengo la pointi dhidi yake na vinara Liverpool na waliopo nafasi ya pili Chelsea watakaoumana nao hivi karibuni.
Bao hilo la pili Wickham alilifunga katika dakika ya 83 kabla ya Samir Nasir kusawazisha bao hilo dakika mbili kabla ya mchezo huo kumalizika na kuifanya City kuambulia pointi moja na kufikisha 71, nne pungufu na za Chelsea yenye 75 na sita na ilizonazo Livewrpool yenye pointi 77, huku Sunderland ikisalia mkiani na pointi 26.

Bayern yaua sasa uso kwa uso na Dortmund Kombe la Ujerumani

http://images.sportinglife.com/12/02/800x600/Bayern-Munich-celeb-v-Kaiserslautern_2717058.jpgBAYERN Munich imezinduka toka kwenye vipigo mfululizo vya Ligi Kuu ya Ujerumani kwa kuifumua Kaiserslautern kwa mabao 5-1 na kutinga fainali ya Kombe la FA (DFB-Pokal).
Ushindi huo iliypopata nyumbani imeifanya Bavarians hao kukutana na mahasimu wao Borussia Dortmund iliyotangulia hatua hiyo ya fainali tangu jana kwa kuilaza Wolfsburg kwa mabao 2-0.
Bayern ilipata ushindi wake huo kwa mabao ya Schweinsteiger aliyefunga dakika ya 23,Tom Kroos dk ya 32, Thomas  Müller kwa penati dakika ya 50 kabla ya wageni wao kufunga dakika ya 60 kupitia Zoller.
Mabao mengine ya washindi yalifungwa na Mandžukić dakika ya 78 na Mario Götze dakika za lala salama.