STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 16, 2014

Bayern yaua sasa uso kwa uso na Dortmund Kombe la Ujerumani

http://images.sportinglife.com/12/02/800x600/Bayern-Munich-celeb-v-Kaiserslautern_2717058.jpgBAYERN Munich imezinduka toka kwenye vipigo mfululizo vya Ligi Kuu ya Ujerumani kwa kuifumua Kaiserslautern kwa mabao 5-1 na kutinga fainali ya Kombe la FA (DFB-Pokal).
Ushindi huo iliypopata nyumbani imeifanya Bavarians hao kukutana na mahasimu wao Borussia Dortmund iliyotangulia hatua hiyo ya fainali tangu jana kwa kuilaza Wolfsburg kwa mabao 2-0.
Bayern ilipata ushindi wake huo kwa mabao ya Schweinsteiger aliyefunga dakika ya 23,Tom Kroos dk ya 32, Thomas  Müller kwa penati dakika ya 50 kabla ya wageni wao kufunga dakika ya 60 kupitia Zoller.
Mabao mengine ya washindi yalifungwa na Mandžukić dakika ya 78 na Mario Götze dakika za lala salama.

No comments:

Post a Comment