STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 7, 2014

Spurs, Everton yapeta Ligi Ndogo Ulaya, 2 zikifuzu mtoano

Benjamin Stambouli (left) and Asteras' Pablo Mazza battle for the ball at the Theodoros Kolokotronis Stadium
Kizaazaa katika pambano la Spurs wakati ikishinda 2-1
Andros Townsend opened the scoring for the English side converting a penalty he won after being fouled in the box
Andors Townsend akifunga bao la kwanza la Spurs
Phil Jagielka akishangilia bao la pili la Everton
Osmond akishangilia bao la kuongoza la Everton nyumbani jana dhidi ya Lille
32min: Mind you, Osman is looking handy now as his cross results in Lukaku glancing a header just off target.
Naismith akifunga bao la tatu la Everton jana
Lukaku akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa Lille
TIMU za soka za Tottenham Hotspur na Everton za England zimeendelea kutamba kwenye michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europe League) baada ya kupata ushindi katika mechi za zilizochezwa viwanja tofauti.
Everton ikiwa nyumbani Goodson Park, walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Lille ya Ufaransa katika mechi ya kundi H na kuwafanya wasaliwe pointi chache kabla ya kufuzu hatua ya mtoano.
Mabao ya washindi yaliwekwa kimiani na leon Osman katika dakika ya 27, Phil Jagielka Dk 42 na la kipindi cha la Steven Naismith.
Everton imefikisha pointi nane sawa na Wolfsburg wanaoshika nafasi ya pili nyuma yao.
Nayo Spurs ikiwa ugenini  nchini Ugiriki ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Asteras Tripolis na kuongoza kundi C.
Andors Townsand alifunga bao la kuongoza dakika ya 36 kwa mkwaju wa penati kabla ya Harry Keane kufunga bao lake la nane katika mechi nane za Spurs dakika ya 42.
Wenyeji walipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 90 huku Spurs ikimpoteza Feredico Fazio kwa mchezo mbaya.
Katika michezo mingine Dinamo Moscow ilipata ushindi wa bao 1-0 na kujihakikishia tiketi ya kucheza hatua inayofuata kwa kuilaza Estoril, huku Qarabağ ikikubali kipigo nyumbani cha mabao 2-1 dhidi ya Dnipro Dniprop.
Zürich ilishinda nyumbani mabao 3-2 dhidi ya Villarreal, Apollon ililala 2-0 nyumbani mbele ya Borussia M'gla.
HJK  nayo ilitakata kwao kwa kuilaza Torino kwa mabao 2-1, huku    København ilifumuliwa kwao kwa mabao 4-0 na Club Brugge wakati
Beşiktas ilishinda nyumbani 2-1 dhidi ya Partizan.
Mechi nyingine zilishuhudia Astra na Celtic zikitoshana nguvu kw akufungana bao 1-1,         Dinamo Zagreb ikilala kwao kwa mabao 5-1 mbele ya Salzburg na     Panathinaikos ikafungwa mabao 3-2 na PSV.
Timu ya Saint-Étienne na Inter Milan zilifungana bao 1-1, huku Feyenoord ikiitambia wageni wao Rijeka kwa mabao 2-0, Sevilla ikiwa nyumbani ikailaza Standard Liège mabao 3-1 na
Wolfsburg ikaicharaza Krasnodar kwa mabao 5-1 na Sparta Prague ikaicharaza Slovan Bratislava kwa mabao 4-0.
Napoli ya Italia ikiwa nyumbani iliitambia Young Boys kwa mabao 3-0 na  Dynamo Kiev     ikashinda nyumbani kwa mabao 2-0 dhidi ya AaB, nayo Rio Ave na Steaua Bucharest zilitoka sare ya 2-2, Guingamp ikashinda 2-0 dhidi ya Dinamo Minsk, huku Fiorentina na PAOK zikifungana bao 1-1 kama ilivyokuwa kwa timu za Lokeren na Trabzonspor, huku Legia Warszawa     iliifunga mabao 2-1 Metalist.

Sikia Uzushi Huu Eti, Mwisho wa Dunia 2032

http://straphaelcc.org/pictures/Curious%20Catholic/the-end-of-the-world-2012.jpg
Picha za Propaganda za kutaka kuwaaminisha watu kwamba Wanasayansi wamebaini Dunia imefika mwishoni kinyume na mafundisho ya dini kwamba anayeijua siku hiyo na Mungu pekee
 http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02433/_end-of-the-world_2433119b.jpgWAKATI mafundisho wa dini za Kiislam na Ukristo ukiweka bayana kwamba HAKUNA AIJUAYE Siku wala Saa, kwani ANAYEFAHAMU Siri ya MWISHO WA DUNIA ni MUNGU MUUMBA (ALLAH SW), Wanasayansi wameibuka na kudai kuwa Mwisho wa dunia unatarajiwa kuwa mwaka 2032.
Tarifa hiyo inakuja wakati binadamu wakiendelea na mipango yao ya kuifanya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi kimazingira, kiulinzi na usalama.
Utabiri mpya wa kutisha unaonesha kuwa mwaka 2032 ndiyo mwisho wa sayari hii ya tatu katika mfumo wa jua. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali katika mitandao ya internet, Sayari iitwayo Nibiru, ambayo kisayansi inafahamika kama Planet X ipo njiani kuigonga dunia na hivyo kusababisha majanga mbalimbali kutokea.
ITAONEKANA ANGANI KAMA MWEZI
Kwa mujibu wa mitandao hiyo ya kisayansi, sayari hiyo ambayo inaisogelea dunia kwa kasi kubwa, itaonekana kubwa na angavu wakati wa usiku angani na kuwa katika umbo la mwezi na hivyo kufanya miezi ionekane miwili.
DALILI KWAMBA IPO JIRANI
Taarifa zaidi za kisayansi zinasema kuwa, kadiri sayari hiyo inavyozidi kusogea, dunia itaanza kutikisika na kusababisha matetemeko ya ardhi kuongezeka sehemu mbalimbali. Mbali na dunia kutikisika na matetemeko, milipuko ya volcano nayo itatokea huku idadi kubwa ya milipuko hiyo mipya ikiongezeka, vimbunga vikubwa kama Tsunami vitaibuka na mwishowe dunia itapigwa na bomu la miamba midogo na vimondo kutokea angani.
DUNIA ITAKUMBWA NA GIZA NENE
Wakati volcano zote duniani zitakapoanza kulipuka na zingine mpya kujitokeza, dunia itafunikwa na giza nene  na matope kwa wakati wote wa usiku na mchana huku watu wakitakiwa kusoma maandiko na mafundisho ya Mitume walioyafunua kwenye vitabu vikieleza wasifu huo.
NI TUKIO LA AINA YAKE KARNE YA 21
Nibiru inatajwa kama kitu kinachoisogelea dunia kinachoaminiwa kusababisha madhara makubwa ambapo kama hakitaigonga dunia, kitasababisha mtikisiko usio wa kawaida kitakapopishana nayo. Baadhi ya wanasayansi wanaamini kuwa kitendo hicho kitatokea mapema katika karne ya 21 (tuliyonayo sasa). WANASAYANSI WAPINGANA
Baadhi ya wanasayansi wanapinga kwa maelezo kwamba hakuna ushahidi wowote wa kitafiti unaoonesha wazi kwa mabingwa wa anga za juu waliobobea wa masuala ya nyota.
MWANAMKE ALIWAHI KUOTA NDOTO
Kwa mara ya kwanza jambo hilo lilitokea mwaka 1995, wakati mwanamama Nancy Lieder muasisi wa mtandao wa ZetaTalk, aliwahi kudai kuoteshwa ndoto kwamba, Mei 2003 kuna kitu kitaingilia mfumo wa jua (solar system) na kusababisha dunia kutoboka tundu litakalosambaratisha sehemu kubwa ya kizazi cha binadamu. Lieder aliifafanua kuwa, kitu hicho kitakuwa na ukubwa wa mara nne ya dunia.
BAADA YA NDOTO
Baada ya mwanamama Lieder, mtu wa kwanza kuizungumzia Nibiru alikuwa Mark Hazlewood, mwanachama wa zamani wa mtandao wa ZetaTalk ambaye mwaka 2001 alichapisha kitabu kilichoitwa Blindsided na kusema kuwa mwisho wa dunia ungekuwa mwaka 2003 baada ya kuwasili kwa sayari ya kumi (Nibiru). Katika mfumo wa sasa, baadhi ya wanasayansi wanasema sayari ziko 12, wakizitaja kwa namba 1. Jua 2. Mercury 3. Venus 4. Dunia 5. Luna (mwezi) 6. Mars 7. Jupiter 8. Saturn 9. Uranus 10. Neptune 11. Pluto 12. Nibiru.
IMANI NYINGINE ZASEMAJE
Hata hivyo, utabiri mpya uliotolewa na watu wa jamii ya Vikings jijini New York, Marekani uliwahi kusema kuwa mwisho wa dunia ungekuwa Februari 22, mwaka huu baada ya ule wa Oktoba 21 mwaka juzi kushindwa kutokea huku aliyeendesha kampeni hizo akiwahi kufa kabla ya kuona huo mwisho wa dunia.. Mitandao mbalimbali pamoja na gazeti maarufu la Daily Mail la Uingereza lilielezea utabiri huo uliofanywa na jamii hiyo ukidai kuwa mwisho wa dunia utatokana na Mungu Odin kupigana na kuuawa na shetani Wolf Fenrir, hivyo kuiachia dunia anayoishikilia. Wamesema baada ya kuiachia dunia itafurika maji ambayo yatakuwa na sumu, hivyo viumbe wote watateketea.
WATUMISHI WA MUNGU TANZANIA
Baadhi ya watumishi wa Mungu nchini wamekuwa wakisimamia andiko la kwenye Biblia linalosema kuwa, hakuna mwanadamu anayeijua siku wala tarehe ya mwisho wa dunia na ni siri ya Muumba. Makanisa mengi nchini Tanzania yana sera tofauti lakini yanaongozwa na Biblia moja. Makanisa hayo ni Romani Katoliki, Lutheran (KKKT), Anglikana na makanisa ya kiroho kama Full Gospel& Bible Fellowship la Zakaria Kakobe. Kadhalika viongozi wa Kiislam ambao mara nyingi hawapendi kujikita kuzungumzia suala hilo za kuhubiri mafundisho wa Quran na Sunnah za Mtume Muhammad SAW kuwa dalili za awali za kutokea Kiama zimeshaonekana ikiwamo WANAWAKE kukosa haya, Wazazi kukosa huruma kwa watoto na Watoto kutowaheshimu wazazi wao, kujengwa miji na barabara mpya na dunia kuwa kijiji kimoja na ukatili kupindukia, njaa na magonjwa ya ajabu ajabu na kwamba bado badili 10 ambazo zitathibitishwa kuja kwa Masih Jadal (nabii wa uongo) atakayekuwa na jicho moja ambaye hata hivyo atakuja kuhamamizwa miaka 40 baadaye na Nabii Issa AS.

FREEMASON WABARIKI
Jamii ya Freemason tayari imebariki mwisho wa dunia kwamba umefika na dunia inatarajie tukio kubwa la pamoja. Mitandao ya jamii hiyo inataja kama hizi ni nyakati za mavuno kwa maana kwamba, upande wa Mungu na shetani kushindania watu huku waendao upotevuni  wakiwa wengi.
MFUMO WA DUNIA TANGU KUUMBWA
Kwa mujibu wa kitabu kinachoitwa Panorama ya Biblia, ulimwengu tangu kuumbwa kwake umekuwa na matukio makubwa kila baada ya miaka 2000 (inaweza isitimie au ikapita kidogo). Tangu kuumbwa kwa Adamu na Eva mpaka gharika inadaiwa ni miaka 2000. Gharika hadi dunia kubadili mfumo wa mawasiliano (Mnara wa Babeli) ni miaka 2000. Kuzaliwa kwa Yesu hadi saa ni miaka 2000 ambapo katika karne hii, dunia huenda ikaingia katika tukio kubwa sana ambalo halijawahi kutokea.

Polisi yathibitisha 37 kujeruhiwa, wa4 hoi ajali ya Happy Nation

ABIRIA wanne kati ya 37 waliojeruhiwa katika ajali ya basi iliyotokea mapema leo hii wilaya ya Mbalali, Mbeya baada ya tairi la basi hilo kupasuka wakati dereva akijaribu kumkwepa mwendesha baiskeli na kupinduka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi amethibitisha muda mfupi uliopita kuwa watu 37 wamejeruhiwa vibaya, wanne wakiwa katika hali mbaya zaidi na walikuwa wakifanya mpango ya kuwahamisha kutoka Kituo cha Afya walipokimbizwa kwa matibabu ya awali ili kupelekwa Hospitali ya Rugaa ya Mbeya.
Kamanda Msani alisema kwa mujibu wa mashuhuda mwendo kasi ni tatizo lililosababisha ajali hiyo ambayo mmoja wa wajeruhi ni mtoto mdogo.
"Nipo eneo la tukio kwa sasa na tunafanya mpango wa kuwahamisha majeruhi walioo katika hali mbaya, kwani jumla ya abiria 37 akiwamo mtoto mmoja wanawake 16 wamejeruhiwa," alisema Kamanda huyo akihojiwa na Redio One Stereo.
Dereva wa ajali hiyo kwa mujibu wa Kamanda Msangi alipata upenyo na kutoroka baada ya ajali hiyo na kwamba vijana wake wameanza msako wa kumsaka popote alipo.

Simba wamcharukia Malinzi, waapa kufa na Dk Ndumbaro

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/kiki.jpg
Rais wa Simba Evance Aveva (kulia)
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgL1LPgdchJFD1adg4pCb0Bka71FkdEYaLCebHqzuZj394iyl0gPdzuaSuhfdPDPCUfr3xHmouPBJf8kQ4CDaLpwoDGdnPe79JH20dEGBRlv9KMIySyX5wRElLkomaWlOOLC7-12vaN8eg/s1600/3.jpg
Dk Ndumbaro (kulia)
UONGOZI wa Klabu ya Simba umelivaa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhusu kauli yao ya kuzitaka klabu kutojihusisha na wakili wa kujitegemea Damas Ndumbaro kupitia kampuni yake ya Maleta & Ndumbaro Advocate.
Rais wa Simba, Evans Aveva, amefunguka kuwa kwa upande wao bado wanaendelea kumsapoti Ndumbaro kwa asilimia 100 kwa sababu wao ndiyo waliomtuma na kudai kuwa watashirikiana naye kama kawaida katika masuala ya soka.
“Kamati iliyoshughulikia suala hilo ni huru na kwa upande wetu Simba tupo mstari wa mbele kuhusu suala hilo na tunamsapoti.
“Tutaendelea kumtumia Ndumbaro kama kawaida kwani tunatetea haki yetu na tunapinga vikali makato ya asilimia tano ya mapato.
“Hakuna waraka wowote tuliopewa klabu kuhusu jambo hilo,” alisema Aveva.
TFF ilitangaza kumfungia Ndumbaro kujihusisha na soka kwa miaka saba kutokana na kile kilichoelezwa kukiuka kanuni kadhaa za shirikisho hilo.

SALEH JEMBE

Aibu! Huu ndiyo waraka ulionaswa na UKAWA, Serikali yajitetea


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQVSm8E31wk1Jp_U2mmpWrcXbH6mgu_fwkTutJQyIq563kVgdwvSVBmIjI4rpufX0TN47VUQ15FkEJLKiy63fbXZ-jXPKBrJ2cUtaFT36e4Xh62GuQ4Wqe69UpStKY1LLCavYlWUgS9xE/s1600/10697324_10152511503926156_3540962510431235374_o.jpg










HUU ni Waraka ambao ulinaswa na Umoja wa Katiba wa Wananchi (UKAWA) ambao umedaiwa kutolewa na serikali kwa ajili ya kuelekeza vyombo vya habari kuhakikisha wanasaidia KURA za NDIYO dhidi ya Katiba Pendekezwa wakati zoezi la upigaji kura kuipitisha kuwa Katiba Kamili kuibeba KATIBA hiyo inayopingwa na baadhi wananchi kutokana na ukweli imepuuza baadhi ya MAONI ya Wananchi na KUWEKWA MAONI ynayodaiwa kuwa masilahi kwa vigogo wa Chama Tawala kinachoiongoza nchi kwa sasa. Mapema leo asubuhi Msemaji wa Ikulu, Salva Rweyemamu alinukuliwa na BBC akikiri kuwepo kwa waraka huo akidai ni wa KAWAIDA na HAKUNA haja ya WATU  kupotoshwa kuwa ni MBINU za serikali KULAZIMISHA KATIBA hiyo hata kama ni kweli wapo wanayoipinga. Kwa hali hii ni kweli upo UHURU wa MAWAZO kwa WANANCHI?! IKULU inahusiana vipi na Kampeni Hii wakati suala hili?! Hii uthibitisho wa madai na vilio vya watu wengi kuwa KATIBA iliyopendekezwa siyo ya WANANCHI bali ni ya WATAWALA. MICHARAZO MITUPU yetu MACHO!

.

Newz Alert! Basi la Happy Nation lapinduka Mbeya


Picha kwa Hisani ya Joseph Mwaisango
TAARIFA ambazo zimepatikana kutoka mjini Mbeya zinasema kuwa  Basi la Happy Nation limepata ajali muda huu baada ya dereva wa basi ilo kufanya juhudi za kutaka kumkwepa mwendesha baiskeli kushindikana na kupelekea kutokea kwa ajali hiyo. Ajali hii imetokea eneo la  Igurusi na pia basi hilo lilitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam kwa basi hilo kupinduka kama livayoonekana pichani, Inaelezwa kuwa hakuna maafa isipokuwa watu kadhaa wamejeruhiwa katika ajali hiyo.