STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 7, 2014

Polisi yathibitisha 37 kujeruhiwa, wa4 hoi ajali ya Happy Nation

ABIRIA wanne kati ya 37 waliojeruhiwa katika ajali ya basi iliyotokea mapema leo hii wilaya ya Mbalali, Mbeya baada ya tairi la basi hilo kupasuka wakati dereva akijaribu kumkwepa mwendesha baiskeli na kupinduka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi amethibitisha muda mfupi uliopita kuwa watu 37 wamejeruhiwa vibaya, wanne wakiwa katika hali mbaya zaidi na walikuwa wakifanya mpango ya kuwahamisha kutoka Kituo cha Afya walipokimbizwa kwa matibabu ya awali ili kupelekwa Hospitali ya Rugaa ya Mbeya.
Kamanda Msani alisema kwa mujibu wa mashuhuda mwendo kasi ni tatizo lililosababisha ajali hiyo ambayo mmoja wa wajeruhi ni mtoto mdogo.
"Nipo eneo la tukio kwa sasa na tunafanya mpango wa kuwahamisha majeruhi walioo katika hali mbaya, kwani jumla ya abiria 37 akiwamo mtoto mmoja wanawake 16 wamejeruhiwa," alisema Kamanda huyo akihojiwa na Redio One Stereo.
Dereva wa ajali hiyo kwa mujibu wa Kamanda Msangi alipata upenyo na kutoroka baada ya ajali hiyo na kwamba vijana wake wameanza msako wa kumsaka popote alipo.

No comments:

Post a Comment