STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 9, 2016

Liverpool yaingia vitani kumwania Jamie Vardy

https://metrouk2.files.wordpress.com/2015/04/football-leicester-citys-jamie-vardy-celebrates-after-scoring-their-first-goal.jpg
Jamie Vardy
LIVERPOOL ipo tayari kuingia kwenye vita ya kumwania straika wa Mabingwa wa England, Jamie Vardy.
Kwa mujibu wa Daily Star, The Kop imekuwa ikimwania mkali huyo wa mabao mwenye umri wa miaka 29 kwa misimu miwili sasa.
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp, tayari ndani ya kikosi chake kina wanaume wa shoka katika safu yake ya ushambuliaji ikiongozwa na Daniel Sturridge, Divock Origi, Christian Benteke na Danny Ings.
Hata hivyo inaelezwa kuwa Vijogoo hao wa Anfield wapo tayari kumuuza mmoja wa mastraika hao, huku Benteke akihusishwa zaidi ili kumpisha Vardy, kwa vile ni kama hayupo kwenye mipango ya Kocha Klopp.
Klabu ya Arsenal imekuwa nayo ikimsaka straika huyo, ila mwenyewe amedaiwa hajaamua lolote kwa sasa mpaka baada ya michuano ya fainali za Euro 2016 inayoanza kesho Ijumaa huko Ufaransa akiiwakilisha nchi yake ya England.

Luke Shaw amtumia ujumbe Mourinho tayari kwa kazi OT

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2014/10/28/08/Luke-Shaw-2.jpgYUPO tayari kwa kazi, asikuambie mtu. Beki mahiri  wa pembeni wa Manchester United, Luke Shaw amemtumia ujumbe Kocha wake mpya, Jose Mourinho akisema kwamba yupo fiti kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.
Nyota huyo aliyeshindwa kuitumia Mashetani Wekundu kwa msimu mzima kutokana na kuvunjia mguu mara mbili wakati akiipigania klabu yake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya PSV Eindhoven, alitumia akaunti yake ya instagram kumfikishia ujumbe kocha wake.
"Nipo tayari" alisema Shaw.
Siku baada ya siku naendelea vema na nazidi kuimarika," aliongeza beki huyo wa zamani wa klabu ya Southampton.

Maskini Agger! Aamua kutundika daluga bila kupenda

http://i1.manchestereveningnews.co.uk/incoming/article660491.ece/ALTERNATES/s615/C_71_article_1584808_image_list_image_list_item_0_image.jpgHANA namna. Maumivu ambayo yamekuwa yakimuandama mara kwa mara nyota wa zamani wa Liverpool, Daniel Agger yamemfanya atundike daluga. Agger ametangaza kustaafu soka akiwa  ndio kwanza ana umri wa miaka 31 tu. Beki huyo amekuwa akisumbuliwa kwa kipindi kirefu cha soka lake la majeruhi aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuelezea uamuzi wake huo. Agger aliandika katika twitter akiwashukuru wale wote waliomuunga mkono katika kipindi chote na kuongeza japo ni uamuzi mgumu, lakini anadhani ni sahihi kwa afya yake.
Beki huyo wa kimataifa wa Denmark aliyeondoka Liverpool mwaka 2014 baada ya kuitumikia kwa miaka nane na kurejea katika klabu yake ya utotoni ya Brondby, amewahi kuichezea nchi hiyo mechi 75. Mkali huyo ameingia katika orodha ya nyota waliowahi kustaafu soka mapema kabla ya wakati wao kwa sababu mbalimbali ikiwamo majeruhi yasiyoisha.

Ronaldo, Messi hawashikiki kwa mkwanja mnene duniani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgY8PvBrWzFoQIsf0lo44zBa1a5LOgQGVqaoJ90UrwDJJgXi6t_8HUQACiYEVoOsmc7yvAiWq9bU1MxejhpuojP57RhYySRr985IDkhFY-SDoKpnHzRkpsJcPrNdqi1JLmYe4aRX5wQzxo/s1600/lionel_messi_vs_cristiano_ronaldo.jpgWANANUKA pesa. Labda ubishe tu, lakini imefichuliwa kuwa nyota wanaochuana kwa sasa duniani, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ndio wanamichezo wanaolipwa zaidi duniani.
Kwa mujibu wa Jarida maarufu la Forbes la Marekani limewataja nyota hao kuwa vinara duniani kwa kuvuta mkwanja wa maana wakiwazidi wanamichezo wengine.
Nyota wa Real Madrid, Ronaldo ndiye anayeongoza orodha hiyo kwa kukunja kitita cha Pauni Milioni 60.9 katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, huku nyota wa Barcelona Messi akijikusanyia kiasi cha Pauni Milioni 56.3.
Mkali wa mchezo wa Gofu, Tiger Woods na bondia Floyd Mayweather ndio waliokuwa wakitawala orodha hizo kwa muongo mmoja uliopita, lakini Woods akiandamwa na majeruhi na kushuka kiwango na Mayweather akiwa amestaafu Ronaldo na Messi wamepanda na kuongoza orodha hiyo kilaini.
Ronaldo anakuwa mwanamichezo wa pili kutoka katika timu baada ya nguli wa mpira wa kikapu Michael Jordan kuongoza orodha hizo toka jarida hilo lilipoanza kukokotoa vipato vya nyota vya wanamichezo mbalimbali mwaka 1990.
Nyota wengine waliopo katika orodha hiyo ni nyota wa mpira wa kikapu Lebron James anayeshika nafasi ya tatu kwa kuingiza Pauni Milioni 53.4, nyota wa tenisi Roger Federer anashika nafasi ya nne akiingiza Pauni Milioni 46.9 na mkali mwingine wa Kikapu, Kevin Durant anakamilisha Tano Bora kwa kuingiza Pauni Milioni 38.6.
Mastraika matata kwa kufumania nyavu Neymar, Zlatan Ibrahimovic na Gareth Bale ndio wachezaji soka wengine pekee waliopo katika orodha hiyo wakiwa katika nafasi ya 21, 22 na 25 kwa kuingiza kiasi cha Pauni Milioni 25.8, 25.7 na 24.7.

Real Madrid yawinda rekodi mpya kwa Pogba

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2015/08/25/20/pg-64-pogba-1-getty.jpg
Paul Pogba anayeingia rada za Real Madrid
MWENDO wa noti tu. Klabu ya Real Madrid ipo tayari kumwaga mkwanja wa nguvu ili kuipiku Manchester United inayotaka kumrejesha kikosini, Paul Pogba anayekipiga Juventus.
Klabu hiyo imedaiwa ipo tayari kutoa Pauni Milioni 94 ili kunasa saini ya Pobga anayewindwa na klabu yake ya zamani Man United walio tayari kuvunja benki na kumwaga Pauni Milioni 78.
Kwa mujibu wa gazeti maarufu la michezo la Gazzetta dello Sport la Italia limesema kuwa, Real Madrid imepania kumnasa kiungo huyo fundi kutoka Ufaransa, licha ya kwamba katika mbio hizo pia Matajiri wa Manchester City wapinzani wakuu wa Man United nao wanammendea kimyakimya.
Iwapo Rela itafanikiwa kumnasa Pogba kwa kiwango hicho cha fedha itakuwa imevunja rekodi inayoshikilia kwa sasa ya kumnasa Gareth Bale misimu mizili iliyopita ilipomwaga kiasi cha Pauni Milioni 80.
Gazeti hilo limefichua kuwa, Mkurugenzi wa Juventus Giuseppe 'Beppe' Marotta wiki ijayo anatarajiwa kutua Hisapnia kwa ajili ya mazungumzo ya uhamisho wa Alvaro Morata, lakini pia suala la Pobga litagusiwa.
Mashetani Wekundu pia walikuwa wakimnyatia Moratta, lakini inaonekana wazi Jose Mourinho atachemsha mbele ya mabosi wake wa zamani Real Madrid.

http://img.kiosko.net/2016/06/09/it/gazzetta_sport.750.jpg
gazeti lililodokeza mipango ya Real kutaka kuvunja rekodi ya kumnyakua Pogba

Rodriguez azigonganisha Manchester City, United

https://metrouk2.files.wordpress.com/2014/06/875x10001.jpg
James Rodriguez

KLABU ya Manchester City imeingia kwenye vita dhidi ya mahasimu wake, Manchester United katika mbio za kumwania nyota wa Real Madrid, James Rodriguez.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia amekuwa akiwindwa pia na mabingwa wa Ufaransa, PSG, lakini duru la kispoti zinadokeza kuwa, Rodriguez ambaye kusalia kwake Santiago Bernabeu ni majaliwa anawindwa na mabingwa hao wa zamani wa England.

City chini ya kocha mpya, Pep Guardiola imevutiwa na Mfungaji Bora huyo wa Kombe la Dunia 2014 na kwamba wapo tayari kumwaga kitita ili kumnyakua.
Klabu za PSG na Bayern Munich iliyo chini ya Kocha mpya, Carlo Ancelotti aliyewahi kumnoa Rodriguez wakati akikinoa kikosi cha Blancos, nao wanatajwa kumnyemelea mkali huyo ambaye amekuwa hana raha Real Madrid kutokana na kuishia benchini.
Rodriguez ambaye ni nahodha wa Colombia kwa sasa yupo kwenye vita ya kuisaidia timu yake kufanya vema katika michuano ya Copa America 2016 inayochezwa Marekani.

Paul Pogba awaota kina Pele, Diego Euro 2016 watamkoma!

http://bolavip.cdnfsn.com/img/rankings/x/n1406834042.jpg
Paul Pogba
MBONA mtamkoma. Kiungo nyota wa Juventus aliyewahi kukipiga kwa Mashetani Wekundu, Manchester United, Paul Pogba amefunguka kwa kudai kuwa anataka akumbukwe kwa soka lake kama ilivyokuwa kwa kina Diego Maradona wa Argentina na Pele wa Brazil.
Pogba ambaye atakuwa na jukumu la kuisaidia nchi yake kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya (Uefa Euro 2016) inayofanyika kwao Ufaransa, alisema kuwa,  amepania kufikia malengo yake hayo kwa kujituma na kuhakikisha kila siku anaimarika.
Kiungo huyo aliyeiwezesha Juventus kunyakua mataji manne ya Ligi Kuu ya Serie A na kucheza fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka jana, amekuwa akizidi kuimarika na kuwa mmoja ya nyota wanaomezewa mate kwa ubora wake wa soka.
Pogba aliondoka United kuelekea kwa Kibibi Kizee cha Turin mwaka 2012 na akihojiwa na runinga ya ESPN, Pogba alisema  kwasasa hadhani kama ameshafanya lolote la maana katika soka kwa vile bado kuna mataji mengi hajawahi kushinda ikiwamo Ligi ya Mabingwa Ulaya, Kombe la Dunia na hata Euro.
Hivyo amesema kuwa atapambana kiume katika ushiriki wake wa soka ili kuona anafika kule ambako kina Diego na Pele walifikia kiasi cha kubaki kuwa gumzo licha ya kustaafu kitambo na kuibuka kwa nyota mbalimbali duniani kwa sasa.

Adidas yaiomba radhi Colombia kwa kuchapia tangazo

Tangazo lililozua gumzo kwenye mitandao ya kijamii hasa twitter ambapo Adidas ilishambuliwa kabla ya kuliondoa na kuomba radhi
WAUNGWANA. Kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas imeonyesha uungwana kwa kuomba radhi kwa kosa la kuliandika vibaya jina la Colombia katika matangazo yake yanayohusu jezi mpya wanazotumia timu ya taifa ya nchi hiyo katika michuano ya Copa America 2016.
Tangazo hilo ambalo linawaonyesha wachezaji wa Colombia wakiwa katika jezi nyeupe liliondolewa baada ya mitandao ya kijamii kushambulia kwa kwa kuliandika vibaya jina la nchi hiyo ambapo badala ya kuandika Colombia waliandika Columbia.
Katika taarifa yake kampuni hiyo yenye makao yake makuu huko Portland, Oregon imedai kuwa wanathamini ushirikiano wao na Shirikisho la Soka la Colombia na kuwaomba radhi kwa makosa hay
o yaliyofanyika. Kampuni hiyo imekuwa ikitengeneza sare za Colombia tangu mwaka 2011.

Neymar Jr matatani kwa udanganyifu, kuburuzwa kortini


MSAMBWENI. Straika nyota wa Brazili anayeichezea klabu ya Barcelona, Neymar Jr, ameingia matatani baada ya Waendesha Mashitaka nchini Hispania kutaka ashitakiwe kwa kosa la udanganyifu.
Waendesha Mashitaka hao kutoka Mahakama ya Juu ya Makosa ya Jinai Hispania, wanamtuhumu Neymar na baba yake kuficha ukweli wa thamani halisi ya uhamisho wake kutoka Santos kwenda Barcelona.
Barcelona ilitangaza kumnunua Neymar kwa kitita cha Euro Milioni 57 mwaka 2013, huku wazazi wake, Neymar da Silva Santos na Nadine Goncalves sa Silva Santos wakivuta mkwanja wa haja wa Euro Milioni 40 na klabu yake ya zamani Santos wakipata Euro Milioni 17.
Lakini waendesha mashtaka hao wamesema ada ya uhamisho ya nyota huyo ilifikia kitita cha Euro Milioni 83, ingawa pande zote mbili zimekanusha kufanya jambo lolote baya kwenye uhamisho huo.

Tattoo zamponza msela, apasuliwa mara 25 kuzifuta usoni

Akianza matibabu
zilipokuwa zikiondolewa kwa operesheni maalum
Picha tofauti kuelekea kuziondoa tattoo zake usoni
http://www.smh.com.au/content/dam/images/1/m/u/g/a/image.related.articleLeadwide.620x349.1mug6.png/1320183665650.jpg
Alivyo sasa bila Tattoo
AMA kweli ujanja mwingi mbele kiza. Hebu soma kisanga kilichompata huyu jamaa ambaye alikuwa kinara wa kundi moja la wakora nchini Ujerumani.
Msela huyo kwa kutaka kujifanya anaenda na wakati alijichora tattoo kadhaa mwilini mwake, lakini mwishoni wa yote amejikuta akipata maumivu na kutoboka kiasi kikubwa cha fedha baada ya kufanyiwa upasuaji mara 25 ili kuzifuta tattoo hizo za usoni.
Inaelezwa jamaa huyo, Bryon Widner alitumia kiasi cha Pauni 20, 233 ambazo ni kama Shs. 63.9 Milioni, huku akisimulia namna alivyopata maumivu makali kwa ajili ya kusafisha uso wake kuondoa tattoo hizo.
Widner alisema kuwa, alipitia maumivu makali sana ili kusafisha sura yake na kuzitoa tattoo hizo na alitumia muda wa miezi 16 katika operesheni hizo 25 ili kuweka sawa sura yake.
Upasuaji huo wa kuondoa tattoo hizo za usoni kati ya tattoo kibao alizojichora mkora huyo ulifanywa na Dk Bruce Shack wa Vanderbilt University Medical Center kilichopo mjini Nashville.
Kitu cha kufutia ni kwamba licha ya kadhia zote hizo, kwa sasa Widner amesafishika sura yake akiwa hana kovu lolote usoni, jambo linalompa faraja.