STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 9, 2016

Liverpool yaingia vitani kumwania Jamie Vardy

https://metrouk2.files.wordpress.com/2015/04/football-leicester-citys-jamie-vardy-celebrates-after-scoring-their-first-goal.jpg
Jamie Vardy
LIVERPOOL ipo tayari kuingia kwenye vita ya kumwania straika wa Mabingwa wa England, Jamie Vardy.
Kwa mujibu wa Daily Star, The Kop imekuwa ikimwania mkali huyo wa mabao mwenye umri wa miaka 29 kwa misimu miwili sasa.
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp, tayari ndani ya kikosi chake kina wanaume wa shoka katika safu yake ya ushambuliaji ikiongozwa na Daniel Sturridge, Divock Origi, Christian Benteke na Danny Ings.
Hata hivyo inaelezwa kuwa Vijogoo hao wa Anfield wapo tayari kumuuza mmoja wa mastraika hao, huku Benteke akihusishwa zaidi ili kumpisha Vardy, kwa vile ni kama hayupo kwenye mipango ya Kocha Klopp.
Klabu ya Arsenal imekuwa nayo ikimsaka straika huyo, ila mwenyewe amedaiwa hajaamua lolote kwa sasa mpaka baada ya michuano ya fainali za Euro 2016 inayoanza kesho Ijumaa huko Ufaransa akiiwakilisha nchi yake ya England.

No comments:

Post a Comment