STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 9, 2016

Luke Shaw amtumia ujumbe Mourinho tayari kwa kazi OT

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2014/10/28/08/Luke-Shaw-2.jpgYUPO tayari kwa kazi, asikuambie mtu. Beki mahiri  wa pembeni wa Manchester United, Luke Shaw amemtumia ujumbe Kocha wake mpya, Jose Mourinho akisema kwamba yupo fiti kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.
Nyota huyo aliyeshindwa kuitumia Mashetani Wekundu kwa msimu mzima kutokana na kuvunjia mguu mara mbili wakati akiipigania klabu yake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya PSV Eindhoven, alitumia akaunti yake ya instagram kumfikishia ujumbe kocha wake.
"Nipo tayari" alisema Shaw.
Siku baada ya siku naendelea vema na nazidi kuimarika," aliongeza beki huyo wa zamani wa klabu ya Southampton.

No comments:

Post a Comment