STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 9, 2016

Adidas yaiomba radhi Colombia kwa kuchapia tangazo

Tangazo lililozua gumzo kwenye mitandao ya kijamii hasa twitter ambapo Adidas ilishambuliwa kabla ya kuliondoa na kuomba radhi
WAUNGWANA. Kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas imeonyesha uungwana kwa kuomba radhi kwa kosa la kuliandika vibaya jina la Colombia katika matangazo yake yanayohusu jezi mpya wanazotumia timu ya taifa ya nchi hiyo katika michuano ya Copa America 2016.
Tangazo hilo ambalo linawaonyesha wachezaji wa Colombia wakiwa katika jezi nyeupe liliondolewa baada ya mitandao ya kijamii kushambulia kwa kwa kuliandika vibaya jina la nchi hiyo ambapo badala ya kuandika Colombia waliandika Columbia.
Katika taarifa yake kampuni hiyo yenye makao yake makuu huko Portland, Oregon imedai kuwa wanathamini ushirikiano wao na Shirikisho la Soka la Colombia na kuwaomba radhi kwa makosa hay
o yaliyofanyika. Kampuni hiyo imekuwa ikitengeneza sare za Colombia tangu mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment