STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 9, 2016

Neymar Jr matatani kwa udanganyifu, kuburuzwa kortini


MSAMBWENI. Straika nyota wa Brazili anayeichezea klabu ya Barcelona, Neymar Jr, ameingia matatani baada ya Waendesha Mashitaka nchini Hispania kutaka ashitakiwe kwa kosa la udanganyifu.
Waendesha Mashitaka hao kutoka Mahakama ya Juu ya Makosa ya Jinai Hispania, wanamtuhumu Neymar na baba yake kuficha ukweli wa thamani halisi ya uhamisho wake kutoka Santos kwenda Barcelona.
Barcelona ilitangaza kumnunua Neymar kwa kitita cha Euro Milioni 57 mwaka 2013, huku wazazi wake, Neymar da Silva Santos na Nadine Goncalves sa Silva Santos wakivuta mkwanja wa haja wa Euro Milioni 40 na klabu yake ya zamani Santos wakipata Euro Milioni 17.
Lakini waendesha mashtaka hao wamesema ada ya uhamisho ya nyota huyo ilifikia kitita cha Euro Milioni 83, ingawa pande zote mbili zimekanusha kufanya jambo lolote baya kwenye uhamisho huo.

No comments:

Post a Comment