STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 31, 2014

Chelsea yazidi kujiimarisha, Kagawa arejea Dortmund

KLABU ya Chelsea imezidi kujiimarisha baada ya kukamilisha uhamisho wa Loic Remy kwa dau la Pauni Milioni 8 kutokaq QPR, huku Mjapan Shinji Kagawa wa Manchester United akirejea klabu yake ya zamani ya Borrusia Dortmund.
Remy aliyekuwa anatakiwa pia na Arsenal, anakwenda kuziba nafasi ya Fernando Torres aliyehamia AC Milan kwa mkopo wa muda mrefu.
Uhamisho huu ni faraja kwa Remy ambaye sasa anakwenda kujiunga na klabu inayocheza Ligi ya Mabingwa Ulaya. Kocha Mreno, Jose Mourinho alihitaji mshambuliaji baada ya kumtoa kwa mkopo Torres.
Katika kuelekea mwisho wa kufungwa kwa dirisha la usajili barani Ulaya, Shinji Kagawa ambaye hakuwa akipewa nafasi kubwa ndani ya Mashetani WEkundu amerejea Ujerumani kuichezea Dortmund.
Kiungo huyo amerejea Dortmund kwa dau la Pauni Milioni 6.3, miaka miwili tu tangu aondoke klabu hiyo ya Ujerumani.
Kagawa atasaini Mkataba wa miaka minne na Dortmund, ambayo ilimuuza Mjapani huyo United mwaka 2012 kwa Pauni Milioni 12.
Shinji Kagawa akikabidhiwa uzi wake mpya wa Dortmund baada ya kuondoka Manchester Utd

Remy: 'When I heard Chelsea wanted me I said "let's go" because they are one of the best clubs in the world.'
Remy akisaini mkataba wa kujiunga na Chelsea
Akionyesha uzi mpya wa klabu yake ya Chelsea

Arsenal bado haijatulia, Sanchez aendelea kufunga

Alexis Sanchez scores his first Premier League goal for Arsenal
Sanchez akifunga bao la Arsenal
Jamie Vardy goes close to putting Leicester 2-1 in frontYaya SanogoARSENAL imeendelea kugawa pointi bada ya kulazimishwa sare ya pili mfululizo katika Ligi Kuu ya Engaland dhidi ya timu ya Leicester City uwanja wa ugenini.
Vijana wa Arsene Wenger walilazimisha sare ya 2-2 na Everton kabla ya leo kupata sare ya 1-1 kwa Leicester City waliotanguliwa kufungwa bao katika dakika ya 20.
Bao hilo liliwekwa kimiani na Alexis Sanchez kabla ya Leonardo Ulloa kulirejesha dakika mbili baadaye.
Kwa matokeo hayo Arsenal wameongeza kibindoni pointi moja na kufanya wafikishe tano baada ya mechi tatu na itarejea nyumbani kuisubiri mabingwa watetezi Manchester city katika mechi ya ligi hiyo wiki mbili zijazo yaani Septemba 13.
Bao la Sanchez ni la pili katika mashindano baada ya katikati ya wiki kufunga bao pekee lililoivusha Arsenal hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Falcao akana taarifa za kuitamani Real Madrid

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/002/646/272/hi-res-174611730-radamel-falcao-of-monaco-looks-on-during-the-the-pre_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75MSHAMBULIAJI Ramadel Falcao amekanusha taarifa kwamba anaitamani Real Madrid na kudai taarifa iliyoandikwa kwenye akaunti ya Twitter haikuandikwa na yeye ndiyo maana ilikuwa hewani kabla ya kufutwa.
Mchezaji huyo toka Colombia anayeichezea Monaco amesema bado yupo Monaco na hajui chochote kuhusu kutaka kujiunga Real Madrid.
Awali mitandao mbalimbali vilidokeza kiu ya Falcao kutaka kwenda Bernabeu Santiago na kuiacha kwenye mataa Manchester City iliyokuwa ikitajwa kumnyemelea.
Done deal? Colombian international tweeted about his move to the Bernabeu before the message was deleted

Yanga wamrejesha Bin Kleb, Mayay Jangwani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEigmMCsDvsvatO7Ks4FTRpYb65iIPD0Xa862O2e8CK7v0EhDcHssDgIXyv_bJwPuDmW59cl7Zc-Nh5AD4uAMSCAvfWlJKxXtEXn9UELzVdH7lBM-WosGhcclfjP5-3dbz961KZuVxvLyn8/s1600/MAYAI+NA+MOSHA.jpg
Mayay
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgA5YySWRcd9L8IvN54wEhFTqZ-Q07h1s-mM2-pigTTJdzAF3bAu_Zf0UTublQc5qMflINX5-w3hdCTK0dKYtUDTLYbf9PsyRB8Ft_Z2Ity3wXAqyYXfsTiJVPtVvc2Az0TPm-D4GQdEPw/s1600/kleb.jpg
Bin Kleb (kushoto)
KLABU ya Yanga imeendelea kutangaza kamati zake ambapo safari hii katika uundwaji wa kamati hizo imewarejesha kundini Abdallah Bin Kleb na Ally Mayay.
Ebu zisome mwenyewe hapo chini;
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WAJUMBE Wenza wa Kamati ya Utendaji ya YANGA (Maendeleo ya Michezo), Ndugu Seif Ahmed na Engineer Isaac Chanji, wanapenda kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wanaYANGA, wameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji ya YANGA zifuatazo:

   1) KAMATI YA UFUNDI Wajumbe:
 1)  Duduma, Nassoro
 2)  Lamlembe, Roger
 3)  Malulu, Pascal
 4)  Msolla, Peter
 5)  Zangira, Steve

2) KAMATI YA SOKA YA VIJANA NA WANAWAKE Wajumbe:
1) Katwila, Shaban
2) Kabisa, Jessica (Advocate)
3) Mazwile, Isack  
4) Mwita, George
5) Tembele, Ally Mayay
3) KAMATI YA MASHINDANO   
Wajumbe:  
1)  Cheyo, Magembe      
2)  Didi, Ibrahim                  
3)  Hussein, Ndama Risasi      
4)  Katabalo, Moses             
5)  Katunzi, Mudhamiri        
6)  Kihanga, Pascal   
7)  Kingo, Ray Shauri
8)  Kleb, Abdallah Bin
9)  Luhago, David  
10) Lukumay, Samwel  
11) Macha, Innocent   
12) Maige, Jackson   
13) Mahende, Mugaya   
14) Makay, Sule       
15) Malebo, Michael    
16) Malume, Paul   
17) Matata   
18) Mbise, Anandumi Timothy   
19) Mlangwa, David   
20)  Mogha, John  
21) Mutaboyerwa, Joseph John
22) Ntimizi, Said  
23) Nyambaya, Lameck
24) Nyika, Hussein  
25) Nyumbamkaly,
26) Ramadhan, Fulgence 
27) Rashid, Ahmed    
28) Suleman, Majid    
29) Tenga, Frank    
30) Tindwa, Beda  
31) Zakaria, Dr.    
   
Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamati za YANGA zilizotajwa hapo juu.
Ndugu Seif Ahmed na Engineer Isaac Chanji Wajumbe Wenza wa Kamati ya Utendaji ya YANGA (Maendelo ya Michezo) watakuwa Wenyekiti Wenza wa Kamati zilizotajwa hapo juu.
Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze ketenda kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA.
(YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO)
 (BENO NJOVU)  
KATIBU MKUU WA YANGA

Balotelli aiongoza Liverpool kuisambaratisha Spurs kwao, Villa yaua



Liverpool beat Tottenham
Nahodha Steven Gerrard akifunga bao la pili la Liverpool kwa mkwaju wa penati
Gabby Agbonlahor
Mshambuliaji wa Aston Villa akishangilia bao la kwanza jioni hii
MSHAMBULIAJI mtukutu kutoka Italia, Mario Balotelli ameanza na mguu mzuri katika klabu ya Liverpool baada ya kuiongoza kupata ushindi mnono ugenini jioni hii dhidi ya Tottenham.
Liverpool ilitoka kuangushiwa kisago na mabingwa watetezi waliishindili Spur kwa mabao 3-0 na kutibua rekodi ya wenyeji kushinda mfululizo katika Ligi Kuu ya England.
Mabao ya Raheem Sterling katika dakika ya nane akimalizia kazi ya Hernandez na mengine ya kipindi cha pili toka kwa Nahodha Steven Gerrard dakika ya 49 na Alberto Moreno la dakika ya 60 yaliwapa ahueni vijogoo wa Anfield kw kuvuna pointi tatu muhimu.
Mara baada ya kuhakikisha mabao matatu yametinga katika nyavu za wenyeji, kocha Branden Rodgers alimpumzisha Balotelli kuonyesha kuridhika na kazi aliyofanya uwanjani akishirikiana na wenzake.
Katika mechi nyingine Aston Villa ikiwa nyumbani iliisasambua Hull City kwa mabao 2-1 na kuvuna pointi tatu na kuipeleka hadi katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 7 ikiporomosha Spurs iliyopigwa na Liverpool zenye pointi sita kila mmoja.
Punde timu iliyorejea ligi kuu, Leicester City itaikaribisha Wapiga Mitutu wa London, Arsenal katika mechi ya mwisho kwa siku ya leo.

Jaydee afunguka tuhuma za kutoka dogodogo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgL_DpQDx_nAdT5tOkF7w7CRqf4ZEqOhdfaungIvQQOm2-kejqZl4c_br2e4pdFO3ujVgpDsYRF7zWn42K6xuC1tnZKuhadKif6fA33VmJ0W9jQZcd_ctk8bqBGb8J9xnF3QbvS1mtdQGo_/s400/DSC05503.JPGNYOTA wa muziki na mmoja wa wasanii wenye mafanikio makubwa nchini lakini asiye na makeke, Judith Wambura Mbibo 'Lady Jaydee' a.k.a Anaconda ameamua kujibu habari iliyoandikwa katika gazeti moja la udaku kuhusu kuwa na uhusiano na aliyewahi kuwa mtuma salamu maarufu kwenye redio, Meddy Ahmed aka ‘Mtoto wa Vitoto’.
Kwenye habari hiyo, gazeti hilo linalotoka mara mbili kwa wiki lilidai kuwa Jaydee ambaye anadaiwa kuachana na mume wake Gadner G Habash ameonekana mara kadhaa na Mtoto wa Vitoto na kwamba amewahi kuonekana akiwa na gari lake.
Kupitia Instagram, Jaydee ameandika:
"Kuna habari za kuniudhi Ila hii imenichekesha. Kwahiyo mtoto wa vitoto ndio bwana angu???? Basi sawa nashukuru naona mmenianzia tena sasa picha za February Na nilizi post mwenyewe humu insta leo ndio mmeziona? Ukweli mnaujua mmeamua tu kuzingua ,,, wangapi wameshapiga picha na hiyo Range? Duuuh! !!!!! Shkamoooni Moyo wangu chuma. Pigeni mawe mpk mchoke Kama ambavyo mmekuwa mkifanya miaka yote na bado nipo hapa hapa.

Huyu ndiye Shishiiii, Shilole achaaaa!



KWA jina maarufu kama Shilole a.k.a Shishhhii Baby....wazazi wake walimpa jina la Zuwena Mohammed hapa ni katika mtokolezeo wake kupitia mtandao wa Instagram ni Hatareeeeeeee







Hali ya Hewa yatahadharisha upepo mkali

Manchester Utd yakaribia kumnasa Blind

http://completesportsnigeria.com/wp-content/uploads/2014/07/Daley-Blind.jpg
Delay Blind
KLABU ya Manchester United imekubaliana na Ajax Amsterdam ya Uholanzi kutoa kitita cha pauni millioni 13.8 kumnunua mlinzi wa timu hiyo Daley Blind.
Blind ambaye ana umri wa miaka 24 alikuwa katika kikosi cha Kombe la dunia cha Uholanzi chini ya mkufunzi Louis Van Gaal na inaelezwa amesalia kidogo kutua mikononi mwa kocha huyo anayeinoa kwa sasa Mashetani Wekundu ambao bado 'hawajatulia' katika Ligi Kuu ya England.
Blind anaweza kucheza kama beki wa kushoto na pia beki ya kati na iwapo makubaliano hayo yatatiwa sahihi, huyo atakuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na klabu hiyo.
Manchester imeshatumia zaidi ya pauni millioni 130 katika msimu huu pamoja na kuvunja rekodi ya England kwa kusajili Angel Di Maria kwa kitita cha pauni 59.7 kutoa Real Madrid, pia  memnunua beki wa kushoto Luke Shaw, Marco Rojo na kiungo matata Ander Herrera.

Hashim Lundenga, Mudhihir waula YANGA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj4yNL9q6uZ3_Y7ChyphenhyphenVWuLmfwNb_d9RBKB_R_ZJnFvooPtDi93j6iUaRjWGU2KbL1T0QHStuRuv55PC-NQS7W9GWal5a-IpWotn8XCCqvjGpiP-fpjxlwrdvp_ecOr902eAsio1uJr8hTc/s400/7.JPG
Hashim Lundenga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiUIOuKG1gEFHQ75A4FWOuoi7qU0z6y2quohlAWohSDzFhA8e-ufICebVNT3caSrlB2lYCCcrBM8VwFlCtgfA4IVuX0p0X07lmMtZRw2vAJpi6Enbb9ds0M-OgEGGwnI-WnclsNl_p27LM/s1600/9.jpg
Mudhihir M Mudhihir (kulia)
KLABU ya Yanga imetanga majina ya Kamati zake mbalimbali ambapo Mratibu wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga na Mbunge wa zamani wa Mchinga na mmiliki wa bendi ya Mchinga Sound, Mudhihir M Mudhihir ni baadji ya waliokula 'shavu' Jangwani.
Soma mwenyewe majina ya wanachama waliotangazwa na uongozi wa wababe hao wa soka nchini;
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA –(Utawala Bora) anapenda kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wana YANGA,ameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji wa YANGA zifuatazo:

1) KAMATI YA MAADILI
Wajumbe:
 
1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate)
2) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate) 
3) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate)
4) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate)
5) Tenga, Cathbert (Advocate)
 
2) KAMATI YA NIDHAMU
Wajumbe:
 
1) Karua, Tedy 
2) Lamlembe, Roger
3) Kihanga, Pascal 
4) Mahenge, Burton Yesaya
5) Mudhihir, Mudhihir (Advocate)

3) KAMATI YA SHERIA NA KATIBA 
Wajumbe:
 
1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate)
2) Gikas, Farija (Advocate)
3) Kabisa, Jessica (Advocate)
4) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate) 
5) Kambamwene, January (Advocate)
6) Lupogo, Herman (Advocate)
7) Madibi, Richard (Advocate)
8) Mahenge, Burton Yesaya
9) Mgongolwa, Alex (Advocate)
10) Mkucha, Elisha (Advocate)
11) Mudhihir, Mudhihir (Advocate)
12) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate)
13) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate)
14) Tenga, Cathbert (Advocate)
15) Tenga, Ringo Dr. (Advocate)
16) Vedasto, Audax (Advocate

4) KAMATI YA UCHAGUZI
Wajumbe:
 
 1)  Kajole, Mustafa
 2)  Lundenga, Hashim Ibrahim
 3)  Makele, Bakili
 4)  Mlelwa, Daniel 
  5) Ngongolwa, Alex (Advocate)

Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamati za YANGA zilizotajwa hapo juu.

Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA – (Utawala Bora) atakuwa Mwenyekiti wa Kamati zilizotajwa hapo juu.

Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze kutenda kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA.

(YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO)

(BENO NJOVU)
KATIBU MKUU WA YANGA

Falcao aitosa Man City kumfuata Ronaldo Madrid

https://pbs.twimg.com/profile_images/3079281026/5ddb6ef52b6aa1e61e9196fac65bf9a0.jpeg 
NDOTO za klabu ya Manchester City kumnasa nyota wa Colombia anayeichezea Monaco, Ramadel Falcao zinaendelea kuyeyuka baada ya kuwepo taarifa mshambuliaji huyo anajiandaa kutua Real Madrid.
Mshambuliaji huyo ameeleza nia yake ya kutataka kutua Madrid kuungana na akina Ronaldo na James Rodriguez
Falcao aliweka taarifa yake kwamba ndoto yake ya kwenda Madrid itakamilika.
Alieleza hilo kupitia mtandao wa jamii wa Instagram. Lakini baada ya muda mchache akaitoa post hiyo.
Hali ambayo imeonyesha uhamisho wake unaendelea kushughulikiwa.
Man City ilikuwa inapambana kumpata Falcao ambaye anaendelea kuichezea AS Monaco ya Ufaransa.
Mchezaji huyo jana alikuwa jukwaani wakati 'chama' lake kiliambulia sare ya 1-1 dhidi ya Lille katika Ligue1.

Ronaldo amtabiria makubwa Di Maria

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Cristiano+Ronaldo+Angel+Di+Maria+Real+Madrid+OQaX2hmg7S7l.jpgMSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo, amemtabiria mafanikio mchezaji mwenzake wa zamani Angel Di Maria katika klabu yake mpya ya Manchester United. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina jana alianza makeke yake akiwa na kikosi chake kipya ambacho hata hivyo kilishindwa kufurukuta ugenini baada ya kulazimishwa suluhu na timu iliyopanda daraja Burnley.
Usajili wa nyota huyo umevunja rekodi nchini Uingereza na ilikuja baada ya kushindwa kupata nafasi katika kikosi cha Carlo Ancelotti huku akipewa jezi namba saba ambayo imewahi kutimiwa na Ronaldo wakati akiwa United. 
Ronaldo ambaye alicheza misimu sita na United, anaamini kuwa uhamisho huo ndio Di Maria aliokuwa akihitaji na ana uhakika nyota huyo anaweza kuisaidia timu hiyo kubadili mwelekeo baada ya kuanza vibaya msimu mpya wa Ligi Kuu. 
Akihojiwa Ronaldo ambaye jana ametunukiwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka barani Ulaya katika sherehe zilizofanyika jijini Monaco, amesema Di Maria kwenda United ni jambo ambalo litamsaidia kwani anaamini amekwenda katika moja ya klabu bora duniani hivyo anamtakia mafanikio akiwa huko. 
Ronaldo aliendelea kudai kuwa amezungumza naye na kumwambia kuwa jezi namba aliyopewa ina majukumu makubwa lakini anadhani ataitendea haki jezi hiyo kwani ni mchezaji mahiri.

HUYU NDIYE MSHINDI WA TMT 2014


MSHIRIKI kutoka Mtwara, Mwanaafa Mwinzago ameibuka kidedea katika Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.
Katika shindano hilo ambalo washiriki 10 walikuwa wakizitolea macho Shilingi milioni 50, Mwanaafa aliweza kuzoa kura nyingi zaidi na hivyo kujiwekea kibindoni mamilioni hayo na kuwatimulia vumbi washiriki wengine.
Awali kabla ya kutangazwa mshindi, Mwenyekiti wa Kampuni ya Proin Promotions, Johnson Lukaza alitoa ahadi kwamba kampuni hiyo itajitolea kumsomesha mtoto Mwanaafa ili aweze kufanikiwa kufikia malengo yake.
Mwanaafa ndiye mshiriki mdogo kuliko wote katika shindano hilo lililoandaliwa na Proin Promotions ambapo miongoni mwa majaji watatu, wawili walikuwa waigizaji maarufu nchini, Single Mtambalike ‘Ritchie Rich’ na Yvonne Cherie ‘Monalisa’. Jaji Mkuu alikuwa Roy Sarungi.
Mara baada ya kutangazwa mshindi, Mwanaafa aliangua kilio cha furaha kuonesha kutoamini kwamba amefanikiwa kunyakua mamilioni hayo huku akihaha huku na kule kumtafuta mama yake jukwaani.
Hata baada ya kuitwa na kukabidhiwa hundi ya Shilingi milioni 50 na Mwenyekiti wa Proin Promotions, Mwanaafa aliendelea kububujikwa machozi ya furaha kuonesha kabisa kutoamini kinachotokea usiku huo.

Spurs, Liverpool ni vita tupu, Arsenal kujiuliza ugenini

http://screaming-eagles.com/wordpress/wp-content/uploads/2013/12/Tottenham-vs-Liverpool.jpghttp://337sports.net/wp-content/uploads/2014/08/Leicester-City-vs-Arsenal.jpg
WAKATI jinamizi baya likiendelea kuiandama Machester United baada ya kulazimishwa suluhu na timu iliyopanda daraja Burnley, huku majirani zao Machester City wakibamizwa nyumbani na Stoke City, leo ni zamu za Tottenham Hotspur na Liverpool kuonyeshana kazi katika Ligi Kuu ya England.
Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu itapigwa kwenye uwanja wa White Hart Lane, London ya Kaskazini Spurs ikitaka kuendeleza maajabu yake ya kupata ushindi mfululizo katika ligi pia wakitaka kurejea kileleni baada ya kuenguliwa na Chelsea iliyoifumua Everton ikiwa uwanja wa ugenini mabao 6-3.
Mbali na mechi hiyo leo pia katika ligi hiyo kutakuwa na mechi nyingine mbili Arsenal ikiwa ugenini itavaana na Leicester City na Aston Villa kuikaribisha Hull City.
Liverpool ambayo ilimnyakua mshambuliaji mpya toka AC MIlan, Mario Balotelli imetamba kuwa itaanza kumtumia mchezaji huyo katika mechi hiyo, ikiamini atashirikiana na wenzake kurejesha heshima baada ya wiki iliyoipita kufumuliwa mabao 3-1 na mabingwa watetezi Manchester City.
Vijana hao wa Branden Rodgers wanahitaji ushindi katika mechi hiyo ya ugenini ili kuwatuliza mashabiki wao ambao wanaamini pengo la Luis Suarez aliyewapa raha msimu uliopita bado halijapata wa kuliziba labda baada ya ujio wa 'mtukutu' Mario Balotelli aliyerejea katika ligi ya England baada ya miezi kadhaa.
Mbali na mashabiki wa kandanda kuwa na hamu ya kutaka kuona Supr Mario atafanya kitu gani leo mbele ya Spurs inayotambia nyota kadhaa akiwamo Emmanuel Adebayor na ambayo haijaruhusu wavu wake kuguswa tangu ligi hiyo ilipoanza Agosti 16.
Katika pambano la Arsenal iliyoanza kwa ushindi kabla ya kuponea chupuchupu kipigo toka kwa Everton wiki ijayo itakuwa na hamu ya ushindi ili kuendeleza furaha yao ya kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa msimu wa 17 mfululizo baada ya kuilaza Besiktas ya Uturuki katikati ya wiki.
Baoa la nyota wake mpya kutoka Chile, Alexis Sanchez lilitosha kumtuliza Arsene WEnger ambaye amekuwa akimkingia kifua mashambuliaji huyo baada ya kuanza ligi bila kuonyesha vitu vyake vilivyomfanya Arsenal wamsajili baada ya Kombe la Dunia la nchini Brazili akitokea Barcelona.
Je, ni Spurs itakayoendeleza wimbi la ushindi au LIverpool itakayofufukia mikononi mwa Super Mario au ni Arsenal kupata ushindi ugenini leo? Tusubiri!

INATISHA! VIKONGE 38 WAUWAWA SHINYANGA

Jumla ya vikongwe 38 wameuawa  mkoani Shinyanga katika matukio tofauti, yakiwamo ya kuhusishwa na uchawi na ushirikina na wengine kudaiwa kutowapa urithi watoto wao matokeo yake watoto kuua wazee wao
Akizungumza na waandishi wa habari juzi kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga SACP Justus Kamugisha,alisema vikongwe wamekuwa wakiuawa, bila ya kuwa na hatia kutokana na kuhisiwa kuwa ni wachawi.
Alisema mbali na imani za kishirikina vikongwe wengine wamekuwa wakiuawa kikatili wakidaiwa kung’ang’ania mali na kutowagawia watoto wao hivyo watoto hao kuamua kutekeleza mauaji hayo.
Kamugisha alifafanua katika kipindi cha mwezi Januari hadi Desemba mwaka jana (2013), jumla ya vikongwe 27 wameuawa yaani katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga vijijini vikongwe 11, Kahama 9 na   Kishapu 7.
Aliongeza kuwa katika kipindi cha mwezi Januari hadi Julai mwaka huu (2014),vikongwe 11 wameuawa,ikiwa katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga vijijini vikongwe 6,  Kahama 4, Kishapu mmoja.
“Jumla kuu ya vikongwe waliouawa katika kipindi cha mwaka jana hadi Julai  mwaka huu wa 2014,ni 38”,alisema kamanda Kamugisha
Kufuatia mauaji hayo kamanda Kamugisha aliwataka wakazi wa mkoa wa Shinyanga kuacha kuendekeza imani za kishirikina,ambazo zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa mauaji hayo ya vikongwe, huku akiwataka vijana kushighulisha ili kujipatia kipato na kuacha dhana tegemezi ya mirathi.
Kamugisha alisema katika msimu wa mwaka huu wa mwaka 2014/2015, atahakikisha anakomesha uhalifu mkoani Shinyanga, pamoja na kutokomeza mauaji hayo ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). 
Aidha aliwataka wananchi likiwamo na jeshi la jadi sungu sungu kushirikiana kwa pamoja na  kuhakikisha, wanawakamata wahalifu, ili kuwafikisha katika vyombo vya dola, na kuchukuliwa hatua kali za kisheria ili liwefundisho kwa watu wengine.
Aliongeza kuwa hivi sasa anatarajia kusambaza polisi kata, kwa kila kata kwani baadhi ya kata hazina polisi hao, hali ambayo itasaidia kushirikiana kwa ukaribu na wananchi katika kuhakikisha anawatia nguvuni waharifu.

Simba yairarua KMKM x5 Zenji

Tambwe akishangilia moja ya mabao yake na Ramadhani Singano 'Messi'
KLABU ya soka ya Simba imeirarua bila huruma mabingwa wa Zanzibar, KMKM kwa kuicharaza mabao 5-0 katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyochezwa usiku wa kuamkia leo visiwani humo.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Amaan,  ilishuhudia vijana wa kocha Ally Bushiri ‘Bush’ ambayo katikati ya wiki walichezea kichapo cha mabao 2-0 toka kwa Yanga ikienda mapumziko ikiwa tayari imeshashindiliwa mabao 4-0.
Simba ilipata mabao yake kupitia kwa  Amisi Tambwe aliyefuinga mawili,, Amri Kiemba, Shaaban Kisiga ‘Marlone’ na Elias Maguli.
Kiemba alianza kuifungia Simba bao dakika ya tatu ya mchezo baada ya kumalizia pasi murua ya Pierre Kwizera kabla ya Tambwe kufunga la pili dakika ya 14 na kuongeza jingine dakika  23 kabla ya Kisiga kufunga la nne dakika ya 37 na katika kipindi cha pili Maguli kuhitimisha karamu hiyo ya magoli.

Friday, August 29, 2014

Samuel Eto'oo afunguka 'Sina bifu na Mourinho'

MSHAMBULIAJI mpya wa Evetrion, Samuel Eto'o ametupilia mbali madai kuwa ana bifu na Jose Mourinho wakati timu yake ikijiandaa kuivaa Chelsea katika mechi ya Ligi Kuu tya England kesho Jumamosi.
Eto’o, Mchezaji wa Kimataifa wa Cameroon, na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho walikuwa pamoja huko Inter Milan na kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI pamoja na akaja England Mwaka mmoja uliopita kuungana na Mourinho huko Chelsea.
Lakini uhusiano wa Eto’o na Mourinho ulipata msukosuko pale Mreno huyo aliponaswa kwenye Kamera bila kujijua akidhihaki Umri wa Eto’o na kudai ni Mzee kupita Miaka inayodaiwa anayo.
Mara baada ya tukio hilo Eto’o, mwenye Miaka 33, alifunga Bao akiichezea Chelsea na kwenda kushangilia mithili ya Mzee akishika Kibendera cha Kona kama Mkongojo huku akijishika Kiuno ili kumdhihaki Mourinho.
Akiongea na Wanahabari mara tu baada ya kutambulishwa kama Mchezaji mpya, Eto’o alipuuza madai hayo ya kuwa na bifu na Mourinho na badala yake kusema anamshukuru Mourinho kwa kumleta Ligi Kuu England.

Nae Meneja wa Everton Roberto Martinez amedokeza kuwa huenda Mkongwe huyo wa Cameroon akaivaa Chelsea Jumamosi wakati watakapopambana Goodison Park katika Mechi ya Ligi Kuu England.

Mashali kumvaa Mkenya Novemba 4

 Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam. Wanaoshudia kushoto ni Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ustaadh' na promota wa mpambano huo Khamis Ally.
 Rais wa TPBO Yassin Abdallah akirekebisha mkataba wa bondia Thomas Mashali katikati atakayepambana na mkenya Henry Wandera Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam kulia ni  promota wa mpambano huo Khamis Ally 
Bondia Thomas Mashali katikati akiwe Dole Gumba katika mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4.
****
BONDIA Thomas Mashali 'Simba Asiyefugika' anatarajia kupanda tena ulingoni Novemba 4 kumvaa Mkenya Henry Wandera katika pambano litakalofanyika katika ukumbi wa New Madiba zamani Korini.
Mashali anapigana akiwa na historia ya kupoteza mpambano wake wa mwisho zaidi ya bondia Mada Maugo ambapo walicheza katika uwanja wa taifa na kupoteza kwa pointi mpambano huo.
Akizungumzia mpambano huo Mashali amesema hatokubali kupoteza tena mchezo huo ukizingatia anachezea nyumbani mahali alipozaliwa na ndipo alipoanzia ngumi maeneo ya Tandale.
"Sintokubali niaibike mbele ya ndugu zangu hivyo nawaambia wapenzi waje kwa wingi kuangalia Mashali anavyofanya kazi yake ya mchezo wa masumbwi.
Naye promota wa mpambano huo Khamis Ally amewahakikishia kuwa sehemu ya kuegeshea magari ni kubwa na ulinzi ni wa kutosha kifupi katika ulinzi tumejipanga vizuri pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine mazuri ya utangulizi ambapo mabondia wengi wamejitokeza kucheza siku hiyo.
Siku hiyo pia kutakuwa na uuzwaji wa DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.
Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Pacquaio, Floyd Maywether, Amir Khan, Muhammed Ali, Mike 'Iron' Tyson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani.
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi.

Kikwazo cha Tanzania kuandaa AFCON 2017 HIKI HAPA!

http://bigeye.ug/wp-content/uploads/2014/08/afcon-trophy.pngSHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeliandikia Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kutaka kipengele cha kutaka kwanza nchi iandae Fainali za Afrika kwa Vijana ndiyo iwe na sifa ya kuandaa Fainali za Afrika (AFCON) kiondolewe.
TFF ilishapeleka barua CAF kutaka kipengele hicho kiondolewe, na kutaka kijadiliwe katika Congress (Mkutano Mkuu) ijayo ya CAF.
Tanzania imeshaiandikia CAF barua kuomba uenyeji wa Fainali za AFCON za 2017 baada ya Libya iliyokuwa imepewe uenyeji huo kujitoa. Uamuzi wa Tanzania kuomba kuandaa fainali hizo ulifanywa na Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24 mwaka huu.

Malinzi kuzuru Kanda ya Kaskazini, mechi za Electronic kupigwa TA, BK

http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2013/10/Jamal-Malinzi.jpgTIMU za Mgambo Shooting na African Sports za Tanga zitapambana Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) katika mechi ya majaribio ya matumizi ya tiketi za elektroniki itakayochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kwa kiingilio cha sh. 1,000 tu.
Mechi nyingine ya tiketi za elektroniki siku hiyo itachezwa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kwa kuzikutanisha timu za Kagera Sugar na Geita Gold SC ya mkoani Geita. Geita Gold iko Daraja la Kwanza.
Kabla ya mechi hizo, Ijumaa (Agosti 29 mwaka huu) saa 3 asubuhi kwenye viwanja hivyo kutakuwa na mafunzo ya matumizi ya tiketi za elektroniki pamoja na jinsi mfumo huo unavyofanya kazi.
Washiriki wa mafunzo hayo ni wasimamizi wa vituo vya Tanga na Bukoba, viongozi wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Kagera (KRFA) na Tanga (TRFA), makatibu na maofisa habari wa klabu za Kagera Sugar, Mgambo Shooting, African Sports na Geita Gold, mameneja wa viwanja vya Kaitaba na Mkwakwani na wasaidizi wao, maofisa usalama wa TRFA na KRFA, wachanaji tiketi, wasimamizi wa milangoni, wasaidizi (stewards) na waandishi wa habari.
Wakati huo huo Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atatembelea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
Katika ziara hiyo atakutana na viongozi na kuangalia hali hali ya mpira wa miguu katika mikoa hiyo na mahitaji yake. Pia atazungumzia maono (vision) ya TFF katika mpira wa miguu.
Rais Malinzi atawasili mkoani Manyara, Agosti 29 mwaka huu, na ataanza ziara rasmi katika mkoa huo Agosti 30 mwaka huu. Agosti 31 mwaka huu atakuwa Arusha, na kumalizia Septemba 1 mkoani Kilimanjaro.
Katika ziara hiyo, Rais Malinzi atafuatana na Mkurugenzi Msaidizi (Wanachama) wa TFF, Eliud Mvella. Pia Septemba 8 mwaka huu, Rais Malinzi ataanza ziara ya mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe.

Kenya, Rwanda, Uganda kuandaa pamoja Afcon 2017?

http://www.thepeople.co.ke/wp-content/uploads/2014/04/Screen-Shot-2014-04-12-at-8.13.22-AM.png
Sam Nyamweya
NAIROBI, Kenya
KENYA, Rwanda na Uganda zinajadili uwezekano kupeleka maombi Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kuandaa kwa pamoja fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka nchini Kenya (FKF), Sam Nyamweya Jumatano alithibitisha kuwa mipango iliyopo ni kwa nchi tatu kuungana kuomba kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ya Afrika ili kupunguza gharama.
 "Ni mwenye furaha kwamba Uganda na Rwanda wamepokea kwa mikono miwili wazo la FKF la kuungana kuomba uenyeji wa Mataifa ya Afrika 2017 ambayo ipo wazi kutokana na Libya kujitoa kuwa mwenyeji," alisema Nyamweya.
Libya haitakuwa mwenyeji wa Afcon 2017 kutokana na mapigano ya kisiasa nchini humo ambayo yamesababisha kuchelewa kwa mipango ya ujenzi wa viwanja vitakavyotosha timu 16 zinazoshiriki michuano hiyo.
Nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika ilipanga kujenga viwanja 11 kwa gharama ya Dola za Kimarekani 314 ikiwa ni pamoja na unaochukua watazamaji 60,000 eneo la kambi ya jeshi jijini Tripoli.
CAF imekaribisha maombi kwa nchi zinazohitaji kuandaa michuano hiyo, na milango ipo wazi hadi Septemba 30. Uamuzi wa nchi itakayopewa nafasi hiyo ya Libya utatolewa mwakani.

Waamuzi, makamisaa kutahiniwa Sept 5

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGe9znsbu8-SC-K7pcwh_X4R1keXlQEZ6eKkKsYFEcEiMd59lZ-pvZBtMypkT-3vsbM6KKk8-HTX-AtQvj4Qa97tZCeIIr-3noVEg8sxx5YnUqt3q9IZm6Ar3VB-IJWfyVSQQ5vhOcAT9D/s1600/DSC_8192.JPG
Waamuzi wanatakiwa kuwa fiti kama hivi wawapo uwanjani
MTIHANI wa utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wanaotaka kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu utafanyika katika vituo viwili kuanzia Septemba 5-6 mwaka huu.
Waamuzi watakaoshiriki mtihani huo ni wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na wale wa class one. Pia kutakuwa na semina wa makamishna wanaotaka kusimamia mechi za VPL na FDL ambayo itafanyika Septemba 7 mwaka huu.
Vituo vya mtihani huo ni Dar es Salaam na Shinyanga. Kituo cha Dar es Salaam ni kwa waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.
Kituo cha Shinyanga ni kwa waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Arusha, Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Rukwa, Shinyanga, Simiyu, Singida na Tabora.
Waamuzi wote ambao wamechezesha VPL na FDL msimu wa 2013/2014 na kupata matatizo au kuondolewa kwenye ligi hawahusiki na mtihani huo.
Washiriki wanatakiwa kufika kituoni siku moja kabla.Wasimamizi ni Charles Ndagala, Israel Mujuni, Issarow Chacha, Joan Minja, Pascal Chiganga, Riziki Majala, Said Nassoro, Salum Chama, Soud Abdi, Victor Mwandike na Zahara Mohamed.

KOZI YA UKUFUNZI WA UTAWALA YA FIFA KUFANYIKA DESEMBA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-2-gEQjN-kUTDr5XYxr2xEbeHBZeqpiBVaxDBdXtEHTCTfXJMtFnrt4_lV5Gtu_cfAfZtDPsXoHZdVtbLhyphenhyphenBQsa9f8OgTtpmurttsK_XY2cD3KZVsKqVdjpzI97j-jLPVmU6Qy3ft4BE/s1600/mwesigwa.JPG
Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa aliyesimama
SHIRIKISHO la Soka Tanzania,TFF kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wameandaa kozi ya ukufunzi wa utawala itakayofanyika Desemba mwaka huu.
Kozi hiyo itakayoendeshwa na wakufunzi kutoka FIFA itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 1 hadi 5 mwaka huu, ambapo sifa ya chini ya elimu kwa wanaotaka kushiriki ni kidato cha nne.
Kwa wanaotaka kushiriki kozi hiyo wanatakiwa kutuma maombi yao kwa Katibu Mkuu wa TFF. 
Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 5 mwaka huu ambapo wanatakiwa pia kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya kitaaluma.

Wenger akiri Giroud kuwa nje, akiwakana Falcao, Song Emirates

http://static.goal.com/310700/310713_heroa.jpg
Arsene Wenger
http://www.footmercato.net/images/a/falcao-cible-potentielle-des-gunners_101362.jpg
Falcao
http://www.standard.co.uk/incoming/article8026635.ece/alternates/w620/alex-song.jpg
Alex Song
MENEJA wa Arsenal , Arsene Wenger amethibitisha kuwa Olivier Giroud anatarajiwa kuwa nje ya uwanja hadi angalau Desemba kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu lakini akasisitiza kuwa hana mpango wa kusaka mshambuliaji mwingine yeyeote akiwakana Radamel Falcao, Alex Song na Danny Welbeck.
Giroud (27), ambaye alikuwa mfungaji bora wa Arsenal msimu uliopita akitupia mabao 22 katika michuano yote, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa kufikia miezi minne kufuatia kufanyiwa upasuaji wa 'enka' aliyoumia katika mechi ya Jumamosi iliyomalizika kwa sare ya 2-2 ugenini dhidi ya Everton katika Ligi Kuu ya England.
Alipoulizwa kuhusu Falcao, Wenger alisema nyota huyo wa Napoli hayumo katika mipaka ya bei anayoweza kutoa na akabainisha kwamba pia hamhitaji Welbeck. Kuhusu uwezekano wa kumsajili Song, Mfaransa huyo alisema: "Alex Song hatarejea hapa."
Kocha huyo akasema kuhusu nyota wa Chile, aliyefunga goli la ushindi katika mechi ya "kapu" ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Besiktas: "(Alexis anaweza kucheza kama mshambuliaji wa kati) kwa miezi mitatu ama minne? Anaweza kucheza pale maisha yake yote.
"Nilimnunua acheze kama mshambuliaji wa kati, siyo kwenye wingi. Naamini huwezi kununua kila pale mchezaji anapoumia. Kama umepata majeruhi Septemba mosi bado utatakiwa kuishi nalo.
"Nilimnunua Sanchez awe mshambuliaji, Walcott anaweza kuwa mshambuliaji mzuri, (Lukas) Podolski anaweza kucheza pale, (Yaya) Sanogo ni mshambuliaji mzuri sana, (Joel) Campbell ukimuuliza yeye ni nani, atasema ni mshambuliaji. Wote ni wachezaji wa ubora wa juu.
"Kupata wachezaji bora zaidi ya tulionao itakuwa ngumu sana."

BRAD PITT NA ANGELINA JOLIE WAOANA!


Jolie na Pit walichumbiana mwaka 2012
NYOTA wa filamu duniani, Brad Pitt na Angelina Jolie ambao wameishi kwa muda mrefu kama mke na mume, wamefunga ndoa rasmi.
Pitt, mwenye umri wa miaka 50 na Jolie mwenye umri wa miaka 39, walifunga pingu za maisha nchini Ufaransa Jumamosi na kumaliza miaka mingi ya sintofahamu ikiwa watawahi kuoana.
Waigizaji hao inaarifiwa walioana katika sherehe iliyofanywa kimya kimya katika kanisa ndogo eneo la Chateau Miraval Ufaransa.
Sherehe hio ilifanyika kwa faragha na kuhudhuriwa tu na familia za wawili hao pamoja na marafiki zao.
Watoto wao pia walihusishwa katika sherehe hiyo.
Jolie aliambatana na wanawe wakubwa wa kiume, Maddox na Pax, wenye umri wa miaka 13 na 10 mtawalia.
Watoto wao wa kike Zahara na Vivienne, wote waliwarushia mauwa wazazi wao walipokuwa wanatembea kuelekea kanisani. Inaarifiwa sherehe hiyo haikufuata dini yoyote.
Wacheza filamu hao walianza uhusiano wao wa kimapenzi mwaka 2005 walipoigiza katika filamu ya 'Mr and Mrs Smith'. Walichumbiana Aprili mwaka 2012.
Kabla ya ndoa yake kwa Jolie, Pit alikuwa amemuoa muigizaji, Jennifer Aniston, wakati Jolie alikuwa ameolewa na Jonny Lee Miller na Billy Bob Thornton. Ndoa yake kwa wawili hao ilivunjika
BIG

Thursday, August 28, 2014

Ronaldo ndiye Mchezaji Bora Barani Ulaya

http://www.free-top10.com/Data/Sites/1/Free/Free%20Video/Free-Video-Ronaldo-European-Football-Player-Of-The-Year.jpg 
http://www.sokkaa.com/wp-content/uploads/Neuer-Christiano-and-Robben.jpg
Waliokuwa kwenye Tatu Bora Ulaya
MSHAMBULIAJI nyota wa Ureno anayeichezea klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Ulaya.
Mkali huyo alipata tuzo hiyo baada ya kuwaangusha wachezaji wenzake wawili wanaoichezea Bayern Munich ya Ujerumani.
Ronaldo alitangazwa jioni hii kushinda tuzo hiyo mbele ya Arjen Robben na kipa Manuel Neuer wa Bayern Munich.

Haya ndiyo makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2014

MAKUNDI ya Ligi ya Mabingwa Ulaya yametangazwa jioni hii ambapo Mabingwa wa Engand, Manchester City wamejikuta wakiangukia kundi moja na Bayern Munich huku Liverpool ikiangukia kundi B lenye vigogo Real Madrid.
Kwa mara nyingine Arsenal wameangukia kundi gumu, safari hii wakiwa D lenye timu za Arsenal, 
Borussia Dortmund, 
Galatasaray na Anderlecht.
Chelsea wao wako kundi G lenye timu za 
Schalke, 
Sporting
 na Maribor.
Yacheki makundi yote hapo chini:
Kundi A


Atletico Madrid, Juventus,
 Olympiacos na 
Malmo
Kundi B
Real Madrid, 
Basle, 
Liverpool,
 Ludogorets
Kundi C
Benfica, 
Zenit St. Petersburg,
 Bayer Leverkusen na Monaco
Kundi D
Arsenal, 
Borussia Dortmund,
 Galatasaray na Anderlecht
Kundi E
Bayern Munich,
 Man City, 
CSKA Moscow na 
Roma
Kundi F
Barcelona, 
PSG, 
Ajax, 
Apoel Nicosia
Kundi G
Chelsea,
Schalke, 
Sporting
 na Maribor
Kundi H
FC Porto,
 Shakhtar Donetsk,
 Athletic Bilbao 
na BATE