STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 31, 2014

Balotelli aiongoza Liverpool kuisambaratisha Spurs kwao, Villa yaua



Liverpool beat Tottenham
Nahodha Steven Gerrard akifunga bao la pili la Liverpool kwa mkwaju wa penati
Gabby Agbonlahor
Mshambuliaji wa Aston Villa akishangilia bao la kwanza jioni hii
MSHAMBULIAJI mtukutu kutoka Italia, Mario Balotelli ameanza na mguu mzuri katika klabu ya Liverpool baada ya kuiongoza kupata ushindi mnono ugenini jioni hii dhidi ya Tottenham.
Liverpool ilitoka kuangushiwa kisago na mabingwa watetezi waliishindili Spur kwa mabao 3-0 na kutibua rekodi ya wenyeji kushinda mfululizo katika Ligi Kuu ya England.
Mabao ya Raheem Sterling katika dakika ya nane akimalizia kazi ya Hernandez na mengine ya kipindi cha pili toka kwa Nahodha Steven Gerrard dakika ya 49 na Alberto Moreno la dakika ya 60 yaliwapa ahueni vijogoo wa Anfield kw kuvuna pointi tatu muhimu.
Mara baada ya kuhakikisha mabao matatu yametinga katika nyavu za wenyeji, kocha Branden Rodgers alimpumzisha Balotelli kuonyesha kuridhika na kazi aliyofanya uwanjani akishirikiana na wenzake.
Katika mechi nyingine Aston Villa ikiwa nyumbani iliisasambua Hull City kwa mabao 2-1 na kuvuna pointi tatu na kuipeleka hadi katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 7 ikiporomosha Spurs iliyopigwa na Liverpool zenye pointi sita kila mmoja.
Punde timu iliyorejea ligi kuu, Leicester City itaikaribisha Wapiga Mitutu wa London, Arsenal katika mechi ya mwisho kwa siku ya leo.

No comments:

Post a Comment