STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 24, 2013

Serikali Kenya yatangaza maombolezo ya siku tatu idadi ya waliouwawa ni 72

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta

NAIROBI, Kenya
RAIS Uhuru Kenyata ametangaza siku tatu za maaombolezo kufuatia tukio la Ugaidi lililofanywa na wanamgambo wa Al Shabaab.
Jumla ya watu 72 wameuawa katika tukio hilo huku wanajeshi sita wa Kenya wakiwa wamepoteza maisha wakati walipokuwa wakijaribu kuokoa maisha ya watu anaoshikiliwa mateka na magaidi wa al Shabab katika jumba lenye maduka la Wastgate jijini Nairobi.

Askari wengine 8 wanaripotiwa kuwa mahututi baada ya kujeruhiwa katika mapambano hayo yanayoendelea hadi sasa.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) Jenerali Julius Karangi.

Duru za Kenya zinaripoti kuwa hadi sasa watu 72 wakiwemo raia sita wa nchi za nje wamethibitishwa kuwa wameuawa pamoja na magaidi kadhaa wamekamatwa na wanahojiwa vyombo vya ulinzi na usalama kuhusiana na tukio hilo katika jengo la maduka la Westgate nchini Kenya.

Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Amina Mohammed amesema kuwa Wamarekani wawili au watatu na Mwingereza mmoja wamehusika katika shambulizi lililofanywa na magaidi dhidi ya jumba la maduka la Westgate jijini Nairobi. 

Balozi Amina Mohammed amesema washambuliaji hao walikuwa wakishirikiana na wenzao katika maeneo mbalimbali ya dunia kwa ajili ya kuua watu mwishoni mwa wiki mjini Nairobi. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya amesisitiza kuwa shambulizi la sasa mjini Nairobi limefanyika kitaalamu.
Jengo la Maduka la Westgate
 Baadhi ya watu waliookolewa kutoka katika jengo la Westgate. 
Wanambambo wa Al Shabaab.

KWISHA KAZI! JESHI LAFANIKIWA KUWAFYEKA MAGAIDI, WAHANGA WALIOKUWA WAFIKIA 70



News just in indicates that the Westgate Mall siege is over after Kenya Defence Forces (KDF) took control of the building by killing all the terrorists and rescuing the remaining hostages.

Multiple sources said the Kenya Defence Forces are currently moving out of the building after mopping it out in the early hours of the day.

A total of six terrorists have been killed and the number is expected to rise as forensic experts search for more terrorists’ bodies, who were slaughtered after a 4-hour heavy gun battle on Tuesday morning.

The building is currently being secured by General Service Unit (GSU). A total of 70 people have died and hundreds injured following Saturday’s terror attack on the mall.

Police have asked Kenyans who had abandoned their vehicles at an adjacent mall that houses Nakumatt Ukay to go for them as security clears the building.

More updates to follow……..


The Kenyan DAILY POST

Khadija Mwanamboka, balozi wa Oxfam aja na mradi mpya wa Kilimo

 MBUNIFU WA MITINDO YA MAVAZI NA BALOZI WA OXFAM TANZANIA -KHADIJA MWANAMBOKA AMEZINDUA PROJECT-VVK-GROW CAMPAIGN PROJECT
 HII NI KAMPENI ILIYOBUNIWA NA KUENDESHWA NA BALOZI WA OXFAM KHADIJA MWANAMBOKA NA IKIWA NA LENGO LA KUAINISHA CHANGAMOTO ZA SOKO KWA WAKULIMA WA CHAKULA HASA WANAWAKE.KUANIKA DHULUMA WANAYOFANYIWA WAKULIMA WA CHAKULA WANAWAKE NA KUHAMASISHA WATUMIAJI WA BIDHAA ZA CHAKULA MIJINI.KUTAMBUA THAMANI YA CHAKULA NA KUWA SOKO LENYE TIJA KWA WAKULIMA WA CHAKULA HASA WANAWAKE
 KAMPENI HII INAHUSISHA WASICHANA"GROW GIRLS" AMBAO NI WANAMITINDO -MODELS WATAKUWA WANAPITA KWENYE MIKUSANYIKO MBALI MBALI, MAOFISINI NA KWENYE TAASISI MBALI MBALI KUHAMASISHA NA KUUZA BIDHAA ZA WAKULIMA WADOGO WANAWAKE.
MWEZI WA NNE MWAKA HUU OXFARM ILIMTAMBULISHA MABALOZI WAKE WAPYA WA KAMPENI YA GROW. MBALI NA KHADIJA MWANAMBOKA WENGINE NI DINA MARIOS, MASOUD KIPANYA, SHAMIM MWASHA, HALIMA MDEE (MB), SHYROSE BHANJI (MB) NA JACOB STEPHEN 'JB'.
AMBAPO KILA BALOZI ATAKUJA NA MRADI WAKE UNAOHUSISHA CHAKULA NA KILIMO NA KHADIJA MWANAMBOKA AKIJA NA MRADI HUO ALIOUTAMBULISHA.
DM

Baby Madaha awaangukia mashabiki wake

Baby Madaha
 STAA wa filamu na muziki wa kizazi kipya nchini, Baby Madaha, amewaomba mashabiki wake kumpa sapoti wakati akifanya kazi chini ya kampuni ya Candy n Candy ya Kenya.
Aidha wimbo mpya wa msanii huyo aliyoutoa chini ya kampuni hiyo alioingia nao mkataba wa miaka miwili wa 'Summer Holiday' umeanza kubamba katika vituo vya redio na runinga baada ya kuusambaza.
Mkali huyo aliyewahi kutamba na wimbo wake ulokuja kuzaa albamu yake ya kwanza ya 'Amore', alisema anaomba sapoti ya mashabiki ili aweze kusonga mbele katika mwanzo wa mafanikio yake katika anga la kimataifa sasa akifanya kazi Kenya na Bongo.

Haya ndiyo majina ya washukiwa wa tukio la Wastgate-Kenya

Jeshi Kenya lakaribia kumaliza kazi yaua magaidi 9

NAIROBI

JESHI la Kenya limedaiwa limedhibiti kwa asilimia kubwa jengo la Westgate, ikidaiwa wamewaua magaidi 9 na kuhisiwa gaidi mmoja au wawili tu ndiyo waliosalia kwenye jengo hilo na wakati wowote watashughulikiwa na kumaliza utekaji wa siku nne sasa.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa na AFP, inasema kazi kubwa ya kupambana na magaidi hao kutoka kikundi cha Al Shabaab cha Somalia, wamefanikiwa kulidhibiti jengo hilo baada ya mapambano makali ya siku mbili mfululizo.
Mirushiano ya risasi baina ya pande hizo mbili zimepungua kwa hivi sasa kulingana na hali ilivyokuwa jana, ambapo pilikapilika zilikuwa za kutosha huku watu wakiwa na taharuki.
Hata hivyo mpaka sasa bado taarifa zinasema waliofariki katika tukio hilo ni watu 62 na wengine 63 hawafahamiki walipo huku watu zaidi ya 200 wakiwa wamejeruhiwa japo baadhi yao wametibiwa na kuruhusiwa kurudi majumbani mwao.
Muda mchache uliopita imeripotiwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Kenya, Jomo Kenyatta alikuwa akijiandaa kulihutubia taifa kuwapa ukweli wa tukio hilo na takwimu halisi la operesheni hiyo ambayo imefanikishwa na vikosi vya ulinzi na usalama wa nchini hiyo ya Afrika Mashariki.
Magaidi hao wa Al Shaaban waliojinasibu kuhusika na tukio hilo walivamia jengo hilo lenye maduka ya bidhaa mbalimbali na kuwafyatulia risasi wateja na watumishi wa maduka hayo siku ya Jumamosi na kusababisha maafa hayo makubwa.
Hili ni tukio kubwa kufanywa na kundi hilo linalodaiwa linafadhiliwa na Al Qaida baada ya lile la mwaka 2010 mjini Kampala, Uganda wakati mashabiki wa soka zaidi ya 70 kulipuliwa kwa mabomui wakati wakiangalia Fainali za Kombe la Dunia katika runinga.
Msemaji wa kundi hilo alinukuliwa juzi kubwa wamefanya mauaji hayo kushinikiza serikali ya Kenya kuliondoa jeshi lake nchini Somalia wanapolinda amani katika jeshi la Umoja wa Mataifa, kitu ambacho serikali ya Nairobi imesisitiza hawataondoa jeshi lao.

Hivi ndivyo ilivyokuwa hekaheka za ukombozi wa jengo la Westgate, Nairobi Kenya


Siege: Kenya security personnel take cover outside the Westgate Mall after shooting started inside the mall early Monday morning, Sept. 23, 2013
Assault: Kenya Security personnel take cover outside the Westgate Mall after firing started inside the mall early Monday morning - Kenya's military launched a major operation at the upscale Nairobi mall and said it had rescued "most" of the hostages
Ongoing Military Operation: Kenya security personnel take cover outside the Westgate Mall
Waiting and Watching: Onlookers gather on a hill to observe the Westgate Mall after a bout of heavy gunfire just after dawn in Nairobi, Kenya Monday, Sept. 23, 2013
kwa picha zaidi bofya soma zaidi
Standoff: A Kenyan police officer (L) and a Kenya Defense Forces soldier (R) prepare for an incoming fire at the Oshwal Centre adjacent to the Westgate shopping mall where the hostage situation continues in Nairobi, Kenya on early Monday morning
Patience: Members of Kenya's security forces man a checkpoint outside the Westgate Mall in Nairobi, Kenya early Monday, Sept. 23, 2013
Kenyan policemen gather for a briefing near the Westgate Shopping Centre in the capital Nairobi, September 23, 2013. Heavy and sustained gunfire was heard from the Kenyan shopping mall on Monday morning
A truck of security forces arrives at the Westgate Mall after a bout of heavy gunfire just after dawn in Nairobi, Kenya Monday, Sept. 23, 2013.



Kenyan paramilitary officers walk towards a small shopping arcade adjacent to the Westgate shopping mall where the hostage situation continues in Nairobi, Kenya on Sunday
Rescue mission: An image from AFP TV shows military forces taking position inside the shopping mall
Kenyan police officers take cover to prepare for the incoming fire at the Oshwal Centre adjacent to the Westgate shopping mall where the hostage situation continues in Nairobi, Kenya, in the early hours of 23 September 2013
Assault: A Large number of troops from the kenya defence force arrived to strengthen the already formidable numbers of troops available as a Kenyan army helicopter flies low near the Westgate mall in Nairobi on Sunday
Tense: Kenyan paramilitary officers walk towards a small shopping arcade adjacent to the Westgate shopping mall where the fate of the hostages remained unclear on Monday morning
Armed response: Kenyan troops with machine guns take up position in the mall. The terrorist group al Shabaab demanded that Kenyan troops leave Somalia where they have pushed the militants on to the defensive in the past two years as part of an African Union-backed peacekeeping mission
Fleeing to safety: A soldier directs people up stairs inside the Westgate shopping mall after a shootout in Nairobi, Kenya
Laying siege: Armed police crouch down and take position during a gun battle with Islamic terrorists at the Westgate Mall in Nairobi, Kenya on Saturday
Lock-down: Kenya security personnel walk to their positions outside the shopping mall as the siege continued yesterday

Ashanti Utd kuzindukia Tabora? Itavaana na Rhino Rangers waliopanda nao Ligi Kuu

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/ashanti-aug23-2013.jpg
Ashanti United
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjfKSZcZys5ESjlNhn6Du0VkOqGFVkb8gUCv3UzZirPkcebsNYfANbRVhAOAl1OqftHcSm5puEpVqo5axdm__Ah1pbye4T7d3Eg-l_zw18-_m9V3fncdtkMQFlUkVN689pvjUj0mNOjNsc/s1600/TIMU+YA+RHINO.JPG
Rhino Rangers

Na Boniface Wambura
IKIWA inaburuta mkia katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ashanti United kesho inatarajiwa kuvaana na Rhino Rangers ya Tabora katika pambano pekee la ligi katikati ya wiki hii kujaribu kuzinduka ikizingatiwa wenyeji wao ni kati ya timu mbili waliopanda wote katika ligi hiyo.
Ashanti iliyotoka kupokea kipigo cha mabao 3-0 toka kwa Kagera Sugar haijaonja ushindi wowote katika mchezo huo zaidi ya kuambulia pointi moja ilipoumana na Azam wiki iliyopita.
Timu hiyo iliyorejea katika ligi hiyo itahitaji kesho kuibuka na ushindi ama angalau kuambulia pointi ili kuweka hai matumaini ya kusalia katika msimu ujao vinginevyo inaweza kurejea ilipotoka.
Pambano hilo la Rhino na Ashanti litachezwa kwenye uwanja wa Ali Hassani Mwinyi, mjini Tabora likiwa ni mchezo wa raundi ya sita ya ligi hiyo inayozidi kuchaanja mbuga katika duru lake la kwanza.

Katika mechi iliyopita Rhino Rangers ilitoka sare ya bao 1-1 jijini Tanga dhidi ya wenyeji wao Mgambo JKT huku ikiwa imejikusanyia pointi 4 kutokana na sare nne iliyopata na kupoteza mechi moja dhidi ya Azam.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014      
                                    P  W  D  L   F   A  GD  PTS
1.  Simba                      5   3   2   0  13  4    9   11
2.  JKT Ruvu                5   3   0   2   6   2    4    9
3.  Azam                       5   2   3   0   8   5    3    9
4.  Ruvu Shooting          5   3   0   2   6   3    3    9
5.  Coastal Union          5   2   3   0   5   2    3    9
6.  Kagera Sugar           5   2   2   1   6   3    3   8
7.  Mbeya City              5   1   4   0   5   4   1    7
8.  Yanga                       5   1   3   1  10  7   3   6
9.  Mtibwa Sugar           5   1   3   1   3  4   -1   6
10.Rhino Rangers           5   0   4   1   5  7   -2   4
11.Oljoro                       5   1   1   3   3   6  -3   4
12.Mgambo                   5   1   1   3   2  10 -8   4
13.Prisons                      5   0   3   2   2   8  -6   3
14.Ashanti                      5   0   1   4   2  11 -6   1

Twiga Stars kuanza na Wazambia Afrika

Na Boniface Wambura
TIMU ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) imepangiwa kucheza na Zambia katika mechi za kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika mwakani nchini Namibia.

Twiga Stars itaanzia ugenini jijini Lusaka ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Februari 13 na 15 mwakani wakati ile ya marudiano itafanyika kati ya Februari 28 na Machi 2 mwakani jijini Dar es Salaam.

Iwapo Twiga Stars itafanikiwa kuitoa Zambia, raundi ya pili ambayo ndiyo ya mwisho itacheza na mshindi kati ya Botswana na Zimbabwe. Mechi ya kwanza itakuwa Dar es Salaam kati ya Mei 23 na 25 mwakani wakati ile ya marudiano itakuwa kati ya Juni 6 na 8 mwakani.

Nchi 25 zimeingia katika mashindano huku mabingwa watetezi Equatorial Guinea, makamu bingwa Afrika Kusini na Cameroon iliyoshika nafasi ya tatu katika fainali zilizopita zikiingia moja kwa moja katika raundi ya pili.

Mabingwa wa ARS kupongezwa Dar

TIMU ya mpira wa miguu ya wasichana ya Airtel Raising Stars (ARS) ya Tanzania imeandaliwa hafla ya kuipongeza kwa kunyakua ubingwa katika mashindano ya Afrika yaliyofanyika nchini Nigeria.

Hafla hiyo ya kuipongeza pamoja na kupata chakula cha mchana itafanyika leo (Septemba 24 mwaka huu) saa 6 mchana kwenye hoteli ya Kilimanjaro Kempinski na kuongozwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara.

Timu hiyo iliyorejea nchini jana (Septemba 23 mwaka huu) usiku katika mchezo wa fainali ya mashindano hayo iliifunga Kenya. Kwa upande wa wavulana, timu hiyo ilitolewa na Zambia katika hatua ya nusu fainali.

Michuano hiyo ilishirikisha timu kutoka nchi za Burkina Faso, Chad, Congo Brazzaville, Gabon, Ghana, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Kenya, Madagascar, Malawi, Niger, Nigeria, Tanzania, Uganda na Zambia.

Kombaini ya timu hizo zilizokuwa chini ya makocha Rogasian Kaijage na Abel Mtweve iliundwa baada ya mashindano ya Airtel Raising Stars yaliyohusisha wasichana na wavulana wenye umri wa chini ya miaka 17 na kufanyika jijini Dar es Salaam wiki ya kwanza ya Septemba mwaka huu.


Washukiwa 10 wakamatwa tukio la Westgate Kenya

jengo lililokuwa likionekana kwa mbali likifoka moshi
WAKATI jeshi la Kenya likikaribia kumaliza udhia katika tukio la kigaidi lililotokea jengo la Westgate, Nairobi inaelezwa watu 10 wametiwa mbaroni wakihusishwa na tukio hilo lililosababisha vifo vya watu karibu 70 na wengine 180 walio majeruhi.
Kwa mujibu wa matangazo ya BBC yaliyomkunuu Waziri wa Mambo ya Usalama wa Kenya, Joseph Ole Lenku, alisema watu hao walikamatwa kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa ya Jomo Kenyatta na maeneo mengine baada ya kushukiwa siyo watu wazuri.
Hata hivyo waziri Lenku alisema kukamatwa kwa watu hao hakuna maana kwamba ndiyo wamemaliza operesheni au ni watuhumiwa halisi wa tukio hilo, isipokuwa wanaendelea kufanya uchunguzi kwa kina ili kubainia kama wanahusika au la kisha kujua hatua za kuwachukulia.
Kuhusu operesheni inayoendelea katika tukio hilo lililotokea juzi, waziri alisema jeshi na vikosi vya polisi vimefanikiwa kuthibiti jengo hilo na kusema muda wowote watakamilisha kazi kwa kuwatia mikononi waliohusika na tukio hilo ambapo mpaka sasa watekaji wawili wanadaiwa kuuwawa.
Waziri huyo alidokeza kuwa watekaji hao wanaodaiwa ni kikosi cha Al Shabaab walijaribu kujinusuru kwa kuchoma sehemu ya jengo na kusababisha kuonekana kwa moshi mkubwa angani mchana wa jana, lakini jeshi lilifanikiwa kulikamata jengo hilo kwa asilimia kubwa.

JKT Ruvu yakiri mambo magumu, ila...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjd4C_5b7DKHskUY74rJib8BoB0TsKIbBbv0QxyF_mRFh8S5UNwR6zasgpSq8laOW1bRuK1uUh7XsEEyA37aBCARBQAy1ZL5CCn7c2A_qnfXl0CB2I02EMNfDlo4nUqtyF7DxfW5pp-enQ4/s1600/MBWANA+MAKATTA.jpg
Kocha wa JKT,  Mbwana Makatta

KOCHA wa JKT Ruvu, Mbwana Makatta amesema vipigo viwili mfululizo ilivyopewa timu yake na kushushwa kileleni mwa msimamo mwa Ligi Kuu ni makosa yao wenyewe na sasa wanajipanga ili kuweza kuishikisha adabu Simba Jumapili.
Simba na JKT watavaana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam siku ya Jumapili katika mfululizo wa ligi hiyo ya Tanzania Bara itakayoingia raundi ya sita.
Makata alisema kutokana na umuhimu wa mchezo huo wa Jumapili wachezaji wake wataingia leo kambini baada ya mapumziko mafupi, lengo likiwa ni kuhakikisha wanarekebisha makosa yao na kupata ushindi mbele ya Simba.
Kocha huyo alisema vipigo viwili walivyopewa kutoka kwa Ruvu Shooting na Oljoro JKT vilitokana na umakini mdogo waliokuwa nao wachezaji wake kwa vile walitengeneza nafasi nyingi za kufunga mabao, lakini wakazipoteza.
Makatta anafahamu kwamba ukifanya makosa unastahili kuadhibiwa na anakiri kuwa ndicho kilichowakuta.
"Katika mechi zote tulitengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini wachezaji hawakuwa makini, labda kukosa bahati nako kumetuangusha, hivyo tunajipanga ili Jumapili tuweze kupata ushindi mbele ya Simba," alisema.
Makatta, kipa wa zamani wa klabu za Coastal Union, Tukuyu Stars na Yanga, alisema anajua Simba ni timu kubwa na ngumu, lakini Ruvu haitakubali kupoteza mechi ya tatu mfululizo.
Kocha huyo pia alisema amefurahia matokeo mabaya yaliyozikumba timu zilizokuwa zikiwafukuzia kwa nyuma na kuwafanya wasalie kwenye nafasi ya pili ya msimamo kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
"Kuboronga kwa wenzetu waliokuwa nyuma yetu kumetusaidia kupumua ndiyo maana tunaamini mipango yetu ya kumaliza katika nafasi mbili za juu za msimamo wa ligi mwishoni mwa msimu bado iko sawa," alisema Makatta.
JKT Ruvu ilianza ligi hiyo kwa kasi ikishinda mechi zake zote tatu za awali kabla ya kusimamishwa na ndugu zao Ruvu Shooting na Oljoro na kuwafanya wasalie na pointi 9 wakiiacha Simba kileleni inayoongoza ikiwa na pointi 11.