STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 31, 2014

Shi....Shilole achia ngoma mpya iitwayo Chuna Buzi

Shilole
BAADA ya kutamba na kibao chake cha 'Nakomaa na Jiji', msanii Zuwena Mohammed 'Shilole' ameachia kazi mpya iitwayo 'Chuna Buzi' na kuwataka mashabiki wake kumuunga mkono kama walivyofanya katika kazi zake za nyuma kuanzia 'Lawama', 'Dume Dada' hadi 'Paka la Baa'.
Wimbo ni utunzi wa Barnaba Boy ambaye ameutendea haki kwa kum back-up mkali huyo anayekimbiza katika filamu pia.

AZAM kukipiga na Ferreviario de Beira Chamazi


* CAF yaruhusu uwanja wake wa Chamazi

chamazi_2
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika CAF leo tarehe 31 Januari 2014 limeupa kibali cha kuchezea mashindanoya kimataifa yanayoandaliwa na CAF uwanja wa Azam Complex Chamazi na kuufanya uwanja wa kwanzaunaomilikiwa na klabu Afrika Mashariki  kuruhusiwa kuandaa (ku-host) mashindano makubwa ya vilabu
Kwa mujibu wa barua pepe iliyotumwa leo na CAF kupitia kwa naibu mkurugenzi wa mashindano Bwana Khaled Nassar, Uwanja wa Azam Compex Chamazi umepita vigezo vyote vinavyohitajika na CAF kuchezewa mashindano ya kimataifa hivyo kuanzia tarehe ya leo, uwanja huu unaruhusiwa “kuchezewa mechi za CAF
Bwana Khaled ameandika katika taarifa yake ya barua pepe kwenda TFF na Azam FC kuwa CAF ilimtuma mkaguziwake toka nchini Zimbabwe Bwana Wilfried Mukuna kuja kukagua uwanja huu. Bwana Mukuna aliwasilisha ripoti CAF iliyopelekea shirikisho hilo kutoa kibali kwa Azam FC na TFF kuruhusiwa kuutumia uwanja huu kwa mechi zinazoandaliwa na CAF
Uongozi wa Azam FC umetoa shukrani kwa mkaguzi wa CAF Bwana Mukuna, Uongozi wa TFF chini ya Rais Jamal Malinzi, na uongozi wa CAF Cairo Misri hasa Bwana Khaled Nasser kwa kuwezesha zoezi hili kufanyika kwa uwazi na uweledi wa hali ya juu uliopelekea uwanja wetu kupata kibali cha kutumika kwenye michezo ya kimataifa.
Azam FC sasa imewatangazi
wapenzi wake kuwa kuanzia msimu huu mechi zake za  CAF zitachezwa Azam Complex Chamazi

Yanga yakanusha Cannavaro, Niyonzima kuzichapa Mkwakwani

Niyonzima (kulia) na Cannavaro (kati) wakiwa na Chuji (24)

BENCHI la Ufundi la klabu ya Young Africans limekanusha taarifa kwamba nyota wawili wa timu yao, nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' na Haruna Niyonzima 'Fabregas' walipigana katika mchezo dhidi ya Coastal Union uliochezwa juzi jijini Tanga.
Kwa mujibu wa taarifa kupitia mtandao wa klabu hiyo wa www.youngafricans.co.tz , umemnukuu Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Charles Boniface Mkwasa 'Master' akisemataarifa hizo hazina ukweli wowote bali ni katika kutaka kuharibu twasira ya timu.
Mkwasa amesema benchi la ufundi wameshangazwa na taarifa hizo baada ya kuziona na kuzisoma leo na kusisitiza walioandika wamefanya hivyo kwa ajili ya maslahi yao tu.
Kila mtu alikuwepo uwanjani na aliweza kushuhudia mchezo huo, hakuna aliyeona Cannavaro na Niyonzima wakipigana katika kipindi chote cha dakika 90 za mchezo, nashikwa wasi wasi na waandishi waliokuwepo uwanjani kama walikua makini kufuatilia mchezo na kuandika kitu tofauti na walichokiona.
"Sheria za soka zipo wazi, mchezaji au wachezaji wapigana ndani ya uwanja mwamuzi anawatoa nje ya uwanja kwa kuwapa kadi nyekundu, sasa tumeshangazwa na taarifa hizo zilioripotiwa leo kuwa kuwa kuna wachezaji wetu walipigana ili wachezaji wote walicheza kwa dakika 90 "alisema Mkwasa.
Nadhani imefika wakati tuisaidie jamii kuelewa uhalisia wa jambo husika liliotokea, kwani kuandika tofauti na kilichotokea kunasababisha jamii kuamini/kuelewa jambo ambalo silo lililotokea.
Katika mchezo wowote wachezaji kuelekezana/kukumbushana majukumu ni jambo la kawaida na ndicho kilichotokea katika mchezo dhidi ya Coastal kati ya Cananavaro na Yondani na Niyonzima na Cannavaro na si kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
"Hata mara baada ya mchezo wachezaji wote walikuwa pamoja na kupeana pole kutokana na ugumu wa mechi, kisha wote kuondoka kuelekea hotelini kupumzika, na sisi kama viongozi hatujaona wachezaji kutofautiana kitu chochote hata kufikia hatua ya kusuruhishwa kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari " aliongeza Mkwasa .
Kuhusu maandalizi ya mchezo wa jumapili Mkwasa amesema vijana wake leo wamefanya mazoezi asubuhi kujiandaa na mchezo huo, na hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja kwani Hamis Kiiza, Hassana Dilunga waliokuwa wagonjwa wameshaungana wenzao kambini na Athuman Idd "Chuji"  aliyekua amesimamishwa kurejeshwa kundini.

Bodi ya Ligi Kuu yazipiga jeki klabu za FDL

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetoa sh. milioni 1.5 kwa kila klabu ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Uamuzi wa kuzisaidia timu hizo ulifanywa katika kikao cha TPLB kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam ambapo fedha hizo zitalipwa kupitia kwenye akaunti za klabu husika. 

Hivyo klabu ambazo hazijawasilisha akaunti zao TPLB zinatakiwa kuwasilisha haraka.
Klabu za FDL ni African Lyon, Burkina Moro, Friends Rangers, Green Warriors, Kanembwa JKT, Kimondo, Kurugenzi Mafinga, Lipuli, Majimaji, Mkamba Rangers, Mlale JKT na Mwadui.
Nyingine ni Ndanda, Pamba, Polisi Dar es Salaam, Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Morogoro, Polisi Tabora, Stand United, Tessema, Toto Africans, Trans Camp na Villa Squad.

TFF mpya yatimiza siku 100 madarakani, Rais Malinzi kuteta Ijumaa

Rais wa TFF, Jamal Malinzi
Na Boniface Wambura
KAMATI mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya Rais Jamal Malinzi, Februari 4 mwaka huu inatimiza siku 100 tangu iingie madarakani katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 28 mwaka jana.
Hivyo, Rais Malinzi atazungumza na waandishi wa habari Februari 7 mwaka huu kuelezea utekelezaji wa Ilani yake ya uchaguzi. Muda na mahali utakapofanyika mkutano huo mtaarifiwa baadaye.


Serengeti Boys kuanza na Afrika Kusini mchujo wa Afrika

Na Boniface Wambura
TIMU ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) itacheza na Afrika Kusini katika mechi za mchujo kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa umri huo zitakazofanyika mwakani nchini Niger.
Serengeti Boys ambayo pamoja na nchi nyingine 17 zimeingia moja kwa moja katika raundi ya pili itaanzia mechi hiyo nyumbani kati ya Julai 18-20 mwaka huu wakati ile ya marudiano itafanyika nchini Afrika Kusini kati ya Agosti 1-3 mwaka huu.
Ikifanikiwa kuitoa Afrika Kusini, Serengeti Boys itacheza mechi ya raundi ya tatu na ya mwisho na mshindi wa mechi kati ya Misri/Sudan vs Congo Brazzaville.
Nchi nyingine ambazo zimeingia moja kwa moja raundi ya pili ni Afrika Kusini, Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Congo Brazzaville, Ethiopia, Gabon, Ghana, Ivory Coast, Mali, Morocco, Nigeria, Rwanda, Senegal, Tunisia na Zambia.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inatarajia kutangaza benchi la ufundi litakaloiongoza Serengeti Boys hivi karibuni.

Simba, Oljoro kesho hapatoshi, Ashanti Utd kutoka vipi Chamazi

Simba
Oljoro JKT
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kuwania ubingwa wa Tanzania inaingia raundi ya 16 wikiendi hii kwa mechi nne ambapo kesho (Februari 1 mwaka huu) Simba itakuwa mwenyeji wa Oljoro JKT katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Viingilio katika mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni ni sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A. Refa atakuwa Nathan Lazaro kutoka mkoani Kilimanjaro wakati Kamishna ni Hakim Byemba wa Dodoma.

Uwanja wa Azam uliopo Mbagala siku hiyo kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Ashanti United na Mgambo Shooting kutoka Handeni mkoani Tanga kwa viingilio vya sh. 3,000 kwa sh. 10,000.
Jumapili (Februari 2 mwaka huu) ni Yanga vs Mbeya City (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, saa 10 kamili jioni), na Azam vs Kagera Sugar (Uwanja wa Azam Complex, Chamazi saa 10 kamili jioni).
Ligi hiyo itaendelea Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kwa mechi kati ya Tanzania Prisons vs Coastal Union (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora), na JKT Ruvu vs Ashanti United (Uwanja wa Azam Complex, Chamazi).

Thursday, January 30, 2014

Huu ndiyo usajili dirisha dogo England

ARSENAL
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Chuba Akpom (Brentford, mkopo), Anthony Jeffrey (Wycombe, mkopo)

ASTON VILLA
WALIOSAJILIWA
Grant Holt (Wigan, mkopo)
WALIOONDOKA
Stephen Ireland (Stoke, huru), Michael Drennen (Carlisle, mkopo)

CARDIFF
WALIOSAJILIWA
Magnus Wolff Eikrem (Heerenveen, £2m), Mats Moller Daehli (Mold,ada haikutajwa),
Jo Inge Berget (Molde, ada haikutajwa), Kenwyne Jones (Stoke, mabadilishano)
WALIOONDOKA
Rudy Gestede (Blackburn, ada haikutajwa), Filip Kiss (Ross County, mkopo), Nicky Maynard (Wigan, mkopo), John Brayford (Sheffield Utd,mkopo), Peter Odemwingie (Stoke, mabadilishano)

CHELSEA
WALIOSAJILIWA
Bertrand Traore (Association Jeunes Espoirs De Bobo-Dioulasso, ada haikutajwa), Nemanja Matic (Benfica, £21m), Mohamed Salah (Basel £11m)
WALIOONDOKA
Bertrand Traore (Vitesse Arnhem, mkopo), Kevin de Bruyne (Wolfsburg, £17m), Josh McEachran (Wigan, mkopo), Michael Essien (AC Milan, ada haikutajwa), Sam Walker (Colchester, mkopo), Nathaniel Chalobah (MIddlesbrough, mkopo)

CRYSTAL PALACE
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Jason Banton (Plymouth, huru), Jimmy Kebe (Leeds, mkopo), Kwesi Appiah (Notts County, mkopo), Matt Parsons (Plymouth, ada haikutajwa)

EVERTON
WALIOSAJILIWA
Aiden McGeady (Spartak Moscow, ada haikutajwa), Lacina Traore (Monaco, mkopo)
WALIOONDOKA
Nikica Jelavic (Hull, ada haikutajwa)

FULHAM
WALIOSAJILIWA
Clint Dempsey (Seattle Sounders, mkopo)
WALIOONDOKA
Bryan Ruiz (PSV, mkopo)

HULL
WALIOSAJILIWA
Nikica Jelavic (Everton, ada haikutajwa), Elliott Kebbie (Atletico Madrid, mkopo), Shane Long (West Brom, £6m)
WALIOONDOKA
Tom Cairney (Blackburn, £500,000), Conor Townsend (Carlisle, mkopo), Eldin Jakupovic (Leyton Orient, mkopo), Cameron Stewart (Leeds, mkopo), Nick Proschwitz (Barnsley, mkopo).

LIVERPOOL
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Adam Morgan (Yeovil, huru), Tiago Ilori (Granada, mkopo)

MANCHESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
John Guidetti (Stoke, mkopo), Albert Rusnak (Birmingham, mkopo)

MANCHESTER UNITED
WALIOSAJILIWA
Juan Mata (Chelsea, £37.1m)
WALIOONDOKA
Jack Barmby (Hartlepool, mkopo), Anderson (Fiorentina)

NEWCASTLE
WALIOSAJILIWA
Luuk de Jong (Borussia Monchengladbach, mkopo)
WALIOONDOKA
Yohan Cabaye (Paris-Saint Germain, £23m), Jonas Gutierrez (Norwich, mkopo)

NORWICH
WALIOSAJILIWA
Jonas Gutierrez (Newcastle, mkopo)
WALIOONDOKA
Daniel Ayala (Middlesbrough, £350k)

SOUTHAMPTON 
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Lee Barnard (Southend, mkopo)

STOKE CITY
WALIOSAJILIWA
John Guidetti (Man City, mkopo), Stephen Ireland (Aston Villa, huru), Juan Agudelo (New England Revolution, huru)
WALIOONDOKA
Brek Shea (Barnsley, mkopo), Jamie Ness (Leyton Orient, mkopo), Juan Agudelo (FC Utrecht, mkopo)

SUNDERLAND
WALIOSAJILIWA
Marcos Alonso (Fiorentina, mkopo), Santiago Vergini (Estudiantes, mkopo), Oscar Ustari (Almeria, huru)
WALIOONDOKA
Mikael Mandron (Fleetwood, mkopo), Ji Dong-won (Ausburg, ada haikutajwa), Billy Knot (Port Vale, mkopo)

SWANSEA
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Alan Tate (Aberdeen, mkopo)

TOTTENHAM
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Jermain Defoe (Toronto, £6m), Simon Dawkins (Derby, ada haikutajwa), Shaquile Coulthirst (Leyton Orient, mkopo), Jon Obika (Brighton, mkopo), Ryan Fredericks (Millwall, mkopo)

WEST BROMWICH ALBION
WALIOSAJILIWA
Hakuna
WALIOONDOKA
Lee Camp (Bournemouth, huru)

WEST HAM
WALIOSAJILIWA
Roger Johnson (Wolves, mkopo), Antonio Nocerino (Milan, mkopo), Marco Borrielo (Roma, mkopo)
WALIOONDOKA
Blair Turgott (Rotherham, mkopo)

Kiungo Yohan Cabaye rasmi PSG

Cabaye asaini rasmi Paris St Germain.
MABINGWA wa Ufaransa PSG, hatimaye imemsajili kiungo,Yohan Cabaye kutoka Newcastle United kwa kiasi cha pauni milioni 20.
Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 28 amesaini mkataba wa miaka mitatu na nusu kwa klabu hiyo ya Ligue 1.
Cabaye alisema kuwa”Ninafuraha sana kurejea Ufaransa,ofa kutoka kwa PSG ilikuwa ngumu sana kuikataa,nataka kushinda mataji na nina furaha kubwa kupata nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa barani ulaya.”
Nyota huyo ambaye pia ni kiungo wa timu ya Taifa ya Ufaransa aliichezea Newcastle United jumla ya michezo 79 na kufunga goli 17.
Pia Cabaye katika kipindi cha usajili uliopita wa majira ya kiangazi,alishawahi kutaka kuiacha klabu hiyo ya Uingereza huku akilazimisha kuhamia Arsenal bila mafanikio

Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee Malecela aibuka mbio za Urais 2015

WAZIRI MSTAAFU SAMUEL MALECELA AKIONYESHA FULANA ILIYOANDIKWA JINA LA LOWASSA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI --30/01/2014



Ndugu zangu waandishi wa habari, awali ya yote naomba niwasalimie na niwapongeze kwa kufika -mwaka mpya 2014, pia naomba niwapongeze kwa kazi kubwa ambayo mmekuwa mkiifanya hasa kuhakikisha watanzania wanapata habari kwa kila jambo linaloendelea kila kona ya taifa letu la Tanzania.

Ndugu waandishi wa habari nimewaita hapa ili kuzungumza nanyi na mnisaidie kufikisha ujumbe kwa watanzania hasa kuhusu jambo hili ambalo limekuwa gumzo kwa watanzania wengi la mbio za urais 2015 kwa baadhi ya watu ndani ya chama changu cha mapinduzi (CCM), kilichonisukuma zaidi na kupata hamu ya kuongea nanyi ni baada ya kumsikia -na kumuona kijana wetu ndani ya chama cha mapinduzi bwana Paul Makonda akiwa na ujasiri wa kukemea vitendo mambo haya yanayofanywa na baadhio ya viongozi bila uwoga wowote naomba tuchukue fursa hii kumpongeza sana kijana huyu.

Nadiriki kusema nampongeza kijana huyu hasa kwa kauli zake nzito na za kijasiri kwa maslahi ya chama changu cha CCM ili chama kiendelee kupendwa na kuchaguliwa na watanzania.

Pia itakuwa si busara kama sitawapongeza vijana wangu katibu mkuu wa chama ndugu ABDULRAHMAN KINANA na NAPE NNAUYE kwa juhudi zao za dhati za kujenga chama na kuendelea kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya chama cha mapinduzi (CCM) kwa kuwakemea viongozi wasiofaa bila kujali cheo na umaarufu wao ndani ya chama na serikali, nawaomba waendelee -na juhudi zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watru wanaowabeza naomba wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ndani ya chama na serikali ni msingi wa chama chochote kilichounda serikali.

Aidha nawaomba watanzania wenzangu wazalendo wasikubali kukatishwa tama na kikundi cha watu wachache wasio na mapenzi mema na taifa letu ambalo limekuwa mfano wa kuigwa kwa amani, upendo, utulivu na mshikamano urithi tulioachiwa na baba yetu wa taifa mwalimu julias kambarage nyerere ndani na nje ya mipaka ya bara letu la afrika.

Ndugu zangu waandishi wa habari naomba niwaambie kuwa msemaji wa UVCCM kijana wetu Paul Makonda namuunga mkono kwa -kitendo chake cha ujasiri cha kumkemea ndugu EDWARD NGOYAI LOWASSA bila uwoga kwa jinsi anavyokivuruga chama chetu kwa lengo la kutaka urais 2015 huku secretariet ya chama ikiwa imekaa kimya wakati inajua kuwa muda wa kuanza mbio hizi bado na kufanya hivi kwa sasa ni kukiuka misingi na katiba -ya chama. Hapa najiuliza kuwa ile misingi imara ya uongozi ndani ya chama chetu cha mapinduzi iko wapi? Mpaka tumuachie mototo ndio akemee haya? Je, hapa chama kiko wapi?

Ukweli ni kwamba wanachama wetu na vijana wamekuwa njia panda huku wakitamani kusikia tamko au karipio la chama juu ya suala hili la harakati za urais 2015 bila mafanikio.

Naomba niseme kuwa bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia pesa zao hadharani kwa lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa vijana ili kupata madaraka wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya chama.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuona juhudu za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni pamoja na sekretarieti inayoongozwa na katibu mkuu ABDULRAHMANI KINANA na katibu mwenezi NAPE NNAUYE za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga.

Ninaomba juhudi hizi zisibezwe na watu wenye nia njema na chama. Ukweli ni kwamba vijana hawa wamekuwa na juhudi kubwa sana ya kujenga na kuimarisha chama chetu -kwa wananchi kila pembe ya taifa letu kwa kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. Swali: Je! Chama hakioni haya mpaka vijana ndio waone?

Kwa hili ni lazima tubadilike ili kujenga chama chetu na naishauri -secretariet ya chama lazima ichukue hatua mara moja, kijana huyu paul makonda asingesema haya yote kama hana uhakika wa ushahidi wa wa haya aliyoyasema na nampongeza sana.

Vijana na wanachama wengi wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka kujua msimamo wa chama chao bila mafanikio na ndio sababu ya baadhi ya-wengine kupoteza mwelekeo.

Sisi tulikijenga chama hiki kwa taabu sana hapakuwa hata mtu mmoja aliyediriki kutumia fedha zake kutaka madaraka. Nidhamu, busara na uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa maslahi ya wananchi ndio vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi ndani ya chama na serikali, ndio maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka kutekwa na wenye fedha kwa uchu wa madaraka, mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi pesa wanatoa wapi? Na haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa maslahi ya nani? Huku watanzania wakiendelea kuwa maskini.

Mfano hivi karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana kwenye vyombo vya habari,vitendo hivi havina tija kwa chama na wala havileti umoja na mshikamano ambao umedumu ndani chama kwa muda mrefu.

Mwisho Ninaomba sekretarieti ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu makonda na kweli kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi kwamba utaleta kutokuelewana ndani ya chama kusiko kuwa na lazima.


JOHN SAMWELI MALECELA

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Yanga yaiendea Mbeya City Bagamoyo

Yanga watashangilia kama hivi hiyo Jumapili kwa Mbeya City?
Dua za Mbeya City zitaleta maajabu Taifa mbele ya Yanga Jumapili?
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wameiendea kambini mjini Bagamoyo timu ya Mbeya City, ikiwa ni mikakati ya kuhakikisha wanapata ushindi siku ya Jumapili wakati watakapoumana nao.
Yanga na Mbeya City zinazoshika nafasi ya pili na tatu katika msimamo wa ligi hiyo nyuma ya Azam, zitaumana Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Timu hizo zitaumana zikiwa na kumbukumbu ya kupata sare katika mechi zao zilizopita Yanga ikitoka suluhu na Coastal Union jijini Tanga na Mbeya City ikibanwa na Ruvu Shooting na kutoka sare ya 1-1 kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi Pwani.
Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto amenukuliwa jijini Dar es Salaam akisema kuwa timu yao imeenda kuweka kambi Bagamoyo tangu mchana wa leo kwa ajili ya kujiweka vyema kabla ya kuwakabili wapinzani wao.
Yanga inayonolewa na kocha mpya 'Johannes van Der Pluijm, inakumbuka ilipolazimishwa sare ya 1-1 na wapinzani wao katika pambano lao la kwanza lililochezwa Septemba 14, mwaka jana walipoumana uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Watetezi hao waliokuwa nchini Uturuki kwa kambi ya wiki mbili, bado haijawaridhisha mashabiki wake kama kweli walikuwa Ulaya tofauti na duru lililopita waliporejea toka huko na kutoa vipigo vikali kwa wapinzani wao.
Hata hivyo, Kizuguto alisema kikosi chao kipo vyema kwa ajili ya mechi hiyo ya Jumapili ili kuhakikisha wanashinda na kurejea kwenye uongozi wa ligi hiyo uliochukuliwa jana na Azam baada ya kuishinda Rhino Rangers kwa bao 1-0 wakati Yanga ikitoka suluhu Mkwakwani Tanga.
Nayo Mbeya City iliyokwishawasili jijini Dar, imetamba kuwamba wamekuja Dar kuthibitisha kuwa sare walioipata Sokoine walipoumana na Yanga haikuwa ya kubahatisha na hasa ikizingatiwa tayari ligi wameshaizoea tofauti na mechi hiyo ya mwaka jana.
Kabla ya pambano hilo la Jumapili, siku ya Jumamosi kutakuwa na mechi mbili za ligi hiyo ambazo zote zitachezwa jijini Dar kwa pambano la Simba dhidi ya Oljoro JKT katika uwanja wa Taifa na pambano jingine litakuwa uwanja wa Chamazi kati ya Ashanti United dhidi ya Mgambo JKT.
Katika mechi za awali baina ya timu hizo, Simba na Mgambo zilizwasinda wapinzani wao kwa bao 1-0 kila moja na hivyo Ashanti na Oljoror zitakuwa na kazi ya kutaka kulipiza kisasi siku hiyo.

Mhe. Temba, Cassim Mganga wana Lavalava la pamoja

Mhe Temba

Cassim Mganga

WASANII nyota wa muziki wa kizazi kipya, Mheshimiwa Temba na Cassim wanatarajia kuachia hadharani kazi yao mpya ya pamoja iitwayo 'Lavalava' Ijumaa wiki hii.
Akizungumza na MICHARAZO, meneja wa wasanii hao Said Fella, alisema wimbo huo umerekodiwa katika studio za Burn Records chini ya prodyuza Sheddy Clever.
Fella alisema 'kolabo' hiyo ni mwanzo tu kwa wasanii hao kutoka TMK Wanaume Family na ukoo wa Tip Top Connections kufanya kazi kwa pamoja ikiwamo kuja kuzalisha albamu kamili.
"Katika kuendelea udugu baina ya wasanii mbalimbali nchini, Mhe. Temba na Cassim Mganga wametengeneza wimbo wa pamoja uitwao 'Lavalava' na utaachiwa hewani kuanzia Ijumaa ijayo na kama mambo yakienda vyema wasanii hao wanaweza kuja kutoa albamu ya pamoja," alisema Fella.
Cassim anayefahamika kama 'Tajiri wa Mapenzi' anatamba kwa sasa na wimbo wake uitwao  I Love You', huku Mhe Tamba anakimbiza kupitia kibao chake kiitwacho 'Toroka Uje' alichoimba na Dogo Aslay na akiwa mbioni kuachia dokomentari yake iitwayo 'Maskini Jeuri'.