STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 6, 2013

Ronaldo aizamisha Manchester United na kuing'oa Ulaya

Kocha wa Real Madrid, Jose Morinho akimtuliza Nani baada ya kulimwa kadi nyekundu
Luca Modric akisawazisha bao la Real Madrid jana


 

'Muuaji' Real Madrid akiwajibika uwanjani jana OT

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Manchester United, Cristiano Ronaldo usiku wa kuamkia leo alikuwa mwiba mbali kwa vinara hao wa Ligi Kuu ya England baada ya kufunga bao la ushindi na kuiondosha Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ronaldo aliyepata mafanikio makubwa akiwa na klabu hiyo ya Old Trafford, jana alirejea kivingine kwa kuifungia Real Madrid bao la pili na la ushindi na kuifanya timu yake kufuzu robo fainali za Ulaya kwa jumla ya mabao 3-2.
Katika mechi ya awali iliyoisha kwa sare ya bao 1-1 mjini Madrid, Ronaldo ndiye alifunga bao la kuasawazisha na jana alionyesha alivyo muhimu kwa kikosi hicho cha Morinho kwa kufunga bao lililoipa Real ushindi wa 2-1 uwanja wa Old Trafford.
Madrid waliwapa matumaini vijana wa Sir Alex Ferguson alimuanzishia benchi Wayne Rooney, baada ya Sergio Ramos kujifunga bao baada ya kipindi cha pili kabla ya kurekebisha kosa lake kwa kusaidia kupatikana kwa bao la kusawazisha lililofuingwa na Luca Modric aliyetokea benchi.
Manchester United iliyomuanzisha benchi nyota wake, Wayne Rooney ilijikuta ikimpoteza winga wake mahiri, Luis Nani aliyemchezea rafu Alvaro Albeloa kadi iliyolalamikiwa na Sir Ferguson kabla ya Ronaldo kuja kuwazamisha.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana mabingwa wa Ujerumani, Borussia Dotmund iliungana na Real baada ya kuing'oa Shakhtar Donetsk kwa jumla ya mabao 5-2 baada ya kupata ushindi nyumbani wa mabao 3-0 wiki mbili tangu walipolazimisha sare ya mabao 2-2 ugenini.
Michuano hiyo itaendelea tena usiku wa leo kwa mechi nyingine mbili, Juventus ya Italia itakuwa nyumbani kuialika Celtic walioitungia kwao mabao 3-0 na Valencia itaifuata PSG nchini Ufaransa wakiwa nyuma ya mabao 2-1 iliyofungwa ilipocheza nyumbani Hispania.