STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 20, 2012

TANZANIA YAPANDA VIWANGO VYA FIFA

KIkosi cha timu ya soka ya Tanzania iliyopanda kiwango cha ubora duniani kwa mujibu wa FIFA

TANZANIA imepanda kwa nafasi nne katika viwango vya ubora wa soka duniani vilivyotolewa jana na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ambapo sasa inakamata nafasi ya 130 duniani kutoka ya 134 iliyokuwa ikiishikilia mwezi uliopita.
Kwa mujibu wa viwango hivyo, Tanzania imepanda baada ya ushiriki wake katika michuano ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Chalenji) iliyomalizika hivi karibuni jijini Kampala, Uganda.
Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) ambayo ndiyo inayoangaliwa na FIFA, iliishia katika hatua ya nusu fainali na matokeo yaliyoangaliwa katika kuipangia nafasi yake kwenye viwango ni ya mechi ya nusu fainali waliyolala 3-0 dhidi ya Uganda, robo fainali waliyoshinda 2-0 dhidi ya Rwanda na pia za hatua ya makundi walizoshinda 7-0 dhidi ya Somalia, 1-0 dhidi ya Sudan na kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Burundi.
Katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Tanzania inakamata nafasi ya 6 kati ya nchi 11. Mabingwa wa Kombe la Chalenji, Uganda wanaongoza kwenye ukanda huu huku wakishika nafasi ya 84 duniani, wakifuatiwa na Sudan (101), Ethiopia(110), Burundi iliyopanda kwa nafasi 24 na kushika nafasi ya 104 na Tanzania (130).
Kenya na Rwanda ziko pamoja katika nafasi ya 134 na kufuatiwa na Somalia (195), Eritrea (196), Sudani Kusini (199) na Djibout inakamata nafasi ya mwisho kwenye ukanda wa CECAFA baada ya kushika nafasi ya 202 duniani.
Barani Afrika, Ivory Coast ya kina Didier Drogba inaendelea kukamata nafasi ya kwanza huku ikiwa ya 14 katika viwango vya dunia na kufuatiwa na Algeria inayokamata nafasi ya 19, Mali (25), Ghana (30), Zambia (34), Misri (41), Gabon (42), Jamhuri ya Afrika ya Kati (52), Libya (54) na Guinea inayoshika nafasi ya 60.
Hipania ambao ni mabingwa wa Kombe la Dunia na Ulaya wanaendelea kuongoza kwa kushika nafasi ya kwanza katika viwango vya ubora duniani, wakifuatiwa na nchi za Hispania, Ujerumani, Argentina, Italia, Colombia, England, Ureno, Uholanzi, Urusi na Croatia.

YANGA, PRIME TIME WAINGIA MKATABA



Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Clement Sanga (kushoto) na Mkurugenzi wa kampuni ya Prime Time Promotions Josheph Kusaga (kulia) wakisaini mkataba mbele ya waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga jana
Klabu ya Young Africans leo imeingia mkataba na kampuni ya Prime Time Promotions ya jijini Dar es saaalm kwa ajili ya kuandaa shuguli za mkutano mkuu wa wanachama utakaofanyika Januari 19, 2013 ambapo kampuni ya Prime Time imetoa mil 105,000,000 kwa ajili ya kuratibu shughuli hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari, makamu mwenyekiti wa klabu ya Yanga Clement Sanga amesema wamefikia hatua hiyo kuipa nafasi kampuni ya Prime Time kuweza kuuendesha mkutano huo kisasa zaidi, ambapo unategemewa kufanyika na kuonyesha moja kw amoja  (live) kupitia kituo cha Luninga ya Clouds.
Prime Time pia imepewa fursa ya kusaka masoko na wadhamini wa klabu ya Yanga ili kuhakikisha klabu inajijenga vizuri kiuchumi kwa kubuni miradi mbali mbali, ambapo kwa kuanzia itaanda mchezo mmoja wa kirafiki na timu kubwa barani Afrika mwanzoni mwa mwezi Januari 2013.
Naye Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Joseph Kusaga amesema amefurahishwa kwa kampun yake kupewa nafasi hiyo na kusema wanaahidi watafanya kazi nzuri kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Aidha Kusaga alisema milango iko wazi kwa timu yoyote kuomba kushirikiana nao, kwani hawana itikadi ya timu yoyote bali lengo lao ni kufanya timu zote ziwe katika nafasi nzuri kiuchumi na kujitangaza kimichezo na kimasoko.
CHANZO:BIN ZUBEIRY

ZUKU TZ NA MAXCOM WAJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA MALIPO 

 Meneja  Mkazi wa Zuku Tanzania, Fadhili Mwasyeba akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa kutia saini makubaliano ya ushirikiano baina yao na kampuni ya Maxcom, kupitia huduma ya maxmalipo. Kulia ni Mwendeshaji Mkuu wa Kampuni ya Maxcom, Ahmed Lussasi.
Mwendeshaji mkuu wa Kampuni ya Maxcom, Ahmed Lussasi akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.
Mwendeshaji Mkuu wa Maxcom, Ahmed Lussasi akizungumza, hukui maafisa wenzake kutoka Zuku Tanzania wakimsikiliza.
Mwendeshaji Mkuu wa Kampuni ya MaxCom, Ahmed Lussasi, (kulia) akionesha mashine ya Maxmalipo  wakati wa mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa kutia saini makubaliano ya Ushirikiano na Kampuni ya Zuku Pay Tv, ambapo wateja wa Zuku watalipia ada zao za mwezi kupitia huduma ya Maxmalipo. Kushoto ni Meneja  Mkazi  Zuku Tanzania, Fadhili Mwasyeba.


KAMPUNI ya Wananchi Satellite Ltd inayomiliki televisheni ya kulipia ya Zuku kikishirikiana na kampuni ya Max Com zimeingia mkataba wa kuanza kutoa huduma rahisi ya malipo kwa wateja wa televisheni hiyo kwa nchi nzima kutumia huduma ya Maxmalipo.
Uzinduzi wa huduma hizo ulifanyika jana jijini Dar es Salaam baada ya viongozi wa pande hizo mbili kusaini mkataba huo mbele ya waandishi wa habari katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond, uliopo  Ubungo.
Meneja wa Wananchi Satellite kwa hapa nchini, Fadhili Mwasyeba alisema wameamua kurahisisha huduma ili kuwapa fursa wateja wao kufanya malipo kwa njia nyepesi na ya haraka tofauti na siku za nyuma kwa kutumia Maximalipo.
"Tuna furaha juu ya ushirikiano huo mpya na utakaowajali wateja wetu wa Zuku. Ahadi yetu ni kutoa ufumbuzi rahisi kwa wateja wetu wafanyabiashara na wauzaji na ufumbuzi huui utatuwezesha kufika mbali zaidi ya matarajio ya vwateja wetu." alisema.
Aidha Mwasyeba aliongeza kuwa wakati wakiwarahisishia unafuu wa kulipa malipo ya kila mwezi kwa wateja wao, pia kampuni yao inaendelea na promosheni yao ya kuwazawadia wateja wao iitwayo Zuku Tunakuthamini-Pata Tv Bure'.
Alisema kinachotakiwa kwa wateja kuwaunganisha wateja watano kujiunga na Zuku na kulipia malipo na kisha kujishindia runinga kati ya inchi 22 na wale watakaofikisha idadi ya wateja 10 watanyakua rungina ya inchi 42 na walioungwanishwa nao wakiambulia 'offer' nyingine zinazotolewa na kampuni yao kupitia promosheni hiyo.
Naye Msimamizi Mkuu wa kampiuni Maxcom, Ahmed Lussasi, alisema kuanza kutoa huduma hiyo kwa wateja wa zuku ni fursa ya kuwapa unafuu wateja wa televisheni hiyo popote walipo nchini kutokana na kampuni yao kuwa na vituo vya malipo ya Max malipo zaidi ya 3500 nchi nzima.
"Tunajitahidi kufanya kazi kwa ufanisi kwa malipo ya ushirikiano wa kipekee na zuku ili kuwafikia wateja kwa ukaribu zaidi," alisema na kuongeza;
Tuna furaha kufanya kazi na Zuku na tunaamini huu ni mwanzo tu wa ushirikiano wa kibiashara," alisema.
Televisheni ya Zuku inatoa uchaguziu mpana wa stesheni za burudani ikiwa ni pamoja na habari, michezo na sinema, majarida na muziki ikiwa imejumuisha chaneli za kimataifa kama BBC, MTV Base. Sentanta Sports, MGM Movies na nyinginezo ka gharama nafuu kwa ubora na kiwango cha hali ya juu.