STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 20, 2012

TANZANIA YAPANDA VIWANGO VYA FIFA

KIkosi cha timu ya soka ya Tanzania iliyopanda kiwango cha ubora duniani kwa mujibu wa FIFA

TANZANIA imepanda kwa nafasi nne katika viwango vya ubora wa soka duniani vilivyotolewa jana na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ambapo sasa inakamata nafasi ya 130 duniani kutoka ya 134 iliyokuwa ikiishikilia mwezi uliopita.
Kwa mujibu wa viwango hivyo, Tanzania imepanda baada ya ushiriki wake katika michuano ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Chalenji) iliyomalizika hivi karibuni jijini Kampala, Uganda.
Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) ambayo ndiyo inayoangaliwa na FIFA, iliishia katika hatua ya nusu fainali na matokeo yaliyoangaliwa katika kuipangia nafasi yake kwenye viwango ni ya mechi ya nusu fainali waliyolala 3-0 dhidi ya Uganda, robo fainali waliyoshinda 2-0 dhidi ya Rwanda na pia za hatua ya makundi walizoshinda 7-0 dhidi ya Somalia, 1-0 dhidi ya Sudan na kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Burundi.
Katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Tanzania inakamata nafasi ya 6 kati ya nchi 11. Mabingwa wa Kombe la Chalenji, Uganda wanaongoza kwenye ukanda huu huku wakishika nafasi ya 84 duniani, wakifuatiwa na Sudan (101), Ethiopia(110), Burundi iliyopanda kwa nafasi 24 na kushika nafasi ya 104 na Tanzania (130).
Kenya na Rwanda ziko pamoja katika nafasi ya 134 na kufuatiwa na Somalia (195), Eritrea (196), Sudani Kusini (199) na Djibout inakamata nafasi ya mwisho kwenye ukanda wa CECAFA baada ya kushika nafasi ya 202 duniani.
Barani Afrika, Ivory Coast ya kina Didier Drogba inaendelea kukamata nafasi ya kwanza huku ikiwa ya 14 katika viwango vya dunia na kufuatiwa na Algeria inayokamata nafasi ya 19, Mali (25), Ghana (30), Zambia (34), Misri (41), Gabon (42), Jamhuri ya Afrika ya Kati (52), Libya (54) na Guinea inayoshika nafasi ya 60.
Hipania ambao ni mabingwa wa Kombe la Dunia na Ulaya wanaendelea kuongoza kwa kushika nafasi ya kwanza katika viwango vya ubora duniani, wakifuatiwa na nchi za Hispania, Ujerumani, Argentina, Italia, Colombia, England, Ureno, Uholanzi, Urusi na Croatia.

No comments:

Post a Comment